Discipline: Somo zuri kutoka kwa marehemu Bruce Lee

Discipline: Somo zuri kutoka kwa marehemu Bruce Lee

Kuna story huwa ipo mtaani eti alipigana na maninja 12 akawashinda hii inaukweli kweli? Ukichukulia kuwa maninja huwa wanatumia uchawi na nyenzo zao si mchezo
Yawezekana ni kweli bruce lee ana rekodi ya kutowahi kupigwa hata siku moja. Pambano ambalo hakushimda alikua anamiaka 13 kama sijasahau..alitoka Draw
 
Mabaharia kila siku kushindana na papuchi sijui watafanikiwa lini
Wakijitambua tu watafanikiwa. Ubaharia wangeutumia kujuzana mbinu za kumake bingo..sasa wao wanatumia kutafuta mademu
 
Uongo mkubwa sana. Mateke sita ndani ya Sekunde? Uongo huu muwe mnasimuliana mkimaliza kusoma ile usiku wenyewe mnaita prepo. Labda hujui sekunde inakuaje. Akili za kuambiwa changanya na zako.



Bruce-Lee-as-Kato-1967-restored.jpg
Salute
Jina Bruce Lee sidhani kama ni jina ngeni kwa mtu yoyote mwenye umri kuanzia miaka 100
mpaka 10, hivyo haiana haja kumzungumzia kua ni nani hasa.! Bruce alikua mwalimu wa kung fu
na mgunduzi wa staili za Jet kune-do, muigizaji na mwanafalsafa..Ni moja kati ya binaadamu
wachache ambao wameweka rekodi ambazo hazitokuja kuvunjwa baadhi yao ni Leonard Da'Vinci,Yesu wa Nazareth,Genghis khan,Michael Jackson Newton, Paulo wa Tarso (mtume) n.k n.k

Bruce katika maisha yake ya miaka 32 tu aliyoishi hapa Duniani kaacha historia mbalimbali
ambayo sidhani kama kuna mtu wa karne hii ya 21 anaweza kuja kuivunja, baadhi ya rekodi
alizoaacha amabazo hakuna aatakaye zivunja ni kama vile...

⦁ ●Bruce lee alikua anaweza kupiga ngumi karatasi ambazo zinaninginia hewani akazitoboa
(Mimi na wewe tukipiga ngumi karatasi tutaichana sio kuitoboa)
⦁ ●Alikua na speed kubwa ambapo kipindi anacheza muvi zake walikua wanaweka slow motion ili kuweza kuona mapigo yake, inasemekana yeye ndie binaadamu pekee
aliyekua na spidi kali zaidi kwenye kurusha mateke na ngumi.
⦁ ●Ndani ya sekunde moja alikua anaweza kurusha mateke sita.
⦁ Alikua anaweza kupiga push-up 1500 kwa mikono miwili bila kupumzika, Push up 400
kwa mkono mmoja, alikua anaweza kupiga push up 200 kwa vidole viwili (Mimi sizidi 40
kwa mikono miwili)

Hizo ni baadhi ya rekodi ambazo kaacha Marehemu Bruce tujiulize Bruce alikua anafanya vipi hadi kuweza kuacha alama hizo duniani, pia akaweza kumtengeneza mwanae Brandon nae kiasi
chake akafanya makubwa , lengo kuu la kuleta mada hii nimetaka tushee baadhi ya vitu
ambavyo alikua anafanya hadi kuweza kufikia kuacha rekodi hizo ambazo zinaishi.

Ukimchunguza Bruce Lee utangundua alikua anatembea na vitu viwili vikuu ambavyo
vilimuwezesha kufanikiwa kuacha alama duniani.
1. Bruce alikuwa Integrity Person (Mtu mwadilifu) alihakikisha anafanya kile
ananchokifanya kama jinsi kinavyotakiwa kufanyika..kwa kujituma na kwa moyo wake
wote.
2. Bruce alikua Disciplined Person (Mtu mwenye Nidhamu) alikua ana nidhamu ya hali ya
juu hasa kwa kile anachokifanya.

Basi lengo la mada yangu ni kuangalia jinsi Nidhamu katika vile vitu tunavyofanya yaweza
kutufikisha katika hatua ya kutimiza malengo mbalimbali ambayo tumejiwekea. Bruce alikua na
nidhamu katika mchezo wa ngumi ndio maana kafanikiwa kutengeneza historia na rekodi hizi
ambazo leo hii twazisoma. Ili kutimiza malengo yake aliweza kutengeneza Formula yake akawa
anaiheshimu na kuifuata wote yaweza kutusaidia katika kufanikisha kufikia vile vitu ambavyo
tunatamani kuvifikia maishani (Malengo)....Tuipitie.

⦁ ●Je wewe ni Mwanfunzi/ Kuna kitu unajifunza?
Kama jibu ni Ndio basi nenda kafanye mazoezi juu ya kitu hicho (kajisomee)...kama jibu ni
Hapana basi tafuta kitu ambacho hukiwezi na unapenda kujifunza kisha kakifanyie
mazoezi/Kajisome.
⦁ ●Je katika taaluma yako kuna mtu ni bora zaidi yako?
Kama jibu ni Ndio basi Endelea kujifunzana kufanya mazoezi... Kama jibu ni Hapana basi nenda
katafute mtu ambae ni bora zaidi katika taaluma yako jilinganishe nae kisha kafanye
mazoezi/kajifunze zaidi
⦁ ●Je umemaliza kujifunza/kufanya mazoezi?
Kama jibu ni Ndio basi nenda kalale upumzike, kisha amka endelea kufanya mazoezi
/kujifunza...Kama jibu ni Hapana basi Endelea kufanya mazoezi.
⦁ ●Je Uko unafanya mazoezi/unajifunza muda huu?
Kama jibu ni Ndio basi endelea kujifunza kila kitu kilichoko mbele yako na kamwe usiache
kujifunza vitu Vipya.

Hizo hapo juu ni kanuni alizo jiwekea Bruce lee ili kuweza kutimiza malengo yake, hivyo basi
kama utaona yanafaa ili kutimiza malengo yako basi yafuate. kama unagonga Code ndelea
kujifunza na kufanya mazoezi siku moja utatoboa, kama ni mtu Mechanical endelea kujifunza na
kufanya mazoezi siku moja utatengeneza gari lako, kama unataka kuplan Heist (Wizi wa kutumia
akili) endelea kujifunza jinsi ya kufanikisha tukio lako siku moja utafanikisha, Kama unatamani
siku moja uje kua mwanasiasa na mwandiplomasia bora endelea kujifunza siku moja utaacha
historia nzuri kwenye taifa lako...Nidhamu ndio kila kitu katika kufanya kitu ulichokusudia,
heshimu unachofanya na ukipendehata kama watu wengine wanakubeza "I assure you
brother one Day sun will shine to You"
Brothers n Sisters hatukuumbwa kushindwa,
mafanikio ndio hatima tuliyopewa ila tutayapata pale tu tutakapo weka nidhamu kwayale
tuyafanyayo. Never Give up! Never stop Learning, Dont Never in anything.
Twaweza ku-Archive kila tunachotamani kama tutatembea na vitu hivi vitatu..
▪Discipline ▪Integrity ▪Ambition
Guys wake up, the future is on your Hand

-Learning Never Exahust Mind!
Leonardo Da Vinci
El Maestro
~Da'Vinci
 
Uongo mkubwa sana. Mateke sita ndani ya Sekunde? Uongo huu muwe mnasimuliana mkimaliza kusoma ile usiku wenyewe mnaita prepo. Labda hujui sekunde inakuaje. Akili za kuambiwa changanya na zako.
Hahahaaa acha ubishi mkuu. Hata video zipo nyingi tu zaonyesha akifanya hvo
 
Nami nimejiuliza mara mbili mbili. Chumvi ya Uvinza.
Mkuu video zipo kabisa ndio maana zikaitwa rekodi amabazo hazitakuja kuvunjwa. Hebu google hzo video ujionee
 
Mkuu video zipo kabisa ndio maana zikaitwa rekodi amabazo hazitakuja kuvunjwa. Hebu google hzo video ujionee
Hebu wewe mwenyewe upload hapa hiyo video clip mahsusi kwa ajili ya kuthibitisha hilo ili na wewe ikuondoe kwenye lawama za kuzusha jambo.
 
The Master himself
FB_IMG_1567929811624.jpg
 
Kwa hyo nayo ni rekodi ya kusema akumbukwe????

Harafu ulivyokuwa huna aibu unawalinganisha hao viumbe vyako na Yesu kundi moja daaah!!!

Mkuu leo umetoa boko!!!

Takataka yako pale juu edit tena.
Harafu! wewe ni wa kanda maalumu?
 
Katika somo zuri tusisahau Huu uzi Kuna chumvi pia
 
Ila kuna KAMBA nyingi kwenye story yako
 
Back
Top Bottom