Division 1 ya point saba imepoteza hadhi, Shule kama Saint Francis wanafunzi "wote" wamenyoosha, nashauri kuanzishwe division 1 ya 6 na 1 ya 5

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Hii imekuwa too much sasa, hawa mabinti wa saint francis wanaifedhehesha Necta πŸ˜‚

Division 1 ya saba kwao imekuwa kama kumpa samaka mtihani wa kuogelea, kila mwanafunzi anaibonda !!

Shule imesha master mbinu ya kuwafanya wanafunzi wote wapate division 1 ya saba.

Nashauri kuongezwe division za ziada kama 1 ya 5 na 1 ya sita maalum kwa hizi shule,

A za kawaida zilete 1 ya 7, A za kuanzia 90 zilete 1 ya 6, A za kuanzia 95 ziwe 1 ya 5


 
One iliheshimika mwisho mwaka 2012.

Ukipata hata div two wewe ni mwamba, baada ya hapo tulianza kushuhudia maigizo kibao, mara div five, sijui distinction na ngonjera kibao.
 
We mzee unawa,a zile Div One za Ihungo, Bihawana, Msalato, Mazengo, Wereweru, Moshi tech, Kibaha nk ile miaka ya 80 hadi 90 zilivyokuwa ngumu.

Mambo yamebadilika, lugha ya kiingekeza siyo kikwazo tena kwa vijana wetu, elimu hasa ya kulipia ipo vizuri. ukitaka kuona ugumu wa Div One ya 7 chungulia shule za kata.

Kwa hivyo hiyo 7 - ibaki vile vile.
 
Shule nyingi za kata ni majengo, bado hazina hadhi ya kuitwa shule.
 
Kwani hio point 7 O-level inapatikanaje hadi useme iwe point 5 au 6?
 
HAO WAKIENDA UNIVERSITY WANAKULA C SANA TU.
 
Elimu yetu haijasawi kuwa vizuri, nikukaririshwa na kusolve past papers ili tu mtu afaulu mtihani, ila kichwani ni zero.
Kuso
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…