Dkt. Kahyoza: Magufuli alifanya makosa makubwa kuhamishia Serikali Dodoma, gharama zimekuwa mara mbili

Dkt. Kahyoza: Magufuli alifanya makosa makubwa kuhamishia Serikali Dodoma, gharama zimekuwa mara mbili

Nipe sababu moja tu ya maana ya kulazimisha kuhamisha makao makuu ya nchi baada ya kushindwa kutekelezwa kwa miaka zaidi ya 40 yaani umuhimu wake mkubwa hasa ni nini?
Itoshe kukuambia kuwa, mtu akiwa timamu kisha akapewa nafasi ya kuwa kiongozi wa taasisi ya uraisi, basi anapewa na nyenzo zote za kufanyia kazi, kufikiri, kuona, kutambua, etc

Wewe peke yako, huna na huwezi kuona na kujua anayoyajua mwenye nyenzo zote; hivyo sitakupa sababu kwa minajiri hiyo, ila amini wewe sio CLEVER kuliko wao!
 
Mkuu ushahidi upo wa kutosha, usijitoebufahamu kwa sababu ya mahaba uchwara.

Unajifanya una mapenzi naye kuliko hata familia yake. Mwendazake alikuwa katili kupita kiasi, lilikuwa ni kosa kubwa kwenye historia ya Tanzania.
Uko wapi?
 
Sasa kosa la Magufuli ni lipi? Kama viongozi wenyewe hawataki kuishi dodoma kosa la magufuli ni lipi?

Tatizo la viongozi ni kuishi kwa mazoea Mwili uko dodoma akili zipo dar.

Ilitakiwa ipitishwe sharia bungeni kwamba serikali yote ni lazima iwe dodoma kinyume na hapo ni uvunjaji wa katiba ya nchi.
 
Hoja ya vumbi na hali ya hewa haina mashiko ,hivi dar ndio kuna hali ya hewa nzuri ? ,kama wanaogopa vumbi mbona wanapenda sana kwenda dubai hivi kati ya dodoma na dubai wapi kwenye vumbi sana maana dubai ni jangwa
Dubai😃😃😃🥺🤣
 
BARD AI nadhani Dr hayuko sahihi....anachotakiwa kufanya ni kuwashauri viongozi kutulia katika mji wa kiserikali Mtumba ili kupunguza matumizi ovyo ya Kodi za wananchi....
Ingekuwa wote wamehamua idodoywa hapo sawa,.meneja awe Dodoma ,mkurugenzi Dar,katibu Dodoma,waziri dar,ilisha wezekana wapi duniani,lazima watafutane na lazima gharama mlima,hapo bado mla ,auwala kwa kamba hawajaunda mchongo🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️🤸‍♂️
 
Mtaalamu wa masuala ya Uchumi, Dr. Bravious Kahyoza amesema uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma ulikuwa ni kosa kubwa kwasababu umeongeza gharama zaidi za uendeshaji ikiwemo kutumia vibaya fedha za Walipa Kodi.

Ametolea mfano Safari za Viongozi na Watumishi ambao mara kwa mara wanaenda Dar au Dodoma kwa Ndege na wakati huo Magari yanasafiri kuwafuata Airport na kuwapeleka kwenye shughuli zao na baadaye wanarejea kwa Ndege tena huku magari yakiwafuata kwa njia ya Barabara.
View attachment 3017571
Pia Soma: Ilikuwa ni jambo jema Serikali kuhamia Dodoma maana Kivukoni na Posta ni Bandarini, Ashukuriwe Shujaa Magufuli!
Hilo jina lake tu linaonyesha ni mnufaika wa escrow!
 
Actually kwa kiasi kikubwa serikali Iko settled dodoma

Safari to dar and other regions ni za kawaida

Dar haikwepeki… ni commercial capital,

Fikiria if hadi leo dar ingeku capital… mji ulishazidiwa

Huyo msomi hawazi kwa upana wa jambo… anaangalia only one factor
Mji huzidiwi, tatizo ni mipango miji mibovu tu.
 
Dar wanakua wanaoenda kufanya nini?
Makao makuu ya nchi ni Dodoma na ofisi ziko DOdoma nadhani gharama zinakua za watu binafsi wanaoenda shopping Dar.

Nadhani bado kuna watu wanahoma ya Dar na hawapendi Dodoma.
Baada ya miaka kama 10 ijayo itakua imeshazoeleka Dodoma ni makao makuu ya nchi na hizi homa za Dar zitakua zimeisha.
Tutakuwa tushahama tupo zetu Dar
 
Huyo Dr Kahyoza ndio midokta mipuuzi ambayo hayafikirii mbali somi gani hili linafikiria kwa urefu wa pua. Kuhamisha mji kuupeleka makao Dodoma wenge lake kutulia linaweza kuchukua hata miaka 50.

But ni lazima mabadikiko yawepo. Hali ikitulia sheria zikitungwa vizuri ndio mtaanza kuona faida. Haiwezekani kila kitu kiwe Dar. Lazima miji mingine ipewe fursa ya kukua.

Pia vile vile hata wenzetu wazungu wana miji ya kibiashara. Na miji ya serekali mf Newyork na Washington DC

Misomi ya Tanzania mingi haina akili kama huyu
Nakuona mgogo wa Chamwino unavyotetea mji wako kama jangwa la Kalahari
 
Taasisi nyingine zilizobaki zinahamia dom,nina ndugu yupo tbs anasema wanahamia dom muda si mrefu
Hivi kuna ulazima gani ya ofisi zote kuhamia Dodoma? Kuna ofisi makao makuu yanatakiwa yawepo Dar, mfano Bandari, TRA, TBS etc. Halafu unakuwaje na makao makuu ambayo hayana international airport? Mhh
 
Hivi kuna ulazima gani ya ofisi zote kuhamia Dodoma? Kuna ofisi makao makuu yanatakiwa yawepo Dar, mfano Bandari, TRA, TBS etc. Halafu unakuwaje na makao makuu ambayo hayana international airport? Mhh
Sasa si ndio msalato inajengwa.

Tatizo tumeshakariri kila kitu Dar, akili za viongozi wetu ziliishia hapo wakaiacha miji mingine kama Mwanza kuwa dhoofu
 
Mtaalamu wa masuala ya Uchumi, Dr. Bravious Kahyoza amesema uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma ulikuwa ni kosa kubwa kwasababu umeongeza gharama zaidi za uendeshaji ikiwemo kutumia vibaya fedha za Walipa Kodi.

Ametolea mfano Safari za Viongozi na Watumishi ambao mara kwa mara wanaenda Dar au Dodoma kwa Ndege na wakati huo Magari yanasafiri kuwafuata Airport na kuwapeleka kwenye shughuli zao na baadaye wanarejea kwa Ndege tena huku magari yakiwafuata kwa njia ya Barabara.
View attachment 3017571
Pia Soma: Ilikuwa ni jambo jema Serikali kuhamia Dodoma maana Kivukoni na Posta ni Bandarini, Ashukuriwe Shujaa Magufuli!
Ila mchambuzi akili huna,serikali ilihamishiwa dodoma na alihamisha ofisi zote.sasa huyo aliewafanya wafanye vikao dar ndio alaumiwe acheni kuogopa
 
Wabeba jeneza hawataelewa, huduma zile zile, Dar na Dom, lakini unatumia trilions kuhamisha makao makuu as if kuna dharura
Hili jambo lilishawekwa kwenye mipango ya nchi hata katika ilani. Iweje muanze kumlaumu mtekelezaji. ?
 
Back
Top Bottom