TANZIA Dkt. Masumbuko Lamwai afariki dunia

TANZIA Dkt. Masumbuko Lamwai afariki dunia

RIP..
Generation flani hivi ndio inakabidhi kijiti sijui kama vijana wengi wanafahamu au watatunza kumbukumbu ya tulipotokea.
 
1. Ndiye mtanzania wa kwanza kutunukiwa Shahada ya udaktari wa Falsafa katika sheria (Criminal and Procedural Law - LLD) Chuo Kikuu Oxford, moja ya vyuo vinavyoheshimika sana duniani.

2. Ndiye mwanafunzi wa kwanza kutoka Afrika kusoma kozi ya miaka minne kwa miaka miwili chuoni hapo. PhD in Criminal &Procedural Law (Oxford) ni miaka minne (full time) na miaka 6 hadi 8 (part time). Lakini Lamwai aliomba kusoma miaka miwili na akahitimu.

3. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 akiwa Mhadhiri UDSM alishirikiana na wanaharakati wenzie kuanzisha vuguvugu la kudai mfumo wa vyama vingi.

4. Mwaka 1994 aligombea udiwani Kata ya Manzese kupitia NCCR. Alishinda lakini CCM wakachakachua. Akaenda Mahakamani matokeo yakabatilishwa. Uchaguzi ukarudiwa, akagombea na kushinda.

5. Akiwa diwani pekee wa upinzani Manispaa ya Kinondoni aligombea Umeya na kupata kura moja (ya kwake). Alipoulizwa kwanini aligombea wakati alijua hatashinda, alijibu "nisingegombea ningelazimika kumpigia mgombea wa CCM au kuharibu kura. Yote mawili ni makosa. Hivyo niliamua kugombea ili nimpe kura mgombea sahihi"
_
6. Ndiye Mbunge wa kwanza wa upinzani jimbo la Ubungo baada ya kushinda uchaguzi mkuu 1995.

7. Yeye na Mabere Marando wakiwa bungeni waligomea kiapo cha Utii kwa Rais, kwahoja kuwa wabunge hawapaswi kumtii Rais kwa sababu bunge ni mhimili unaojitegemea. Baada ya mabishano makali ya kisheria, Spika Msekwa alikubaliana na hoja yao. Kiapo cha wabunge kikafanyiwa marekebisho na kuondoa sehemu ya "utii kwa Rais" kisha wabunge wote wakaapa upya.

8. Mwaka 1996 aliongoza kesi maarufu ya uchaguzi iliyomvua ubunge aliyekua Mbunge wa Temeke, Ramadhani Kihiyo kutokana na kughushi taarifa za elimu yake. Mbali na kesi hiyo ameshiriki pia kusimamia kesi mbalimbali nje na ndani ya nchi. Mwaka 2006 alishiriki kuandaa muongozo wa Haki za binadamu kwa nchi za jumuiya ya madola.

9. Mwaka 1999 baada ya kupitia misukosuko mingi ya kisiasa ikiwemo mali zake kupigwa mnada, kufilisiwa na kufutiwa leseni ya uwakili aliamua kurudi CCM.

10. Dr.Masumbuko Lamwai ni kaka yake Mhe.Joseph Selasini (Mbunge wa Rombo). Majina yake kamili ni Dr.Emmanuel Masumbuko Roman Selasini Lamwai.!

PICHANI: Mwanasheria wa Chadema John Mallya akiwa na mwalimu wake Dr.Masumbuko Lamwai (PhD) mwaka 2012 wakati Mallya alipohitimu shahada yake ya kwanza ya sheria (LLB).!View attachment 1441225
Hata Joseph Selasini anatembelea nyota ya kaka yake Dr Masumbuko!
 
Huyu baba alikuwa ni kichwa alafu bonge moja la mtu mstaarabu. Chuoni ilikuwa bora nikose pindi lingine ila sio la Lamwai!

R.I.P Dr. Lamwai, Bwana akupe pumziko la amani 🙏
 
Mwanasheria nguli, Msomi Kindakindaki aliyeichachafya CCM Hadi ikatia NIDHAMU.
Rest in eternal peace
Nilipata kuelezwaharakati za jamaa huyu, nilibaki na mshangao maana wahenga wanasema alikuwa kisiki kweli kweli.

Msomi, shupavu na aliyesimamia alichokiamini. Anastahili kukubukwa kwa mchango wake kwa mageuzi ya vyama vingi kwa nchi hii.
 
Huyu baba alikuwa ni kichwa alafu bonge moja la mtu mstaarabu.
Chuoni ilikuwa bora nikose pindi lingine ila sio la Lamwai!

R.I.P Dr. Lamwai, Bwana akupe pumziko la amani 🙏
Wali-enjoy sana waliofundishwa na huyu jamaa. Msomi wa Shahada ya Uzamivu (Ph.D in Laws) University of London 1983.

The guy has left a legacy. Wahenga wanatamani chama kikuu cha upinzani cha sasa (CHADEMA) kingepata angalau wabunge 10 vichwa kama huyu jamaa
 
TIP Diwani wetu na Mbunge wetu 1995. Ulitetemesha sana. Nikikumbuka ule uchaguzi wa Temeke, Kihiyo alivyotaka kulikimbia jukwaa la Kampeni - nakumbuka ndipo ulianza msamiati wa 'vihiyo'
 
Nakumbuka pia walivyotetemesha Bunge lao la kwanza kwa kukataa kula kiapo hadi kilipobadilishwa, Nakumbuka spika Pius Msekwa alimwambia mwanasheria wa serikali siku hizo kuwa jipange sawasawa maana hili siyo bunge la mchezo
 
Dah! poleni sana, Siasa za kiswahili bana! kwa nini alifirisiwa Mali zake na yeye ni Mwanasheria? yaani wanasiasa hawakujali mdomo wake wala wa kisomi kweli? tena waliomfanyizia hawana elimu km yeye! Oxford UK kwa nini alirudi Bongo?

Alishau Wa-Bongo hawana Imani!
 
Kote huko Savannah , kote humo ni kwangu. Tumecheza muziki sana pale Tour and Huntes kwa Mzee Makassy enzi hizo. (sasa amekaa Gwajima na utapeli).

Kamanyola na Maquis pale Savvanah, White House. Kwa Manywele tulikuwa tunakula bia na nyma choma. Enzi hizo UDA ilikuwa inaishia Maji. Mitaa ya Chai unaifahamu?
Iko iko iko na Bana Ngenge yeah!! Fataki Los Los Lokasa na Masumbuko ya Dunia.....aaaiiiii!!!!
Umenikumbusha mbali sana!!!! Enzi ya Savanna Inn...

Hebu nitajie majina ya watemi wa Kibo kipindi ile……..
 
Iko iko iko na Bana Ngenge yeah!! Fataki Los Los Lokasa na Masumbuko ya Dunia.....aaaiiiii!!!!
Umenikumbusha mbali sana!!!! Enzi ya Savanna Inn...

Hebu nitajie majina ya watemi wa Kibo kipindi ile……..
Mzee Paisi unamfahamu? Mzee Komba? nakuja baadaye
 
Back
Top Bottom