Dkt. Dorothy Gwajima: Kama unataka nitumbuliwe ili uchukue nafasi yangu, fanya kazi zaidi yangu sio ufitini

1. ACHENI KUIBA DAWA
2. ACHENI KUNYANYASA WAGONJWA
3. ACHENI KUSEMA UONGO
4. TOENI HUDUMA KWA KUFUATA MAADILI YA KAZI ZENU.
Hawataki kukosolewa wala kuguswa yani wao wawe kama walivyo wao ndio wao,kisa wanajiona ni watu muhimu wanatibu watu.
 
Wizara ya afya ni nyeti sana kama ilivyo ya ulinzi, inahitaji utulivu na umakini sana kuiongoza.

Huyu mama ana nia njema ila njia anayotumia ya kupayuka hadharani ndio mbovu.

Asipokuwa makini ataishia njiani.

Nyerere baada ya uhuru alimchagua Dereck N M Bryceson huyu hakuwa mwanasiasa na mambo yalienda vizuri tu, baadae tatizo lilianza pale Rais alipokuwa analazimisha wana sayansi kuingia katika siasa ili wawaongoze wenzao kwa ulaghai na sio kufuata ukweli wa uhalisia kama pale Chiduo alipochaguliwa utakuta akiwa ofisini alikuwa mwanasiasa na akiingia Muhimbili alibaki kuwa.doctor huku akimlamba kisogo mwajiri wake, kitu hii imedumu kwa muda mrefu lakini mara mojamoja watu kama Dorothy huteuliwa na kuchapa kazi kama mwajiri anavyotaka lakini kamwe huwa wanadharauliwa Sana na wenzao ambao wapo kwenye field na hiyo ni kawaida toka enzi na enzi na ndio sababu ya migomo baridi ya mara kwa mara ndani ya wizara hii
 
Hawataki kukosolewa wala kuguswa yani wao wawe kama walivyo wao ndio wao,kisa wanajiona ni watu muhimu wanatibu watu.
Tunatambua umuhimu wao, lakini nao wanapaswa kutambua umuhimu wetu, watuthamini kama binadamu wenzao, na wajue kuwa tunastahili kupata huduma bora za afya, siyo bora huduma za afya. Sisi tunaopewa huduma ndiyo tunaweza kutoa tathimini sahihi ya huduma zao.
 
Unangeea utopolo tu wew uanfikiri watu wananunua dawa mda wote kwamba hela ya kufanya hivyo ipo tu MDA wote
Ni sawa na kufungua bar halafu useme unadhani mwenyewe bar muda wote ana hela ya kuweka stock za bia (can you see how shallow your point is), besides ppl can audit their income to verify kama kweli hiyo hela hawana.

Halafu sidhani kama hospitali zinanunua dawa on cash wanapata credit kutoka bohari ya dawa.

Ni hivi si rahisi kumuongopea Dr Gwajima kama walivyozoea huko nyuma kuwaongopea mawaziri na maafisa wengine wa serikari ndio maana akawaambia yeye ni field Marshall kwenye hiyo wizara na mtaalamu wa health management. Kwani uongo si walionyesha wenyewe dawa zilipo baada ya kuwakagua kwa muda mfupi tu na ndio kilichopelekea kukasirika yaani wanataka kumuongopea ata yeye anaefahamu hiyo wizara kuanzia chini mpaka juu.

Mtu mwingine wanaweza mchezea siyo yeye.
 
"Mpaka Mheshimiwa akimaliza muda wake tutakuwa na vichaa wengi sana"

👣
 
Lugola nilimpenda sana alivyokataza tochi za matakoni...
 
Mtahangaika sana mwaka huu
Jirekebisheni watumishi wa Afya (baadhi)!
 
You have a point.
 
Hivi wanapitaga humu JF kweli waone wanavyokosolewa
 
Amesema kama unataka yeye atumbiliwe ili uchukue nafasi yake fanya kazi zaidi yake sio umfitini na kumtengenezea vijimaneno
Unataka kutuaminisha kwamba afanyayo ndiyo kazi ya Minister?Namna anavyowadhalilisha wanataaluma wenzie in front of cameras ndiyo supportive supervision?
 
Acha awadhalilishe, they are good for nothing...

Sekta ya afya ni mdororo, ilihitaji waziri who is in the mold of JPM, hard nosed, bullet headed, highly charged reformer.... she is just the right fit for the job..
 
Unahitaji zawadi kwa maneno ya hekima mkuu,mawazo pevu sana hayo,maisha yetu yako kwa mungu pekee lakini kupitia madaktar maisha na afya zetu vinaimarika,so kuwa na mabadiliko ya policies kwenye wizara ya afya ni jambo busara sana,kwa watumishi na wahitaji wa huduma za afya.
 
Unatia huruma kamachujui kitu Kaa kimya eti wanannunua kwa credit kutoka msd na msd tunanunua kwa credit kutoka kwa nini na ninani analipia hilo deni Kama serikali haipeleke pesa huko
 
Muda ni mwalimu mzuri sana.
Baada ya muda na matatizo kuzidi ndio utajua vizuri huyo mama ni kiazi kibovu kabisa.
Huwezi kuendesha wizara ya Afya kwa kufoka foka na kupayuka kama anavyofanya huyu mama. Ujuaji, mikwara na mipasho haviwezi kutatua matatizo katika sekta ya afya.
 
Huyu mama kila nikiona clip yake kwenye social media huwa nai Skip haraka nisiingalie..
Mana anatia aibu sana, yan mtu professional kabisa kweny taaluma ya Afya unaongea porojo porojo tu.
Porojo wakt ukweli mnatka mpige tu nyie

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Kwenye baa hagawi bia bure anahakikisha kila anayekunywa analipia ili zikiisha spate hela ya kumliapa mhudum umeme na gharama za bia yenyewe sasa huko kwetu tukaambiwa tusicharge chochote kwa Akina mama mama watoe na Waze ambao kimsingo wanaweza 80 ya mahudhurio yote ya hospitali na vituo vyote vya afya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…