Dkt. Mwigulu Nchemba ateua wadau watakaotoa elimu ya mlipa kodi; wamo Hamisa Mobetto, Edo Kumwembe na Mbwana Samatta

Dkt. Mwigulu Nchemba ateua wadau watakaotoa elimu ya mlipa kodi; wamo Hamisa Mobetto, Edo Kumwembe na Mbwana Samatta

Nyie mnaopinga hapo juu mnajielewa? Wewe uliyesoma upo mbwinde huko na mbwana samatta au edo kumwembe nani ana fan base kubwa na anaweza kusikilizwa akihamasisha kodi?
Hata siku moja kodi haiwezi kulipwa kutokana na HAMASA!!au kampeni bali ni kiwango hicho cha kodi kama ni rafiki kwa mlipa kodi, umeshawahi kujiuliza ni kwanini wazungu hawatumii nguvu nyingi kwenye ukusanyaji kodi?!!kocha wa uganda aliwaambia makocha wa Tz, kuwa badala ya kufundisha mbinu za mpira kwa timu za taifa, wao muda mwingi wanautumia kwenye HAMASA!!HAmasa haziwezi kushinda uwezo!!inshu sio kuwa na fan base kubwa kwenye mitandao eti ndio uweze kumahasisha watu kulipa kodi?mbona hakuna hata uhusiano?!!
 
Hii ndo nimewahi kuisemea. Kuna watu wajinga kiasi kwamba hata kujinyonga hawawezi! Mwigulu anasemekana ana PhD. PhD inaweza kuwa kwenye kichwa kibovu kiasi hiki? Ni tatizo sana.

Yaani aonavyo hao ni wawakilishi wa mlipa kodi wa maana nchi hii? Au alimaanisha mabalozi wa elimu ya usanii? Vijana wapende michezo na usanii.


Tena ni zaidi ya usanii maana wengine hawana uadilifu hata kidogo.

Wavaa vichupi kwa hiyo wengine wahamasike kuvaa vichupi ili waje wateuliwe ubalozi?

Tunajenga jamii ya aina gani?

Ya wasio waadilifu kuonekana wanafaa?

Seriously?
 
Watu hawaelewi kwamba apo ameangalia watu wenye fan base kubwa kuna watu kwa kuona sura ya mobeto watalipa kodi bila shuruti

Sent from my TECNO-J5 using JamiiForums mobile app
Foolish! Ukitaka ku-promote kondom hapo sawa! Kodi? Nchi gani duniani unaijua yenye watu wajinga kama wewe na mwigulu kuwa na maono kama hayo?
 
Sijawahi kumuelewa, kumkubali wala kumuamini Mwigulu hata kwa jambo moja. Naona kama ni miongoni mwa mfano mbaya wa wasomi wetu.
 
Huwenda Mwigulu yupo sahihi sana
Hawa ni watu wenye influence kwenye jamii

kuwatumia hawa inafanya elimu watakayotoa kufikia watu wengi zaidi
Na matokeo yanaweza kuwa mazuri

Mfano mimi ningekuwa ndiyo afisa mwenye taaluma yangu ya maswala ya kodi ningetumia chombo gani kutoa elimu ili iwafikie wengi zaidi ingebidi nitumie gharama kubwa na mda mwingi na huwenda nisingefikia watu wengi kama Hamisa atakavyopost kwenye mitandao yake

dunia imebadilika watanzania hatuhitaji kutumia Maguvu ni akili kidogo na mambo yanaenda
Haihitaji wawe na taaluma hiyo kinachohitajika kutoka kwao ni huo ushawishi walio nao tu watachopewa wao ni semina ya nini cha kusema kuhusu maswala hayo ya kodi mbele ya wananchi
Maswala mengine ya kitaalamu wataalam wapo tu kwaajili hiyo

Watu hupelekea matangazo yao redioni kwa kuwa redio zinasikilizwa na watu wengi ni kitu kimoja na hichi alichofanya Mwigulu big up kwake

Leo kuwa na ushawishi/followers Ni mali ndiyo maana watu wanatangaza biashara kupitia hii mitandao na wanafanya vizuri sana sasa kwanini jambo hilo tu ndiyo liwe baya

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Huwenda Mwigulu yupo sahihi sana
Hawa ni watu wenye influence kwenye jamii

kuwatumia hawa inafanya elimu watakayotoa kufikia watu wengi zaidi
Na matokeo yanaweza kuwa mazuri

Mfano mimi ningekuwa ndiyo afisa mwenye taaluma yangu ya maswala ya kodi ningetumia chombo gani kutoa elimu ili iwafikie wengi zaidi ingebidi nitumie gharama kubwa na mda mwingi na huwenda nisingefikia watu wengi kama Hamisa atakavyopost kwenye mitandao yake

dunia imebadilika watanzania hatuhitaji kutumia Maguvu ni akili kidogo na mambo yanaenda
Haihitaji wawe na taaluma hiyo kinachohitajika kutoka kwao ni huo ushawishi walio nao tu watachopewa wao ni semina ya nini cha kusema kuhusu maswala hayo ya kodi mbele ya wananchi
Maswala mengine ya kitaalamu wataalam wapo tu kwaajili hiyo

Watu hupelekea matangazo yao redioni kwa kuwa redio zinasikilizwa na watu wengi ni kitu kimoja na hichi alichofanya Mwigulu big up kwake

Leo kuwa na ushawishi/followers Ni mali ndiyo maana watu wanatangaza biashara kupitia hii mitandao na wanafanya vizuri sana sasa kwanini jambo hilo tu ndiyo liwe baya

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Mkuu Watu wanalipa Kodi Kwa Kuwa Influenced? How Comes? Hili la Mobeto, Kumwembe, Samata Ni Aibu Sana Kwa Vijana wanaosota Vyuoni Wakisomea Kodi. Tungekua Na Viongozi ambao Wako Serious na Majukumu yao, Hizi Nafasi zingeshindaniwa na wanafunzi IFM, TIA, CBE, nk
 
Wafanyabiashara Wanahitaji Elimu Ya Kulipa Kodi, Kwamba Leo Nikilipa Kodi Hyo Kodi Yangu Itaenda Kufanya 1,2,3 Wala Business Tycoons Hawahitaki Kuwa Influenced na Msanii au Mpiga Soga Za Sipotisi Maredioni. Shida Yenu Watu wakija na Hoja Za Msingi Nyie Mnakimbilia Kusema Watu Wanahasra Kwa Sababu YaTeuzi Za Udisii
 
Watu hawaelewi kwamba apo ameangalia watu wenye fan base kubwa kuna watu kwa kuona sura ya mobeto watalipa kodi bila shuruti

Sent from my TECNO-J5 using JamiiForums mobile app

Unless walipa kodi ni wanaume wakware tupu, otherwise this mission is unsuccessful even before it takes of!

Vunja bei ana cheo gani CCM kwa sasa? Hamisa ni nani yake Vunja bei?
 

Tulisema humu ngoma ya watoto haikeshi,huyu Mama alivyopata urais kaanza kuponda misingi aliyoikuta ya ukusanyaji wa kodi,kaanza nakutukana TRA kuwa hawatumii weredi ktk kukusanya kodi, wakati hata Ulaya anakotegema msaada hawabembelezi Mtu/wafanyabiashara kulipa kodi,yeye eti watu walipe kodi kwa hiyari.

Sasa hivi anaanza kuteua vikundi vya wasanii eti waende mitaani kuamashisha watu kulipa kodi,huu ni upotevu mkuu wa mapato yetu , wakati watu wenyewe hawana elimu ya kuelimisha jinsi ya kulipa kodi, Kodi inakusanywa kwa taratibu na mujibu wa Sheria,sio vikundi vya ngoma wala wasanii,Hapa atuna Rais tuna rais wa Wasanii.
 
Back
Top Bottom