Dini si imani, Mimi mkristo nimekubali kuoa ndoa ya kiislamu, ndoa ya kikristo inampa kiburi mwanamke na ni ngumu kusuluhisha matatizo

Dini si imani, Mimi mkristo nimekubali kuoa ndoa ya kiislamu, ndoa ya kikristo inampa kiburi mwanamke na ni ngumu kusuluhisha matatizo

We nae unadeka sana. Sasa mwanamke anakusumbua vipi kichwa chako hadi unakosa direction kiasi hiki?

Haya ndio matokeo ya kuwajaza watoto wa kiume ujinga vichwani halafu wanakutana na vitu tofauti.

Unakuta mzazi especially akina mama,anamwambia mtoto wake wa kiume, "Mwanamke hapigwi" "usije ukamfokea mtoto wa watu ongea nae kwa upole","mpende mkeo kuliko chochote kama unavyonipenda","mwanamke anapewa pesa usije ukamnyima pesa" na upuuzi mwengineo.

Hii inawajenga vijana wa kiume na mentality ya upunda au ukondoo kiasi kwamba wanashindwa muwajibisha mwanamke kwa uovu wake pale anapofanya.

Mwanamke anatoka nje ya ndoa ukija uliza eti sababu ulikuwa hautengi muda wa kukaa na mimi nikawa mpweke sana. Hapo mtu alikuwa nje kupambana na maisha ili kuleta pesa ndani ya familia.

So ni kaina fulani ka uzembe wa kifikra kakujitakia. Unajifunga kwa fikra zako mwenyewe. Kwa Kila mwanamke anaeondoka kuna wanawake 1000 zaidi wa kuja kuwa nao katika ngazi ya kata unayoishi hapo hatujaenda ngazi ya wilaya, mkoa, na taifa na Dunia.

Why sasa ukae ukisumbuana na mtu ambaye ukiuliza anakupa kiasi gani kwa mwezi zaidi ya bills unakuta ni zero. Mimi ninakuwa na mawazo sana gari yangu ikiwa inahitajika kufanyiwa service kuliko mwanamke akiwa analazimisha kupewa pesa kwa kauli zao zile "nataka unihudumie" kama mgonjwa au mzee asiyejiweza. Ufala tu.

Acha kupoteza muda na kujiweka tegemezi na mwanamke m'moja, mradi wewe hauna changamoto basi, tafuta mwingine life isonge.
 
Kwa kipindi kirefu nimekuwa nasita kuoa, kwa umri wangu wa miaka 28 nimeona ni wakati sasa niwe na ndoa official, Si mara ya kwanza kufikiria hili jambo, ni tangu nipo 25 nafikiria ila sheria za ndoa za kikristo zilikuwa zikinipa hofu kubwa mno hasa kwa tunayojionea kwa wahanga, Ni lazima tukubali wanawake wa sasa sio kama mama zetu wa enzi zile ambao tayari walikuwa wamefundwa kuishi maisha ya ndoa na mwanaume na ndio maana hakukuwa na vimbwanga vingi kama sasa. Ndoa za kikristo kwa sasa zimekuwa mtihani jamani.


Ndoa za kikristo ni ngumu kusuluhisha matatizo

Kwa mama zetu miaka hiyo ahsafundwa majukumu ya ndoa, kuishi na mwanaume, n.k. lakini siku hizi hali ni tofauti yani ukiongezea mambo ya usawa, wanawake walioelimika, ushauri wa mashosti watukutu, n.k. ndoa zimeingia kwenye matatizo mengi sana, Huko kanisani usuluhishi unaotumika ni ule wa kina mama zetu ambao angalau walikuwa waelewa ila kwa hawa wanawake wa sasa ni kama kumpigia mbuzi gitaa, na hapo ndipo watu wanakimbilia mahakamani wanaona kanisani ni kupoteza muda tu, kwa hili tu unaona ni wazi kabisa usuluhishi wa kikristo umefeli, Kwanini wakimbilie mahakamani na sio kwa wachungaji ?

Kuoa upya ni ngumu kwenye ukristo

Ndoa ya kikristo imejaa bureacracies nyingi sana, mnaweza kauchana hata miaka miwili hurusiwi kuoa upya mpaka kanisa litoe kibali chao, ukilazimisha kuoa upya shoka la sheria linakukata, what is ithis ?

Ndooa ya kikristo inampa mwanamke kiburi cha usawa

Mwanamke anajua ukishamvisha pete ashakubana hapo kuchomoka ngumu, Anajua fika kabisa hata afurukute mtaenda kanisani kwa wachungaji wataokuwa wanawabembeleza kila siku mkayamalize, anajua huna uhuru wa kuoa upya kirahisi, anajaua mkiachana ana mali zako pasu kwa pasu, n.k.

Ndoa za kikristo zinaleta tamaa ya mali

Pia katika suala la wale majambazi wanaoingia kwa nia ya kula timing muachane ili wapate mgao wa mali katika ndoa za kikristo ni rahisi sana, katika uislamu mwanaume hana wajibu huo, hapa pia adabu inaongezeka kwa mwanamke, hata mwanamke akikaza waweza kumpiga biti utaongeza wenzake watatu asiingilie mgao wao
.........................................................................

Binafsi nimekata shauri kwamba tamaduni za ndoa za kiisalamu ndio zitanipa ahueni zaidi ya kuishi maisha ya ndoa, mwanzoni nilikuwa nikisita kwa kuunganisha imani na dini kuwa kitu kimoja lakini kwa sasa nimeweza kukubali imani na dini ni vitu viwili tofauti nimeona ni sawa tu kuoa kwa misingi ya dini ya kiislamu, lakini kwa imani bado mimi ni mfuasi ya Yesu / Mkristo,
Pole sana kijana kwanza umri wako bado, hata hivyo ndoa Haina dini, iwe ya kikristo, kiislam, kimila, kihindu n. k bado tu itakuwa na changamoto kwa sababu wanadamu ni walewale ni nani akiyekudanganya kuwa ndoa za kiisalam hazina changamoto?
 
Aliyesema mahakama Ni mambo ya kijeni, napinga, Ni yetu wanachi na tumeiunda wenyewe, je Bible ulishirikishwa? Uliletewa na kukariri tu! Ukizingatia sana hizo Imani za kizungu utakufa masikini na Bible yako mikononi. Aliyefanikiwa na Bible mikononi Ni maujanja tu!!!
 
Umebadili dini na kuwa muislamu au wewe bado ni mkristu ila umefunga ndoa ya kislamu?
 
Eti nimeoa kiislam ila mimi kiimani ni mkristo.

Acha kuifariji jamii mkuu, mimi nitaoa kikristo na dini haitanifunga kuachana kama akisaliti na mali zangu nilizotolea jasho zitabaki kua zangu daima.
 
Umri wako 28 bado unasitasita kuoa kutokana na urasimu (bureaucracy) huko uliko.
Fanya maamuzi kiume , oa huyo mke wa dini nyingine au wa dini yako ndoa ya kiserikali. Hakuna urasimu, gharama ndogo, hakuna unyanyapaa. Mengine utashauriwa jinsi ya kutengeneza. Wangapi wameamua hivyo na kuondokana na kuteswa na msongo wa mawazo?
 
Back
Top Bottom