Diaspora tukutane hapa: Tupeane ushauri wa kuanza maisha mapya Tanzania

Diaspora tukutane hapa: Tupeane ushauri wa kuanza maisha mapya Tanzania


Hebu angalia tarehe za hizo habari na majina ya hayo magazeti. Ni matabloid ya udaku. Yanaweza kuandika chochote. Tunayaona kwenye maduka yamepangwa kwa keshia. Unasoma halafu unayaacha hapo hapo. Tunajua ni ya upuzi. Sikuzungumzia magazeti hayo. Bahati mbaya Tanzania tuna baadhi ya magazeti ya hivyo ambayo habari zake zinajadiliwa mpaka bungeni.
 
Hebu mfananishe Myweather kwa hela zake zitokanazo na kuoteshwa manundu na Bill gates nani mwenye ulimbukeni wa kijinga kati hao wawili.BLACKS TUNA MATATIZO UKATAE USIKATAE NDO HIVYO.

Wewe endelea tu mkuu, tunapiga ngoma tofauti!

Ila kumbuka ni watu weusi hao unaosema wana laana ndio waliotumia akili zao na kuweza kusimamia hili jukwaa la mtandao ambalo unalitumia kutoa hoja zako.
 
Wewe endelea tu mkuu, tunapiga ngoma tofauti!

Ila kumbuka ni watu weusi hao unaosema wana laana ndio waliotumia akili zao na kuweza kusimamia hili jukwaa la mtandao ambalo unalitumia kutoa hoja zako.
Ni kweli ila haiondoshi ukweli.Mmoja katika 10000 ni sawa hamna kitu
 
Mayweather mfananishe na wacheza mieleka wa kizungu. Bill Gates mfananishe na kina Oprah. Wale wacheza mieleka wengi wamefungwa jela kwa kila aina ya balaa. Kuna aliyekojolea washabiki uwanjani. Kuna alielipa kodi kwa dola feki. Kuna aliyechezesha kamari nyumbani kwake. Kuna aliyepiga mwanamke. Kuna aliyeiba dukani. Kuna aliyekamatwa na unga. Kuna aliyebaka. Chagua mwenyewe balaa ipi ambayo hawana wazungu wa vile.
 
Inasemekana watu walioishi nje ya nchi haswa ulaya na america akili hutanuka tofauti na yule aliyeishi hapa nchini muda wote.

Ni wakati wa kutumia fursa ulizozipata uko na kuja kuziwekeza huku hautatoka patupu.
Kama ulienda ughaibuni kushangaa mataa ndo utasota ukirudi bongo.
 
Princemwalejr na Nyagabu swala ni ninyi kutoa mwanga kwa vijana wapate hizo fursa mnazopata ingekua vizuri kama watu wa western Africa has a Wanigeria wa kabila moja na Wasenegali wanavyosaidiana wapeni njia vijana wa kibongo nao waweze kupiga hizo 150,000 USD...na nyuzi hizi mngekua mnazungumzia sana hayo maana wakitoka wengi pia maendeleo Bongo yataongezeka kama Uganda walivyo maendeleo yanafanywa na wengi wanaoishi nje hata Zimbabwe pia na isiwe sehemu ya kubishana hii hela Ndogo au kubwa au Mimi nilishawahi ishi huko aisadii kitu..ni kutoa mwanga kwa vijana ili muwe wengi mnaosaidia maendeleo ya Tanzania kupitia fedha zinazopatikana nje ya Nchi...
 
Princemwalejr na Nyagabu swala ni ninyi kutoa mwanga kwa vijana wapate hizo fursa mnazopata ingekua vizuri kama watu wa western Africa has a Wanigeria wa kabila moja na Wasenegali wanavyosaidiana wapeni njia vijana wa kibongo nao waweze kupiga hizo 150,000 USD...na nyuzi hizi mngekua mnazungumzia sana hayo maana wakitoka wengi pia maendeleo Bongo yataongezeka kama Uganda walivyo maendeleo yanafanywa na wengi wanaoishi nje hata Zimbabwe pia na isiwe sehemu ya kubishana hii hela Ndogo au kubwa au Mimi nilishawahi ishi huko aisadii kitu..ni kutoa mwanga kwa vijana ili muwe wengi mnaosaidia maendeleo ya Tanzania kupitia fedha zinazopatikana nje ya Nchi...

Mbona nimeshaeleza zinavyopatikana kiurahisi ukiacha kujali hali na ukajishughulisha.

Namjua jamaa mmoja wa Sierra Leone ana kibachela (shahada) chake hata sijui cha nini. Ana kazi mbili za kulea machizi. Moja ya ofisini kuandika ujinga ujinga tu. Chizi ni chizi hatabadilika. Hapa anakunja dola elfu 57 kwa mwaka.

Kazi yake ya pili ni ya kuwatembeza hao machizi jioni na wikiendi mitaani. Baadae anaenda nyumbani kwao kuwapa dawa zao. Hiyo anachukua 52 elfu. Mpaka hapo ana laki na elfu tisa.

Akifanya ovataimu, akilipwa kwa kufanya kazi siku za sikukuu anaongeza kama elfu kumi nyingine kwa mwaka. Tayari ana laki na kumi na tisa.

Hiyo haimzuii kununua gari akampa mtu amuendeshee Uber akaingiza kitu kama elfu kwa mwezi. Elfu 12 kwa mwaka hizo. Tayari ana laki na thelathini na moja.

Anaweza akapangisha sehemu ya nyumba yake anayoishi akachukua kitu kama elfu kumi nyingine. Laki na arubaini na moja hiyo.

Akiwa na mke anayeingiza elfu 50 kwa mwaka wana laki na tisini elfu.

Vitu ni vingi vya kufanya ukiamua kuchachalika. Tofauti na Bongo ni kuwa dili za Marekani hazina ubabaishaji zimenyooka.

Ni juu yako kufanya “pimp decision” uwe meneja au mkurugenzi mahali majukumu kibao na visafari vya hovyo. Roho mkononi hujui lini utafukuzwa kazi. Yote hayo kwa elfu 87 kwa mwaka. Au utumie muda wako kuchanganya kazi na figisu nyingine upige laki na nusu au zaidi kwa mwaka.

Mimi kazi nafanya ili nisivuruge bima na pension. Lakini nimegundua kwenye biashara ndio kwenye pesa iliyotakata. Kumbe hata bwege mie naweza kufungua kampuni Marekani.
 
Ila ujue ukiingia viwanjani namna hiyo huwezi kuhudhuria sherehe za wabongo kila jumamosi.
 
Kuna mwingine wa Sierra Leone anafanya kazi ya ofisi anachukua elfu sitini. Ila jumamosi anaenda mnadani kununua magari halafu anayauza yeye na mkewe.
Biashara ya magari inawatoa sana jamaa wa west Africa. Ushuru wao sio wa kukomoana kama wa Bongo.
 
OK Mkuu nimekuelewa vizuri nachozungumzia ni jinsi ya vijana kuja huko wao kazi yeyote watafanya kulingana na mazingira ili wapate kipato maisha yaende na kutoa mbinu zilizonyooka kwa wao kuweza kufika huko...
 
OK Mkuu nimekuelewa vizuri nachozungumzia ni jinsi ya vijana kuja huko wao kazi yeyote watafanya kulingana na mazingira ili wapate kipato maisha yaende na kutoa mbinu zilizonyooka kwa wao kuweza kufika huko...

Ni kuoa/kuolewa na mmarekani. Hapo hata Trump na vijana wake hawakugusi. Siku hizi mambo rahisi mitandao kibao mpaka ya kutafuta wachumba. Ukipata mchumba akikuelewa tena unaweza kupata bahati akakubeba hata ukifika Marekani. Kuna rafiki yangu kafanya hiyo kitu.

Vilevile kwa wabongo walio na uraia waalike familia zao na kuoa nyumbani.

Waethiopia wanafanya sana hiyo kitu. Ukipanda ndege yao kutoka Washington mpaka Addis ni wao tu kwa jinsi walivyo wengi.

Halafu kwa Marekani wana umoja na ushirikiano. Wanapeana madili. Kwa mfano biashara ya parking za magari wamejaa wao sijui wana mpango nayo gani.
 
Kisheria maana yake nipambane na serikali kama Acacia. Ninue ardhi, niipe hisa serikali halafu nikivuna mahindi nigawane na serikali nusu kwa nusu. Debe kwa debe. Nikizingua mahindi yatakamatwa kama mchanga wa makanikia[emoji23][emoji23][emoji23]

Kuna ushauri ulitolewa hapa eti sisi wa Marekani tunasema sana mbona wa Uingereza wanafungua akaunt. Yaani niweke dola zangu kwenye akaunti kwa kutumia barua feki ya mwenyekiti wa mtaa? Hela niliyoitolea jasho kihalali nije kuiweka mwewe kinyamanyama hicho namna hiyo?

Kwanza sijui wabongo wanajuaje wakikuona tu wanajua umetoka nje. Kuna siku niko Kariakoo muuza duka akaniambia wewe hutanunua nguo hapa hiyo fulana yako umenunua nje hapa hupati hiyo.
Daah we jamaa wewe. Mahindi unagawanaje na serikali!! Tena debe kwa debe!! Nashangaa kwa sababu ndio biashara yangu, sawa bwana unaamua kujitetea kwa namna yoyote hata uongo.
Unasema kufungua account kwa kutumia barua feki ya mwenyekiti wa mtaa, ufeki unakujaje kama imesainiwa na mwenyekiti na kugongwa muhuri wa mwenyekiti??
Usitake kundanganya kuwa ulikataliwa kufungua account kwa sababu wewe ni diaspora. Mi mwenyewe nna account ambayo huwa napokelea hela kutoka nje.
We jamaa kwanza njoo tuyajenge, by 2020 tuwe na kiwanda chetu hapa, jana nimekutana na gari linatoka S.A limebeba tyres zilizofanyiwa retreading
 
Kupanga ni kuchagua, naamini ukiishi hapa bongoland ukajituma japo utakumbana na changamoto za hapa na pale lakini utaishi angalau maisha mazuri, pia hata huko nje naamini maisha hawagawi bure bure lazima upambane hata kama huduma za kijamii ni nzuri bila kujituma naamini bado unaweza kuishia pabaya tu.
 
Daah we jamaa wewe. Mahindi unagawanaje na serikali!! Tena debe kwa debe!! Nashangaa kwa sababu ndio biashara yangu, sawa bwana unaamua kujitetea kwa namna yoyote hata uongo.
Unasema kufungua account kwa kutumia barua feki ya mwenyekiti wa mtaa, ufeki unakujaje kama imesainiwa na mwenyekiti na kugongwa muhuri wa mwenyekiti??
Usitake kundanganya kuwa ulikataliwa kufungua account kwa sababu wewe ni diaspora. Mi mwenyewe nna account ambayo huwa napokelea hela kutoka nje.
We jamaa kwanza njoo tuyajenge, by 2020 tuwe na kiwanda chetu hapa, jana nimekutana na gari linatoka S.A limebeba tyres zilizofanyiwa retreading

Kwanza uelewe maana ya diaspora. Watu wanaoishi nje ya nchi yao kama walivyoishi wayahudi nje ya nchi yao miaka kadhaa.

Wewe kama ni mtanzania uko nje. Wewe ni tofauti na Mmarekani mwenye asili ya Tanzania ambaye ndio mimi.
Kitambulisho cha Tanzania sina wala paspoti ya Tanzania sijui ina rangi gani siku hizi.

Lakini paspoti yangu ya Marekani imeandikwa nimezaliwa Tanzania. Ila kwa sheria za Tanzania walikataa nisitumie paspoti hiyo kama kitambulisho.

Ndio inabidi uende kwa mwenyekiti wa mtaa akuandikie barua kuwa wewe ni mkazi wa mtaa wake ukafungulie akaunti. Sasa akaunti ya hivyo nitaiamini kuweka pesa ya maana?
 
Kwa Marekani utaratibu unafanana. Benki ina hiari kukubali au kukataa kumfungulia akaunti mgeni. Ila wakikubali huyo mgeni itabidi awe na anuani ya Marekani.
Inawezekana wale watu wa benki wa Tanzania wako sawa. Ila hawakunipa maelezo ya kueleweka. Nitawarudia tena ikibidi kikao na bosi wao.
 
Back
Top Bottom