Dkt. Mwigulu: Chanjo za Corona zimefanyiwa utafiti nchi za baridi zitawafaaje watu wa Dar es Salaam?

Umetetea ujinga tupu...!! Kazi Yao ni nini ,? Kwa hyo wapo pale kusubir kauli ya Raisi , acheni exaggeration kwenye vtu vya msingi....kwamba Raisi alikuwa amekataa aisee....
 
Kumwita Baby kihiyo si sawa, hatujui kwa nini hakuuliza swali hilo lkn Baby si kihiyo, ni mmoja wa watangazaji bora nchini na mwenye exposure kubwa sana sana! Mfuatilie kwa jicho la karibu utaniunga mkono siku moja. The best in Tanzania!
Hawa wakuu wanakuja na mikwala kwenye interview mpaka waandishi mnasahau maswali!!!
 
Tatizo mnajifanya mnajua kila kitu. Plasmodia ni endoparasites. Anaishi popote pale ambapo mwenye nao ataishi. Ambaye haishi kwa baridi ni mbebaji wa pili wa plasmodia, yaani mbu, anopheles.
Kirusi sio mdudu. Na provided kinatoka kwa mtu kwenda kwa mtu, hakiwezi athiriwa na hali ya hewa.
 
Huyu bwana ni miongoni mwa mawaziri ambao muda wote midomo yao ipo kama ya panya zinazotafuta mazao ghalani.Muda mwingi ni nyenyenye Mwingine ni jafo.
 
... joto la mwili wa binaadam mwenye afya ni lilelile akiwa nchi za baridi au za joto (36 degrees centigrade)!
... people who argue without research will call batshit 'black rice'!
👊 😅✌️💥
 
Sijaelewa kwanini corona peke ake ndio huwa wanaihusisha na baridi na joto. Kwanini madawa au chanjo nyinginezo huwa hawatoi huu utopolo.
 
Pale mwanasiasa anapojaribu kuingilia suala la kisayansi ili kulinda tu ugali wake.

Kwa hiyo Mwigulu anataka kutuaminisha ya kwamba yeye ana akili kuliko hao scientist?
Nimuulize zile chanjo nyengine zinazotumika kwenye cold chain hapa nchini zilitengenezwa na ku testiwa wapi?
 
Siku hizi Wachumi nao wanatoa ushauri kuhusiana na magonjwa?
Kama ugonjwa huo ungekuwa wa Wazungu tu mbona umefika huku Africa?
 
Hizi Ph.D za kuchapia ndio taabu yake; Waziri mzima hajui kuwa Ulaya na Marekani kuna sehemu zenye hali ya heba sawa na Tanzania!!
 
Marekani yote ni baridi? Japan je? China je? Iran jee Israel je? huko pia ni baridi?
Hawa watu ni wapuuzi tu. Kwanza hawajui hata majaribio yalifanyika wapi. Wanafikiri majaribio yalifanyikia sehemu moja. Kuna nchi zenye joto kama nchi za Uarabuni? Mbona wameshanja watu wao wengi tu. Lakini huyu simshangai sana. Ndiye aliyesema tusitoe takwimu na kupewa uwaziri,.
 
Mbona ARV hazikufanyiwa utafiti tangu zimeingia 2004 na zimewasaidia wengi kuendelea na maisha kama kawaida?
 
Trump aligeuka daktari. Mpaka kufikia jana Wamarekani 500,000 wamekwenda na Korona. Wataalamu wanasema kama angesisitiza tu watu wachukue tahadhari kwa kuvaa barakoa na social distancing vifo hivyo vingeweza kupunguzwa zaidi ya nusu. Inaonekana kitu kile kile kinatokea hapa kwetu pia. Kila mwanasiasa sasa ni daktari ili tu kumfurahisha mfalme. Sad !!!

 
Wangemuuliza kwanini kila chanjo yetu (TB, Pepopunda, tetanus, Surua, ndui etc.) imeletwa na mabeberu? Lini zamu yetu na sisi wa nchi za Joto kutengeneza yetu?
 
Muulizeni Mwigulu, utafiti wa chanjo ya polio ilifanyikia Sudan?. Kama ni ulaya, mbona yeye na watt wake wafanyiwa chanjo hiyo?.
Elimu za siku hizi naona ni ora mtu apate kazi, na sio kuelimika.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…