Dully mwenyewe hahudhurii misiba ya watuWe kwenye huo msiba ulikwenda? msiba ulipangwa? Dully aligawa kadi? Wewe na Dully huwa mna hudhuria kila msiba? Mbona mna promote msiba kama show? Kwani ni lazima kwenda kwenye msiba? Ange kwenda kila msiba mngekuwa wa kwanza kusema ana kwenda kuuza sura...au anapenda kuonekana kila msiba! Hata Jk alivyo kuwa ana hudhuria misiba kuna baadhi mlianza kumkejeli kuwa anapenda misiba!
Kwanza huyo mfiwa ana watia aibu wale walio kwenda maana anaonesha kuwa wao hawana maana bali kuna watu alikuwa anataka waende!
Nimegundua kwenye hili kuna swala lingine zaidi ya msiba..
"Watanzania wengi ni wachawi sema hawajijui"
kwel kabxa yankweli dangote we ni msanii wa nchi duu yani mshikaji kamind utafikir wasanii wengine hawaja enda bhana dogo kaza una nyota kali
Ndo maana nikasema hivi, iwe hajaenda Diamond au yeyote yule, Dully hakutakiwa kulalamika... kama wa kulalamika, wangelalamika wengine kwa niaba yake! Si busara kumlalamikia mtu kwamba mbona hukuja kunitazama wakati naumwa au kwanini hukuja kwenye msiba wa ndugu yangu... likitokea jambo kama hilo unatakiwa kukausha huku ukifahamu kwamba kumbe niliokuwa nawadhania ni wenzangu; sio wenzangu!Chief ni kwamba mtu anapokua juu tunategemea awe mnyenyekevu kwa watu wengine ili maisha ya kitanzania yasonge. Kwa mfano rafiki yako mfano mbotoki kawa mke wa mfalme na wewe kuna siku unapata shida utategemea huyo bi mfalme ndo awe wa kwanza KUJA au sio
Sijapata kuona nchi ya watu wa hovyo kama Tanzania yetu! Yaani mtu analaumiwa kwa sababu hajaenda msibani! Yaani Diamond kumuita Dully kaka kwa kumuheshimu tu ingawaje sio kaka ake ndo ishakuwa nongwa!!! Kuna wasanii wangapi hawajaenda... WHY ONLY DIAMOND?! Hatutashangaa tukisikia kwamba Dully ndo kamtoa Diamond, upuuzi mtupu!!! Davido kushirikishwa kwenye My Number One, anataka anyenyekewe, Dully nae kuitwa kaka (wa heshima), ndo basi tena keshajiona ana haki kumlalamikia asie ndugu yake kutokwenda msibani... upuuzi mtupu, akili za kukosa kazi hizi!
Ndo maana nikasema hivi, iwe hajaenda Diamond au yeyote yule, Dully hakutakiwa kulalamika... kama wa kulalamika, wangelalamika wengine kwa niaba yake! Si busara kumlalamikia mtu kwamba mbona hukuja kunitazama wakati naumwa au kwanini hukuja kwenye msiba wa ndugu yangu... likitokea jambo kama hilo unatakiwa kukausha huku ukifahamu kwamba kumbe niliokuwa nawadhania ni wenzangu; sio wenzangu!
Binafsi niliwahi kukutwa na misiba miwili... mmoja wa m-sure wangu na mwingine wa sister angu kipenzi! Kwa bahati mbaya, sikuwapo! Nilipofika miezi kadhaa baadae, nikamuomba my best friend, I repeat, MY BEST FRIEND! Huyu bwana nikamuomba anipeleke akanioneshe kaburi la m-sure na sister! Sikuamini hata kidogo aliponiambia hakuhudhuria mazishi ya yeyote kati ya hao kwahiyo alikuwa hajui makaburi yalipo!!!! Hii ni true story, sijawahi kumwambia yeyote na siri hiyo ndo naitoa hapa kwa mara ya kwanza! Na wala mshikaji sikumuuliza na wala sijamuuliza ni kwanini hakuhudhuria... ikabaki siri yangu ingawaje niliumia kishenzi!!!!! Sikumuuliza kwa sababu nilihisi labda aliona misiba ile haikumuhusu...! Panapo msiba ni wako peke yako na sherehe ndiyo ya wote... kwahiyo unatakiwa tu kumsubiria rafiki wa kweli aje na asiyekuja huna sababu ya kuhoji kwanini hakuja... labda aanze kueleza mwenyewe kwanini hakuja!
Ujawah kuckia msanii amepangiwa melody za kuimba itakua ujui chochote kuhusu mziki !!
Mwengine nani ?
Kwani dully amesema kua ameumia diamond kukosa kumzika baba ake ?
Dully kasema wasanii wana roho za ajabu kwa kushindwa kumpa sapoti katika safar ya mwisho ya mzee wake
Ila nyie mashabiki marboro mnayaweza
Hapo umenena.
Na kwa mtazamo wangu wala Diamond hakutakiwa kujieleza.
acheni tuwe masikini
Ifikie time watu wa karibu wa diamond wamshauri maswali ya kujibu na namna ya kuyajibu, unless anawatafutia waswahili cha kuongea, hili ni la muhimu sana kwa afya ya heshima ya kipenzi chetu diamond (kwa Wale tunaompenda na kumtakia mema) mi naamini humu wapo watu wa karibu na Diamond sana Akina Romy, Esma , kifesi na managers wake, kwenye swala kama hili hakutakiwa kutoa maelezo meeeeengi lakini alitakiwa kujibu technically! Cc Ruttashobolwa chige Dinazarde Kim nana