Dkt. Magufuli alipokuwa Waziri, aliwahi kukusanya sadaka Kanisani kama alivyofanya leo katika Ibada ya Christmas?

Kanisa litueleze kama sadaka tuzitoazo zimegeuzwa kuwa kodi za serikali! Si kila muumini anaweza kuinuka na kuanza kukusanya sadaka bila ya kuteuliwa na kanisa, he, TRA imeingia kanisa ni kutafiti makusanyo ya sadaka?
 
Usishangae huu ni mwendelezo wa maigizo na impact ya cannabis sativa .
 
Unajua maana ya kushindwa?
Huyo kada wa Lumumba, anauhesabu huo "uchafuzi" uliopita kuwa ni miongoni ya chaguzi Huru na Haki?

Hivi uchaguzi gani ambao Jiwe anawaamrisha Wasimamizi wote wa uchaguzi kuwa vibarua vyao vitaota nyasi, iwapo atatokea msimamizi yeyote atakayethubutu kumtangaza mpinzani kwenye eneo lake kuwa ameshinda?
 
Hii thread haina mantiki wala maslahi kwa nchi.Akusanye sadaka wakati huo au sasa haitusaidii na wala siyo jambo la maana la kuingizwa kwenye historia ya nchi yetu.
 
Hii thread haina mantiki wala maslahi kwa nchi.Akusanye sadaka wakati huo au sasa haitusaidii na wala siyo jambo la maana la kuingizwa kwenye historia ya nchi yetu.
Nilitarajia ungeipuuza na kupitia kimya kimya!
 
Ule ulikuwa uchafuzi na sio uchaguzi na wao hilo wanalijua japo hawawezi kukiri.
 
Teh teh teh 🤣🤣🤣 we jamaa pumzika bhana acha kumsakama mh Rais.
 
Sasa mkuu, ya kanisani yanakupasa yakufae Wewe, ukiyaleta hapa tunaanza kukushangaa Kwa sababu Mungu sio mbea!!

Ungemfuata umuulize ili akufundishe nini Maana ya hicho afanyacho, vingenevyo Huu ni umbea usio mfaa mtu wa kanisani
Umbea wakati picha unaziona?Kama imekuuma kunywa panadol upunguze maumivu.
 
Nyerere never did that.

And he was going to church almost everyday.

He understood the meaning of "Separation of Church and State".

Magufuli is a country bumpkin.
 
Kwani shida iko wapi bwashee

Sent using Jamii Forums mobile app
Separation of Church and State.

Viongozi wa Serikali hawatakiwi kuonekana wanajiingiza sana kwenye shughuli za kidini.

Ndiyo maana miaka yote ya urais wa Nyerere na Mkapa hakujakuwa na habari kama hii.

Walielewa "Separation of Church and State" ni nini.

Magufuki ama haelewi, ama hajali.
 
Ahaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Petty issues. Matatizo ya kujadili Tanzania yamekwisha? Ina maana unayoyafanya leo hii uliyafanya tangu zamani.

Rais na yeye ni raia. Anahitaji hapo unakuwa unamuonea!
Magufuli anavyopenda attention, anaweza kwenda kwenye msiba halafu akataka aingie kwenye jeneza yeye ili watu watoe heshima za mwisho.

Wakati bado hajafariki.

Nyerere na Mkapa walijua "Separation of Church and State" ni nini. Ndiyo maana Nyerere alikuwa anaenda kanisani karibu kila siku alivyokuwa Dar, hapo St. Peters, lakini hakufanya hivi.

Mkapa katika urais wake wote hata kusimama mbele tu kanisani St. Immaculata sikumbuki.

Magufuli ama hajui "Separation of Church and State" ni nini, ama hajali.

Because he is a country bumpkin.
 
JPM ni zao la Seminari na jasiri aachi asili!
Mkapa alikuwa mseminari kuliko Magufuli, na hajafanya maigizo haya.

Nyerere alikuwa anakwenda kanisani kila siku, sio Jumapili na sikukuu tu, kila siku alivyokuwa Dar.

Akitokq Msasani asubuhi anapitia St. Peters Mbuyuni pale. Kila siku.

Lakini hajafanya maigizo haya.

Alijua "Separationnif Church and State" ni nini.

Magufuli ama hajui, ama hajali.

Hana kile kitu Wafaransa wanaita "savoir faire". Uwezo wa kujua hapa ni mahala pangu, hapa si pangu niwaachie wengine.
 
Wewe hujui ukiandikacho. Wapi Rais Magufuli kaingilia Kanisa? Kukusanya sadaka? You must be out of your mind. Allegations za udini na ukabila zinatolewa na myopic thinkers. Sijui kama unakumbuka Mwl. Nyerere aliwahi kusemaje kuhusu kumpata kiongozi bora.
 
Alikusanya sadaka akiwa rais hivyo hivyo kama si mwaka huu basi ni mwaka jana! Kanisa Katoliki ni kawaida tu!
 
Nimekuuliza unaelewa "Separation of Church and State" ni nini.

Hujajibu.

Huyo Mwalimu Nyerere uliyemtaja alikuwa anakwenda kanisani kila siku akiwa Dar.

Karibu kila siku, alikuwa akisali St. Peters.Si mpaka Jumapili na Christmas.

Na hakutoza sadaka hata siku moja maisha yake yote. Hakuna rekodi hiyo.

Alijua maana ya "Mpeni Kaizari cha Kaizari, na Mungu cha Mungu".

Alijua akisimama kutoza watu sadaka, watu wengine watajiuliza sasa hizi hela tunazompa Julius Kaizari huyu ni sadaka za kwenda kwa Mungu au tunaunga mkono juhudi za utawala wake?

Watu wengine watatoa sadaka kwa sababu anayetoza ni rais, si kwa sababu wanataka kutoa sadaka kanisani.

Yani suala zima la kwenda kanisani kutoa sadaka kidini linagubikwa wingu la siasa.

Ndiyo maana Nyerere na Mkapa hawakufanya maigizo haya.
 
Sasa mkuu, ya kanisani yanakupasa yakufae Wewe, ukiyaleta hapa tunaanza kukushangaa Kwa sababu Mungu sio mbea!!

Ungemfuata umuulize ili akufundishe nini Maana ya hicho afanyacho, vingenevyo Huu ni umbea usio mfaa mtu wa kanisani

Jamani, we are greater thinkers, tufanye kwa nafasi zetu! Kuna shida gani Mhe.Rais JPM kumtumikia Mungu katika maisha yake binafsi?! Hayo ni mahusiano yake binafsi na Mungu tumwachie yeye!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…