Diamond aachia wimbo mpya "Acha nikae kimya"

Diamond aachia wimbo mpya "Acha nikae kimya"

Domo bana GSM ndio mabwana zake Kwahiyo lzm afuate masharti ya bashite
 
Nimesa comment zenu wengi naona uchambuzi wa sanaa umewapita kushoto,jaribuni kuchukua muda wenu msikilize walau mara mbili mara tatu mtamuelewa sana diamond,mama ake kamwambia akae kimya...je ukisikiliza hiyo nyimbi mmeuona huo ukimya? Kaongelea masakata ya vyeti vya bashite, kaongelea kuhusu nape,roma na bunge...mwishoni akawa anaisikitikia tanzania wapi tunakoenda....sanaa inahitaji mtu utuluze akili sana ili uielewe
Limbwata la WCB kali sana
 
roma ametekwa na wavuta bange wenzake acha ujinga wewe
Bwana sijui bibi gonzo, soma alama za nyakati....wavuta bangi?!wamemteka ili iwaje?!wachukue misokoto iliobaki?!bashite anataka kuhit katika media....hapo tu, taratibu wahariri watalegeza kama wakiingia mtego wake...pale panafanywa ni mtakuja
 
Unatakiwa ujue kutafsiri ujumbe through wimbo mzima na sio neno moja.....kwa ujumla anakemea mambo yote yanayoendelea Tanzania km taifa tunaenda wapi? tumepoteza upendo na utaifa.tushikamane tuijenge Tanzania.

Mfate mwalimu wako wa kiswahili akufundishe kazi ya sanaa popoma wewe!
Limbwata la WCB kali kweli
 
Wewe ndio unasema juu ya uoga.

Mjifunze kuheshimu maamuzi ya binadamu wengine, sio lazima kila mtu atafute pesa kupitia kiki ya Kiongozi kwa kufata mkumbo wa uongo unaotungwa.

Mnapenda kuamulia watu kama vile, nyie mnaishi kwa kuamuliwa.

Amewapa ukweli na maisha ni yake.

Makonda oyeeeeee
Mbona nawe unataka kumuamulia mawazo yake juu ya wimbo. Kama upo fair, kwanini unaona mawazo yake ni makosa? Unajifanya upo neutral wakati unaonyesha bias waziwazi.
 
Diamond ni mnafiki.,ask me why,nitajibu kwa kifupi

1.kama mama yake amemwambia akae kimya kwanini katunga wimbo??Huo ndio ukimya??

Nyerere ambaye ndiye aliwekwa kwa cover ya Huo wimbo alikuwa hakai kimya,alikuwa anaonya,kukemea na Tena akawaencourage vijana wawe na ujasiri WA kuhoji,,Leo hii diamond anasema tukae kimya.,,ubashite huu.

Pia,ameonesha kukerwa na swala la kudiscuss vyeti vya bashite!!,hivyo hakupenda wimbo WA naytruboy!!!,hivyo alitaka wasanii wote wakae kimya!!!!wasihoji,,huyu kijana anawaangusha watz,,sisi tunahoji alipo Roma,wasanii wenzake wamekusanyika kutia juhudi ili mwenzao apatikane,yeye itakuwa alikuwa anarecord(hakutokea pale)

Kwahiyo tiffa akipotelea pasipofahamika napo atakaa kimya?au ni kwa sababu hayajamkuta yeye,??
Kwani tiffa mtoto wake,? Atakaa kimya tu
 
Walimwambia atunge kuneutralize chemical impacts za sifongo ya ney wa mitego wapo, na ile Tanzagiza
 
Jina la huo wimbo tu Mama kaniambia nikae kimya unabeba ujumbe mzito sana ambayo inaonyesha hofu iliyotanda nchi nzima sasa kufuatia vitisho mbali mbali kwa Watanzania kutoka kwenye utawala huu.

Kumbuka hata kujadili uwepo wa njaa kulitolewa vitisho mtu anaweza kuishia lupango. Yule Butiku alitoa kauli kwamba Rais anayejiona yeye ni Tembo hatufai Watanzania na kinana naye juzi kazungumza katika mistari inayoshabihiana sana na kauli ya Butiku.

Kuna wingu zito nchini ambalo limeondoa furaha na amani ya Watanzania walio wengi nchini.


Duuu....Kinana kaongea ln hayo maneno mkuu....KWELI CCM HAWATABIRIKI
 
Miaka miwili jamaa wamelewa madaraka mwisho wa walio nyuma ya vitendo vya kialifu wajue uongozi unapita wasije jikuta wanafunwa jela maisha
 
Roho hainunuliwi,ukishakwenda umeenda,

mimi nilikuwa nawangaa kina ,Brucelee miaka ile wamekazana,"safari hii hatutakubali mswahili kutawala tena nchi hii"

nikawa nawambia acheni udini nyinyi,kwanza waswahili hawashobokei madaraka kama nyinyi halafu wana hekima ya kutawala kuliko nyie,
nyie bado mnapenda vya duniani na mkipata madaraka mnajiona mmekua miungu,hamjui kuwa kila kitu kina mwisho"


acheni sasa mnyooshwe na mtanyooka tu.
next time vote wisely
 
Nilichokiona hapa, wote waliotolewa povu na huu wimbo ni kile kipengele cha "watu wanaacha kutafuta sent wanabishana tu kuhusu vyeti" ukiangalia hajakosea japo siungi mkono mtu kufoji cheti ila kuna watu wanavidai mpaka unajiuliza wakishaoneshwa kwa mfano watafanyaje unashindwa ku imagn, ila kiukweli Diamond kajitahid kubalance sana kwenye huu wimbo.
Kuwa karbu na mtu ambaye watu wengine hawampendi na wew hajawah kukufanyia chochote cha ubaya ni wakat mgumu sana mpaka ueleweke....
 
Ujue ukiwa Kwenye Peak halaf wakakosekana wapinzani wa kukutoa kifuatacho unajitoa mwenyewe, Hakuna ubishi mpk nje ya mipaka ya nchi jinsi Mkuu alivyokua anasifiwa, wakenya waliokua wanamtaman asaiv wanamchora kweny magazet ya vikatuni, asaiv hata waliompa kura wengi wanajuta, bashite nae alikua na kundi lake kubwa tuu, wote hao Mambo yao wenyewe bila shinikizo yamefanya wamepoteza iman kwa waliokua na iman nao. Diamond siasa zitamponza mwenyewe,
 
Kukaa kimya nalo jibu katika wakati anao stahili kuchunga kauli na kuweka akiba ya maneno ni huu time will tell kila la kher mondi
Achague kubaki na sanaa yake au kuwa mwanasiasa isije jirudia historia ya marlaw Mr pipiiii
 
Back
Top Bottom