Dkt. Gwajima: Tukatae utapeli, Binti aliyedai anaishi na nyoka akiri haikuwa kweli

Dkt. Gwajima: Tukatae utapeli, Binti aliyedai anaishi na nyoka akiri haikuwa kweli

BINTI ALIYEDAI ANAISHI NA NYOKA AJISALIMISHA KWA WAZIRI DKT. GWAJIMA

Aomba radhi, adai hajawahi kufanya hivyo alidanganya.

DAR ES SALAAM.

Itakumbukwa hivi karibuni ilienea video mitandaoni kupitia televisheni ya MBENGO TV ikionesha Binti mmoja aliyekuwa amebeba nyoka mkubwa huku akidai kwamba, hufanya naye mapenzi ili kupata fedha.

Kufuatia hali hiyo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Dkt. Gwajima , alichukua hatua ya kukemea kitendo hicho na kumtaka ajitokeze kuomba radhi kwa Umma na kuondoa taarifa hiyo mtandaoni kutokana na kukiuka maadili.

Baada ya mmiliki wa Mbengo TV, Tarzan Mustapha aliyeambatana na mtangazaji Lenny kuomba radhi Mei 11, 2024, walielekezwa kumtafuta binti huyo waliyemrekodi vinginevyo wachukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka sheria ya usajili wao kwa kushirikiana kupotosha jamii kwa habari za utapeli.

Leo 20 Mei, 2024 Binti huyo aitwaye Veronica Bernad Anton aliyekuwa amebeba nyoka huyo naye amejisalimisha kwa Waziri Dkt. Gwajima na kuomba radhi kama video inavyoonesha.

Waziri Dkt. Gwajima ameelekeza kutafutwa kwa mmiliki wa nyoka au ajitokeze mwenyewe kabla hatua za Serikali kumtafuta hazijaanza ambapo, itaongeza makosa yake ya kutotoa ushirikiano kwa Serikali.

Waziri Dkt. Gwajima ameiasa jamii ya wanahabari na wasanii kuachana na utapeli na mambo yote yanayochochea mmonyoko wa maadili maana akiwa Waziri mwenye dhamana na Jamii yenye makundi maalum hatafumbia macho uongo, utapeli na uovu huo.

MWISHO

NB; nawasihi wanajamii wote kuheshimu Sheria kwa maendeleo na ustawi wa jamii na kutunza maadili.

View attachment 2995537
View attachment 2995538
Mama hongera sana kwa hili.

Lakini nikukumbushe pia kuna huko makanisani hasa haya yasioeleweka ni ya dhehebu gani, umeona kilichofanywa na hao wa nyoka, basi kitu hicho hicho kinafanywa makanisani na wanaohusishwa kutoa shuhuda za uongo zinazofedhehesha ni wanawake na watoto.

Clips zipo nyingi sana mtandaoni. Naomba unapotoa warnings kwa hawa iweke general kwa wote wanaoutumia wanawake na watoto kufikisha shuhuda za uongo zinazodhalilisha.

Dkt. Gwajima D
 
Kazi nzuri muheshimiwa.

Japo na swali dogo nakunukuu

"Waziri Dkt. Gwajima ameelekeza kutafutwa kwa mmiliki wa nyoka au ajitokeze mwenyewe kabla hatua za Serikali kumtafuta hazijaanza ambapo, itaongeza makosa yake ya kutotoa ushirikiano kwa Serikali."


Muheshimiwa hivi ikitokea serikali haitoi ushirikiano kwa raia, je raia anatakiwa kufanya nini ama taratibu ipi inafanyika?

Pole na hongera kwa majukumu muheshimiwa

Serikali inashirikiana na raia wake kila siku ndio maana ipo nchini, isingekuwa inashirikiana na raia bas kusingekuwa na polisi, serikali za mtaa, mahakama n.k huenda hata ofisi zisingekuwepo
 
Huyo alitakiwa achapwe bakora tu

Ova
😂
Kwa hiyo nmahati miliki na mavazi hayo si Ndio? Vazi hili Dini flan vazi lile din flan Loh
Kwa hiyo nmahati miliki na mavazi hayo si Ndio? Vazi hili Dini flan vazi lile din flan Loh
Kwa hiyo nmahati miliki na mavazi hayo si Ndio? Vazi hili Dini flan vazi lile din flan Loh
Sasa unataka kusema hayo ni mavazi ya dini gani bro au unajizima data kwani makobadh huwa wanavaa waislam tupu lkn mbona wanaitwa wavaa kobadh?
 
Tena hizi online tv zinazoripoti habari za uzushi zinazidi kwa nyingi, TCRA wapo kimya tu. Upotoshaji mwingi unafanyika na hizi online tv ili wapate watazamaji wengi kwa makusudi ya kulipwa na Youtube.
Mitandao hii pia hutumiwa na wanasiasa wanaotafuta kiki,kwani huwa zinatoa taarifa zs upande mmoja wa habari inayombeba mtu aliyewapa wito,na hivyo kutoa habari za kumfurahisha,na kuwaaminisha Watanzania kuwa Kiongozi fulani ndio pekee anafanya kazi.
Na viongozi wanaopenda kiki kufanya kazi na vyombo hivi vya habari.
 
Usitake kunitowa jasho la meno bro ila ukweli unaujuwa asili ya vazi la baibui na mtandio ni la dini gani
Sasa Hapo yupo kanisani Au msikitini?
Kwanza sidhani hata kama ile interview yake ya upotoshaji kuwa analala na joka uliitazama alijitambulisha kuwa jina lake ni latifa kumbe ni veronica kwahiyo katafute wa kubishana nae bro sio mimi
 
Usipaniki dogo,ukute hata hayo majina sio yake.

Wewe una shida flan kichwani usikalili kwamba mavazi flan ni ya Dini flan umeelewa.

Sisi kanisani tunapiga suti,haaanishi mtu akivaa Suti ni mkristo Sawa.
 
Usipaniki dogo,ukute hata hayo majina sio yake.

Wewe una shida flan kichwani usikalili kwama mavazi flan ni ya Dini flan umeelewa.

Sisi kanisani tunapiga suti,haaanishi mtu alivaa Suti ni mkristo Sawa.
Mwenyeshida kichwani huwa hajioni😂 sasa hapa unazungumziwa ww kuvaa suti kanisani au ww ukitaka vaa hata singlend na boksa hizo ni shida zako hazinihusu😊 hapa anazungumziwa veronica aliyejiita latifa na akavaa uhusika wa latifa😂
 
Usipaniki dogo,ukute hata hayo majina sio yake.

Wewe una shida flan kichwani usikalili kwama mavazi flan ni ya Dini flan umeelewa.

Sisi kanisani tunapiga suti,haaanishi mtu alivaa Suti ni mkristo Sawa.
Kisha me siwezi kupanic kwa mambo ya kipumbavu ila ww mwanaume ulieshindwa kujishkilia na ukaja kunijibu kuwa mavazi tumejimilikisha utadhani nilikwambi mimi ni muislam😂ndio nikakujibu kuwa sio kujimilikisha ni tayari alijitambulisha kwa jina la kislam mpaka ubini ulikuwa wa kiislam kumbe ni mkristo sasa hapo kipi hujaelewa jombi
 
Usipaniki dogo,ukute hata hayo majina sio yake.

Wewe una shida flan kichwani usikalili kwama mavazi flan ni ya Dini flan umeelewa.

Sisi kanisani tunapiga suti,haaanishi mtu alivaa Suti ni mkristo Sawa.
Na kama mavazi hayo si ya waislam basi kama unawatoto wa kike kawanunulie hijab na mabaibui jpili muende zenu kanisani kama hawatokushangaa😂
 
Na yule anayejiita Dr. Sure wamwite atueleze pesa za Majini zinapatikanaje ili nasi tupate mchongo wa pesa bila jasho.
Yule ni tapeli na muongo na ni mganga wa kienyeji kama waganga wengine tu sawa na dokta mwaka kuuza dawa za nguvu za kiume halafu Mke kamkimbia na analalamika jamaa shughuli ya kichovu
 
BINTI ALIYEDAI ANAISHI NA NYOKA AJISALIMISHA KWA WAZIRI DKT. GWAJIMA

Aomba radhi, adai hajawahi kufanya hivyo alidanganya.

DAR ES SALAAM.

Itakumbukwa hivi karibuni ilienea video mitandaoni kupitia televisheni ya MBENGO TV ikionesha Binti mmoja aliyekuwa amebeba nyoka mkubwa huku akidai kwamba, hufanya naye mapenzi ili kupata fedha.

Kufuatia hali hiyo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Dkt. Gwajima , alichukua hatua ya kukemea kitendo hicho na kumtaka ajitokeze kuomba radhi kwa Umma na kuondoa taarifa hiyo mtandaoni kutokana na kukiuka maadili.

Baada ya mmiliki wa Mbengo TV, Tarzan Mustapha aliyeambatana na mtangazaji Lenny kuomba radhi Mei 11, 2024, walielekezwa kumtafuta binti huyo waliyemrekodi vinginevyo wachukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka sheria ya usajili wao kwa kushirikiana kupotosha jamii kwa habari za utapeli.

Leo 20 Mei, 2024 Binti huyo aitwaye Veronica Bernad Anton aliyekuwa amebeba nyoka huyo naye amejisalimisha kwa Waziri Dkt. Gwajima na kuomba radhi kama video inavyoonesha.

Waziri Dkt. Gwajima ameelekeza kutafutwa kwa mmiliki wa nyoka au ajitokeze mwenyewe kabla hatua za Serikali kumtafuta hazijaanza ambapo, itaongeza makosa yake ya kutotoa ushirikiano kwa Serikali.

Waziri Dkt. Gwajima ameiasa jamii ya wanahabari na wasanii kuachana na utapeli na mambo yote yanayochochea mmonyoko wa maadili maana akiwa Waziri mwenye dhamana na Jamii yenye makundi maalum hatafumbia macho uongo, utapeli na uovu huo.

MWISHO

NB; nawasihi wanajamii wote kuheshimu Sheria kwa maendeleo na ustawi wa jamii na kutunza maadili.

Pia soma: Epuka kusambaza maudhui yasiyo na maadili. Anayedai kumiliki nyoka na kushiriki naye tendo, ajisalimishe
View attachment 2995537
View attachment 2995538
Kuomba msamaha hakubadilishi ukweli au uhalisia wa jambo. Ni kwamba Serikali bila kuthibitisha au la inawalazimisha waombe radhi, kutokana na kutofautiana kimtazamo na waziri, wala sio Serikali. Wanaomba msamaha kumridhisha waziri!
 
Na yule anayejiita Dr. Sure wamwite atueleze pesa za Majini zinapatikanaje ili nasi tupate mchongo wa pesa bila jasho.
Yule mganga njaa kama mimi tu ila mie dalali ye mwenzangu tapeli kwa kivuli cha uislam,,, hana tofauti na manyaunyau, kamchape, lambalamba etc. Ikiwa huyu Veronica kakili utapeli wake basi ni zamu ya yule anaejiita dokta sule nae atuthibitishie hayo majini yanaletaje ela,, mpumbavu tu yule njaa zake zinafanya auchafue uislam..
 
Binti anaitwa Veronica Bernard Anton lakini amevaa kama bint wa kiislam yote hiyo kuchafua waislam waonekane wanapenda kujishirikisha na ushirikina😂 ila hii nchi inavichaa sanaa

Na wewe unajiita mscleopatra unaongea kama muislamu ili ionekane ni Mkristo usiye na akili. Kuna mavazi ya kiislam kweli duniani? Una elimu gani?
 
Back
Top Bottom