Dkt. Kikwete: Ninaandika kitabu cha historia yangu ambacho ninaelezea mambo mengi hata yale msiyoyajua!

Dkt. Kikwete: Ninaandika kitabu cha historia yangu ambacho ninaelezea mambo mengi hata yale msiyoyajua!

Rais mstaafu wa awamu ya 4 mh Mrisho Jakaya Kikwete amesema kwa sasa anaandika kitabu cha historia ya maisha yake ambacho kitaelezea mambo aliyoshiriki, aliyoyashuhudia na aliyoyaona katika maisha yake binafsi na yale ya siasa.

Kikwete amesema hayo wakati wa mahojiano na mwandishi Salama Jabir katika kipindi cha Salama leo.

Chanzo: Eatv.

Maendeleo hayana vyama!
Kitabu hakijatoka tu toka aseme anaandika?!
 
Si mbaya pia katika hadidu za rejea akafafanua maneno ya kiingereza kama "dark arts" au "under hand.
 
Rais mstaafu wa awamu ya 4 mh Mrisho Jakaya Kikwete amesema kwa sasa anaandika kitabu cha historia ya maisha yake ambacho kitaelezea mambo aliyoshiriki, aliyoyashuhudia na aliyoyaona katika maisha yake binafsi na yale ya siasa.

Kikwete amesema hayo wakati wa mahojiano na mwandishi Salama Jabir katika kipindi cha Salama leo.

Chanzo: Eatv.

Maendeleo hayana vyama!
Amekula chumvi nyingi muache ajiandalie uchuro wake
 
Mie nimewaza Mkapa kamaliza kuandika akazindua tu, then in a year or two he was no more...
Nafikiri tunatakiwa kuwa na hii mentality..

Kufa, tutakufa tu hata tukikaa kimya, kwa hivyo ni bora kuacha kumbukumbu itakayoishi.
Screenshot_20210107-230450.jpg
 
Amefanya mengi mazuri yanayofaa kuwa urithi wa taifa kisiasa, kiuchumi - kitabu chake kitapendeza na kuvunja rekodi
 
Vitabu ni urithi mzuri sana kwa vizazi vijavyo. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amelifanyia mengi taifa hili. Mbali na kuwa rais kwa kipindi cha miaka10 amehudumu kwenye serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania tangu akiwa kijana.
Kwangu mimi JK anabaki kuwa shujaa aliyeweza kutegua mtego wa kumuingiza mtuhumiwa wa ufisadi ikulu na kutuletea Chuma JPM💪

Naamini kuna vingi tutajifunza kupitia kitabu chake

Mungu ampe maisha marefu yenye afya na furaha tele Jakaya Kikwete
Amelitafuna sana taifa hili. Ni basi tu hatuna misingi mizuri ya sheria ndo maana bado yupo uraiani. Otherwise asingekuwa uraiani. JPM iwe 10 tena
 
Rais mstaafu wa awamu ya 4 mh Mrisho Jakaya Kikwete amesema kwa sasa anaandika kitabu cha historia ya maisha yake ambacho kitaelezea mambo aliyoshiriki, aliyoyashuhudia na aliyoyaona katika maisha yake binafsi na yale ya siasa.

Kikwete amesema hayo wakati wa mahojiano na mwandishi Salama Jabir katika kipindi cha Salama leo.

Chanzo: Eatv.

Maendeleo hayana vyama!

Tangu tusikie juu ya kitabu hiki ni miaka kadhaa imepita. Bado tu hakitoki? Uandishi ni uwezo na karama. Kama huna ni busara kukaa kimya. Kikitoka tutakiona.
 
Tunakisubiri kwa hamu kubwa Mh. Rais Mstaafu J.M. Kikwete.
 
Wakianza tu kuandika vitabu huwa awachelewi, watawala wa kiafrica huwa na akili kabla ya kuingia na baada ya kutoka.Sijui kule kuna nn wote huwa wanaanza vizuri kabla ya kulewa.

Si ajabu jiwe akawa Mwalimu mzuri Sana wa demokrasia na kujutia aliyoyatenda siku mfumo ukimtupa.Hata Nyerere baada ya mfumo kumtupa aliandika Sana na alitoa speech nyingi Sana zilizoponda Utawala wake.

Mfano:
Uhuru na maendeleo,

Tujisahihishe.nk.

Wakiwa madarakani wanajua KILA kitu awashauriki Hadi wakishavurunda ndipo uja kuwaomba msamaha wananchi kupitia kuandika vitabu Hali wanakuwa wameshaacha madhara makubwa Sana kwenye nchi.
 
Rais mstaafu wa awamu ya 4 mh Mrisho Jakaya Kikwete amesema kwa sasa anaandika kitabu cha historia ya maisha yake ambacho kitaelezea mambo aliyoshiriki, aliyoyashuhudia na aliyoyaona katika maisha yake binafsi na yale ya siasa...
Hata sitamani afanye hvyo mzee wetu maana imeonesha mtu akitoa tu kitbu kinacho husu maisha ya basi anatangulia, mfano Mkapa na Mengi
 
Back
Top Bottom