Kanzastone
JF-Expert Member
- Jan 14, 2021
- 244
- 357
Kiongozi unatakiwa uwe msikilizaji sana kuliko kuwa muongeaji sana, nafikili hili liko tofauti kwa Dr. Dorothy GwajimaKwa style ile ya uongozi asitegemee Output nzuri hata kidogo mana hata ethics za kiungozi zaidi ya mihemko ni hatari kwa sisi wananchi kuwa na waziri kama huyo its a big shame
MSD hela za dawa wanapewa na serikali sehemu kubwa ya budget ni hela za walipa kodi wewe ndio hujui.Unatia huruma kamachujui kitu Kaa kimya eti wanannunua kwa credit kutoka msd na msd tunanunua kwa credit kutoka kwa nini na ninani analipia hilo deni Kama serikali haipeleke pesa huko
Yaani hii mbaula imechoka kabla haijaanza kupandisha Kitonga. Amekaa kimipasho mipasho hadi kuwashikia kiuno wafanyakazi anao waongoza. Na ukimchunguza sana machoni wakati anafoka foka ana dalili zote za kustahili kuwa na faili pale Mirembe.Wakuu habari za mchana.
Naomba walio karibu na huyu mama waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na watoto, wampe semina ya ku-behave kama top government official. Naona hilo linamshinda. Mama atulize ubongo aje na solutions. Aache majungu na malalamiko kila kukicha.
Hizi clip tunazoziona hazimpi heshima kabisa. Anajiita Field Marshall wa wizara lkn mimi namuona bado sana.
Kama ana vinyongo na maumivu ya huko nyuma, asahau. Ajulishwe majukumu yake kama waziri. Aache kuleta viswahili kama vya vijiwe vya kina mama wakiwa peke yao.
"Sizani" mwalimu gani wa shule ipi alikufundisha utumbo huu?! Sidhani√Huyo mama ni remix ya kangi lugola.
Sizani kama atamaliza miaka miwili kwenye hiyo wizara.
Jiandae kutumbuliwaNaunga hoja Mkono !!
Ummy aliacha madudu wizaraniMtahangaika sana mwaka huu
Jirekebisheni watumishi wa Afya (baadhi)!
Jana au juzi Bashe huko kwao kakuta mradi wa billioni mbili wa unwagiliaji ambao ushatengenezwa kwa lengo la kusambaza maji kwa hector 2000 unatumiwa na mkulima wa hector 2 mbili tu tangia ukamilike miaka 3 nyuma.Muda ni mwalimu mzuri sana.
Baada ya muda na matatizo kuzidi ndio utajua vizuri huyo mama ni kiazi kibovu kabisa.
Huwezi kuendesha wizara ya Afya kwa kufoka foka na kupayuka kama anavyofanya huyu mama. Ujuaji, mikwara na mipasho haviwezi kutatua matatizo katika sekta ya afya.
Huyu mama system yote ya afya anaijua
Acha awanyooshe....
Hvi watanzania wanataka nini????
Ova
Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
Chizi nini? unyeti wake uko wapi? Kwenye kuiba madawa na kuyauza kwenye maduka binafsi. Acha awape kibano!Wizara ya afya ni nyeti sana kama ilivyo ya ulinzi, inahitaji utulivu na umakini sana kuiongoza.
Huyu mama ana nia njema ila njia anayotumia ya kupayuka hadharani ndio mbovu.
Asipokuwa makini ataishia njiani.
Dorothy Gwajima ni pure mental case...precise mirror of the appointing authority!Tahadhima kwenu wajumbe wa bodi huru!
KWA muda sasa nimekuwa nikimfuatilia kwa karibu Waziri huyu toka alipoteuliwa na Rais Magufuli kuwa Waziri wa Afya. Namzungumzia Dk. Dorothy Gwajima.
Kila ofisi zilizochini yake anapoingia huwadhalilisha sana madaktari wenzake. Dk. Gwajima anamtazama kila mtu kuwa ni mwizi na kujitapa kuwa hakuna anayejua kila kitu katika wizara hiyo kama yeye.
"Hivi mnajua mimi ni Field Marshal wa sekta ya afya?" anawafokea madaktari Bingwa zaidi yake na kuongeza, "kama ningekuwa Mwanasheria mngenidanganya sana" kuonesha kuwa mtangulizi wake Mwanasheria, Ummy Mwalimu alikuwa akidanganywa sana. Huku ni kumdharau Waziri mwenzie aliyeaminiwa na Rais Magufuli.
Lakini hata "body language" ya mama huyu inaonesha kuhemka mno kiasi Cha kufanana na kina mama "ndala ndefu" wa huko Tandale wanaochambana bombani huku ameshika kiuno.
Cha ajabu, kama alivyowahi kufanya Dk. Hamisi Kigwangala "mzee wa kukurupuka" naye kila anapotaka kuwadhalilisha wahudumu wa sekta hiyo ni lazima awe mbele ya kamera ili aonekane. Huyu mama ameenda mbali kiasi Cha kutorokwa hata na haiba na staha ya mwanamke wa Kitanzania mbele ya wanaume.
"Field Marshal" ni cheo Cha juu na Cha mwisho jeshini. Hivi, Dk. Gwajima anadhani ni Bingwa wa afya kuliko maprofesa wote wa tiba nchini? Kwani kuongoza ni lazima kudhalilisha wenzako hadharani?
Wakati yule "mkata viuno" aliyetembea na Ilani ya CCM akijiita "ninja" huyu kaja na skafu ya bendera akijiita "Field Marshal". Mwendo uleule wa kukurupuka na kujipendekeza.
My Take: Napendekeza madaktari wafuatilie faili lake la matibabu anakotibiwa kuona anasumbuliwa na ugonjwa gani? Yapo baadhi ya magonjwa ambayo humfanya mtu ku-react ukichaa kama mama huyu.
Lakini pia wadadisi wachunguze mahusiano yake ya ndoa. Je, ana familia au ni mtalikiwa? Maana mahusiano ya ndoa na familia yakiwa salama pia huleta utulivu katika uongozi wenye staha, hekima, busara na maarifa. Huwezi kukufanya kuwa wizara hiyo imeoza kiasi kwamba waliopita kabla yake hawakufanya chochote. By the way, si tunaambiwa utawala wa Magufuli umeondoa ufisadi na uzembe kazini?
Nawasilisha.
Pure Mental Case😂
Ni kweli kila anapopita Waziri anakutana na madudu yanayofanywa na watendaji wake, kuongea au kukaa kimya na kwenda kuyafanyia kazi ni hulka ya mtu, lakini pia kama kiongozi kuwaambia watendaji ukweli wa anachokijua haswa pale wanapomdanganya ni sawa.
Na kwa mambo anayokutana nayo waziri ni wazi kuwa wizara imekosa controls; ni kama vile hakuna process flows sahihi na manuals.... kitu kinachotoa mwanya kwa watendaji kufanya ubadhirifu wa mali na muda. Na kama zipo basi zina gap au hakuna monitoring
Ni bahati kwamba Waziri ni mtaalam wa sekta anayosimamia na naamini atakapokaa chini na wasaidizi wake akafanya review atakuja na suluhu
Maendeleo hayana vyama kolola 😍😍
Umeandika kitu usichokifahamu kabisa.Sekta ya Afya ni Sekta nyeti sana na in Sekta ambayo Serikali na wafadhili mbalimbali wamekua wakinwaga mifedha mingi ajabu ni Fedha nyingi sana zimepigwa na viongozi wa Sekta hiyo yani ma DMO na MaDED... Ukieenda saivi ktk hospital za Serikali yan Vituo vya Afya,Zahanati na Hospital za Wilaya huwezi amini HAKUNA MADAWA zaidi ya Diclopa,Aluu na Dawa za kuharisha... ma Dr wengi wameiba sana hadi kufungua Dispensary zao na Pharmacy zao... Dr Gwajima amekua Tamisemi upande wa Afya anaijua fika Sekta hii... Tusimkatishe Tamaa aendelee kutumbua plus kuwafokea maana wameiba vyakutosha
Watu wa sekta ya ndio wengi wao wanaomchukia yule mama kwa kuwasimanga,lakini kiukweli awanyooshe tu wamezidi wizi,majivuno na uzembe,wanyooshwe tuMbona hata Jaffo hajarelax kwenye wizara yake lakini hajaanzishiwa mada?
Mabadiliko ni kitu endelevu yalishaanza na yanaendelea. Uozo unaoungolea wewe ni upi?Habari za jioni Mama D, jana kuna thread wewe na mimi tulijadili kuhusu CCM Mpya ya mabadiliko.
Kwa ulichokiandika hapa ningependa kuuliza, tuanze kuhesabu mabadiliko kuanzia lini?
Maana inaonekana miaka mitano iliyopita haijaweza kufuta uozo kwenye sekta ya afya, tena kwa anayoyaibua huyu waziri wa sasa unaweza kusema ndiyo uozo uliongezeka zaidi.
Haya tupe kiasi cha hela ilypelekwa msd ili vituo vipate dawa kwa mwaka 2019 /20 , ukiona kituo kina dawa baadhi kimejitutumua kikanunua kwa kuitumia mapato yao ya ndani kwa kadiri inavyoweikana hii ni kwa level ya hospitali tu .kwa zahanati sio rahis maana mapato yao ni kidogo sana maana huduma zao ni karibia na bureMSD hela za dawa wanapewa na serikali sehemu kubwa ya budget ni hela za walipa kodi wewe ndio hujui.
Ni hivi ubabaishaji basi tena kwenye hiyo wizara, ngoja nikupe mtririko ambao angeufanya.
Kungekuwa hakuna dawa angekaguwa mapato yao ata kama kweli wananua cash.
Huko nyuma keshasema pharmacy za hospitali zinatakiwa kuboresha inventory control maana yake nini wana historical data za kujua usage ya stock zao za dawa mbali mbali, ivyo wanajukumu la ku-toa order za dawa kutoka MSD in time kwa kuzitangia stock movements and lead time ya kuanzia unapo order mpaka dawa inapofika; ni marufuku hospitali kukosa dawa kama MSD zipo.
Ina maana kama dawa zingekuwa hakuna kweli mziki uliokuwa unafuata wa uzembe and incompetent.
Wewe ndio huna unachokijua unadhani ana bahatisha she knows her stuff, kuwa M.D aina maana unaufahamu wa health management pia like her.
Kwani kama kuna tatizo kama la dawa kuibiwa mpaka apige kelele mbele ya camera?Jibuni hoja acha nalalamiko yaliyojaa kashfa.
Mimi namfuatilia na yupo sahihi. Dawa zinaibiwa sana.
CHAPA KAZI BIBIE. MPAKA TUJUE DAWA ZINAENDA WAPI...
Mabadiliko ni kitu endelevu yalishaanza na yanaendelea. Uozo unaoungolea wewe ni upi?