Dkt. Dorothy Gwajima: Kama unataka nitumbuliwe ili uchukue nafasi yangu, fanya kazi zaidi yangu sio ufitini

Kwa style ile ya uongozi asitegemee Output nzuri hata kidogo mana hata ethics za kiungozi zaidi ya mihemko ni hatari kwa sisi wananchi kuwa na waziri kama huyo its a big shame
Kiongozi unatakiwa uwe msikilizaji sana kuliko kuwa muongeaji sana, nafikili hili liko tofauti kwa Dr. Dorothy Gwajima
 
Unatia huruma kamachujui kitu Kaa kimya eti wanannunua kwa credit kutoka msd na msd tunanunua kwa credit kutoka kwa nini na ninani analipia hilo deni Kama serikali haipeleke pesa huko
MSD hela za dawa wanapewa na serikali sehemu kubwa ya budget ni hela za walipa kodi wewe ndio hujui.

Ni hivi ubabaishaji basi tena kwenye hiyo wizara, ngoja nikupe mtririko ambao angeufanya.

Kungekuwa hakuna dawa angekaguwa mapato yao ata kama kweli wananua cash.

Huko nyuma keshasema pharmacy za hospitali zinatakiwa kuboresha inventory control maana yake nini wana historical data za kujua usage ya stock zao za dawa mbali mbali, ivyo wanajukumu la ku-toa order za dawa kutoka MSD in time kwa kuzitangia stock movements and lead time ya kuanzia unapo order mpaka dawa inapofika; ni marufuku hospitali kukosa dawa kama MSD zipo.

Ina maana kama dawa zingekuwa hakuna kweli mziki uliokuwa unafuata wa uzembe and incompetent.

Wewe ndio huna unachokijua unadhani ana bahatisha she knows her stuff, kuwa M.D aina maana unaufahamu wa health management pia like her.
 
Yaani hii mbaula imechoka kabla haijaanza kupandisha Kitonga. Amekaa kimipasho mipasho hadi kuwashikia kiuno wafanyakazi anao waongoza. Na ukimchunguza sana machoni wakati anafoka foka ana dalili zote za kustahili kuwa na faili pale Mirembe.
 
Jana au juzi Bashe huko kwao kakuta mradi wa billioni mbili wa unwagiliaji ambao ushatengenezwa kwa lengo la kusambaza maji kwa hector 2000 unatumiwa na mkulima wa hector 2 mbili tu tangia ukamilike miaka 3 nyuma.

Watu walishajimegea mashamba huko mpaka ya hector 700 na wala hawana interest za kulima. Hiyo ndio serikali mliyoizoea Bashe alitumbua watu palepale muda wa nonsense umepita.

Huo ndio kama ouzo wa wizara ya afya pia tofauti yake ni technical kuelewa anachofanya kwenye trouble shooting kwa wengi.

Mfano uwezi kuwa na kitengo cha macho kina mtaalamu, ana ofisi, anapokea mshahara halafu miaka miwili akifanyi kazi kisa mashine ya millioni tano imearibika. Ndio mambo mnayotaka hayo.
 
Kwingine anasifiwa kwingine anapondwa.........!

Mitano Teena
 
Wizara ya afya ni nyeti sana kama ilivyo ya ulinzi, inahitaji utulivu na umakini sana kuiongoza.

Huyu mama ana nia njema ila njia anayotumia ya kupayuka hadharani ndio mbovu.

Asipokuwa makini ataishia njiani.
Chizi nini? unyeti wake uko wapi? Kwenye kuiba madawa na kuyauza kwenye maduka binafsi. Acha awape kibano!
 
Dorothy Gwajima ni pure mental case...precise mirror of the appointing authority!
 

Habari za jioni Mama D, jana kuna thread wewe na mimi tulijadili kuhusu CCM Mpya ya mabadiliko.

Kwa ulichokiandika hapa ningependa kuuliza, tuanze kuhesabu mabadiliko kuanzia lini?

Maana inaonekana miaka mitano iliyopita haijaweza kufuta uozo kwenye sekta ya afya, tena kwa anayoyaibua huyu waziri wa sasa unaweza kusema ndiyo uozo uliongezeka zaidi.
 
Umeandika kitu usichokifahamu kabisa.
Nani alikuambia kuna pesa za Afya za kutosha zimepelekwa huko kwenye Halmashauri?
Hivi kuna halmashauri yoyote ina dawa muhimu za kutosha kwa sasa?
Yaani halmashauri zote nchini ziibe dawa za serikali zilizopelekwa?
Yaani DED aibe dawa!

Kuijua mifumo ya sekta ya afya ni jambo moja, na kuongoza wizara ya afya ni jambo lingine tofauti kabisa. Mama Gwajima hafai kuwa waziri wa Afya. She is too local, primitive and unprofessional. Mpayukaji tu.
 
Mbona hata Jaffo hajarelax kwenye wizara yake lakini hajaanzishiwa mada?
Watu wa sekta ya ndio wengi wao wanaomchukia yule mama kwa kuwasimanga,lakini kiukweli awanyooshe tu wamezidi wizi,majivuno na uzembe,wanyooshwe tu
 
Mabadiliko ni kitu endelevu yalishaanza na yanaendelea. Uozo unaoungolea wewe ni upi?
 
Haya tupe kiasi cha hela ilypelekwa msd ili vituo vipate dawa kwa mwaka 2019 /20 , ukiona kituo kina dawa baadhi kimejitutumua kikanunua kwa kuitumia mapato yao ya ndani kwa kadiri inavyoweikana hii ni kwa level ya hospitali tu .kwa zahanati sio rahis maana mapato yao ni kidogo sana maana huduma zao ni karibia na bure
 
Jibuni hoja acha nalalamiko yaliyojaa kashfa.
Mimi namfuatilia na yupo sahihi. Dawa zinaibiwa sana.

CHAPA KAZI BIBIE. MPAKA TUJUE DAWA ZINAENDA WAPI...
Kwani kama kuna tatizo kama la dawa kuibiwa mpaka apige kelele mbele ya camera?
Kwani hiyo ndo itazuia wizi au anajitafutia tu umaarufu?

Sent from my vivo 1904 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…