Uchaguzi 2020 Diplomasia ya Uchumi kumbeba Magufuli Uchaguzi wa Urais Oktoba 2020

Uchaguzi 2020 Diplomasia ya Uchumi kumbeba Magufuli Uchaguzi wa Urais Oktoba 2020

hata tukipewa huo uhuru wa kujieleza bado kuna changamoto zingine zitakua kikwazo kwetu, inshort maisha ya mwanadam ni changamoto mwanzo mwisho ukitatua hii inakuja nyingine...

hata hao mabeberu wanaojifanya kup4ania haki za wengine bado wana makando kando yakuminya uhuru wa wanaoenenda kinyume na matakwa yao bt kwa kua waafrika ni watu wakuimc nyimbo za wazungu bila kutafakari basi tuaendelea kuwa wajinga mpaka mwisho wa safari.
Kwa akili zako hizi, unafurahishwa kuona mTanzania mweusi, akimnyanyasa mTanzania mwenziye ?!. Tujiwekee utaratibu wa kuongozana vizuri .

Hii ya wengine kujiona wana haki na taifa hili kuliko wananchi wengine si sawa.
 
Kwa akili zako hizi, unafurahishwa kuona mTanzania mweusi, akimnyanyasa mTanzania mwenziye ?!. Tujiwekee utaratibu wa kuongozana vizuri .

Hii ya wengine kujiona wana haki na taifa hili kuliko wananchi wengine si sawa.
mkuu hata wewe ukipewa kuliongoza taifa kuna kundi litalalama tu juu yako, mfano mzuri kikwete aliwaacha watu wafanye watakavyo je hakulaumiwa? hebu tuache kuwataka viongozi wawe parfect akati hata sisi hatupo parfect...
 
Wengine akili zetu haziendi mbali na tulipo, tukishiba wali na ndizi mbivu msibani mtaani kwetu, tunaomba utokee Tena msiba mwingine mtaani! Lakini unaweza kuwa ni wewe. Huu siyo mchango kwenye hoja iliyotolewa Ila ni kuhimiza Wana jf kujibu hoja kwa makini kwani zinahusu maisha ya wananchi.
 
Magufuri lazima aondoke, amelirudisha Taifa miaka takribani 25 nyuma katika kila kitu kuanzia hicho unachoita diplomasia ya uchumi, na kwenye mambo mengine mengi kama utawala wa bora, mahusiano ya kimataifa, siasa safi, mapambano dhidi ya rushwa, n.k.

Diplomasia ya Uchumi.
Kwanza ujue, katika karne hii, unapoamua kuzunguzia masuala ya kiuchumi katika muktadha wa kidemocrasia maana yake unazungumzia namna uchumi wa Taifa unavyochangamana na uchumi wa kidunia.

Sasa, Kwanza sisi tuliishaamua kujichangamana na uchumi wa kidunia, na ndio maana serikali tatu zilizopita ile ya Mzee Ruksa, Mzee Mkapa, na ya Mjeda, Jakaya Kikwete zilijikita kushirikisha wananchi na makampuni ya ndani na nje kwenye kusimamia uchumi, kabla ya ujio wa magufuri, Tanzania ilikua inaongoza katika kuvutia mitaji kutoka nje katika ukanda wa africa mashariki, wananchi kwa wingi sana walikuwa wanashiriki katika shughuri za kiuchumi KWA FAIDA, na uchumi ulikua unakua kwa viwango visivyopungua 6% (1995-2005) na visivyopungua 7% (2005-2015)

Wakati Rais Mwinyi anaingia Madarakani mwaka 1985, nchi hii kila mtu alikuwa anawajibika kwenye sera za CCM na hasa maelekezo ya Azimio la Arusha, ambayo kimsingi yalikuwa yanakasmisha tena labda kwa lugha ingine, yalikuwa yanawanyang'anya wananchi fursa za kushiriki kwenye uchumi walizokuwa nazo kipindi cha mkoloni na kuzikamismisha kwa serikali, matokeo yake yakawa ni kusimika mizizi ya umasikini katika Taifa.

Mashirika ya kiserikali, yaliyopaswa kuongozwa kwa misingi ya kibiashara, basi lau kufuata misingi ya kiuchumi katika kujiendesha yote yakawa yana matawi ya chama cha mapinduzi, vyama vya ushirika badala ya kusimamisha biashara ya mazao ya kilimo kwa faida za wavujajasho wakulima, vikawa vikiendeshwa kwa matakwa ya ccm, n,k

Huku Nyerere akizunguka kila mahala nchini akisema ni lazima tujitegemee huku akiita wazungu mabeberu nyuma ya pazia alikuwa ni omba omba anayetia aibu kwa mataifa ya kijamaa, Hasa uchina na Urusi, ambao walimzawadia miradi mikubwa mikubwa kama hii ya magufuri ambayo serikali ya chama cha mapinduzi haikuwa na uewezo wa nyenzo, fedha wala ujuvi wa kuviendesha na kuviendeleza, ndio maana mpaka leo kuna maswali tu lakini majibu hakuna, viwanda vile vilivyojengwa wakati wa mwalimu vilienda wapi?

sasa, nikiruka miaka ishirini ya utawala wa Mkapa na Kikwete, ambayo ilitengenezewa mazingira mazuri kabisa ya kubadirisha ama kufuta umasikini na ushenzi wote katika Taifa letu baada ya Mzee mwinyi kulivunja azimio la Arusha na kuvunja mizizi ya u-ccm kwa kuruhusu mfumo wa vyama vingi nchini.

Yaani wakati mimi nairuka kwa kwenda mbele, Magufuri ameiruka miaka hiyo hiyo tena na zaidi na kulirudisha nyuma Taifa. Kwanza achana na matendo yake, matamanio yake yote kama ambavyo amekuwa akiyarudia mara kwa mara ni kulirudisha Taifa katika mfumo wa chama kimoja, more than 35 years back. Anataka kulirudisha Taifa katika mfumo ambao asilimia karibia 50 ya nguvu kazi yake hauufahamu zaidi ya kuhadithiwa namna ulivyokuwa wa kijima na wa hovyo.

Mambo yale yale, na mfumo mbovu wa uchumi ule ule alioutengeneza mwalimu baada ya uhuru, ambao baadae ulikuja kumbadirikia na kuwa kama kaa la moto mkononi hata akaikimbia Ikulu ya Magogoni ndio anaoukumbati Magufuri leo, aina ya uchumi ulioelekezwa na azimia la arusha.

Hizi ni imani mbili kati ya nyingi za TANU/CCM/AZIMIO LA ARUSHA
1. Kwamba ili kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakwenda sawa Serikali lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia muhimu za kuukuza uchumi; na

2.Kwamba ni wajibu wa Serikali, ambayo ni watu wenyewe, kuingilia kati kwa vitendo maisha ya uchumi ya Taifa ili kuhakikisha usitawi wa raia wote na kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine au kikundi kimoja kunyonya kikundi kingine na kuzuia limbikizo la utajiri kufikia kiasi ambacho hakipatani na siasa ya watu wote kuwa sawa.

Maazimio haya, na matokeo yake, nyakati hizo, yalikuwa yanapigiwa upatu na wanaccm vipofu, pamoja na watendaji wa serikali waliokuwa na njaa kali sana vichwani mwao, yalipigiwa upatu sana, hasa na wapambe feki wa mwalimu ambao walifikia hatua ya kulazimisha FIKRA ZA MWALIMU ZIDUMU kama ambavyo leo kuna kundi kubwa pia linalotaka kila mtu AUNGE JUHUDI.

Hakuna utawala uliokamilika, hata hizo tawala tatu zilizopita zilikuwa na matatizo mengi tu, lakini hazikuwahi kujiingiza kwenye kwenye makosa ambayo yanaweza kutetemesha familia zote katika Taifa kama ambavyo ilifanya Awamu ya Kwanza.

1. uraisi hauupati ata uandike kitabu
2. mahusiano na nchi zingine inategemeana kama hayana manufaa ya nn kuyangangania
3. bado nchi nyingi sana tuna mahusiano nao mazuri sana, china na usa hawana mahusiano mazuri na juzi kila mtu amebomoa embassy ya mwenzake,
4. hatupo tayar kurudi kwenye misaada
 
Mtu alijificha kwa wiki kadhaa na kuwaacha wananchi wake wapambane na hali zao mpaka alipojiridhisha kuwa hali si ya hatari na bado hamuoni? Watanzania mmelogwa si utani.

sasa wapi hamna corona unasema kjificha kama alienda nje ya dunia sawa, sasa mtu yupo apo apo tz unasemaje kajificha! kiukwel upinzani mnaboa sana na mada zenu, kwanza kama we sio mfuasi wa magufuli kajiweke karantini saaaahv kama upo town unafuata maono ya mzee baba nyamazisha hilo fuvu
 
Anashiriki uchaguzi
Wakudada! Naona wajumbe wamekukubali baada ya kugawama nao ile pension ya 240M.
Usije msahau mshikaji wako Mtela aliyeharibikiwa kwa kuonja vya wakubwa! Mmetoka naye mbali
 
1. uraisi hauupati ata uandike kitabu
2. mahusiano na nchi zingine inategemeana kama hayana manufaa ya nn kuyangangania
3. bado nchi nyingi sana tuna mahusiano nao mazuri sana, china na usa hawana mahusiano mazuri na juzi kila mtu amebomoa embassy ya mwenzake,
4. hatupo tayar kurudi kwenye misaada
Unanichekesha sana. hemu kasome budget yenu
 
Kamanda jipime
Kwa akili zako hizi, unafurahishwa kuona mTanzania mweusi, akimnyanyasa mTanzania mwenziye ?!. Tujiwekee utaratibu wa kuongozana vizuri .

Hii ya wengine kujiona wana haki na taifa hili kuliko wananchi wengine si sawa.
 
Umejenga hoja kuntu
1. uraisi hauupati ata uandike kitabu
2. mahusiano na nchi zingine inategemeana kama hayana manufaa ya nn kuyangangania
3. bado nchi nyingi sana tuna mahusiano nao mazuri sana, china na usa hawana mahusiano mazuri na juzi kila mtu amebomoa embassy ya mwenzake,
4. hatupo tayar kurudi kwenye misaada
 
Back
Top Bottom