Pre GE2025 Dkt. Mpango aomba apumzike kuwa Makamu Rais akimaliza muda wake, Rais Samia aridhia ombi hilo

Pre GE2025 Dkt. Mpango aomba apumzike kuwa Makamu Rais akimaliza muda wake, Rais Samia aridhia ombi hilo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ilikua swala la muda tu!
Hakuna aliye dhani angeendelea , hata hivyo alichelewa sana.

Ajabu wenye umri mdogo wanaomba kupumzika ila vikongwe wanaingia kazini
 
Wasiraa anapewa nafasi alafu Mpango kaandika barua ya kujiuzuluu nitakuwa Wa mwisho kuamini hilo maana Nafasi ya umakanu wa rais naona hainaga majukumu ya maana sana mpama mtu aishindwee...!! Mpango kakatwa na inawezekana hakutegemea kapigwa suprise pale maskini daah.
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amemwandikia barua ya kuomba apumzike Umakamu wa Rais ambapo amesema baada ya kutafakari ameridhia ombi hilo.

Lakini kwa sasa Dkt. Mpango ataendelea kuwa Makamu wa Rais hadi utakapofanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025.

Akiongea leo January 19,2025 kwenye Mkutano Mkuu Maalum Jijini Dodoma, Rais Samia amesema

""Dkt. Philip Mpango ndiye Makamu wa Rais miezi ya karibuni hapa amekuja kuniona kuniomba apumzike, ana sababu kadhaa lakini sio za kazi, anasema yeye sasa ana miaka 68 na angependa kuishi zaidi kwahiyo naomba nipumzisheni.

Nikambishia bishia Wiki iliyopita hapa akanikabidhi barua yangu hii ( ya kujiuzulu?) na barua sikumjibu, nilipoenda kwenye Kamati Kuu nikawaeleza hiyo hali na kwa pamoja wote tukakubali tumpumzishe"


View attachment 3206674

Source: Millard Ayo
Hapo kuwa ana miaka 68 na anataka aendelee kuishi ina maana kama angeendelea kuwa makamu na hatimaye kuwa mgombea mwenza maisha yake yangekuwa hatarini na yeye bado anataka kuishi. Hii inaashiria kuwa huko CCM kuko kwa moto sana.
 
Kwa kipindi chote alichohudumu hiyo nafasi hajaisaidia Kigoma kwa chochote kile wakati wenzie wanajenga Kizimkazi.

Dr Mpango ni mzigo acha apumzike.
Huko nchi gani mkuu, mpaka dakika hii Kwa hilo tangazo Kigoma ni msiba mkubwa, mambo mengi kawafanyia swali ni je serikali itayamalizia, kuna Hospital ya kanda, chuo kikuu cha kanda, barabara, miradi kibao ya maji na mengine ambayo nimesahau ila hayajakamilika
 
Back
Top Bottom