Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda

Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda

Tuwapeni muda viongozi wetu wasimamie kumalizika kwa mradi....

Kwa mradi mkubwa kama huu wa Trilioni 6.5 ni lazima kuwe na kuhoji...lakini pia ni lazima tuwe na mizani ya kujua kuwa "miluzi mingi humchanganya mbwa".....
 
Hata muitengeneze haiwezi kutokea...Aliwazidi akili kwaku document kila event na ku share na general public...Kil uzushi utakuwa na counter attack yake...Ukajipange upya!
Unampaja mtu asie na uzoefu kutekeleza mradi mkubwa kama huo?

Yale yale ya Richmond.
 
Unampaja mtu asie na uzoefu kutekeleza mradi mkubwa kama huo?

Yale yale ya Richmond.
We kaendelee kutengeneza tamthilia njoo nayo uone tutakavyokupangua...Hii ni karne nyingine siyo enzi zile ambazo mliwaokota raia kwakukosa knowledge
 
Kwahiyo ndio Mpango wa kufifisha ujenzi wa bwawa hilo umeanza? Kisha watasema kasma hamna, kisha Mwezi wa kwanza na genge lake lote la msoga watasema tununue umeme wa dharula, paaap wamerudi, kazi inaendelea!

Eti mkandarasi hana uzoefu, kabla ya hii ziara, kuna ziara ya viongozi wastaafu ilitangulia eeenhe?
Unaota ndoto au tayari umepata kinywaji
 
Mmmhhh..!! Mh. Mpango anasema mkandarasi hana uzoefu wa kutosha? Sasa alipewaje kazi? Kama ni sub-contractor na hana uzoefu wa kutosha, atajenga ktk viwango vya kimataifa kweli Bwawa letu la umeme? Au ndio mwanzo wa figisu?
Mpango si alikuwa waziri wa Fedha na alikuwa mstari wa mbele ktk ujenzi wa bwawa hili na bungeni alitetea sana, kama mkandarasi hana uzoefu kwa nafasi yake akiwa waziri wa fedha alishindwa nini kusema haya leo anayosema mapema?
Weeeee! Km ungelikuwa wewe ungelisema chochote zaidi ya kusifia?!! Thubutuuuu
 
Zimeanza story kama zile za sgr ilikua 2019, ikaja 2020 ikaja 2021 hadi sasa haijulikani lini mwisho wake. Sisiyemu ni adui namba moja wa taifa ili.

Tena baada ya kifo ata tbc hawaruki tena live kutoka bwawani ahahahaha. Ukweli bwawa la nyerere itachukua muda kukamilika,
 
Arab Contractors imeanzishwa miaka ya 1950.....

Imejenga mradi mkubwa wa kufua umeme "ASWAN DAM"...unasemaje kuwa hawana uzoefu ?!!!
Ndugu hawa ndugu wanajua wanachokitaka....Tutawaona tu sura zao kamili kabla hata mwaka haujaisha
 
Wakati akitoa maelekezo alipotembelea mradi wa kufua wa umeme wa stiglers gorge , Mh. Mpango alipongeza kwa kazi nzuri unayoendelea na kuongea mengi yakiwemo
1. Mkandarasi Hana Uzoefu wa kutosha katika ufanyaji wa kazi zake huku akisema kwasababu anatumia subcontractor kwa karibu kazi zote kila sehemu. Serikali labda ilitaka mkandarasi mkuu afanye kazi zote peke yake, lakini sehemu nyingi ameweka wachina
2. Mkandarasi yupo nyuma ya mpango kazi, na kwamba amechelewa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mafuriko na uvico19. Kauli ambayo Kalemani amekuwa akitudanganya kuwa tupo mbele ya muda na maji yataanza kujazwa Mwezi wa 11 tarehe 15, na kuwasha mitambo June 2022( KAULI AMBAYO NI DHAHIRI ALITUDANGANYA NA ILIKUWA YA KISIASA) Laini Makamu wa Rais ameongea ukweli.

Kutokana na Kauli ya Mh. Makamu wa Rais ni DHAHIRI kuwa Mradi huu hautaweza kukamilika 2022 Wala 2023 Wala 2024 labda 2025.
Kalemani alifundishwa uongo na Magufuli na yeye kabeba tabia ile moja kwa moja. Kipindi chote cha Magufuli data 70% zilikuwa za kupika. Na serikali hii nayo naona inaanza kupika data.
 
Hapa ndipo nategemea waziri ajiuzulu kwa kutudanganya kila kukicha juu ya maendeleo ya bwawa, tatizo utaona wala hawajibiki kwa namna yeyote, tabia hii ipo hadi kwa waziri wa afya pia alipaswa ajiuzulu kuipa nguvu kampeni ya Covid-19, uwepo wake baadhi ya watu hawamwamini kwani alipinga chanjo kipindi cha nyuma, sasa anageuka eti inafaa,!

Waziri nani.
 
Kabla ya kumpa mtu kazi angalia kwanza uzoefu. Brazil, Urusi na China ndiyo hujenga mabwawa kila leo. Sasa wamisri na mabwawa wapi na wapi. Brazil walionyesha siku nyingi interest na hiyo project, na wanauzoefu mkubwa lakini jamaa akajikuta Pan-African.
 
Mkandarasi wa miradi mikubwa kama hiyo anashinda tender kutokana na design yake ya mradi wote kuanzia physical project, ulinzi wa mazingira kama ecosystem, namna ya kuvuta maji and so forth with hydro power project scope.

Anakupa na costs zake za kujenga mradi, work break down structure ya wewe kuweza kufuatilia progress ya mradi kwa makubaliano ya muda wa kazi, etc.

Kazi yenyewe inafanywa na sub-contractors anachosimamia mkandarasi na ku coordinate hatua za kazi, kuangalia quality ya kazi, time, anapanga critical path ya mradi na other supervision roles.

Mtu kama makamu wa raisi awezi kwenda kwenye mradi kama huo bila ya mshauri wa maswala ya project management; hivi mbona tunaviongozi waropokaji halafu wepesi sana vichwani ukiwasikiliza.

Au anadhani huu sawa na miradi wa kujenga barabara. Yaani nchi inaviongozi wa ovyo kweli.

Sijui haya maneno yamelenga kufikia lengo gani? Wakati mwingine watu wanaongea utafikiri Tanzania sasa inaongozwa na chama na serikali nyingine kabisa ambayo si ya CCM.

Hawa viongozi walikuwa wapi kuongea wakati haya mapungufu makubwa hivi yanafanyika? Kwa nini waliwadanganya wananchi kwa kusifia huu mradi wa bwawa la Nyerere? Viongozi wakuu wastaafu walitembelea hilo Bwawa juzi kati wakasifia kumbe na wao walikuwa wanaongelea wasichokijua mbele ya Watanzania. Mh Makamu wa Rais akiwa Waziri wa fedha alikuwa anatoa fedha kulipa mkandarasi asiye na usoefu wakazi. Yajayo mbeleni yanatafakarisha sana.
 
Wakati akitoa maelekezo alipotembelea mradi wa kufua wa umeme wa stiglers gorge , Mh. Mpango alipongeza kwa kazi nzuri unayoendelea na kuongea mengi yakiwemo
1. Mkandarasi Hana Uzoefu wa kutosha katika ufanyaji wa kazi zake huku akisema kwasababu anatumia subcontractor kwa karibu kazi zote kila sehemu. Serikali labda ilitaka mkandarasi mkuu afanye kazi zote peke yake, lakini sehemu nyingi ameweka wachina
2. Mkandarasi yupo nyuma ya mpango kazi, na kwamba amechelewa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mafuriko na uvico19. Kauli ambayo Kalemani amekuwa akitudanganya kuwa tupo mbele ya muda na maji yataanza kujazwa Mwezi wa 11 tarehe 15, na kuwasha mitambo June 2022( KAULI AMBAYO NI DHAHIRI ALITUDANGANYA NA ILIKUWA YA KISIASA) Laini Makamu wa Rais ameongea ukweli.

Kutokana na Kauli ya Mh. Makamu wa Rais ni DHAHIRI kuwa Mradi huu hautaweza kukamilika 2022 Wala 2023 Wala 2024 labda 2025.

Mwarabu gani yuko kibendudi zaidi ya kujua kujilipua tu? Ili kupata wale sabini?
 
Hta
Wakati akitoa maelekezo alipotembelea mradi wa kufua wa umeme wa stiglers gorge , Mh. Mpango alipongeza kwa kazi nzuri unayoendelea na kuongea mengi yakiwemo
1. Mkandarasi Hana Uzoefu wa kutosha katika ufanyaji wa kazi zake huku akisema kwasababu anatumia subcontractor kwa karibu kazi zote kila sehemu. Serikali labda ilitaka mkandarasi mkuu afanye kazi zote peke yake, lakini sehemu nyingi ameweka wachina
2. Mkandarasi yupo nyuma ya mpango kazi, na kwamba amechelewa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mafuriko na uvico19. Kauli ambayo Kalemani amekuwa akitudanganya kuwa tupo mbele ya muda na maji yataanza kujazwa Mwezi wa 11 tarehe 15, na kuwasha mitambo June 2022( KAULI AMBAYO NI DHAHIRI ALITUDANGANYA NA ILIKUWA YA KISIASA) Laini Makamu wa Rais ameongea ukweli.

Kutokana na Kauli ya Mh. Makamu wa Rais ni DHAHIRI kuwa Mradi huu hautaweza kukamilika 2022 Wala 2023 Wala 2024 labda 2025.
Wewe unatudangnya tu,
Tusubili mwezi wa kumi na moja uishe kabla hawajajaza maji kisha ndo uje hapa
 
Kabla ya kumpa mtu kazi angalia kwanza uzoefu. Brazil, Urusi na China ndiyo hujenga mabwawa kila leo. Sasa wamisri na mabwawa wapi na wapi. Brazil walionyesha siku nyingi interest na hiyo project, na wanauzoefu mkubwa lakini jamaa akajikuta Pan-African.
"Aswan Dam" imejengwa na haohao ARAB CONTRACTORS tena miaka ya 1960...... Serikali ya awamu ya 5 haikukosea......
 
Sijui haya maneno yamelenga kufikia lengo gani? Wakati mwingine watu wanaongea utafikiri Tanzania sasa inaongozwa na chama na serikali nyingine kabisa ambayo si ya CCM.

Hawa viongozi walikuwa wapi kuongea wakati haya mapungufu makubwa hivi yanafanyika? Kwa nini waliwadanganya wananchi kwa kusifia huu mradi wa bwawa la Nyerere? Viongozi wakuu wastaafu walitembelea hilo Bwawa juzi kati wakasifia kumbe na wao walikuwa wanaongelea wasichokijua mbele ya Watanzania. Mh Makamu wa Rais akiwa Waziri wa fedha alikuwa anatoa fedha kulipa mkandarasi asiye na usoefu wakazi. Yajayo mbeleni yanatafakarisha sana.
Umuoni alivyofura siku hizi na kunawiri; tafuta picha zake za kabla ya kuwa waziri wa fedha.

Kuna watu wao wanafikiria shibe yao tu, hiyo ndio namna yake ya kukazia mama yupo sahihi kumtimua Kalemani nishati (ukiniuliza mimi Kalemani kajifukuzisha mwenyewe kwa kukaa kimya wakati umeme unakatika ovyo).

Sasa wao kumfurahisha boss wanaongezea na chumvi zao; as the saying goes ‘shibe mwanamalevya, njaa mwanamalegeza’.
 
Huu mradi ni bomu litalokuja kulipuka huko mbeleni.

Haya ni madhara ya mtu mmoja kuaamua kila kitu huku akipigiwa makofi na mazuzu.

Haya yangesemwa na wapinzani wangeshambuliwa vibaya sana na hata kukamatwa au kufanyiwa hujuma.
Kivipi mkuu toa analysis za kitaalamu
 
Back
Top Bottom