Diamond Platnumz adaiwa kodi Sh. Milioni 400 na TRA

Dah!nimechekaaaa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Basi akili lazima ikucheze kama msanii, we unaona bongo movie kuwa upande wa ccm hasa Makonda kumewasaidia au ndo wamejiongezea matusi kwa mashabiki na kuwapoteza zaidi....
Matusi mkuu hayana impact yoyote hususani kutoka kwenye virtual world.

- Hebu jiulize ni mara ngapi watu wamekuwa wakimporomoshea matusi Diamond au Mrisho Mpoto kwa kuunga mkono serikali au kufanya kampeni za CCM ?


- Je, umewahi kuona watu hao hao wakimtukana ALIKIBA au FID Q kwa kufanya mambo hayo hayo ?


In short ni kwamba watukanaji huwa wana chuki tu na mtu fulani wala hata siyo hayo mambo wanayojaribu kutuaminisha na ndio maana SUALA hilo hilo likifanywa na FULANI ni poa ila akifanya mwingine MATUSI Mpango mzima
 
Unavyokomenti shilikisha na ubongo basi, ukishajiona mfanyakazi ndio unajiona wa kujitolea mfano tu. Nimekwambia mfanya kazi anajulikana analipwa tsh ngapi, asilimia kadhaa itaenda bodi na asilimia kadhaa ni paye. Kama haujaweka mfumo wa kuregulate kazi za wasanii unajuaje msanii kaingiza nini na 18% ni kiasi gani? Au tutaishia kukomaa na diamond, wakina manfongo hawatuhusu? Sasa wewe ukisikia mazingira mazuri akili yako sijui inaenda wapi! Sasa kama mwalimu mazingira yake mabaya ndio iwe halali kwa kada nyingine kuwa mabaya? Kwa taarifa yako dunia nzima kada zinazotumia vipaji na michezo ndio kada zinazoongoza kwa kuingiza pesa, ukiona upo kwenye jamii ya bank teller anaishi vizuri kuliko msanii lazima ujiulize tunakosea wapi.
 
Vidacom=Vodacom kwa hisani ya Faiza Foxy
 
Ndio tatizo letu, mbaya zaidi msanii analipwa kwenye hizo campaign. Kuna jamaa yangu alikuwa anaponda wasanii wanaofanya kampeni chama tawala, wakati yeye printing company yake aliprint tshirt na banners za mbunge wa CCM. Ukimwuliza anasema anapiga hela tu kura hawapi. Utafikili yeye peke yake ndio anashida na hela
 
Huwa zinakuwa ni roho mbaya tu na wivu hususani kama wao hawajapewa lakini wakipewa wao na watu hao hao wanachukua halafu wanatoa vijisababu visivyokuwa na mpango. La msingi ni kufanya unachoona kina manufaa kwako - usisikilize watu
 
Kwani ye nano asilipe kodi hakuna namna anadai Mazingira mazuri kuna mtumishi gani wa serikali anamazingira mazuri? Lakini tunakatwa kodi
 
Kuhusu diamond kudaiwa na TRA.
View attachment 507134

Post aliyopost diamond leo.


maoni yangu;
Serikali kama inahitaji pesa za wasanii ainabudi kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanyia kazi, diamond kaongea ukweli sema anaongea kwa uoga sana.
Ndio maana wachezaji wengi karibu wote ulaya na wasanii wana mameneja ni kuajili pia ya kuangalia masuala yao ya kodi. Kwanini mwalimu anayelipwa TZS 300,000 kwa mwezi alipe kodi halafu mtu anayepata pato TZS 10,000,000 kwa masaa chini ya sita asilipe kodi?!!!!!!!!!!

Kila mwenye kipato na afikiwe na mamlaka ya mapato alipe kodi stahiki
 
iyo ndo shida ya showoff account zake watakuwa wanazijua , bashite amtete
 

Ni ngumu sana kwa msanii kukimbizana na kila anaitumia kazi zake ili apate . Nchi nyingine zina collective management organizations (CMOs) zenye nguvu ambazo zinasimamia mapato ya wanachama wake. Kwa hapa nyumbani sijui uimara wa COSOTA ila naamini wanajitahidi japokuwa sidhani kama wanamuziki "wakubwa" ni wanachama. Serikali wanaweza kujua sehemu kubwa ya mapato ya wanamuziki kupitia hizi collective management societies, na pia wanamuziki wanaweza pata mapato mengi kupitia hizi hizi CMOs
 
Umeongea point tupu, huu uzi ungepata comments kama zako ungesaidia sana jamii, tatizo wengi wame comment kishabiki sana.

Watu wasichokijua ni kwamba kukiwa na mazingira ambayo yanaeuhusu kazi za wasanii kuibiwa basi na serikali inakosa pesa pia.
 
Mimi concern yangu sio wasanii wala mengineyo uliyoongelea.. Hayo mengine watajua serikali pamoja na hao wasanii wenyewe. Siwezi kuisemea serikali chochote maana ni kikundi cha watu kilichoapa kutosikiliza mawazo ya watu..

Nimemshauri Diamond; moja aajiri kijana msomi ashughulikie masuala yake yote ya kifedha, kama mpaka sasa hana mwanasheria binafsi basi atafute.. Masuala ya kodi na sheria ni vitu muhimu sana hasa kwa mfanyabiashara na mwanamuziki mkubwa kama Diamond.. Cha pili, asilie lie na hiyo kodi. Maana anaona eti serikali haijafanya lolote kumsaidia na ni struggles zake pekee ndizo zimemfikisha hapo. Yaweza kuwa ni kweli, lakini hata wajasiriamali wanapitia hayo hayo aliyopitia yeye.. Tena wao wana karaha zaidi ya alizopitia yeye..
 
Akwendeee! Hajui kua serikali haina rafiki eenhe!!!
Wakimgeukia nayeye ataishia kuhamia kwa Zari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…