Dkt. Mwigulu rudi tena useme vizuri kanusho la serikali "kufulia"

Dkt. Mwigulu rudi tena useme vizuri kanusho la serikali "kufulia"

Dk.amesahau dunia ni ya utandawazi!
Siku zote ukiona mtu fulani anapata title ya kielimu mfano u Dr wakati akiwa na madaraka jua amebebwa!
Kibongo bongo ndivyo ilivyo kwa hivyo usiogope mkuu hiyo ni kawaida sana.
We mheshimu mtu aliyepata wadhifa wa kielimu wakati akiwa nobody kwenye jamii yetu!.
Hao sijui Dr Mwigulu, Dr Jafo, Dr Samia nk nk hamnaga kitu humo...ni mwendo wa connection tuu!!!.
 
Haya ni maneno yale yale ya wabaya wetu alisikika “mheshimiwa” akisema……..
Kuna mwalimu wangu mmoja wa falsafa alikuwa anapenda kusema "Masikini siku zote huamini kila mtu anamchukia na kumdharau"

Ilhali unakuta tajiri yuko busy na mambo yake ila masikini anawaza kuwa tajiri hampendi na anataka aendelee kumdidimiza kumbe unakuta hata hayuko akilini mwa tajiri.

Hawa watu wakiwa nyumbani wanaita mabeberu wakienda nje wanaenda kukopa na msafara wa watu.

Halafu mabeberu hao hao wanatujengea hadi vyoo.!!!
IMG_20240711_212509.jpg
 

Heshima kwenu wakuu wenzangu

Kama mtambuka juzi kati member wa JF na Waziri wa Fedha alikuja humu kukana kwamba serikali haijapungukiwa uwezo wa kifedha. Hoja yake ilijikita kuonyesha serikali ina uwezo mkubwa na kujiendesha na kutekeleza miradi yake.

Naomba wakuu wa JF wamuarifu kuna jamaa amekataa maelezo aliyotoa, labda arejee tena kutoa maelezo ya ziada kupitia haya nitakayoeleza.
Binafsi kwa utafiti mdogo nilioufanya, nimebaini mambo kadhaa yanayopingana na kanusho la Mwigulu.

1. Serikali kushindwa kufanya malipo kwa wakati
Watumishi wa serikali, wazabuni na wakandarasi mtaungana na mimi, ya kwamba kumekuwa na ucheleweshaji usio wa kawaida wa serikali kufanya malipo. Wenyewe wasema malipo hayajashuka. Unaweza kusubiri malipo kwa zaidi ya miezi mitatu. Wakuu wa taasisi wamekuwa wakinawa kwamba tatizo ni BOT na Mfumo wa Malipo wa Pamoja wa TSA. Upo ushahidi wa wakuu wa taasisi kupitisha malipo kwenye mfumo wa malipo MUSE, lakini yanabaki hewani kwa muda mrefu.
Zipo nyakati ambapo katika mwezi malipo yamekuwa yakiachiwa kidogo tu hasa kuanzia tarehe 15 kuelekea mshahara. Yaani mnanyunyiziwa kidogo tu.
Inasikitisha sana unaidai serikali, umewasilisha kila kitu, imepita hata miaka miwili, halafu unaambiwa hela zipo nyingi tu. Maelezo ya Waziri ni chonganishi kati ya wadai na wakuu wa taasisi. Kwamba wanafanya makusudi kutolipa.

2. Adhabu ya kuchelewesha malipo kwa wakandarasi na mifuko ya pensheni matrilioni ya fedha

Mh.Dkt Mwigulu uje hapa utuambie serikali imekuwa na mambo mengi kiasi cha kusahau kulipa wakandarasi na wazabuni wake, ila mapesa yapo mengi tu.
Kama fedha zipo na hamtaki kulipa kiasi cha kuongeza gharama za malipo, basi wewe na wenzako mnaingiza nchi kwenye hasara kubwa sana. Kama ni hivyo, basi unatakiwa kuachia ngazi mara tu baada ya kumaliza kusoma bandiko hili. Ili tukuonee huruma basi ukiri humu kwamba hamna fedha za kutosha. Tutatunza hii siri hapa JF watu wasisikie.
Hoja yangu hii itashadadiwa na taarifa za CAG kwa mwaka uliopita. CAG ameonyesha madeni makubwa na adhabu za matriloni ya fedha kutokana na serikali kushindwa kulipa kwa wakati. Hali hii ni tete kwa ngazi zote, serikali kuu na LGAs
View attachment 3046794
View attachment 3046795
View attachment 3046796

3. Serikali kutelekeza miradi mikubwa ya maendeleo

Mfano rahisi ni kwamba, unapanga kujenga nyumba, unaishia kusafisha kiwanja tu na kumwaga vifusi ya mchanga, kisha unapotea. Au unafika mpaka kwenye lenta, mafundi wanakomaa na kudai chao,unakimbia na hupokei simu. Maana yake nini, kama sio umefulia?

Ndio hali ilivyo kwa serikali ya Mwigulu. Miradi mingi ya serikali imeshindwa kabisa kutekelezwa licha ya kuwekwa kwenye mpango, na mingine imetekelezwa sehemu ndogo kutokana na ukosefu wa fedha. CAG ameyasema hayo katika taarifa zake. CAG anaendelea kusema, kuchelewa kwa miradi hiyo kunafanya gharama za miradi kuwa kubwa kutokana na ongezeko la gharama ya vifaa na ufundi.
View attachment 3046800
View attachment 3046801
View attachment 3046805
View attachment 3046806
.....nitaendelea, ngoja kwanza niote jua. Moderator mwiteni Waziri Dr. Mwigulu Nchemba
Wazabuni na wakandarasi toka mwaka jana wanalia njaa malipo hakuna sasa wao kodi na 'other statutory obligations' wanalipa vipi nchi inapata wapi kodi kwa mwendo huo ajira mpya zitatengenezwa vipi mishahara inalipwaje? Kukauka kwa hazina kuko bayana mpaka mfuko wa barabara (Road fund) hauna kitu sio kwaida hii.
 
Wazabuni na wakandarasi toka mwaka jana wanalia njaa malipo hakuna sasa wao kodi na 'other statutory obligations' wanalipa vipi nchi inapata wapi kodi kwa mwendo huo ajira mpya zitatengenezwa vipi mishahara inalipwaje? Kukauka kwa hazina kuko bayana mpaka mfuko wa barabara (Road fund) hauna kitu sio kwaida hii.
Miradi mingi inasuasua tu
 
Sasa hivi wanaiba vifurushi vya data , , wanaiba ukinunua umeme. Tanzania tunaongozwa na vibaka tupu waliotumia fursa ya katiba nzee kufungia bao la mkono, wameanza kutafuta hela za kampeni feki za kanga na kofia na boksa za kuwapa walala hoi, huku wahesabu kura na wanaotangaza wakipewa ahadi, na hela za kulipa vikoba
 

Heshima kwenu wakuu wenzangu

Kama mtambuka juzi kati member wa JF na Waziri wa Fedha alikuja humu kukana kwamba serikali haijapungukiwa uwezo wa kifedha. Hoja yake ilijikita kuonyesha serikali ina uwezo mkubwa na kujiendesha na kutekeleza miradi yake.

Naomba wakuu wa JF wamuarifu kuna jamaa amekataa maelezo aliyotoa, labda arejee tena kutoa maelezo ya ziada kupitia haya nitakayoeleza.
Binafsi kwa utafiti mdogo nilioufanya, nimebaini mambo kadhaa yanayopingana na kanusho la Mwigulu.

1. Serikali kushindwa kufanya malipo kwa wakati
Watumishi wa serikali, wazabuni na wakandarasi mtaungana na mimi, ya kwamba kumekuwa na ucheleweshaji usio wa kawaida wa serikali kufanya malipo. Wenyewe wasema malipo hayajashuka. Unaweza kusubiri malipo kwa zaidi ya miezi mitatu. Wakuu wa taasisi wamekuwa wakinawa kwamba tatizo ni BOT na Mfumo wa Malipo wa Pamoja wa TSA. Upo ushahidi wa wakuu wa taasisi kupitisha malipo kwenye mfumo wa malipo MUSE, lakini yanabaki hewani kwa muda mrefu.
Zipo nyakati ambapo katika mwezi malipo yamekuwa yakiachiwa kidogo tu hasa kuanzia tarehe 15 kuelekea mshahara. Yaani mnanyunyiziwa kidogo tu.
Inasikitisha sana unaidai serikali, umewasilisha kila kitu, imepita hata miaka miwili, halafu unaambiwa hela zipo nyingi tu. Maelezo ya Waziri ni chonganishi kati ya wadai na wakuu wa taasisi. Kwamba wanafanya makusudi kutolipa.

2. Adhabu ya kuchelewesha malipo kwa wakandarasi na mifuko ya pensheni matrilioni ya fedha

Mh.Dkt Mwigulu uje hapa utuambie serikali imekuwa na mambo mengi kiasi cha kusahau kulipa wakandarasi na wazabuni wake, ila mapesa yapo mengi tu.
Kama fedha zipo na hamtaki kulipa kiasi cha kuongeza gharama za malipo, basi wewe na wenzako mnaingiza nchi kwenye hasara kubwa sana. Kama ni hivyo, basi unatakiwa kuachia ngazi mara tu baada ya kumaliza kusoma bandiko hili. Ili tukuonee huruma basi ukiri humu kwamba hamna fedha za kutosha. Tutatunza hii siri hapa JF watu wasisikie.
Hoja yangu hii itashadadiwa na taarifa za CAG kwa mwaka uliopita. CAG ameonyesha madeni makubwa na adhabu za matriloni ya fedha kutokana na serikali kushindwa kulipa kwa wakati. Hali hii ni tete kwa ngazi zote, serikali kuu na LGAs
View attachment 3046794
View attachment 3046795
View attachment 3046796

3. Serikali kutelekeza miradi mikubwa ya maendeleo

Mfano rahisi ni kwamba, unapanga kujenga nyumba, unaishia kusafisha kiwanja tu na kumwaga vifusi ya mchanga, kisha unapotea. Au unafika mpaka kwenye lenta, mafundi wanakomaa na kudai chao,unakimbia na hupokei simu. Maana yake nini, kama sio umefulia?

Ndio hali ilivyo kwa serikali ya Mwigulu. Miradi mingi ya serikali imeshindwa kabisa kutekelezwa licha ya kuwekwa kwenye mpango, na mingine imetekelezwa sehemu ndogo kutokana na ukosefu wa fedha. CAG ameyasema hayo katika taarifa zake. CAG anaendelea kusema, kuchelewa kwa miradi hiyo kunafanya gharama za miradi kuwa kubwa kutokana na ongezeko la gharama ya vifaa na ufundi.
View attachment 3046800
View attachment 3046801
View attachment 3046805
View attachment 3046806
.....nitaendelea, ngoja kwanza niote jua. Moderator mwiteni Waziri Dr. Mwigulu Nchemba
Mimi kama Mtumishi wa Serikali nimepandishwa Daraja la Mshahara mwezi uliopita nimekuwa "Principal Grade IC" na Mfumo wa ESS unanitambua hivyo na mshahara napata. Sasa hayo mengine mi sijui!
 
Mwasibu umeshusha vitu vizito asee, hoja inajibiwa na vielelezo na sio porojo. Chawa wapite mbali huu Uzi sio level yao huu moto wa Mzee wa fedha
 
Unachoshindwa kuelewa ni kwamba Ufafanuzi wa Dr Mwigullu PhD ni wa kisiasa siyo wa kifinance

Taasisi yoyote inayoshindwa kujiendesha kwa Bajeti yake ya ndani ni Mufilisi na hiyo siyo Dhambi 😄😄
Umeongea points
 
Kuna mwalimu wangu mmoja wa falsafa alikuwa anapenda kusema "Masikini siku zote huamini kila mtu anamchukia na kumdharau"

Ilhali unakuta tajiri yuko busy na mambo yake ila masikini anawaza kuwa tajiri hampendi na anataka aendelee kumdidimiza kumbe unakuta hata hayuko akilini mwa tajiri.

Hawa watu wakiwa nyumbani wanaita mabeberu wakienda nje wanaenda kukopa na msafara wa watu.

Halafu mabeberu hao hao wanatujengea hadi vyoo.!!!
View attachment 3047048
Haya ni MADHARAU. huku ma vi8 yakibugia mafuta tu
 
Wakati wa msiba wa Captain Gardner, nilisikia Kasesela akihojiwa. Dah Ile kauli hadi leo naitafakari sipati jibu. Alisema nyakati za jambo fulani linatrend kuhusu serikali yeye of course na wenzake anaowajua yeye walikuwa watamtumia marehemu ku-spin mambo. Dah Ile kauli hadi leo naitafakari ni jinsi gani watawala wanatufanya wazumbukuku. Kifupi hawataki wananchi kuhoji lolote.
 
Back
Top Bottom