Dkt. Mpango: Vijana achaneni na kupenda mashangazi

Dkt. Mpango: Vijana achaneni na kupenda mashangazi

Hana kazi wala majukumu huyo!
Mshahara anapata wa bure na ndio maana hajuwi wala kuelewa cha kuongea!
 
Hii speech ilibidi iwe ya Kiswahili. Kaongea mambo mengi mazuri yanayosababishwa na ujingaujinga wa CCM
 
Wakuu mmesikia huko alichokisema Dkt. Mpango kuhusu Mashangazi?

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philiph Mpango, amesema zinahitajika tafiti za kina pamoja
Yeye amejuaje???
Mishangazi ndo huwa inampelekea malalamiko?
 
Huyo dr ana ubongo kichwani kweli.!????

Ni kweli vijana tuache lakini pia na hao mashangazi waache kutusumbua sisi vijana...

BICHWA KOMWE - hii inakuhusu
Kutumia muda mwingi bila kufanya kazi kwa kushinda Vijiweni, uchezaji kamari, utupaji taka ovyo, uchomaji moto ovyo wa nyasi na misitu pamoja na ubinafsi.
 
Hadi Dr Mpango anajua mashangazi...khaas basi sawaa...watoto siku hizi hawataki kunukka mavi kju bandaniii ila tu wawepo Sports Bar daily....suruali kulegezaa na betting
 
Unapotaka kuzuia tatizo usikomalie upande mmoja, bana au komalia pande zote ili tatizo liishe
 
Wakuu mmesikia huko alichokisema Dkt. Mpango kuhusu Mashangazi?

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philiph Mpango, amesema zinahitajika tafiti za kina pamoja na mikakati katika kufanya mapinduzi ya kitamaduni kubadili tabia na mazoea yasiyofaa yanayojitokeza katika Jamii hivi sasa ambayo ni kikwazo kwa maendeleo.

Dkt Mpango amesema hayo wakati akifungua mkutano wa kusherehekea miaka 30 ya Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) uliyofanyika Jijini Dar es salaam ambapo ametaja baadhi ya mazoea na tabia hizo ni pamoja na kutojali muda, kutokuwa na uaminifu mahali pa kazi pamoja na kutumia njia zisizofaa katika kupata kipato.

Makamu wa Rais ameitaka ESRF pamoja na Watalaam wa Fikra Tunduizi (Think Tank) kuangazia pia tabia za hivi karibuni za Vijana kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wanawake waliyowazidi umri (Mashangazi) kama njia rahisi ya kujikimu, kutumia muda mwingi bila kufanya kazi kwa kushinda Vijiweni, uchezaji kamari, utupaji taka ovyo, uchomaji moto ovyo wa nyasi na misitu pamoja na ubinafsi.

Pia Makamu wa Rais amesema ni muhimu kuangazia tabia nyingine kama vile matumizi makubwa ya fedha katika anasa kuliko kuweka akiba ikiwemo uchangiaji zaidi katika matukio ya sherehe na tafrija kuliko kusaidia gharama za elimu na matibabu kwa familia za kipato cha chini.
Soma: Kuhusu utafiti wa tatizo la ajira, Dkt. Mpango usihadae Watanzania
Isije kuwa anatoa onto kwa kijana fulani, kwa mtindo wa hotuba.
 
Kwamba mna-mapenzi na Wazee 😅

Niko nasubiri bahati yangu kwako, kama utanipenda na umri wangu wa miaka 78 nilionao 😜
Hakuna shidaa, kama unaona unaweza kupendwa ni vyema, si unajua vigezo lakni🤪
 
Wakuu mmesikia huko alichokisema Dkt. Mpango kuhusu Mashangazi?
Mkuu ameshindwa kutambua kua Mashangazi nimatokeo ya wazee kupungua ufanisi wako busy na kazi yakuliibia Taifa wanasagau kama wana wake nyumbani na wanaweka nguvu kwa vibinti vidogo sasa kuepuka ushindani usio wa lazina hawa vijana ambao ajira hamuwapi na mademu zao pia mnawataka kwanini wasijipumzishe kwa mishangazi kuziba hiyo nakisi mnayoyasababisha mana nao ni watu wanahitaji furaha🤣🤣🤣kama mnavyopata kwa watoto wa 2000
 
Back
Top Bottom