Dimba la Taifa: Yanga Africans yatakata kwa ushindi wa goli 3-0 dhidi ya Kagera Sugar

Dimba la Taifa: Yanga Africans yatakata kwa ushindi wa goli 3-0 dhidi ya Kagera Sugar

View attachment 709076

01': Mechi ya Yanga vs Kagera Sugar imeanza hivi punde

04': Haji Mwinyi anarusha mpira kuelekea lango la Kagera baada ya kutolewa, anauchukua Ajib, Ajib anapasia langoni mwa wapinzani, wanaokoa

05': Kagera sasa, anao Atupele Green, pasia pembeni mwa Uwanja, hatariii, Kagera wanakosa nafasi ya wazi

07': Rostand anaanzisha goli kiki, ni baada ya mpira kutoka nje

08: Buswiiiita, namna gani hapa, krosi yake inakwenda nje, ilikuwa ni pasi nzuri ya auta kutoka kwa Ajib

12': Matokeo ni 0-0 mpaka sasa

13': Hatari katika lango la Kagera hapa, Buswiita, anababatizana na mlinda mlango, anaudaka

14': Mpira umesimama baada ya kipa wa Kagera kuumia, Cannavaro naye anapasha nje

15': tayari mpira umeshaanza, kwake Kamusoko, anapiga shuti lakini linatoka nje

16': Offside, Kagare wanaotea, mpira unapigwa kuelekea kwao

18': Kibaya anapata kadi ya njano, ni ya kwanza kwenye mchezo wa leo

19': Faulo, kadi ya pili ya njano inaenda kwa mchezaji wa Kagera, ni baada ya kucheza faulo eneo la hatari, inapigwa langoni mwao

20': Ajib yuko na mpira, anapigaaa, inapiga nyavu za juu

21': Ngonyani naye anapata kadi ya njano baada ya kucheza mazambi, ni ya tatu sasa katika mchezo huu

21': Matokeo ni 0-0

22': Mpira umesimama, Maxime anatoa maelekezo kwa wachezaji wake

23': Fhaki anapiga hapa, hatari langoni mwa Yanga, namna gani mshambuliaji huyu anashindwa kutumia nafasi

25': Kavila anamchezea rafu Chirwa hapa, inakuwa faulo kwenda Kagera

25': Ally Nasoro sasa anaondoka nao kupandisha mashambulizi, anapiga pasi mkaa, anaokoa Yondani

26': Wanaanza Yanga eneo la nyuma, Kessy anampasia Buswita, kwake Kamusoko, Kamusoko anapiga kwake Pato lakini beki wa Kagera anautoa na mpira unakuwa wa kona

28': Mpira anao Kamusoko, anapasia nyuma kwake Yondani, Yanga wanajaribu kutafuta bao hapa

29': Emmanuel Martin, anacheza faulo, mpira unapigwa kuelekea Yanga

30': matokeo ni 0-0, mpaka sasa hakuna timu iliyofanya shambulizi la kutisha kwa mwenzake

31': Goli Kiki upande wa Yanga, unapigwa kuelekea Kagera

32': Kagera waanzisha goli kiki, tayari ushapigwa, faulo, unapigwa kuelekea Kagera

33': Mabadiliko Yanga wanafanya mapema, anatoka Pato na nafasi yake inachukuliwa na Maka

35'; Kagera wanapata kona ya kwanza baada ya Mwinyi Haji kuutoa mpira, inapigwaaa, inapigwa kichwa na mshambuliaji wa Kagera lakini kipa Rostand anadaka

37': Unarushwa sasa kuelekea lango la Kagera, anao Ajib sasa, kwake Martin, unapigwa kwake Buswita, anautuliza kwa njia ya kifua lakini beki wa Kagera anaokoa

39': Anao sasa Ajib, unapigwa langoni, kipa anajitutumua anaupiga na mkono unakuwa wa kurushwa kuelekea langoni kwake, kidogo iwe kona

41': Faulo, Ajib anapiga, anapiga ya chinichini lakini mabeki wanaokoa kwa kichwa

41': Mpira uko mbele sasa upande wa kulia mwa uwanja wanao Yanga, beki wa Kagera anauokoa hapa, unapigwa mbele lakini Maka anautoa nje

Mpira ni mapumziko sasa, Yanga 0-0 Kagera Sugar

45': Kipindi cha pili kimeanza, matokeo ni 0-0

46': Beki wa Kagera anachezewa faulo, mpira unapigwa kuelekea langoni mwa Yanga

47': Hatarii langoni mwa Yanga, Atupele Green anakosa kupiga shuti nje kidogo mwa eneo la hatari, ni faulo,

48': Inapigwaaa, inatoka nje sentimita kadhaa tu, bahati nyingine wanaikosa Kagera Sugar,

50': Yanga wanaanza nyuma taraatibu, beki wa Kagera anautoa nje

51': Penatiiii, Yanga wanapata tuta hapa

51': Ajib ndiyo anapiga tuta, anapigaaa, gooooooli, Yanga wanapata bao la kwanza, sasa ni 1-0

53': Kagera wanaanza upya kati, wanapasiana kuelekea langoni mwa Yanga, inapigwa moja juu, kipa Rostand anaruka kama nyani anaudaka

Dak ya 55, Kagera wamezidi kuamka licha ya kufungwa bao hilo moja, wanamiliki zaidi mpira eneo la kati

Dak ya 57, Ajib sasa na mpira, piga huku pembeni lakini Kagera wanaokoa, inapigwa mbele hukuu, offside

Dak ya 59, Namna gani Kagera wanakosa tena bao hapa, ni nafasi adhimu kabisa hii ndani ya eneo la hatari mwa Yanga, mpira unakwenda nje

Dak ya 61, Kagera wanaanza mashambulizi tena, wanapasiana eneo la nyuma

Dak ya 63, Faulo inapigwa kuelekea Kagera baada ya beki wake kucheza mazambi

Dak ya 64, Yanga wanao mpira hivi sasa, Ajib anajaribu kuzunguka lakini ananyang'anywa mpira, Kamusoko anauwahi

Dak ya 65, Mpira anao Fhaki sasa, pasia kati ya uwanja huku, unarejeshwa kwake Fakhi tena, Kagera bado wanaumiliki, pigwa huku langoni mwa Yanga, offside

Dak ya 68, Kagera wanashindwa kutumia vema nafasi ya kufunga baada ya kupasiana vizuri na kuingia eneo la hatari la Yanga

Dak ya 69, Kona wanapata Yanga, ni ya nne na tano katika mchezo wa leo, Ajib anapiga lakini inaokolewa

Dak ya 70, Chirwaa, anapiga krosi moja ya hewani lakini inatoka nje

Dak ya 71, Mpira umesimaa kidogo, mchezaji wa Kagera ameumia

Dak ya 72, Omary Daga anaingia kuchuka nafasi ya Atupele Green, matokeo bado ni 1-0

Dak ya 75, Yanga wanapata kona, inapigwa na Ajib, pigwa huku Chirwa anapiga kichwa lakini inaenda pembeni, Kagera wanaokoa

Dak ya 75, Emmanuel Martiiiin, anapigaaaa, kipa wa Kagera anakuwa mahiri anaokoa

Dak ya 76, Goooooooli, Martin anaifungia Yanga bao la pili kufuatia krosi nzuri ya Obrey Chirwa, Yanga wana mabao mawili sasa na Kagera 0

Dak ya 79, Yanga wameamka sasa, wanakwenda mbele na mpira, kona! Ajib yu tayari kupiga, anaanza fupi hukuuu, kona nyingine, ni ya 7 sasa, inapigwaaaa, Kagera wanaokoa

Dak ya 81, Kagera wanapata kona pia, inapigwaaa lakini inaokolewa

Dak ya 82, Kagera wanaumiliki mpira tena, wanajaribu kutafuta bao angalau la kufutia machozi

Dak ya 83, Hatari langoni mwa Kagera, kipa anadaka, anaanza taratibu na wenzake nyuma

Dak ya 85, Kagera wanapata kona hapa, inapigwa lakini inatolewa na kuwa kona ya pili, inapigwa tena hukuu, Rostand anadaka na kutulia vizuuri kabisa

Dak ya 87, Yanga wanao sasa, Buswita, kwake Kessy, anarudisha kwa kipa wake

Dak ya 88, Yusuph Mhilu anakwenda na mpira upande wa kulia wa uwanja, anapigaa, gooooooli, Kagera wanajifunga katika harakati za kuokoa, sasa ni 3-0

Dak ya 90, Zimeongezwa dakika tatu pekee mpira umalizike
Thanks for updates
Msukuma tolori mdogo mdogo jiandae mwenye mzigo amekaribia kuuchukua mzigo wake[emoji460] [emoji460]
 
Safi yanga sukumia chini hao wanaoshangilia mwanzo wa ligi
 
Safi yanga sukumia chini hao wanaoshangilia mwanzo wa ligi
Mtajifariji sana ila hii yanga ni timu ya Kawaida kwa aliyeanglia mpira anaelewa hili na wakichukua ndoo itakuwa safi kwan kuna nguvu ya mungu inaiongoza yanga
 
Lile goili alofunga ni nani hasa jaman?
Maana linachanganya
 
Thanks for updates
Msukuma tolori mdogo mdogo jiandae mwenye mzigo amekaribia kuuchukua mzigo wake[emoji460] [emoji460]
Mkuu, unapenda sana kuquote hadi nyuzi ndefu kama hii..?
 
Mtajifariji sana ila hii yanga ni timu ya Kawaida kwa aliyeanglia mpira anaelewa hili na wakichukua ndoo itakuwa safi kwan kuna nguvu ya mungu inaiongoza yanga
Ndoo lazima iende kwa yanga hakuna ubishi hapo
 
Msisahau kesho chama la wana simba vs mtibwa sukari, hapa hapa nyumbani kwetu yaan (UWANJA WA JAMHURI)
Simba hachezi mechi yoyote mpk atoke misri, mtibwa anacheza na prisons nafkiri kesho au jumapili
 
View attachment 709076

01': Mechi ya Yanga vs Kagera Sugar imeanza hivi punde

04': Haji Mwinyi anarusha mpira kuelekea lango la Kagera baada ya kutolewa, anauchukua Ajib, Ajib anapasia langoni mwa wapinzani, wanaokoa

05': Kagera sasa, anao Atupele Green, pasia pembeni mwa Uwanja, hatariii, Kagera wanakosa nafasi ya wazi

07': Rostand anaanzisha goli kiki, ni baada ya mpira kutoka nje

08: Buswiiiita, namna gani hapa, krosi yake inakwenda nje, ilikuwa ni pasi nzuri ya auta kutoka kwa Ajib

12': Matokeo ni 0-0 mpaka sasa

13': Hatari katika lango la Kagera hapa, Buswiita, anababatizana na mlinda mlango, anaudaka

14': Mpira umesimama baada ya kipa wa Kagera kuumia, Cannavaro naye anapasha nje

15': tayari mpira umeshaanza, kwake Kamusoko, anapiga shuti lakini linatoka nje

16': Offside, Kagare wanaotea, mpira unapigwa kuelekea kwao

18': Kibaya anapata kadi ya njano, ni ya kwanza kwenye mchezo wa leo

19': Faulo, kadi ya pili ya njano inaenda kwa mchezaji wa Kagera, ni baada ya kucheza faulo eneo la hatari, inapigwa langoni mwao

20': Ajib yuko na mpira, anapigaaa, inapiga nyavu za juu

21': Ngonyani naye anapata kadi ya njano baada ya kucheza mazambi, ni ya tatu sasa katika mchezo huu

21': Matokeo ni 0-0

22': Mpira umesimama, Maxime anatoa maelekezo kwa wachezaji wake

23': Fhaki anapiga hapa, hatari langoni mwa Yanga, namna gani mshambuliaji huyu anashindwa kutumia nafasi

25': Kavila anamchezea rafu Chirwa hapa, inakuwa faulo kwenda Kagera

25': Ally Nasoro sasa anaondoka nao kupandisha mashambulizi, anapiga pasi mkaa, anaokoa Yondani

26': Wanaanza Yanga eneo la nyuma, Kessy anampasia Buswita, kwake Kamusoko, Kamusoko anapiga kwake Pato lakini beki wa Kagera anautoa na mpira unakuwa wa kona

28': Mpira anao Kamusoko, anapasia nyuma kwake Yondani, Yanga wanajaribu kutafuta bao hapa

29': Emmanuel Martin, anacheza faulo, mpira unapigwa kuelekea Yanga

30': matokeo ni 0-0, mpaka sasa hakuna timu iliyofanya shambulizi la kutisha kwa mwenzake

31': Goli Kiki upande wa Yanga, unapigwa kuelekea Kagera

32': Kagera waanzisha goli kiki, tayari ushapigwa, faulo, unapigwa kuelekea Kagera

33': Mabadiliko Yanga wanafanya mapema, anatoka Pato na nafasi yake inachukuliwa na Maka

35'; Kagera wanapata kona ya kwanza baada ya Mwinyi Haji kuutoa mpira, inapigwaaa, inapigwa kichwa na mshambuliaji wa Kagera lakini kipa Rostand anadaka

37': Unarushwa sasa kuelekea lango la Kagera, anao Ajib sasa, kwake Martin, unapigwa kwake Buswita, anautuliza kwa njia ya kifua lakini beki wa Kagera anaokoa

39': Anao sasa Ajib, unapigwa langoni, kipa anajitutumua anaupiga na mkono unakuwa wa kurushwa kuelekea langoni kwake, kidogo iwe kona

41': Faulo, Ajib anapiga, anapiga ya chinichini lakini mabeki wanaokoa kwa kichwa

41': Mpira uko mbele sasa upande wa kulia mwa uwanja wanao Yanga, beki wa Kagera anauokoa hapa, unapigwa mbele lakini Maka anautoa nje

Mpira ni mapumziko sasa, Yanga 0-0 Kagera Sugar

45': Kipindi cha pili kimeanza, matokeo ni 0-0

46': Beki wa Kagera anachezewa faulo, mpira unapigwa kuelekea langoni mwa Yanga

47': Hatarii langoni mwa Yanga, Atupele Green anakosa kupiga shuti nje kidogo mwa eneo la hatari, ni faulo,

48': Inapigwaaa, inatoka nje sentimita kadhaa tu, bahati nyingine wanaikosa Kagera Sugar,

50': Yanga wanaanza nyuma taraatibu, beki wa Kagera anautoa nje

51': Penatiiii, Yanga wanapata tuta hapa

51': Ajib ndiyo anapiga tuta, anapigaaa, gooooooli, Yanga wanapata bao la kwanza, sasa ni 1-0

53': Kagera wanaanza upya kati, wanapasiana kuelekea langoni mwa Yanga, inapigwa moja juu, kipa Rostand anaruka kama nyani anaudaka

55': Kagera wamezidi kuamka licha ya kufungwa bao hilo moja, wanamiliki zaidi mpira eneo la kati

57': Ajib sasa na mpira, piga huku pembeni lakini Kagera wanaokoa, inapigwa mbele hukuu, offside

59': Namna gani Kagera wanakosa tena bao hapa, ni nafasi adhimu kabisa hii ndani ya eneo la hatari mwa Yanga, mpira unakwenda nje

61': Kagera wanaanza mashambulizi tena, wanapasiana eneo la nyuma

63': Faulo inapigwa kuelekea Kagera baada ya beki wake kucheza mazambi

64': Yanga wanao mpira hivi sasa, Ajib anajaribu kuzunguka lakini ananyang'anywa mpira, Kamusoko anauwahi

65': Mpira anao Fhaki sasa, pasia kati ya uwanja huku, unarejeshwa kwake Fakhi tena, Kagera bado wanaumiliki, pigwa huku langoni mwa Yanga, offside

68': Kagera wanashindwa kutumia vema nafasi ya kufunga baada ya kupasiana vizuri na kuingia eneo la hatari la Yanga

69': Kona wanapata Yanga, ni ya nne na tano katika mchezo wa leo, Ajib anapiga lakini inaokolewa

70': Chirwaa, anapiga krosi moja ya hewani lakini inatoka nje

71': Mpira umesimaa kidogo, mchezaji wa Kagera ameumia

72': Omary Daga anaingia kuchuka nafasi ya Atupele Green, matokeo bado ni 1-0

75': Yanga wanapata kona, inapigwa na Ajib, pigwa huku Chirwa anapiga kichwa lakini inaenda pembeni, Kagera wanaokoa

75': Emmanuel Martiiiin, anapigaaaa, kipa wa Kagera anakuwa mahiri anaokoa

76': Goooooooli, Martin anaifungia Yanga bao la pili kufuatia krosi nzuri ya Obrey Chirwa, Yanga wana mabao mawili sasa na Kagera 0

79': Yanga wameamka sasa, wanakwenda mbele na mpira, kona! Ajib yu tayari kupiga, anaanza fupi hukuuu, kona nyingine, ni ya 7 sasa, inapigwaaaa, Kagera wanaokoa

81': Kagera wanapata kona pia, inapigwaaa lakini inaokolewa

82': Kagera wanaumiliki mpira tena, wanajaribu kutafuta bao angalau la kufutia machozi

83': Hatari langoni mwa Kagera, kipa anadaka, anaanza taratibu na wenzake nyuma

85': Kagera wanapata kona hapa, inapigwa lakini inatolewa na kuwa kona ya pili, inapigwa tena hukuu, Rostand anadaka na kutulia vizuuri kabisa

87': Yanga wanao sasa, Buswita, kwake Kessy, anarudisha kwa kipa wake

88': Yusuph Mhilu anakwenda na mpira upande wa kulia wa uwanja, anapigaa, gooooooli, Kagera wanajifunga katika harakati za kuokoa, sasa ni 3-0

90': Zimeongezwa dakika tatu pekee mpira umalizike

Full Time, Mwamuzi anapuliza kipyenga kumaliza mpira, Yanga 3-0 Kagera Sugar.



Alaaaah, kumbe wachovu wa kimataifa walikuwa wanacheza leo?
 
Back
Top Bottom