Diamond Platnumz aburuzwa Mahakama ya watoto na Hamisa Mobetto!

Diamond Platnumz aburuzwa Mahakama ya watoto na Hamisa Mobetto!

nimeuliza nikidhani umesoma wito wa mahakama aliyo pelekewa Diamond..
Ulishauri Diamond afute case wakati aliyefungua case ni Hamisa..
Wala usijali Diamond haito mgharimu chochote hii case zaidi ya sheria kufata mkondo tuu na hii case atashinda na hakuna million tano itakayo tolewa...
Diamond hajakataa kumtunza mwanae bali Hamisa ndio amekataa kiasi anachopewa ...
Kiasi anachotaka Hamisa hakijawai kuwepo kabisa hapa tanzania na kwa sheria zetu....
Hamisa ana poteza muda...

Hakuna kiwango cha kumlea mtoto wako ni ukosefu wa akili na ustaarabu kusubiri serikali ikupangie kiwango kwa nyama na damu yako mwenyewe,ugomvi wake na mzazi mwenzie usimtoe kwenye mstari wa kua baba bora kwa kua anamudu kufanya kitu ni heri afanye kwa manufaa ya mwanae hizi saga zitamgharimu akumbuke hata yeye yuko mbali na baba ake kisa tu vurumai kati ya baba na mama ake na baba kutomlea ipasavyo kwa nafasi yake bora amlee mtoto wake kama anavyowalea wengine ikitokea mama akaamua kutumia vibaya anachopewa yeye anakua salama inawezekana hata baba ake Diamond alikua anatiwa ujinga na masela zake kua alete usela ila leo anajutia.
 
mkuu nilimaanisha Dai aombe yaishe nje ya mahakama,

inaelekea ushawahi kuguswa,unatoa child support mahali.......lol

hii imeibua 'dejavu'lol........

usimpoteze mwenzio,ana brand mwenzio ya kuichunga...

Hamisa,ana nothing to loose ila Dai ataingia hasara kwa kupoteza fans ....
Mkuu Fanya kesho kwenda Ustawi Wa jamii magomeni ili ujue kinaga ubaga, Amini ninavyokwambia Hapo hakuna kesi...

Narudia tena Hapo hakuna kesi. Tunza hii comment. Hamisa mashoga na wanasheria wapenda fursa watamlia hela zake bure. Sheria Diamond anahitajika kulipa 70,000tsh kwa mwezi kwa malezi ya Mtoto, na hakuna adhabu ya kushindwa kutimiza hicho kiasi kwa sheria za Tanzania.


Hamisa kukosa Shule na ushauri Wa kina mange umempa jeuri akishindwa kujua hii ni Tanzania na tuna taratibu zetu tofauti kabisa na marekani. Kwa sheria za marekani child support ni issue kubwa ila bongo very minor issue .


Time will tell Hakuna kesi hapo ni kupotezeana muda tu
 
haitoshi mkuu,kukubali ni mtoto wako,na kumtunza ni vitu viwili tofauti......................

ill ilo la mke mdogo, unampoteza,

sipendi kusema hivi ila inanibidi,

huyu alioa na kuchukua majukumu akiwa mdogo,

wanaume wanaoa wakiwa 30's

mtu akikuoa below that jua atacheat tu,

wachache sana huwa tayari kusettle down kwa umri huo,
Una maanisha diamond hamsaidii mwanae??? Umejuaje kama hamsaidii??? Kwa kusikiliza upande mmoja Wa kesi ??? Je, hivyo ndivyo tunapaswa kuamua mashauri ???


Nikwambie tu hiyo Ni ya Ustaw Wa jamii , Itapokelewa na kutupwa mikononi mwa probation officers Wa mahakamani ambao kitaaluma ni social workers kusaidia judgment ya mahakama, huko ndipo kesi itakapokwenda kuishia..
 
Una maanisha diamond hamsaidii mwanae??? Umejuaje kama hamsaidii??? Kwa kusikiliza upande mmoja Wa kesi ??? Je, hivyo ndivyo tunapaswa kuamua mashauri ???


Nikwambie tu hiyo Ni ya Ustaw Wa jamii , Itapokelewa na kutupwa mikononi mwa probation officers Wa mahakamani ambao kitaaluma ni social workers kusaidia judgment ya mahakama, huko ndipo kesi itakapokwenda kuishia..

ngoja tuone litakavyokwenda,

Mashilawadu TV,kama nawaona watakavyokua busy,lol

mimi sijaamua lolote kuhusu hii kesi,

and certain I'm not a lawyer,

kama ishu ni kumtunza mtoto na yeye DAI anafanya hivyo,

sasa hii kesi,inatoka wapi??

natumaini huu ni mwanzo wa kuiangalia hio sheria,

labda ilitungwa zamani,(sijui),

ila kutoa laki mbili kwa mwezi ni ndogo,lol

badala ya kuweka kiwango fixed cha kutoa,

waweke pesa kutokana nas mzazi anacho earn,

PATAMU HAPOOOOOOOO ,

Mabazazi wote watatumia akili kabla ya kua undress.
 
Hamisa na kusoma kote sheria LLB-UDSM kashindwa kung'amua hill?
Mimi ningekuwa kaka Wa Hamisa Mobeto kwa kujua Kinagaubaga sheria ya ndoa na Mtoto ya Tanzania. Narudia tena SHERIA YA MTOTO NA NDOA YA TANZANIA Ningemshauri ajilie hela ya Domo taratibu bila ajizi,


Ambacho kimemponza huyu Dogo ni ulimbukeni Wa kutaka kupindua ndoa ya Zari Na Diamond (Najua wengi mnajiuliza Lini wamefunga Ndoa Hawa watu hahahaha kasomeni sheria ya ndoa Ya Tanzania , maana ya Dhana Ya Ndoa ). Diamond Akiachana na zari Leo shauri lake na mgawanyo Wa mali utakuwa tofauti kama akiachana na Hamisa Mobeto. Hapo nazungumzia Dhana ya Ndoa sheria yetu ya ndoa kama ilivyobainisha.
 
Just thinking in a DON CORLEON ways...

domo akatae mtoto sio wake na atake DNA ifanyike...then mafiosso wafanye kazi results zipikwe majibu yatoke na msala umrudie muuza bucha.

Kishujaa tuanze ziara ya sauzi kwa magoti na wazee wa busara watangulie kampala na posa yetu maraaaa paaaaap....ndoa hiyoo mara paaaap...wameuza madale wameamia masaki...maraaa paaap show za tz tunafuta...maraaaa eyoòoòoo laizaaaaaa amehamia sauzi mara paaap...wasaaafiiii records ipo sauzi maraaa paaappp....

hii post nimeandika nikiwa usingizini musiichukulie serious.
 
Rebecca sijui utaratibu wa kurekebisha sheria nani anahusika lakin kama ni Mjengoni (sheria haitobadilishwa kulingana na idadi kubwa ya wabunge kuwa wanaume bila kujali chama kumbuka Mwenyekiti wa Kambi Rasmi nae ana mtoto nje ya ndoa toka humo humo mjengoni. Patamu hapo.
 
Hamisa anazitafuta milioni tano kwa mwezi. Ila haya mambo ya kulazimisha vitu mwisho wake huwa si mnzuri hata kidogo. Pamoja na kwamba matunzo ni haki ya mtoto ila nachokiona Hamisa anazidi kujidhalilisha tu.

..................................................................
Katika pitapita mitandaoni nimekutana na haya::

SHERIA HAILAZIMISHI KUTOA MATUNZO YA MTOTO KULIKO UWEZO WAKO.

Na Bashir Yakub.

Suala la matunzo ya watoto/mtoto lim ekuwa ni suala ambalo wasomaji wengi wamekuwa wakiniuliza sana. Wengi wao wanaouliza ni wale ambao wamezaa nje ya ndoa na hivyo kuna utata wa matunzo ya watoto na wale ambao wamekuwa wana ndoa lakini sasa tayari wametengana aidha kwa talaka au bila talaka. Niseme tu kwa ufupi kuwa suala la matunzo ya watoto linajumuisha mambo mengi nami nitaeleza baadhi tu. 1.

HUWEZI KUMLAZIMISHA MTOA MATUNZO KUTOA AMBACHO HANA. Kumekuwepo na tabia ya wazazi hasa upande wa wazazi wa kike kuwalazimisha wanaume ambao wamezaa nao na kutengana nao kutoa matunzo ya watoto kwa kiwango cha juu kabisa ambacho pengine kinazidi hata kipato cha mtoaji.

Hili si sawa. Ni kweli sheria inamlazimisha mwanaume kutoa matunzo ya mtoto lakini haimlazimishi kutoa kuliko anachopata. Sheria haiseme kwakuwa mwanamke anaishi na mtoto wa mtu basi mwanaume ndio sasa afanywe kitega uchumi.

Inafikia hatua mwanamke hafanyi kazi yoyote isipokuwa anategemea ile pesa ya matunzo ya mtoto ndio iwe kila kitu katika maisha yake. Hii ndio sababu hata akipewa kiasi kinachotosha haoni kama kinatosha kwakuwa kinakuwa na njia nyingi kama saluni, nguo za kuvaa, pesa ya upatu, michango ya harusi na kitchen party na kila kitu kinachohusu maisha yake binafsi.

Ieleweke wazi kuwa kwa mujibu wa sheria pesa ya matunzo ya mtoto haihusiki na haya. Pesa ya matunzo ya mtoto ni pesa ya matunzo ya mtoto kama neno lenyewe lilivyo na linavyojieleza si vinginevyo.

2.INARUHUSIWA KUKATAA IKIWA UNALAZIMISHWA KUTOA MATUNZO YANAYOZIDI UWEZO WAKO. Ikiwa mwanaume analazimishwa kutoa kuliko kipato chake basi anaruhusiwa kukataa hata kama amri hiyo imetolewa na mahakama. Wengine huandikishana polisi lakini bado haibadili maana kwakuwa mtu anatakiwa kutoa kulingana na uwezo wake au kipato chake. Wapo wazazi hasa wa kike ambao huwalazimisha wanaume kutoa matunzo ya kuwasomesha watoto international schools wakati kipato cha mwanume ni shule ya kata.

Sheria inachokataza ni kukataa kabisa kutoa matunzo ya mtoto lakini haimlazimishi mtu kutoa kilichomzidi. Au wengine hulazimisha kuwekewa mpaka wafanykazi wa ndani( house girl) wakati kipato cha mwanaume hakiruhusu jambo hilo. Huu nao ni unayanyasaji kwa upande wa wanaume na haukubaliwi na sheria.

La msingi ni kuwa iwapo utalazimishwa kutoa kuliko uwezo wako we kataa. Na kama uamuzi huo umetolewa na mahakama basi kataa kwa kukata rufaa kupinga kabisa jambo hilo. Sheria inaposema matunzo ya watoto haisemi kuwa watu watoe kuliko uwezo wao hapana. Sheria ni haki na haki huzingatia ukweli na hali halisi ya jambo.

3. UMRI WA WATOTO KUISHI NA MAMA AU BABA. Mara nyingi sheria imeelekeza watoto walio chini ya umri wa miaka kumi yaani kuanzia miaka tisa kushuka chini kuishi na mama. Aidha kuanzia miaka kumi kwenda mbele mtoto anaweza kuchagua aishi na nani kati ya baba au mama.

Kwahiyo iwapo mtoto amefikisha umri wa miaka kumi au zaidi basi baba anaweza kumchukua mtoto wake iwapo pia mtoto atapenda kukaa na baba yake. Wapo wazazi ambao wamekuwa wakiwagangania watoto hata baada ya watoto kuvuka umri huo ili waendelee kuwafanya vitega uchumi kupitia kudai matunzo. Hili si sawa hasa iwapo mtoto yuko tayari kukaa na baba yake.

4. BABA ANAWEZA KUOMBA KUKAA NA WATOTO HATA KAMA NI WADOGO SANA. Hapo juu tumeona kuwa ni lazima mtoto kukaa na mama iwapo ana umri chini ya miaka kumi. Msimamo huu unaweza kubadilika iwapo baba atatoa sababu za msingi za kuomba mama asikae na watoto. Hii haijalishi watoto wana umri gani iwapo tu ana sababu za msingi basi ataomba kukaa na watoto/mtoto wake. Sababu kubwa za kuomba watoto ni iwapo mama ana ugonjwa wa akili na hivyo kuwa hatari kwa ustawi wa mtoto/watoto.

Pia iwapo mama anakaa na watoto katika mazingira hatarishi kama danguro, baa, sehemu za madisco, au mama anajihusisha na vitendo vya ukahaba ambavyo si vyema kabisa kwa makuzi ya mtoto. Hii inajumuisha matendo yote maovu ambayo kukaa na watoto/mtoto yanaweza kuleta athari mbaya kwake na ni hapo baba atakapoomba kuchukua mtoto/watoto na atakubaliwa bila kujali umri wa watoto.

5. HAKI YA KWENDA KUWAONA WATOTO. Wapo watu ambao huzuiwa kuwaona watoto. Wengine huruhusiwa lakini kwa masharti maalum na kwa kupewa muda wa kuzungumza. Hii haikubaliki kisheria mzazi anapaswa kuwaona watoto kwa uhuru na bila masharti yanayolenga kumwondolea haki hiyo.

0784482959, 0714047241 bashiryakub@ymail.com. | sheriayakub.blogspot.com


Asante kwa ufafanuzi mkuu.
 
Rebecca sijui utaratibu wa kurekebisha sheria nani anahusika lakin ni Mjengoni (sheria haitobadilishwa kulingana na idadi kubwa ya wabunge kuwa wanaume bila kujali chama kumbuka Mwenyekiti wa Kambi Rasmi nae ana mtoto nje ya ndoa toka humo humo mjengoni. Patamu hapo.

poa mkuu,

usiku mwema,
 
Daimond futa hii kesi,itakucost kimataifa,watu hawataki kuskiaga umewaneglect watoto wako..............................ifute mapema kabla haijaenea duniani.....................

Huyo anatamba na kutukana watu Instagram.. hajui kuwa hata hiyo dili ya vinywaji alivyofanyia party siku tatu mfululizo atazisikia kwa wengine na mengineyo mengi watamtema pwaaaaa..

Managers wake wanaonyesha wao pesa mbele na sio mengine kama kumshauri ajilinde na...
 
KWENYE SHITAKA LAKUZALILISHWA HAMISA HAWEZI SHINDA maana yeye ndio alianza mzalilisha daimond kwa hapo daimond anaweza kujitetea kwamba ni Jazba maana Hamisa alianza kusambaza ZILE picha ili kumzalilisha Hamisa nazan adil na matunzo ya mtoto tu.. ambayo atapewa eluf 70 ya serikali.. na sio laki mbili.. maana kwa tz sisi bado hatujafikia hatua za marekani kwamba child support inatokana na income ya mzazi
 
KWENYE SHITAKA LAKUZALILISHWA HAMISA HAWEZI SHINDA maana yeye ndio alianza mzalilisha daimond kwa hapo daimond anaweza kujitetea kwamba ni Jazba maana Hamisa alianza kusambaza ZILE picha ili kumzalilisha Hamisa nazan adil na matunzo ya mtoto tu.. ambayo atapewa eluf 70 ya serikali.. na sio laki mbili.. maana kwa tz sisi bado hatujafikia hatua za marekani kwamba child support inatokana na income ya mzazi
Mhh!
 
Back
Top Bottom