Dkt. Harrison Mwakyembe ajilipua suala la Ushoga; Kukabidhi jina la Mwenyekiti wao kitaifa na mikoa kwa Serikali

Dkt. Harrison Mwakyembe ajilipua suala la Ushoga; Kukabidhi jina la Mwenyekiti wao kitaifa na mikoa kwa Serikali

Hakuna,yule kwa kwa mdee alienda kumchunguza kama ni msagaji ama ala.Sema ndo hivyo ilibidi afanye practical. Alikuwa kazini Catherine.
Kwa hiyo akasagwa mazima na Mdee? Practical gani hiyo sasa?!🤣🤣
 
Shida inayokuja ni kwamba mashoga wapo sehemu zote za idara za serikali hata majeshini wapo yaani kwa kifupi nchi imechafuka na huu uchafu inasikitisha sana unaona soja anarendemka kama binti harafu utasikia choko huyo na wala hafukuzwi kazi badala yake anahamishwa kwenda sehemu kituo kingine baada ya pale kushtukiwa.
 
Wanadai mara oooh...Dada wa Watu kajichubua, mara oooh! Uchunguzi wao ni batili.

Mara oooh Waziri Mstaafu Mwakyembe alikuwa wapi kutoa hizi inshu alipokuwa madarakani, kila kitu kina taratibu zake kiuchunguzi na kiushahidi.

Mashoga yamechemka vibaya sana kujibu hoja na kukimbilia kumshambulia yeye binafsi Dr. Mwakyembe na Bi Catherine.
Basi kama taifa tuna safari refu sanaa kupambana na ushoga...machoko yameanza kujitokeza mapema tu..ni kama imepigwa tear gas kweny shimo la nguruwe mwitu...yametoka kwa speed haswa
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu hajatoka hadharani kukanusha taarifa iliyotolewa na Waziri wa zamani wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe kuhusu Wizara yake kutoa vibali kwa mashirika yanayoendesha ushonga nchini...
Kusema kweli hata Mimi sijamwelewa!! Au kwa sababu ni mwanamke hajui madhara ya ushoga kwa watoto maskini wa kitanzania? Ukimya unamaana nyingi
 
jamani tujadili content aliyotuletea jamvini hayo masuala ya kujichubua ni ya kwake binafsi. Je Ushoga ni hoja kweli ya kujadili kwamba tatizo limekuwa kubwa kiasi hiki ?
 
Basi kama taifa tuna safari refu sanaa kupambana na ushoga...machoko yameanza kujitokeza mapema tu..ni kama imepigwa tear gas kweny shimo la nguruwe mwitu...yametoka kwa speed haswa
ha ha ha, Mkuu kuna siku nilikuwa Tanga hotel moja siwezi kuitaja napata moja baridi moja moto huku napunga upepo baada ya kazi ya kutwa, mida ya saa 1 bend huku ikitumbuiza likaja Shoga eti linakaa na mimi, nikalitimua kwa maneno machafu... aiseee kilichonikuta ni balaaa...

Ilibidi nimwabie dereva tusepe zetu, hao jamaa wana mtandao ni balaa !! Kibaya zaidi nilitoa maneno ya kulikashifu huku nikitegemea ntasaidiwa na wanazengo waliokuwa pale, aiseee sikuamini.
 
Nilimsikiliza Mwakyembe wakati anatoa hoja kuhusu Ushoga na Usagaji.

Ni ukweli kuwa Ushoga na usagaji ni matendo machafu mbele ya jamii na mbele za mungu. Hilo halina ubishi labda uwe mwendawazimu.

Uwasilishaji wa Mwakyembe ulikuwa wa kisiasa zaidi kwa lengo la kupata umaarufu wa kisiasa (Cheap politics). Mwakyembe alikuwa waziri mwandamizi kwa miaka mingi.

Kitendo cha kuihusisha serikali na ushoga na usagaji na kuitolea shutuma nzito kuwa wizara ya afya ina engineer na kwamba kila kitu kinajulikana kwa miaka mingi tangu yeye akiwa waziri mwandamizi ni upotoshaji wa wazi wenye kutafuta umaarufu tu.

Mbona siku zote hizo mwekyembe alikuwa kimya huku akijua ushoga na usagaji ni jambo baya. Kwa nini hakuwahi kusema hata bungeni? au kujiuzuru uwaziri kuonyesha kuwa anapinga serikali ku support mashoga na wasagaji?

Kuituhumu Marekani kuwa inatuletea ushoga na kwamba hataki pesa za wamerekani na nchi zingine zilizo na sheria zinazolinda haki za mashoga na wasagaji ni kuichonganisha serikali yetu na marekani ili ku gain cheap politics.

Marekani na nchi zingine zinazotupa misaada (Grants) hawajawahi kutuwekea sharti la kukubali ushoga ndo watupatie misaada.

Kuanza siasa za kuituhumu marekali kuwa inatuletea ushoga bila hata ushahidi na kwenda mbali zaidi eti hatutaki hata pesa zao ni ulimbukeni na ujinga uliokithiri. Nitatoa mifano michache ili hoja yangu ieleweke vyema.

Marekani na nchi zingine ni washirika wetu wakubwa tena wanaotusaidia mambo makubwa kwa sekta muhimu inayogusa maisha ya watanzania wengi.

1. USA inafadhiri mifuko (Funding) lukuki kama Grants. Hatukopi ila tunapewa bure. Nitataja miwili tu mikubwa ambayo ni Global Fund na President's Emergency Plan for Aids Relief (PEPFAR) kupitia Centers for Disease Control and Prevention (CDC). Mifuko hii ina zaidi ya miaka 15 ipo hapa nchini na imenufaisha watanzania wengi kwenye miradi ya Afya kama Malaria, TB & Leprosy, HIV AIDS na mingine mingi.

2. Miradi niliyoitaja hapo juu watanzania wengi imewagusa mmoja mmoja. Kama nchi tunapata dawa za chanjo kutoka WHO kupitia mfuko wa Global Fund. Tunapata dawa wa kufubaza virusi vya ukimwi kwa vituo vyote Tanzania (CTC centers) kupitia mfuko wa PEPFAR, Tunapata dawa za malaria kupitia mfuko wa Global fund, tunapata Dawa za TB na Ukoma (Leprosy) kupitia Global Fund etc

3. Kuna mfuko mwingine unaitwa Health Basket Funding (HBF), pia hii ni Grant siyo mkopo ambao unachangiwa na World Bank na nchi zaidi ya 15 ikiwemo Canada, Denmark, Ireland, Switzerland, German etc. Bila hawa jamaa Health system ya Tanzania ingekuwa ime collapse. Hawa ndo wanatupa pesa za kununua dawa na vifaa kwa ajili ya hospital zetu nchi nzima. Huu mfuko ni mkombozi kwa watanzania kwa afya zetu.

4. Kama kweli nchi zote nilizozitaja hapo juu 1, 2 & 3 zote zina sheria zinazowalinda mashoga ikiwemo marekani. Mbona hakuna kigezo walichoweka cha kwamba lazima ukubali ushoga kama sharti la kupewa fedha zile ambazo tunazipata kila mwaka kwa zaidi ya miaka 15 sasa kama anavyodai Mwakyembe?

5. Ni ujinga wa kiwango cha juu kwa mtu ambaye amekuwa waziri tena mwandamizi kusema hadhalani eti hatutaki misaada ya marekani kwa sababu wana support ushoga huku akijua kuwa marekani na washirika wengine hawajawahi kutuwekea sharti la kutupa pesa ili tukubali ushoga. Hizo ni cheap politics za Mwakyembe.

Hitimisho
1. Ni ujinga kutafuta umaarufu wa kisiasa kwa mwamvuli wa ushoga. Mtu kama anaichukia marekani na washirika wengine kwa sababu zake basi aichukie kama yeye lakini siyo nchi. Marekani na nchi nilizozitaja zikikata Grants, Health system ya Tanzania ita collapse sababu ya wanasiasa wachache wanaotaka kuharibu mahusiano na nchi yetu na Marekani

2. Kama nchi tuangalie chanzo cha tatizo la ushoga na usagaji siyo kuhangaika na matokeo. Ushoga na usagaji ni matokeo tu, hao ni waathirika. Tuanze kuhangaika na mabasha na wasagaji siyo waathirika. Tuwekeze kuihamasisha jamii ichukie mabasha na tutunge sheria kali ya ku deal nao ili tukomeshe ushoga.

3. Kumwadhibu muathirika wa ushoga na usagaji ni uwendawazimu. Haina tofauti na kumwadhibu mtu anayevuta madawa ya kulevya ukamwacha muuza dawa za kulevya.
Bado hujahitimisha Mkuu. Unakubaliana na ushoga?
 
Bila hawa jamaa Health system ya Tanzania ingekuwa ime collapse. Hawa ndo wanatupa pesa za kununua dawa na vifaa kwa ajili ya hospital zetu nchi nzima.

Marekani na nchi nilizozitaja zikikata Grants, Health system ya Tanzania ita collapse

Okay, bila misaada yao sekta ya afya nchini inge collapse.

Kwa hiyo sasa hivi tunatibiwa bure kwa grants za wahisani ???

Na kama tunatibiwa bure Tanzania tunaumwa only TB, Malaria Ukoma na Ukimwi, na siku wakikata misaada healthcare system ita collapse na tutakufa wote na TB, Malaria, Ukimwi na Ukoma ???
 
Mimi ninasema kuwa MTU YEYOTE anayempinga Dr. Mwakyembe ni SHOGA

Mzee wa watu ameweka wazi kuwa Mashoga wana community na Organizations zao, wana wafadhili na akataja baadhi ya makampuni yanayosupport na kueneza Ushoga

Amesema Mashoga wana Mkurugenzi wao na wanapata support kubwa kutoka Marekani

AMEKOSEA WAPI?

Mara anatafuta kiki, Mara ana njaa na blah blah zingine


Si msubiri atangaze hiyo list ya hao Mashoga na Mkurugenzi wao?

Kwanini Mnaweweseka na Mnamjadili yeye badala ya hoja zake?

Au ninyi Mashoga ndio hamtaki Mkurugenzi wenu atajwe?
Hongera,umepigilia msumari
 
Nikipiga hesabu jinsi ambavyo hili swala la ushoga limetrend wakati huu hesabu zinakataa kabisa kukubali kuwa ni campaign ya kawaida. Hapana hapa kuna mtu ama/taasisi ametenga pesa ili kutu-keep busy na hii mada yenye ukakasi.

Sasa ni nani/ kina nani? sijui
Kwanini sasahivi? Sijui
Ana/ wanamalengo gani? Sijui
Dah!..umewaza vizuri mno....hii ni 'spinning' tu kwa ajili ya malengo fulani na Mwakyembe anatumika kufanikisha hiyo 'spinning'...
 
Okay, bila misaada yao sekta ya afya nchini inge collapse.

Kwa hiyo sasa hivi tunatibiwa bure kwa grants za wahisani...
Usichokijua ni kama usiku wa giza.

1. Sekta ya afya 60% ni pesa za Grants ambazo ndo zinatumika kununua dawa na vifaa tiba. Own sources plus Government Grant ni 40% ambayo inatumika ku finance sekta ya afya. Wakiacha kutoa hiyo misaada (Grants) sekta ya afya ina collapse.

2. Dawa unazopewa ukienda hospitali za serikali pamoja na DDH kwa asilimia kubwa zinatokana na mifuko niliyoieleza. User fees, NHIF na Grant kutoka serikali kuu ndo zinachangia hiyo 40%

3. Chanjo zina gharama kubwa sana. Nchi haina uwezo wa kununua chanjo za kutoshereza mahitaji ya nchi.

4. Dawa za TB, Leprosy na HIV zina gharama kubwa sana. Ndiyo maana tunapewa Grants through Global fund na PEPFAR.

Ushauri
Kama jambo hulijui bora ukae kimya na ujifunze kwa wengine kuliko kujifanya unajua kumbe uko mtupu kama uchi wa mbuzi.
 
Back
Top Bottom