Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda

Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda

Nilipitia miradi ya mabwawa mengine Kama Ethiopia na Egypt nikawa najiuliza hili letu Labda Kama limetengenezwa kiwandani ni la kufitisha tu hapo mtoni.
Time frame Ilikuwa ya uongo mkubwa
 
13 October 2021

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Philip Mpango Octoba 12, 2021 atembelea mradi wa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere JNHPP / Stiegler Gorge Rufiji

Source : Millard ayo


N.B
Ni kweli kwa kutazama hata kwa macho inaonesha wazi kuwa bwawa la mradi wa JNHPP haliwezi kujazwa mwezi November 2021 kama alivyosema Dr. Medard Kalemani mbunge wa Chato ambaye alipata kuwa waziri wa Nishati ktk serikali ya Rais John Pombe Magufuli.

Na makamu wa Rais Phillip I. Mpango ametupa sababu hasa ya mradi kuwa nyuma ya wakati uliopangwa kukamilika hatua kwa hatua.
 
Umuoni alivyofura siku hizi na kunawiri; tafuta picha zake za kabla ya kuwa waziri wa fedha.

Kuna watu wao wanafikiria shibe yao tu, hiyo ndio namna yake ya kukazia mama yupo sahihi kumtimua Kalemani nishati (ukiniuliza mimi Kalemani kajifukuzisha mwenyewe kwa kukaa kimya wakati umeme unakatika ovyo).

Sasa wao kumfurahisha boss wanaongezea na chumvi zao; as the saying goes ‘shibe mwanamalevya, njaa mwanamalegeza’.

Mungu atusaidie kama taifa. Mh Makamu wa Rais awambie Watanzania serikali inachukua hatua gani kuzuia hizi fedha za kodi zinazolipia mkopo wa hili bwawa la Nyerere kuhakikisha haziendi tena kumlipa huyu mkandarasi asiye na uzoefu kuepuka kuendeleza madudu ya serikali ya awamu ya tano. Kiongozi anatoa kauli ambazo akimaliza tu kutamka zinageuka kuanza kumuwinda.
 
VP yupo sahihi. Mara nyingi una outsource kazi ambazo wewe mwenyewe huwezi kuzifanya kwa ufanisi au faida kwa sababu yoyote ile. Unafanya kile unachoweza au ambacho kwacho you are the best. Kwa hivyo kama Arab Contractors ame outsource kazi zote maana yake ni kuwa yeye asingeweza au hawezi kufanya kazi husika kwa ufanisi mkubwa (na faida) kwa hapa Tz kuliko hao subcontractors.....ama?
 
Lakini nawaza pia bado kuna uwezekano baada ya JPM kufariki ndo wameanza kufanya huu upuuzi ili kumfanya jiwe aonekane alikua anatudanganya ili wao ndo waonekane bora zaidi wkt kuna uwezekano sio kweli.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mkandarasi wa miradi mikubwa kama hiyo anashinda tender kutokana na design yake ya mradi wote kuanzia physical project, ulinzi wa mazingira kama ecosystem, namna ya kuvuta maji and so forth with hydro power project scope.

Anakupa na costs zake za kujenga mradi, work break down structure ya wewe kuweza kufuatilia progress ya mradi kwa makubaliano ya muda wa kazi, etc.

Kazi yenyewe inafanywa na sub-contractors anachosimamia mkandarasi na ku coordinate hatua za kazi, kuangalia quality ya kazi, time, anapanga critical path ya mradi na other supervision roles.

Mtu kama makamu wa raisi awezi kwenda kwenye mradi kama huo bila ya mshauri wa maswala ya project management; hivi mbona tunaviongozi waropokaji halafu wepesi sana vichwani ukiwasikiliza.

Au anadhani huu sawa na miradi wa kujenga barabara. Yaani nchi inaviongozi wa ovyo kweli.
Ndugu acha Kudanganya watu. Miradi mikubwa kama hii lazima kuwe na Consultant ambaye huwa ni Designer na Main supervisor wa Project husika. Labda
Ututhibitishie kuwa huo mradi wa Umeme Contractor ndio pia Designer wa hiyo Project..
 

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AITAKA TANESCO KUONGEZA NGUVU KATIKA UTEKELEZAJI.



13 Oct 2021

MRADI WA JNHPP / RUFIJI STIEGLER'S GORGE, MKANDARASI ALALAMIKA TANESCO KUWAPATIA 33KV BADALA YA 220 KV KUENDESHA MITAMBO YA UJENZI



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango ameitaka wizara ya Nishati kuchukua hatua za haraka kuhakikisha mradi wa kufua umeme katika Bwawa la Julius Nyerere unakamilika kwa wakati.

Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa majumuisho ya ziara yake ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa kufua umeme katika Bwawa la Julius Nyerere ambapo amesema ni muhimu wizara ya Nishati kupitia shirika la umeme nchini (Tanesco) kuimarisha usimamizi, kuongeza wataalam sehemu zenye upungufu pamoja na kuongeza umeme utakaoendesha vema mitambo ya mkandarasi wakati huu wa ujenzi wa mradi
Source : Fullshangwe tv
 
Miradi mikubwa aijengwi na architecture mwenyewe; sub contractors ndio wanafanya kazi.

Labda kwa sababu hatuna uzoefu wa miradi mikubwa; kinyerezi power plant nadhani ni Germany design sasa ule mradi umejengwa na wajerumani wenyewe au subcontractors na kusimamia na ma-engineer wa kitanzania.

Ungelikuwa mradi wa wachina ungewaona wao tu.
Why using the word Architecture? Kwamba Designer wa project yoyote ile anaitwa kwa hilo jina? Ule mradi unahusisha multiple Disciplines! Electrical, Civil, Mechanical Engineering, Environmental etc...wote ni Architecturals??
 
Siku zote lazima apatikane mtu wa kupewa lawama watalaam humuita scapegoat na serikali haiwezi kubali kuwa scapegoat tena hususani nyakati nyeti kama izi yenyewe inabidi isimame kama sterling wa muvi
EBC27272-241E-4038-8743-9EB47AFD3081.jpeg
2DF9303C-4031-42B2-8D06-6FEE3DAF979E.jpeg
FAF99074-4EBB-4BDB-9138-EBDB29D5C95D.jpeg
 
Arab contractor imeanzishwa kabla makamu hajazaliwa.. na kabla Tanzania haijazaliwa arab contractors ipo duniani.. na imejenga Aswan dam na mabwawa kibao.. ila leo tunaambiwa hawana uzoefu

Mambo ya ajabu sana haya. Na sababu kama sijakosea kuwa na subcontractors wengi ikikuwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa kazi, Hayati alisema mahali. Lakini ukisikiliza hotuba za Mh huyu pale JNIA, kwenye uapisho wa wateule juzi Dodoma, kuna siku nyuma kidogo alisahau jukumu la kumkaribisha Mh Rais akaongea aliyo ya ongea akasepa ili bidi akumbushwe na msimamizi wa shughuli. Hatimaye unakuta yako maswali mengi ya kujiuliza kuliko majibu. Mh Mpango wakati ni Waziri wa Fedha akishuka nondo za nguvu na kwa kutulia mpaka unakubali mnyewe. Sijui nini kinamnyemelea? Takwimu za waliochanjwa hazijatolewa muda sasa.
 
Ohooo ,niliwaambia hii miradi ya mfukoni ,, mkandarasi aliletwa na Sukuma gang Ili wapige pesa ndio maana akina Kalemani walikuwa wanajitahidi kuficha taarifa nk..

Eti na yule Kadogosa alitaka yule mkandarasi wao wa yep Markez apewe tenda bila ushindani.

Mama fukuza hiyo miradi ina upigaji wa kutisha na fukuza watu wa Mwendazake wote.
Isije ikawa Manyanga construction ndio walipewa tenda na mwendazake
 
Mmmhhh..!! Mh. Mpango anasema mkandarasi hana uzoefu wa kutosha? Sasa alipewaje kazi? Kama ni sub-contractor na hana uzoefu wa kutosha, atajenga ktk viwango vya kimataifa kweli Bwawa letu la umeme? Au ndio mwanzo wa figisu?
Mpango si alikuwa waziri wa Fedha na alikuwa mstari wa mbele ktk ujenzi wa bwawa hili na bungeni alitetea sana, kama mkandarasi hana uzoefu kwa nafasi yake akiwa waziri wa fedha alishindwa nini kusema haya leo anayosema mapema?
Baba zima lina ramba sikonkiko za mtu na lenywe lilikuw linatoa pesa leo lina ropoka kma toto dgo
 
Ndugu acha Kudanganya watu. Miradi mikubwa kama hii lazima kuwe na Consultant ambaye huwa ni Designer na Main supervisor wa Project husika. Labda
Ututhibitishie kuwa huo mradi wa Umeme Contractor ndio pia Designer wa hiyo Project..
Nani aliye design huo mradi?
 
Labda kama ulikuwa unisomi humu wakati yupo hai kuna vitu nilikuwa naponda kila siku; vingi tu.

Mie sio mfuasi wa mtu sana bali ideas, na maslahi yangu mapana. Kuna mambo serikali ikifanya yana positive direct and indirect impact kwangu; alikadhalika kuna mengine yana negative consequences too.

So nasimama na yaliyo positive kwangu na kwa jamii kwa upana wake; mtu sina tabia ya kuabudu.
Nimekusoma vizuri tu, mara ya mwisho Leo tu himu ukidhihaki ukweli wa maumivu ya wengine ukiyaita delusions za Twitter na JF. Kama kuna anayekuamini humu mwambie nina daraja aje nimuuzie
 
Why using the word Architecture? Kwamba Designer wa project yoyote ile anaitwa kwa hilo jina? Ule mradi unahusisha multiple Disciplines! Electrical, Civil, Mechanical Engineering, Environmental etc...wote ni Architecturals??
What does an architecture do?
 
Nimekusoma vizuri tu, mara ya mwisho Leo tu himu ukidhihaki ukweli wa maumivu ya wengine ukiyaita delusions za Twitter na JF. Kama kuna anayekuamini humu mwambie nina daraja aje nimuuzie
Kama sijakuelewa vile unauza madaraja, sitaki hata kujua unapohifadhi hizo inventory zako.

Au unataka discussion za realistic energy investment, maana hiyo ndio ilikuwa sababu ya kusema kule Twitter wana mijadala delusional.
 
Back
Top Bottom