Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda

Dkt. Mpango: Mkandarasi wa Bwawa la Nyerere hana Uzoefu, pia mradi upo nyuma ya muda

Tanzania ni zaidi ya uijuavyo...

Kwahiyo, kwa lugha inayoeleweka, Mkandarasi HANA SIFA za kupewa hiyo kazi lakini serikali ya Rais Mtukufu bado ikatoa kazi kwa Mkandarasi asiye na sifa!

Yaani, kwa maana nyingine tulimpa kazi Middle Man...

Na pesa anapewa Middle Man

Middle Man anachukua chake, na kinachobaki anawapa subcontractors wanaofanya kazi yenyewe!!

Yaani ni sawa na mtu unampa kazi Civil Contractor akujengee mjengo halafu nae ana-subcontract kila idara including civil works!
Lazima tufahamu ya kawmba huu mradi umejengwa kwenye eneo la urithi wa asili ulio chini ya UNESCO hivyo makampuni mengi makubwa yalikataa kwa kua yangekua blacklisted.
Hivyo ikabidi nchi iamue kumpa mwarabu ili akisubcontract sawa tu ilimradi mradi huu ukamilike kwa kua tulikuwa hatuna namna wakubwa walitubana.
Makamu wa Rais anajua hii maneno so tusilaumiane km tutalipa mzigo ule ule tuache kazi iendelee.
Mwandishi umesema kua mafuriko ya covid ndio yalisababisha delay si kweli wakati wa covid kazi pale ilifanyika isipokua kuna wakati kuna mafuriko yalitokea ambayo yalisimamisha kazi pale power house.
Tuache siasa kwani hata hapa jf kuna taarifa iliwahi kuandikwa ikieleza kampuni ya Elsewedy ambayo ni mojawapo ya wajenzi wa bwawa ilitakiwa kuwa blacklisted.
Tuseme tu tulikua hatuna pa kwenda ndio maana mwarabu alipewa hiyo kandarasi.
 
Kama sijakuelewa vile unauza madaraja, sitaki hata kujua unapohifadhi hizo inventory zako.

Au unataka discussion za realistic energy investment, maana hiyo ndio ilikuwa sababu ya kusema kule Twitter wana mijadala delusional.

Hapana. Haikuwa kuhusu energy investment.
Unajua these people are so delusional.

Kuna dunia ya JF and real world, wao kabisa wanaamini vile vilio vya wananchi kwenye msiba eti wale watu walikuwa wanafurahia baadhi ya watu hasa matajiri kupata shida.

Asilimia kubwa ya raia wenyewe ukiwauliza wakutajie hata baraza la mawaziri awalijui; mfano shangazi yangu.

Shangazi urithi alioachiwa na mumewe vipesa vyake akakimbiza watoto wake ulaya na yeye mwenyewe kwa sababu wa mwisho alikuwa bado mdogo ilibidi akae nae japo kwa miaka 5.

Kurudi 2001 anakuta viwanja vyake watu washajenga, vingine vinewekewa fense. Kapigana kuanzia muda huo; mpaka Magufuli alipoingia madarakani, miezi sita mingi kavipata vyote. Umwambii lolote kuhusu Magufuli japo maisha yake ya kubangaiza tu mtaani; sio yeye hizo story ni nyingi.

Hawa watu wana Magufuli wao wa JF na Twitter; na raia wana Magufuli wao kwenye maisha yao. Ni Magufuli wawili tofauti.

Yapo mengi naweza kuleta hapa lakini sina haja.
 
13 October 2021

Majumuisho ya Ziara ya Makamu wa Rais : Mradi wa JNHPP / STIEGLER'S GORGE RUFIJI upo nyuma ya muda ulioainishwa ktk mpango kazi


  • Mashine na mitambo
  • Tanesco
  • Udhaifu wa mkandarasi
  • Wafanyakazi wa mkandarasi hawatoshelezi
  • Kuwepo kutoelewana juu ya Tafsiri ya mkataba
  • Sub contractors
  • Mapungufu makubwa ya Uwezo na ujuzi wa main contractor
  • Tanesco wanaupungufu wa wahandisi, wanasheria na wafanyakazi
  • Majaribio ya ku test umeme yatakuwa na mashaka mradi ukukamilika
  • Mvua nyingi
  • Uviko 19
Source : Tanesco Yetu
 
Wakati akitoa maelekezo alipotembelea mradi wa kufua wa umeme wa stiglers gorge , Mh. Mpango alipongeza kwa kazi nzuri unayoendelea na kuongea mengi yakiwemo
1. Mkandarasi Hana Uzoefu wa kutosha katika ufanyaji wa kazi zake huku akisema kwasababu anatumia subcontractor kwa karibu kazi zote kila sehemu. Serikali labda ilitaka mkandarasi mkuu afanye kazi zote peke yake, lakini sehemu nyingi ameweka wachina
2. Mkandarasi yupo nyuma ya mpango kazi, na kwamba amechelewa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mafuriko na uvico19. Kauli ambayo Kalemani amekuwa akitudanganya kuwa tupo mbele ya muda na maji yataanza kujazwa Mwezi wa 11 tarehe 15, na kuwasha mitambo June 2022( KAULI AMBAYO NI DHAHIRI ALITUDANGANYA NA ILIKUWA YA KISIASA) Laini Makamu wa Rais ameongea ukweli.

Kutokana na Kauli ya Mh. Makamu wa Rais ni DHAHIRI kuwa Mradi huu hautaweza kukamilika 2022 Wala 2023 Wala 2024 labda 2025.
Makamu hana maadili na hajui nini cha kusema kwa nani mazingira gani wakati gani na asemeje. Utopian Vp!
 
Well said mkuu, hata mimi kauli ya makamu wa rais imenishangaza sana - binafsi si amini kama Dr.Mpango ameyasema hayo, kama kweli basi kuna tatizo down the line hasa hasa kwa watu wanao mshauri - kwani mkabdarasi mkuu wa Misri kakosea nini kiutendaji, kiutekelezaji na kiufundi - kakosea nini ku-subcontract Wachina ? Ninacho kiona Mimi kuna kundi la watu wamejipanga kukwamisha mradi huu kwa kuendekeza uchonganishi na fitna.

Watu wenye uelewa mpana wa Project Management mradi unaonekana unendeshwa kiufanisi ukiwekea maanani changa moto ya ugonjwa wa kovid na mafuriko/masika, binafsi naona wamejitahidi sana sana, hizi tabia za watanzania wenzetu za kutaka kuchonganisha watu pamoja na hujuma - traits za namna hiyo hazifahi haya kidogo.
Wamisri wakisikia kauli hizi za Mpango haitaleta picha nzuri
 
binafsi si amini kama Dr.Mpango ameyasema hayo, kama kweli basi kuna tatizo down the line hasa hasa kwa watu wanao mshauri - kwani

Bandiko # 83 hapo juu ktk Video Makamu wa Rais bila kumungunya maneno ktk video hiyo ya Tanesco Yetu anelezea mapungufu yote ikiwemo ya main contractor kukosa uwezo na ujuzi. .
 
Hapana. Haikuwa kuhusu energy investment.


Yapo mengi naweza kuleta hapa lakini sina haja.
Basi itakuwa unataka kunitungia uongo maana sina interest ya twitter discussion recently zaidi ya maswala ya nishati.

Either kukurupuka Kwa waziri kuhusu LNG, fantasy za kuuza 20% ya TANESCO etc with their nonsense. Kama ni nje ya hapo labda umechanganya wachangiaji.

Huko kwenye biashara yako ya madaraja good luck.
 
Wakati akitoa maelekezo alipotembelea mradi wa kufua wa umeme wa stiglers gorge , Mh. Mpango alipongeza kwa kazi nzuri unayoendelea na kuongea mengi yakiwemo
1. Mkandarasi Hana Uzoefu wa kutosha katika ufanyaji wa kazi zake huku akisema kwasababu anatumia subcontractor kwa karibu kazi zote kila sehemu. Serikali labda ilitaka mkandarasi mkuu afanye kazi zote peke yake, lakini sehemu nyingi ameweka wachina
2. Mkandarasi yupo nyuma ya mpango kazi, na kwamba amechelewa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mafuriko na uvico19. Kauli ambayo Kalemani amekuwa akitudanganya kuwa tupo mbele ya muda na maji yataanza kujazwa Mwezi wa 11 tarehe 15, na kuwasha mitambo June 2022( KAULI AMBAYO NI DHAHIRI ALITUDANGANYA NA ILIKUWA YA KISIASA) Laini Makamu wa Rais ameongea ukweli.

Kutokana na Kauli ya Mh. Makamu wa Rais ni DHAHIRI kuwa Mradi huu hautaweza kukamilika 2022 Wala 2023 Wala 2024 labda 2025.
Hili John Heche alilisema bungeni wabunge wa ccm ikiwemo Mpango mwenyewe walilipinga na kumzodoa Heche.

Bagamoyotuletee video ya John Heche juu ya mkandarasi kutokuwa mzoefu na ujenzi wa mabwawa ya umeme.
 
Madhara ya chanjo yanaanza kuonekana mapema ....samia karopoka mara kibao ,,, leo tena karopoka makamu ..


Duuh
 
Well said mkuu, hata mimi kauli ya makamu wa rais imenishangaza sana - binafsi si amini kama Dr.Mpango ameyasema hayo, kama kweli basi kuna tatizo down the line hasa hasa kwa watu wanao mshauri - kwani mkabdarasi mkuu wa Misri kakosea nini kiutendaji, kiutekelezaji na kiufundi - kakosea nini ku-subcontract Wachina ? Ninacho kiona Mimi kuna kundi la watu wamejipanga kukwamisha mradi huu kwa kuendekeza uchonganishi na fitna.

Watu wenye uelewa mpana wa Project Management mradi unaonekana unendeshwa kiufanisi ukiwekea maanani changa moto ya ugonjwa wa kovid na mafuriko/masika, binafsi naona wamejitahidi sana sana, hizi tabia za watanzania wenzetu za kutaka kuchonganisha watu pamoja na hujuma - traits za namna hiyo hazifahi haya kidogo.
Power struggle ndani ya CCM nguvu ipo upande wa mama 2025, watu wanafikiria umakamu wa raisi mpaka 2030.
 
Mmmhhh..!! Mh. Mpango anasema mkandarasi hana uzoefu wa kutosha? Sasa alipewaje kazi? Kama ni sub-contractor na hana uzoefu wa kutosha, atajenga ktk viwango vya kimataifa kweli Bwawa letu la umeme? Au ndio mwanzo wa figisu?
Mpango si alikuwa waziri wa Fedha na alikuwa mstari wa mbele ktk ujenzi wa bwawa hili na bungeni alitetea sana, kama mkandarasi hana uzoefu kwa nafasi yake akiwa waziri wa fedha alishindwa nini kusema haya leo anayosema mapema?
CCM imejaa wanafiki na Mpango mwenyewe hoja ya mkandarasi kukosa uzoefu walilipinga bungeni na ccm wenzie.

Nimeshasema hili bwawa huko mbeleni litasimama kujengwa ili wezi wa nchi waanze tena kupiga hela za Tanesco.
Muda utasema
 
Mkandarasi wa miradi mikubwa kama hiyo anashinda tender kutokana na design yake ya mradi wote kuanzia physical project, ulinzi wa mazingira kama ecosystem, namna ya kuvuta maji and so forth with hydro power project scope.

Anakupa na costs zake za kujenga mradi, work break down structure ya wewe kuweza kufuatilia progress ya mradi kwa makubaliano ya muda wa kazi, etc.

Kazi yenyewe inafanywa na sub-contractors anachosimamia mkandarasi na ku coordinate hatua za kazi, kuangalia quality ya kazi, time, anapanga critical path ya mradi na other supervision roles.

Mtu kama makamu wa raisi awezi kwenda kwenye mradi kama huo bila ya mshauri wa maswala ya project management; hivi mbona tunaviongozi waropokaji halafu wepesi sana vichwani ukiwasikiliza.

Au anadhani huu sawa na miradi wa kujenga barabara. Yaani nchi inaviongozi wa ovyo kweli.
Kuna kipindi wajumbe wa kamati ya bunge walienda kukagua ujenzi wa barabara ya lami wakawa wanaibonyeza kwa mikono kujua uimara wake.
 
Bandiko # 83 hapo juu ktk Video Makamu wa Rais bila kumungunya maneno ktk video hiyo ya Tanesco Yetu anelezea mapungufu yote ikiwemo ya main contractor kukosa uwezo na ujuzi. .
Sorry, maoni/ushauri was Dr.Mpango's huko valid kabisa nilikuwa sijasikiliza/angalia video clip yake kwa kuwa ilikuwa pages za nyuma kabisa.
 
Mkandarasi wa miradi mikubwa kama hiyo anashinda tender kutokana na design yake ya mradi wote kuanzia physical project, ulinzi wa mazingira kama ecosystem, namna ya kuvuta maji and so forth with hydro power project scope.

Anakupa na costs zake za kujenga mradi, work break down structure ya wewe kuweza kufuatilia progress ya mradi kwa makubaliano ya muda wa kazi, etc.

Kazi yenyewe inafanywa na sub-contractors anachosimamia mkandarasi na ku coordinate hatua za kazi, kuangalia quality ya kazi, time, anapanga critical path ya mradi na other supervision roles.

Mtu kama makamu wa raisi awezi kwenda kwenye mradi kama huo bila ya mshauri wa maswala ya project management; hivi mbona tunaviongozi waropokaji halafu wepesi sana vichwani ukiwasikiliza.

Au anadhani huu sawa na miradi wa kujenga barabara. Yaani nchi inaviongozi wa ovyo kweli.
Logic!
viongozi wetu ni level za kawaida sana
 
Sasa hapo tumwamini yupi? Kalemani alilihakikishia bunge kuwa tarehe 15 Novemba kabla ya saa 12 jioni bwawa litakuwa limejazwa maji. Kwahiyo mkuu unataka kuniambia tuanze kuliita bwawa la Babeli?
Naomba video plse
 
Mmmhhh..!! Mh. Mpango anasema mkandarasi hana uzoefu wa kutosha? Sasa alipewaje kazi? Kama ni sub-contractor na hana uzoefu wa kutosha, atajenga ktk viwango vya kimataifa kweli Bwawa letu la umeme? Au ndio mwanzo wa figisu?
Mpango si alikuwa waziri wa Fedha na alikuwa mstari wa mbele ktk ujenzi wa bwawa hili na bungeni alitetea sana, kama mkandarasi hana uzoefu kwa nafasi yake akiwa waziri wa fedha alishindwa nini kusema haya leo anayosema mapema?
Mkuu muonee tu huruma mpango jamaa ni puppet kaagiza aseme tu hivyo. Mpango sidhani hata anafurahia kuwa makamu. He is so soft spoken and innocent. Kalazimishwa tu aseme hivyo.
 
Back
Top Bottom