Dkt. Mwigulu, inakuwaje mnatuambia Miradi ya Hayati Dkt. Magufuli inaendeshwa kwa mikopo mikubwa na migumu kuhimilika?

Dkt. Mwigulu, inakuwaje mnatuambia Miradi ya Hayati Dkt. Magufuli inaendeshwa kwa mikopo mikubwa na migumu kuhimilika?

Yaani kwanza bunge lenyewe, lifanywe ' virtual' tu kupunguza gharama za maposho ya kila siku kwa wabunge, kila mbunge akae kwenye jimboni kwake, na wachangie atakachoona kutokea ofisini kwake.... nafikiri tutasevu pesa nyingi.. kazi iendelee.
Sio kupunguza tu posho wazifutilie mbali tu mana bado wana mishahara minono halafu kuna watumishi wana mishahara kiduchu na posho hawana.
I
 
Aaaaah yako mambo ukiyaangalia... unaukumbuka ule usemi "aljununu fununu" - hata uenda wazimu nao ni fani (kila mmoja anayo namna yake)

Haya shime tuongeze juhudi ya mapambio na vigelegele...

 
Nchi inajengwa na mwananchi mwenyewe, nashauri waziri kila Mtanzania ana wajibu wa kulipa kodi ili kujenga nchi yake,uangaliwe utaratibu wa day worker au vibarua wa viwandani,migodini.

Kwenye miradi mbalimbali ya serikali na binafsi nao wanawajibu wa kulipa kodi kama analipwa 5000 kwa siku akikatwa hata 200 inatosha ajira zisizo rasmi zina watu wengi kushinda hata watumishi walio kwenye ajira rasmi, utekelezaji wake ni simple tu kila kiwanda.

Mgodi, au kwenye mradi wowote mkubwa lazima wawe na rekodi ya vibarua wao walio fanya kazi kwa kila siku na kiasi wanachowalipa na wakati wa kuwalipa wanakata kodi kabisa TRA wapo makini sana hii kazi haiwezi kuwa ngumu kwao, nchi za ulaya viwandani hii imeshazoeleka.
Wabunge wako wanakatwa kodi?
 
Kuhimili usafirishaji wa mizigo mizito reli ni muhimu sana, barabara zetu hazina viwango vya kuhimili presha kubwa ya magari ya mizigo na abiria. Ninachoona hapa waziri yuko desperate ni namna gani hiyo miradi itakamilika ndani ya muda mchache na bila kutumbukiza nchi kwenye madeni makubwa ya mikopo...
 
HII nchi inawalipa kodi wengi sana ila nchi yenyewe iko gizani, na viongozi wako gizani. Natamani ningekutana na mama Samia siku moja ningekuwa na LA kumwambia. Watu tulioko chini ni vigumu sana kuonekana.
 
Mwenda zake aliacha akikusanya kodi ya shillingi trillioni 1.9,toka ameondoka machi, april makusanyo yamefikia trillioni 1.3,na kwa sa hv hizi mbio za covid zinazoanzishwa tutafikia bilioni mia 800 hadi 900 mwisho wa mwaka.

Wakati katika kila mwezi tunatakiwa tulipie bilioni 700 kwa ajili ya madeni tu.

Mwendazake aliacha trilioni 9 hazina sasa zipo 6.

Kazi iendelee
Hizi ni pamoja na hela za halmashauri, hela ambazo task force ya TRA walikua wanapora kwenye account za wafanyabishara?
 
Hehehe Lugha imeanza kueleweka siku hizi...

Namba inasomeka vyema huko.
 
Mie kwa kweli nilishangaa kwa miradi mikubwa mingi, kuanza kwa pamoja na kutegemea ' smooth ride' kwa nchi maskini kama yetu'.. Wenzetu kwa hizi big projects, huwa wanajaribu kufanya kitu kinaitwa' Projects stagerring' kujaribu kupunguza matatizo kama haya tuliyokumbana nayo ya kutokuwa na uwezo wa smooth project financing......haya bana, kazi iendelee.
Yaani mradi uwe nje ya muda kisha bado useme hakuna mradi uliosimama?. Kama haujasimama kipi kimefanya usimalizike kwa wakati? Hilo neno kuwa mradi unaouna kwa macho ndio neno lililotumika kuwapambaza watu wa aina yako. Ww ndio wale wakiona mtoto wake kavaa uniform na kubeba madaftari, basi wanaamini huko darasani anasoma.
 
Yaani mradi uwe nje ya muda kisha bado useme hakuna mradi uliosimama?. Kama haujasimama kipi kimefanya usimalizike kwa wakati? Hilo neno kuwa mradi unaouna kwa macho ndio neno lililotumika kuwapambaza watu wa aina yako. Ww ndio wale wakiona mtoto wake kavaa uniform na kubeba madaftari, basi wanaamini huko darasani anasoma.
Naamini tatizo lako laweza kuwa haujawahi kusimamia mradi Wala kujua mradi unavyoendeshwa. Vile vile hujui gharama za kuchelewesha mradi
 
Kwa ujumla, awamu ya 5, zaidi ilitegemea ulaghai ili kutafuta kuungwa mkono, hasa na watu wajinga. Na hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya yeye kuzuia mikutano ya vyama vya siasa, na uhuru wa vyombo vya habari, kwa kuhofia kuwa hata wale wajinga wanaweza kueleimika wakaujua ukweli.
Wewe ni mmojawapo wa watu wajinga tena usiejielewa. Ulaghai kwa vitu ambavyo vinaonekana? kila mradi aliosema na kuahidi, ametekeleza kwa vitendo tena bila kutetereka. Sasa kama warithi wake wameshindwa kukusanya kodi ili wamalizie hiyo miradi, unawezaje kumlaumu yeye?
 
Mwenda zake aliacha akikusanya kodi ya shillingi trillioni 1.9,toka ameondoka machi, april makusanyo yamefikia trillioni 1.3,na kwa sa hv hizi mbio za covid zinazoanzishwa tutafikia bilioni mia 800 hadi 900 mwisho wa mwaka.

Wakati katika kila mwezi tunatakiwa tulipie bilioni 700 kwa ajili ya madeni tu.

Mwendazake aliacha trilioni 9 hazina sasa zipo 6.

Kazi iendelee
Dingi yenu alikuaga mwongo kichizi.

Hizo 1.9trillion unajumlisha na zile pesa za kubambikia watu makosa ya uhujumu uchumi.

Bure Sana yule dingi.
 
Hizi ni pamoja na hela za halmashauri, hela ambazo task force ya TRA walikua wanapora kwenye account za wafanyabishara?
Taja mfano halisi wa account hata moja na kiasi kilichoporwa pamoja na tarehe husika, kitu ambacho naamini watanzania wengi wanadaiwa malimbikizi ya kodi hivyo kulipa kwa mkupuo inakuwa ni shida.
 
Naamini tatizo lako laweza kuwa haujawahi kusimamia mradi Wala kujua mradi unavyoendeshwa. Vile vile hujui gharama za kuchelewesha mradi

Nilijua tu huna jipya. Maana sioni maelezo ya msingi zaidi ya porojo zilezile.
 
Nilijua tu huna jipya. Maana sioni maelezo ya msingi zaidi ya porojo zilezile.
Hata kama porojo ni zile zile lakini hatujawahi kusikia miradi ikikwama kipindi cha hayati JPM. Na hii imechangiwa kiasi kikubwa na mpango mzuri wa makusanyo
 
“Hatujaweka kodi kwenye laini za simu kama ambavyo baadhi ya wananchi wamekuwa wakichanganya, hata kule Bungeni wanachanganya wanasema sasa kila siku itakuwa inakatwa shilingi 10 mpaka 200 kwa hiyo kama ni 200 kwa siku 30 ni shilingi 6000, halafu hata kama hukuweka fedha, siku ukiweka inakatwa kama nipige tafu, hatukuweka hivyo”, alieleza Dkt. Nchemba.

Alibainisha kuwa haimaanishi kwamba shilingi 10 sio mzigo lakini Serikali iliangalia matatizo yaliyopo na kugundua kuwa yanagharimu zaidi, kuliko thamani ya shilingi 10 itakayotozwa kama kodi.

Alifafanua kuwa miradi mikubwa inayotekelezwa nchi ukiwemo wa mradi wa Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere ambao unahitaji zaidi ya shilingi trililioni nne na ujenzi wa Reli ya Kisasa unaohitaji zaidi ya shilingi trilioni 20 ili kukamilika, iwapo fedha zote zitategemea mikopo nchi itapitiliza uwezo wa kukopa na kutokukopesheka hivyo ushiriki wa wananchi ni muhimu.

My Take:
Leo mmeamua kutuvisha zigo la kujenga Reli na Bwawa la Stiegglers kupitia simu zetu wakati mlituambia fedha ipo na mipango ilikuwa tayari mezani. What went wrong?? (In Dk Mpamire`s voice).
Ndugu yangu inaumiza na inakera sana.

Utawala uliopita ulijaa ghiliba sana katika kuendesha nchi. Walisema nchi yetu ni tajiri, na miradi hiyo tunaitekeleza kwa pesa zinazotokana na makusanyo ya mapato yetu ya ndani. Walienda mbali kwa kusema zamani haikuwezekana kwasababu pesa zilikuwa kwa mafisadi, sasa mafisadi yamebanwa na pesa ya miradi inapatikana.

Watanzania wenzetu wengi, wakiwemo wasomi waliamini hiyo kauli ya kitapeli.

Kauli hizo zililenga kujipatia umaarufu wa kisiasa zaidi kuliko uhalisia.

Waziri wa fedha wa wakati huo mara kwa mara alitoa kauli bubgeni kuwa deni letu ni himilivu na kwamba kwa trend ya deni letu la nje bado tuna sifa ya kukopesheka kwa miaka mingine mingi.

Sasa imefika wakati wa sisi wananchi kubebeshwa gharama za madeni bila kujali vipato vyetu.

Wacha cha moto tukione.
 
Mwenda zake aliacha akikusanya kodi ya shillingi trillioni 1.9,toka ameondoka machi, april makusanyo yamefikia trillioni 1.3,na kwa sa hv hizi mbio za covid zinazoanzishwa tutafikia bilioni mia 800 hadi 900 mwisho wa mwaka.

Wakati katika kila mwezi tunatakiwa tulipie bilioni 700 kwa ajili ya madeni tu.

Mwendazake aliacha trilioni 9 hazina sasa zipo 6.

Kazi iendelee
Acha maneno mengi weka data mezani ili tuamini hiko unachosema
 
Ndugu yangu inaumiza na inakera sana.

Utawala uliopita ulijaa ghiliba sana katika kuendesha nchi. Walisema nchi yetu ni tajiri, na miradi hiyo tunaitekeleza kwa pesa zinazotokana na makusanyo ya mapato yetu ya ndani. Walienda mbali kwa kusema zamani haikuwezekana kwasababu pesa zilikuwa kwa mafisadi, sasa mafisadi yamebanwa na pesa ya miradi inapatikana.

Watanzania wenzetu wengi, wakiwemo wasomi waliamini hiyo kauli ya kitapeli.

Kauli hizo zililenga kujipatia umaarufu wa kisiasa zaidi kuliko uhalisia.

Waziri wa fedha wa wakati huo mara kwa mara alitoa kauli bubgeni kuwa deni letu ni himilivu na kwamba kwa trend ya deni letu la nje bado tuna sifa ya kukopesheka kwa miaka mingine mingi.

Sasa imefika wakati wa sisi wananchi kubebeshwa gharama za madeni bila kujali vipato vyetu.

Wacha cha moto tukione.
si ndo huyu VP ?
 
Back
Top Bottom