Dini zimefanywa biashara, michango imekuwa mingi

Dini zimefanywa biashara, michango imekuwa mingi

Salaam!

Mimi nafikirishwa sana na hizi dini za leo za kizungu, binafsi mimi ni mkatoliki lakini naona uchafu uchafu tu.

Hawa wakristo tuwape muda tu hii karne ya 21 ikipita najua hatuta kuwepo wengi humu ila ukristo utakuja kuwa kituko cha karne (22) kutokana na yale tunayo yaamini viongozi wetu wanatuletea mapicha picha ya kutufanya sisi ni misukule yao.

Nimejiuliza swali moja tu mimi kama baba mlezi mtoto alifika hatua ya kipaimara, nikaambiwa eti nitoe shilingi elfu 25,000 ili mtoto akae pamoja na askofu. Yaani yeye askofu anakuja kukaa na watoto hiyo siku ya kipaimara wanakula pale sahani ya wali na soda na stori mbili tatu afu imeisha hiyo. Mimi kipaimara changu hakikuwa hivi sasa hii elfu 25 ni ya nini? Mamichango ya zaka ni lundo.

Kidogo nisahau kuuliza hili swali?

Hivi wakuu na huko kwenye uislamu ni hivi hivi?
Sasa si bora wewe Mkatoliki uliambiwa utoe hiyo 25,000/=

Mimi Mlutheri (KKKT), niliambiwa mwanangu atoe 70,000/= ili aweze kupata kipaimara mwaka Jana, nilishangaa Sana!!!

Nikahoji hiyo elfu sabini yanini?! Kwani kupata kipaimara ni biashara?! Wakajibu atapewa biblia Kama zawadi?!

Sawa hatukatai kupewa biblia, lakini hiyo ndio bei ya biblia?! Na Kama mzazi hana hiyo hela?! Ndio kusema mtoto hapewi kipaimara?! Kiukweli haya madhehebu yetu hakika yamegeuka sehemu ya kuchuma hela Sana Tena kwa lazima, huna hela hupati huduma ya kiroho,

NB:

Watu hawakatai kutoa sadaka, michango n.k. lakini isiwe too much, au upigaji kiasi hicho ,Tena kwa masharti na lazima , hutoi hupatiwi huduma ya kiroho!!

Inasikitisha Sana kiukweli!!

Tunakoelekea huko, sijui,,,!!!

Mungu tu atusaidie!!
 
muhimu sana, maana unaweza mpa jambazi kama hakuna umuhimu kwenye utoaji
Yes ukitoa sehemu isiyo sahihi inakuwa useless,ukitoa kwa watu wenye uhitaji kama mayatima,walemavu/maskini na mafukara wasiojiweza hapo inakuwa umepatia sehemu sahihi na Mungu anakubariki.
Ila ukienda kutoa kwa mtu anayetembelea gari ya milioni 60 na anamiliki nyumba ya milioni 200 au 300 akala yeye binafsi au na familia yake hapo ni sawasawa umeitupa tu.

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Inategemea umempa nani

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
Safi kabisa,

Siku hizi nimeona heri hata nitoe kwa yatima, wagonjwa mahospitalini, masikini wenye uhitaji mbalimbali, wajane maskini na hata wafungwa magerezani,,,!!

Kuliko hawa wanaotoza hela nyingi sana huku wao wanaenda kujenga majumba ya kifahari na kununua magari ya gharama kubwaaaa!!

Bora tuwape masikini na wenye uhitaji akya Mungu!!
 
Safi kabisa,

Siku hizi nimeona heri hata nitoe kwa yatima, wagonjwa mahospitalini, masikini wenye uhitaji mbalimbali, wajane maskini na hata wafungwa magerezani,,,!!

Kuliko hawa wanaotoza hela nyingi sana huku wao wanaenda kujenga majumba ya kifahari na kununua magari ya gharama kubwaaaa!!

Bora tuwape masikini na wenye uhitaji akya Mungu!!
Haswa hivi ndivyo inavyotakiwa ila watu wanafanya kinyume kutokana na uelewa mdogo

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Yes ukitoa sehemu isiyo sahihi inakuwa useless,ukitoa kwa watu wenye uhitaji kama mayatima,walemavu/maskini na mafukara wasiojiweza hapo inakuwa umepatia sehemu sahihi na Mungu anakubariki.
Ila ukienda kutoa kwa mtu anayetembelea gari ya milioni 60 na anamiliki nyumba ya milioni 200 au 300 akala yeye binafsi au na familia yake hapo ni sawasawa umeitupa tu.

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
lakini mtu kumiliki nyumba na kuendesha gari la samani sio tatizo.. je ? anachokusanya kinaenda wapi ... Tujue pia wahitaji wengine hukimbilia huko.. ni muhimu kuongozwa na mtu wako wa ndani ujue unapotoa ni sahihi au chenga chenga
 
ukiristo kwaujimla wake ni biashara.dini yaukweli niuislamu

kunakanisa mahalo mchungaji kuonana namuumini sikuambayo Sio yaibada ni elfu 60 nawaumini wanajazana Hadi wengine wanakosa nafasi yakumuona.

Sasa najiuliza mchungaji kashindwa kuwaombea kawaida Hadi aonane Nao mmojammoja?Tena kwaelfu sitini🤣🤣🤣
Ni dokta wa moyo ama
 
Safi kabisa,

Siku hizi nimeona heri hata nitoe kwa yatima, wagonjwa mahospitalini, masikini wenye uhitaji mbalimbali, wajane maskini na hata wafungwa magerezani,,,!!

Kuliko hawa wanaotoza hela nyingi sana huku wao wanaenda kujenga majumba ya kifahari na kununua magari ya gharama kubwaaaa!!

Bora tuwape masikini na wenye uhitaji akya Mungu!!
Ukisikia sadaka ndio hii sasa
Kila leo tunawaambia watu badala ya kuwapa masikini walio jirani yeye mbio anapeleka kwa jamaa ambae anamlazimisha atoe kila mwezi, sasa sijui kwa mwaka mnatoa ngapi na marejesho ni nini?

Masikini akiomba anapitwa kama hawamuoni huku wakiwa wamependeza wanazipeleka wanakojua
 
lakini mtu kumiliki nyumba na kuendesha gari la samani sio tatizo.. je ? anachokusanya kinaenda wapi ... Tujue pia wahitaji wengine hukimbilia huko.. ni muhimu kuongozwa na mtu wako wa ndani ujue unapotoa ni sahihi au chenga chenga
Huo uwezo wa kuhoji au uwezo wa kudadisi walio wengi ndio hawana.
Mimi nikienda sehemu ya ibada ukiitishwa mchango lazima nisikilize kwa makini na nidadisi huo mchango ni kwa ajili ya shughuli gani?kwa mfano kama ukiniambia ni kwa ajili ya ujenzi basi ni lazima nicheki je kuna ukuta umebomoka?Au kuna paa limeezuliwa?Au kuna finishing inatakiwa kufanyika na ili nishawishike zaidi inabidi niwaone mafundi wako saiti tayari

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
 
Huo uwezo wa kuhoji au uwezo wa kudadisi walio wengi ndio hawana.
Mimi nikienda sehemu ya ibada ukiitishwa mchango lazima nisikilize kwa makini na nidadisi huo mchango ni kwa ajili ya shughuli gani?kwa mfano kama ukiniambia ni kwa ajili ya ujenzi basi ni lazima nicheki je kuna ukuta umebomoka?Au kuna paa limeezuliwa?Au kuna finishing inatakiwa kufanyika na ili nishawishike zaidi inabidi niwaone mafundi wako saiti tayari

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
Sema haya mambo ya kutoa yana mambo mengi sana
 
Ukiwa na ufahamu na maandiko katika kitabu unakuwa huru kwasababu utakuwa unajua halali na batili hautayumbishwa haya makando kando yapo hata ktk baadhi ya Mashekh japo si kwa wingi

Lakini ukweli unabaki kama waumini tukiwa na elimu hatuibiwi tunajua huyu katuchota huyu anasema kweli
 
Uzuri sadaka sio Kodi kwamba ni lazima utoe. Kazi kwako na Iman yako. Jamn watanzania tujaribu kuwa serious na Mambo ya msingi. Hv jambo la hiyari ni jambo la kuja kulalamikia huku. Kutoa sadaka na michango ni hiyari Yako huna haja ya kuja kulalamikia huku coz sio sheria
 
Back
Top Bottom