Pre GE2025 Dkt. Mpango aomba apumzike kuwa Makamu Rais akimaliza muda wake, Rais Samia aridhia ombi hilo

Pre GE2025 Dkt. Mpango aomba apumzike kuwa Makamu Rais akimaliza muda wake, Rais Samia aridhia ombi hilo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Rais Samia, leo kwa maneno yake amesema Dr. Philip Mpango alimwambia anataka SASA kupumzika (yaani amechoka), hataki tena kuendelea na hiyo nafasi. Rais akakataa, lakini Dr. Mpango akamwandikia barua rasmi ya kuomba kutaka kuachana kabisa na hiyo nafasi SASA (kujiuzuru), Rais ameridhia ombi lake hilo kwa sharti kuwa itabidi amalizie miezi tisa ya utawala wake iliyobakia.

Kama hoja itajengwa kuwa, uamuzi wake huo wa kujiuzuru unahusika baada ya huu utawala kwisha Oktoba mwaka huu basi kimantiki tangazo la Rais halina mantiki na ombi hilo la Dr.Mpango halina mantiki kwa kuwa kikatiba wote (Rais na Makamu wake) mikataba yao ya kuongoza inakoma mwishoni mwa oktoba mwaka huu.

Wataalamu wa siasa, sheria, katiba hii imekaaje?
Kwamba jamaa kachoka kula mahela ya walipa kodi yalivo matamu kweli
 
Au labda ndio wale Mkuu wa Majeshi alisema........ wa nchi jirani
Nchi hii ina wakimbizi wengi sana, mwingiliano ni mkubwa sana, tunapishana nao tu mihangaikoni na vitambulisho vyao vya Nida
 

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amemwandikia barua ya kuomba apumzike Umakamu wa Rais ambapo amesema baada ya kutafakari ameridhia ombi hilo.

Lakini kwa sasa Dkt. Mpango ataendelea kuwa Makamu wa Rais hadi utakapofanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025.

Soma:Breaking News: - Uchaguzi 2025 - CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025

Akiongea leo January 19,2025 kwenye Mkutano Mkuu Maalum Jijini Dodoma, Rais Samia amesema

""Dkt. Philip Mpango ndiye Makamu wa Rais miezi ya karibuni hapa amekuja kuniona kuniomba apumzike, ana sababu kadhaa lakini sio za kazi, anasema yeye sasa ana miaka 68 na angependa kuishi zaidi kwahiyo naomba nipumzisheni.

Nikambishia bishia Wiki iliyopita hapa akanikabidhi barua yangu hii ( ya kujiuzulu?) na barua sikumjibu, nilipoenda kwenye Kamati Kuu nikawaeleza hiyo hali na kwa pamoja wote tukakubali tumpumzishe"
Nchimbi ni Jembe.
Kila mtu hana shaka nae.
 
Kasema hatoendelea, maana yake atamaliza ngwe hii, ila hatipanda majukwaani kuomba kura tena uchaguzi ujao.
 
Yaani anajiuzuru leo kwa sababu kachoka na kazi halafu hapo hapo anaendelea kukaa ofisini kuifanya kazi ile ile mpaka mkataba wake unapokwisha. Common sense inatokeaje hapo?

Sote tunajua mtu akijiuzuru leo, basi kesho hayupo tena ofisini, na hapo hapo mtu mwingine anawekwa nafasi yake.
Hata wazir Mkuu wa Kanada alijiuzuru majuzi lakini bado yupo ofisini mpaka April 2025
 
Rais Samia, leo kwa maneno yake amesema Dr. Philip Mpango alimwambia anataka SASA kupumzika (yaani amechoka), hataki tena kuendelea na hiyo nafasi. Rais akakataa, lakini Dr. Mpango akamwandikia barua rasmi ya kuomba kutaka kuachana kabisa na hiyo nafasi SASA (kujiuzuru), Rais ameridhia ombi lake hilo kwa sharti kuwa itabidi amalizie miezi tisa ya utawala wake iliyobakia.

Kama hoja itajengwa kuwa, uamuzi wake huo wa kujiuzuru unahusika baada ya huu utawala kwisha Oktoba mwaka huu basi kimantiki tangazo la Rais halina mantiki na ombi hilo la Dr.Mpango halina mantiki kwa kuwa kikatiba wote (Rais na Makamu wake) mikataba yao ya kuongoza inakoma mwishoni mwa oktoba mwaka huu.

Wataalamu wa siasa, sheria, katiba hii imekaaje?
Nchimbia ameishaajza mauchawi yake
 
Kasema hatoendelea, maana yake atamaliza ngwe hii, ila hatipanda majukwaani kuomba kura tena uchaguzi ujao.
Nani alimwambia ingwe ijayo atapitishwa tena?
Hilo lilihitaji kuandika barua kwa Rais, tena sasa?
Rais alikuwa na sababu yoyote ya kulisema kwetu, tena sasa?
 
Back
Top Bottom