Dkt. Hussein Mwinyi adai Mzee Mwinyi hakuagiza azikwe Mkuranga

Dkt. Hussein Mwinyi adai Mzee Mwinyi hakuagiza azikwe Mkuranga

Punguza emotions zako. Unalalamika nini mtu aliyekuwa mwanasiasa kufikiriwa kisiasa? siasa haifi kwenye misiba, Mwinyi atazungumzwa tu popote pale.

By the way, nani aliyekwambia Mzee Mwinyi anasemwa kwa ubaya? hebu wacha hisia zako potofu.

Kama sisi tusiofahamika na yeyote huko nje misiba yetu huwa haikosi maneno, ndio itakuwa msiba wa Mzee Mwinyi - Rais mstaafu?!

Nakwambia tena ondoa emotions zako kwenye hili jambo, wacha bongo za watu zifanye kazi yake.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Hakuna emotion hapa, ni logic tu.

If anything, wewe unayeleta stories za wosia ambao huwezi kuthibitisha upo ndiye unaleta emotions, huna factual argument, unakataza mtu kuzika baba yake anapotaka, kitu ambacho ni haki yake na familia yake, bila logic.

Sojalalamika mtu aliyekuwa mwanasiasa kusemwa kwa siasa.

Nalalamika mtu yeyote kusemwa kwa uongo.

Mnasema Mwinyi aliacha wosia kuzikwa Mkuranga, nimewataka kutoa ushahidi kwenye hilo mmeshindwa.

Haya mpaka sasa ni maneno ya uzushi tu.

Mnaungaunga vijineno tu, hamna hata aibu.
 
Dada yangu wa kajunjumele,punguza uhana harakati,Mambo ya mwinyi hayo ni ya familia yake,wao ndo wana wosia wa mzee wao,pambana na ya kwako
Kwa siasa hizi za kulazimisha watu wazike wapi baba zao, hawa wapinzani wataburuzwa sana tu.

Kina Mwinyi wana scandal kibao za kuongelea. Mwinyi baba na mtoto.

They are not scandal free.

Halafu wapinzani wanakwenda kuchagua sehemu ya kuzika kama ndiyo topic yao ya kuishambulia familia ya Mwinyi.

This tells me more about the opposition than about the Mwinyis.
 
Kwa siasa hizi za kulazimisha watu wazike wapi baba zao, hawa wapinzani wataburuzwa sana tu.

Kina Mwinyi wana scandal kibao za kuongelea. Mwinyi baba na mtoto.

They are not scandal free.

Halafu wapinzani wanakwenda kuchagua sehemu ya kuzika kama ndiyo topic yao ya kuishambulia familia ya Mwinyi.

This tells me more about the opposition than about the Mwinyis.
Mkuu kuna kosa gani sisi kuripoti alichosema Mtoto wa Marehemu ?
 
Mkuu kuna kosa gani sisi kuripoti alichosema Mtoto wa Marehemu ?
Hakuna kosa nyinyi kuripoti alichosema mtoto wa marehemu.

Lakini, mmesema ambacho hajaripoti mtoto wa marehemu wala marehemu.

Mmesema rais Ali Hassan Mwinyi kaacha wosia azikwe Mkuranga.

Nimewataka muweke ushahidi kwenye hilo, mmeshindwa. Hayo ni maneno ya uzushi tu.

Kama unabisha, weka ushahidi hapa kuwa haya maneno yalisemwa kweli na marehemu.

It is as simple as that unamaliza longolongo zote hapa.

Ukishindwa kuweka ushahidi wa kuthibitisha Ali Hassan Mwinyi akiacha wosia huo, unakuwa mzushi tu.

Huo uzushi ndio mimi naukataa.
 
Hakuna emotion hapa, ni logic tu.

If anything, wewe unayeleta stories za wosia ambao huwezi kuthibitisha upo ndiye unaleta emotions, huna factual argument, unakataza mtu kuzika baba yake anapotaka, kitu ambacho ni haki yake na familia yake, bila logic.

Sojalalamika mtu aliyekuwa mwanasiasa kusemwa kwa siasa.

Nalalamika mtu yeyote kusemwa kwa uongo.

Mnasema Mwinyi aliacha wosia kuzikwa Mkuranga, nimewataka kutoa ushahidi kwenye hilo mmeshindwa.

Haya mpaka sasa ni maneno ya uzushi tu.

Mnaungaunga vijineno tu, hamna hata aibu.
Bado una Emotion ,Punguza preasure

Tatizo lako unataka mawazo yako unayowaza ndio yawe mawazo ya wengine

Mara nyingi watu wasiojiamini kama wewe huwa wanakimbilia kulazimisha hoja moja yenye mapungufu na kuacha maana halisi ya mjadala

Hakuna logic unayotoa ,Hata Rais Mwinyi hajathibitisha wosia wa marehemu wala hajautoa kwa public ni maneno tu katamka kuwa baba yake hakusema azikwe Mkuranga,

Unalazimisha watu watoe wosia wakati mtu unayesema amejibu na yeye hajautoa wosia kwenye public

Kuna wakati uwe unaficha ujinga wako kiongozi kwenye mijadala

Kama ni uzushi hakuna wosia mbona unakubaliana na maneno ya Mwinyi bila wosia kuutoa
 
Wabongo wengi walio watu wa kuunga unga maneno kimajungu niliwauliza huo usia wa Mwinyi aliosema anataka kuzikwa Mkuranga mnaweza kuuthibitisha?

Walishindwa kujibu.
Nina mashaka na uwezo wako wa kuchanganua mambo

Yawezekana umesoma vitabu vingi sana mwisho wa siku umechanganyikiwa bila wewe mwenyewe kujifahamu

Kuna mprofesa wale zamani walisoma sana mwisho wa siku hawakujua hata duniani kina endelea kitu gani

Kichaa sio lazima aokote makopo,Jaribu kufanya self evaluation kwa kuwauliza watu wanakuonaje ?

Wewe mwenyewe huwezi kujiona "Wabongo wengi wana majungu" sijui kwa utafiti upi kuwa wabongo wana majungu?

Ni kichaa tu ndio anaweza kuona watu wanaohoji wana majungu

Hata kama wana majungu lakini si nchi yao na wanataka kufahamu juu ya gharama alizotumia kiongozi wao kuzikwa toka mkuranga mpaka zanzibar

Hao watu wa majungu unaosema wana uhalali wa kuhoji chochote kile juu ya viongozi wao kiwe hata tofauti na mawazo yako wewe

Usipende kulazimisha mawazo yako yaonekane sahihi hapa JF,Kila mtu ana mawazo yake ,Yanaweza kuwa kwako hayafai lakini kwa wengine ni sawa

Hii ni mijadala ,Kwenye mijadala lazima ushushe temper
 
Bado una Emotion ,Punguza preasure

Tatizo lako unataka mawazo yako unayowaza ndio yawe mawazo ya wengine

Mara nyingi watu wasiojiamini kama wewe huwa wanakimbilia kulazimisha hoja moja yenye mapungufu na kuacha maana halisi ya mjadala

Hakuna logic unayotoa ,Hata Rais Mwinyi hajathibitisha wosia wa marehemu wala hajautoa kwa public ni maneno tu katamka kuwa baba yake hakusema azikwe Mkuranga,

Unalazimisha watu watoe wosia wakati mtu unayesema amejibu na yeye hajautoa wosia kwenye public

Kuna wakati uwe unaficha ujinga wako kiongozi kwenye mijadala

Kama ni uzushi hakuna wosia mbona unakubaliana na maneno ya Mwinyi bila wosia kuutoa
Kujamba unajamba wewe, halafu unamlazimisha Hussein Mwinyi athibitishe hajajamba yeye.

How does one prove a negative?

Hussein Mwinyi hata akikuletea wosia wa baba yake, akakwambia wosia huu hapa, mzee hajasema azikwe Mkuranga, kitu gani kitakuzuia wewe usiseme huu si wenyewe, kuna wenyewe mwingine mmeuficha ambao kasema azikwe Mkuranga?

Unamlazimisha mtu aweke wosia wa baba yake, kitu ambacho kashakuambia ni private matter ya ndani ya familia yao, hadharani?

Kwa sababu tu wewe umetunga uongo kuhusu huo wosia?

Nakwambia hivi, nyie Watanzania wa hivi hawa watawala watawaburuza sana.

Kwa sababu mnajichanganya sana.

Huku mnataka uhuru, mnataka katiba mpya.

Huku mnashindwa hata kuelewa uhuru ni nini, mnashindwa kuiachia familia ya Mwinyi kumzika mzee wao kwa uhuru.

Hapo ndipo mnawapa hawa watawala msemo kwamba hamuelewi uhuru ni nini.

Kwa mwendo huu, I can guarantee you hiyo katiba mpya mtaisikia redioni tu.

Yani nyie watu msioelewa basic human right of dying and being buried with dignity ndio nyie nyie mnadai katiba mpya pia?
 
Nina mashaka na uwezo wako wa kuchanganua mambo

Yawezekana umesoma vitabu vingi sana mwisho wa siku umechanganyikiwa bila wewe mwenyewe kujifahamu

Kichaa sio lazima aokote makopo,Jaribu kufanya self evaluation kwa kuwauliza watu wanakuonaje ?

Wewe mwenyewe huwezi kujiona "Wabongo wengi wana majungu" sijui kwa utafiti upi kuwa wabongo wana majungu?

Ni kichaa tu ndio anaweza kuona watu wanaohoji wana majungu

Hata kama wana majungu lakini si nchi yao na wanataka kufahamu juu ya gharama alizotumia kiongozi wao kuzikwa toka mkuranga mpaka zanzibar
Wabongo wengi wanapemda majungu hata kwa kuangalia mazungumzo ya hapa JF.

Mwinyi baba na Mwinyi mtoto, marais wote wawili wana scandals kibao ziko wazi, hazihitaji majungu kuziongelea, lakini watu kwa uvivu wanachagua majungu. Wanaona hii ndiyo habari muhimu kabisa ya kuwakosoa kina Mwinyi. Majungu.Ndiyo utamaduni wao.

Huu mjadala si wa gharama, usihamishe magoli. Huu mjadala ni kwamba rais Mwinyi aliweka wosia azikwe Mkuranga lakini hajazikwa huko kazikwa Zanzibar kwa sababu za kisiasa.

Wosia huo unaosemwa ni maneno ya majungu, uzushi tu.

Na wewe mwenyewe unakubali kutetea uzushi kwa kusema "hata kama majungu".

Umeshayapitisha majungu kama kitu ambacho kinafaa kujadiliwa.

Unathibitisha kauli yangu kwamba wabongo wengi wanapenda majungu.
 
Ko kote ambako Hayati Mwinyi angezikwa bado ni Tanzania! Zanzibar na Mkuranga ziko ndani ya JMT ingawa Zanzibar ni nchi na Mkuranga iko ndani ya nchi ya Tanganyika!
Mzee Ruksa amemaliza mwendo,Familia yake isibughudhiwe! Kazi iendelee kwa Jina la JMT.
 
Ko kote ambako Hayati Mwinyi angezikwa bado ni Tanzania! Zanzibar na Mkuranga ziko ndani ya JMT ingawa Zanzibar ni nchi na Mkuranga iko ndani ya nchi ya Tanganyika!
Mzee Ruksa amemaliza mwendo,Familia yake isibughudhiwe! Kazi iendelee kwa Jina la JMT.
Mkuu,

Kwani unafikiri hawajui hayo? Unafikiri tatizo ni alipozikwa Mwinyi?

Alipozikwa Mwinyi si tatizo. Kina Mwinyi walishaamua kuzikwa Zanzibar. Alifariki Hassan Mwinyi, mtoto wa piki wa Ali Hassan mwinyi, mwaka 2022. Alizikwa Zanzibar.

Tatizo hapa kuna siasa za majitaka tu, watu wanaleta figisufigisu tu. Ili mradi watibue mambo tu.

Majungu, uzushi, siasa za majitaka.

Mpaka msibani.
 
Kujamba unajamba wewe, halafu unamlazimisha Mwinyi athibitishe hajajamba yeye.

Unamlazimisha mtu aweke wosia wa baba yake, kitu ambacho kashakuambia ni private matter ya ndani ya familia yao, hadharani?

Kwa sababu tu wewe umetunga uongo kuhusu huo wosia?

Nakwambia hivi, nyie Watanzania wa hivi hawa watawala watawaburuza sana.

Kwa sababu mnajichanganya sana.

Huku mnataka uhuru, mnataka katiba mpya.

Huku mnashindwa hata kuelewa uhuru ni nini, mnashindwa kuiachia familia ya Mwinyi kumzika mzee wao kwa uhuru.

Hapo ndipo mnawapa hawa watawala msemo kwamba hamuelewi uhuru ni nini.

Kwa mwendo huu, I can guarantee you hiyo katiba mpya mtaisikia redioni tu.

Yani nyie watu msioelewa basic human right of dying and being buried with dignity ndio nyie nyie mnadai katiba mpya pia?
Tanzania ni nchi yetu na tunaipenda sana sana

Watu tumeishi ulaya lakini nyumbani ni nyumbani tu.Hapa JF kuna watu wengi nimeishi nao ufaransa wao wakiwa watu wazima na bado wapo huko lakini wanakuambia watarudi nyumbani na wataishi hapa Tanzania

Wahindi ni matajiri sana na wana majumba canada lakini wanaipenda Tanzania na tunaishi nao hapa


Hakuna anayeburuzwa Tanzania wala kubaguliwa hapa Tanzania kama nje,Ulaya ndio kuna kuburuzwa vibaya sana ,Kuna sheria kali ambazo ukiweka hapa Tanzania hakuna atakayezifuata kwani zinaondoa uhuru wa watu

Huko ulaya watu wanabaguliwa sana sijawahi kuona kwenye maisha yangu

Mimi niliyeishi ufaransa nikiwa mtoto wa college huwezi nirudisha kuishi ufaransa,Unabaguliwa kuanzia darasani mpaka kwenye kupanga apartment tu ilikuwa shida kisa rangi yangu watu wakiona black sipangishi mpaka nawatumia baadhi wazungu wastaarabu

Marekani kwenyewe ambako nimeenda nikiwa mtu mzima kwenye mambo ya kamati za bunge ni hovyo kabisa,Na ni nchi yenye watu weusi kibao zaidi ya ufaransa lakini unakuta jitu jeusi tii kama mkaa bado linakubagua mtu toka Afrika ambao kwa Tanzania sisi wengi sio weusi sana kama wasudan

Kuna kumbi za muziki wakati huo unafika mlangoni ufaransa ,Unakuta mzungu mlangoni anatukatalia watu black

Upweke uliopo ulaya na hata Marekani ndio maana watu wengi wakirudi wanaonekana kama vichaa kichwani

Bora kuendelea kuburuzwa nyumbani lakini sio kuwa mtumwa kwenye Taifa la watu ambalo hata haki ya kuongoza nakosa

Kama ulienda ulaya ukiwa mtu mzima kutafuta maisha najua utakuwa unayavumilia niliyoyaishi mimi miaka hiyo

Hapa Tanzania tuna sheria lakini hazibagui sana wageni isipokuwa kwenye mambo ya ardhi na uongozi wa kisiasa,Huko kuna sheria mpaka za kumlinda paka na mbwa na wengine mpaka kugeuza mbwa na paka kuwa wapenzi wao kimahaba

Kwa sasa najua huko ufaransa sijaenda kitambo nadhani kutakuwa na ndoa za Paka kuolewa na binadamu au Mbwa kufunga ndoa na binadamu
 
Tanzania ni nchi yetu na tunaipenda sana sana

Watu tumeishi ulaya lakini nyumbani ni nyumbani tu.Hapa JF kuna watu wengi nimeishi nao ufaransa wao wakiwa watu wazima na bado wapo huko lakini wanakuambia watarudi nyumbani na wataishi hapa Tanzania

Wahindi ni matajiri sana na wana majumba canada lakini wanaipenda Tanzania na tunaishi nao hapa


Hakuna anayeburuzwa Tanzania wala kubaguliwa hapa Tanzania kama nje,Ulaya ndio kuna kuburuzwa vibaya sana ,Kuna sheria kali ambazo ukiweka hapa Tanzania hakuna atakayezifuata kwani zinaondoa uhuru wa watu

Huko ulaya watu wanabaguliwa sana sijawahi kuona kwenye maisha yangu

Mimi niliyeishi ufaransa nikiwa mtoto wa college huwezi nirudisha kuishi ufaransa,Unabaguliwa kuanzia darasani mpaka kwenye kupanga apartment tu ilikuwa shida kisa rangi yangu watu wakiona black sipangishi mpaka nawatumia baadhi wazungu wastaarabu

Marekani kwenyewe ambako nimeenda nikiwa mtu mzima kwenye mambo ya kamati za bunge ni hovyo kabisa,Na ni nchi yenye watu weusi kibao zaidi ya ufaransa lakini unakuta jitu jeusi tii kama mkaa bado linakubagua mtu toka Afrika ambao kwa Tanzania sisi wengi sio weusi sana kama wasudan

Kuna kumbi za muziki wakati huo unafika mlangoni ufaransa ,Unakuta mzungu mlangoni anatukatalia watu black

Upweke uliopo ulaya na hata Marekani ndio maana watu wengi wakirudi wanaonekana kama vichaa kichwani

Bora kuendelea kuburuzwa nyumbani lakini sio kuwa mtumwa kwenye Taifa la watu ambalo hata haki ya kuongoza nakosa

Kama ulienda ulaya ukiwa mtu mzima kutafuta maisha najua utakuwa unayavumilia niliyoyaishi mimi miaka hiyo
Totally off topic. Nimeku trigger kwa kusema wabongo wanapenda majungu.

Na wewe unathibitisha hilo kwa kutoweza kukaa kwenye mada na kuleta majungu.

Mada ni kwamba Mzee Mwinyi aliacha wosia kuwa azikwe Mkuranga, akazikwa Zanzibar kisiasa.

Thibitisha hilo.

Hayo mengine ni maneno off topic, logical non sequitur, arguments from misplaced patriotism, sina hata muda wa ku ya entertain.
 
Swali ni je Mwinyi ni kabila gani?
Kabila lolote ambalo atakuwa Mwinyi, kama ni Mtanzania, ana haki ya kuzikwa sehemu yoyote ya Tanzania bila kunyanyapaliwa.

Hapa swali la muhimu ni, Mwinyi alikuwa ni raia wa nchi gani?

"Karne hii bado tunaongelea makabila?" - JK Nyerere.
 
Totally off topic. Nimeku trigger kwa kusema wabongo wanapenda majungu.

Na wewe unathibitisha hilo kwa kutoweza kukaa kwenye mada na kuleta majungu.

Mada ni kwamba Mzee Mwinyi aliacha wosia kuwa azikwe Mkuranga, akazikwa Zanzibar kisiasa.

Thibitisha hilo.

Hayo mengine ni maneno off topic, logical non sequitur, arguments from misplaced patriotism, sina hata muda wa ku ya entertain.
Unaandika mambo mengi hueleweki

Jaribu kuandika kwa ufupi(Summarize mawazo yako)
 
Unaandika mambo mengi hueleweki

Jaribu kuandika kwa ufupi
Yani wewe uliyelundika mambo kibao off topic ya sijui umekaa Ufaransa na Marekani ndiye wa kunisema mimi naandika mambo mengi sieleweki?

You are out of your mind. You are projecting your tendencies towards me. This is textbook psychological projection.

Unataka niandike kwa ufupi?

Toa uthibitisho kwamba Ali Hassan Mwinyi aliacha wosia azikwe Mkuranga.

Ukitoa uthibitisho huo unemaliza mjadala.

Ukishindwa unashabikia uzushi tu. Maana hii hoja yote imeanzia hapo.
 
Kabila lolote ambalo atakuwa Mwinyi, kama ni Mtanzania, ana haki ya kuzikwa sehemu yoyote ya Tanzania bila kunyanyapaliwa.

Hapa swali la muhimu ni, Mwinyi alikuwa ni raia wa nchi gani?

"Karne hii bado tunaongelea makabila?" - JK Nyerere.
Zanzibar wana katiba yao ambayo haiwatambui watu wa Tanganyika kama ndugu zao

Mwinyi sio mnzazbar ni mtanganyika wa mkuranga

Mtu wa Tanganyika haruhusiwi kumiliki ardhi zanzibar lakini wanzazibar wanaruhusiwa huku Tanganyika

Mnzazbar anaruhusiwa kugombea uongozi Sehemu yeyote ile Tanzania lakini sisi Tanganyika ni Tanganyika tu
 
Back
Top Bottom