Dkt. Bashiru: Aliye na dola ndiye ananufaika nayo kubaki madarakani, hata CHADEMA ikiingia madarakani ikaondolewa kwenye dola ni uzembe wao

Yupo sahihi,wapinzani waliposusa walisababisha haya yanayotokea sasa. Acha tupambane na hali zetu.

macson

Aina ya akili zinazokwamisha nchi ni kama hizi. Nikuulize swali moja tu hapa. Waliobaki walifanya nini kuhusu mchakato?? Hukumbuki hao ndio waliopitisha rasimu mpya?? Je unasahau Rais akisema katiba mpya haikuwa ajenga ya ccm ya uchaguzi wa 2015?

Kama upinzani hauwezi hata kufanya bajeti ya nchi isipitishwe, unadhani kweli una uwezo wa kurejesha mchakato wa katiba??

It is all about the survival of the strongest/fittest, dont put blame on the weak!!
 
Huyu nae alikuwa mwalimu wa chuo kikuu! Juzi tu bosi wake aliambia ulimwengu kwamba Uchaguzi Mkuu utakuwa huru na wa haki. Halafu yeye anasema waziwazi kwamba CCM iko madarakani kwa kutumia nguvu za dola!
Lakini subirini kidogo, punde ataikana kauli yake. Kwakuwa wanawaona wananchi kama ni panzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani pamoja na maelezo aliyoleta undetaker huyu ole mushi kashindwa kumuelewa bashiru?

Bashiru ameeleweka sana, na kinachomfanya Bashiru apanic na kuishia kutapika huo utumbo, ni kuwa ameona hakuna wapiga kura huku ccm ikijitapa kukubalika, Sasa haya madai ya tume huru ya uchaguzi yanamtisha maana anajua fika hali itakuwa tete iwapo itakuwepo. Ndio maana anaamua kuweka wazi kuwa ccm itatumia dola kubaki madarakani maana anajua fika kupata kura itakuwa ngumu.
 
Bashiru Na waliopo kwenye system sasa ni ngumu kujua umuhimu Wa katiba mpya ni hadi watakapo kuwa nje yafumo.Hata hawa wastaafu kina mkapa,lowasa,sumaye,membe Leo wanaitamani katiba mpya japo waliweka pamba kama walivyo Wa sasa hivo hata bashiru ni baadae atakuja elewa umuhimu Wa katiba mpya wakati huo hawana tena nafasi ya kufanya mabadiliko kama walivowastaafu Wa sasa
 
Katibu mkuu mwenye akili ya kipumbavu. Sijui elimu yake imemkomboa wapi!
 
Something is terribly wrong with Bashiru. How dare he publicly state and concede that the key open secret of repressive regimes applies to our CCM as well? And he has the audacity to attempt justifying it albeit on rather irrational grounds. Are we a banana republic?

Eti hata CHADEMA wakiingia madarakani watatumia dola hivyo hivyo. Halafu hata Trump naye huko Marekani anafanya hivyo hivyo kubaki madarakani! Katibu Mkuu wa chama tawala anakuwaje hamnazo kiasi hiki? Hivi huyu alielewa madai na mchakato uliokwama wa katiba mpya ulilenga nini? Huyu kweli ni dokta wafalsafa? Bila shaka mteuaji wake leo hii anajuta kumfahamu.
 
Katibu mkuu mwenye akili ya kipumbavu. Sijui elimu yake imemkomboa wapi!
Mkuu alichosema ni ukweli mtupu.. Na wanaCCM wote wanajua hivyo na pia wapinzani wanajua hilo. Na huo ndio uhalisia sema yeye naona amekuwa na ujasiri wa kulitamka hilo hadharani. Angekuwa muongo na mnafiki iwapo angesema tofauti. Na hii ni lugha tu ileile ya "bao la mkono" ila imetamkwa kwa maneno tofauti.

They know kwamba hata wakisema haina shida kwao... Watanzania hawana shida kusikia mambo magumumagumu kama haya.. Kwa hili Bashiru binafsi namwona kama shujaa flani hivi kuutangazia ulimwengu kile kinachofanyika.

Ina maana angesema kwamba kila kitu kipo shwari na chaguzi zinafanyika kwa haki ndipo tungemuona msomi? La hasha..
Kila kitu kipo wazi na alichosema ni sahihi tatizo lipo kwetu sisi tunaoujua ukweli, na bado tunataka kuusikia uwongo ili tujifariji.
 
Hili nimeliona siku nyingi tu,nilijua kuna siku watatamka hadharani. Kwa kifupi CCM hawatatoka bila nguvu,na wanatamani wapinzani washike bunduki ili wao ccm wapate uhalali wa kutangaza hali ya hatari na kuingia na mitutu mitaani ili kuusimika rasmi utawala wao wa kijeshi na kuitawala nchi hii kimabavu.What they are doing now is provocation.

Maana yake wamekosa uhalali wa kuongoza nchi kwa njia ya kura na kukubalika na majority. Na niwaambie tu wanakosea sana,maana wanafanya hayo bila kutathmini watanzania wengi wako upande upi na siku wao na wapinzani wakibeba silaha,nani atasapotiwa na walio wengi miongoni mwa watu,hawajiulizi,hilo wamelisahau kabisa.

Hawajui ni kwa namna gani many Tanzanians are waiting for that "opportunity"! Mnavyozidi kulazimisha kutawala ndivyo mnavyozidi kulazimika kutumia mabavu na uvunjifu wa sheria na haki za binadamu,na ndivyo mnavyozidi kujiingiza kambani,ndivyo mnavyozidi kuwalazimisha wapinzani wenu kutumia nguvu,ndivyo mnavyozidi kuindoa order kwenye jamii.
Na sasa naelewa kwanini sasa ukabila na ukanda umeshamiri sana. Watu wameshaona wamekosa legitimacy ya utawala,hivyo wanajihalalisha kwa matabaka yatakayowasapoti hata ikitokea vita.

Madikteta wengi Africa walianguka kwa trend hiyo hiyo.Jichimbieni kaburi.
 
Dr. Bashiru aende akamuulize Marehemu Robert Mugabe, kuhusu wananchi wakimchoka mtawala hali huwa inakua vipi.

CCM wanajidanganya sana, halafu huwa wanajisahaulisha kwamba ipo siku raia wataamua la kuamua.
CCM ya Tanzania ni wajanja, wanabadilisha kiongozi kila baada ya miaka 5 ili kuepusha kuchokwa, tofauti na Zimbabwe ambapo mtawala mmoja alitawala kwa mda mrefu ktk chama kile kile.
 
Sasa kuna maana gani kupoteza kodi zetu kuwekeza kwenye uchaguzi? Kwa nini wasishtakiwe kwa ufisadi wa kodi za wananchi?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Tunapotezeana mda wa kupanga foleni kwa ajili ya kupiga kura wakati kuna chama kimejidhatiti bara bara kushinda uchaguzi kwa kutumia dola.
 
Kumbe Bashiru ni mpumbavu kiasi hiki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…