Dkt. Mwigulu rudi tena useme vizuri kanusho la serikali "kufulia"

Dkt. Mwigulu rudi tena useme vizuri kanusho la serikali "kufulia"

Hivi huko kufulia kunakosemwa hakuwezi kupelekea kusimama au kucheleweshwa kwa utekelezaji wa miradi ya DMDP? Mwaka huu benki ya dunia ilitoa mabilioni kwa ajili ya mradi wa bonde la Msimbazi, barabara za jijini, ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali, masoko, stendi kadhaa, maeneo ya wazi na daraja la pale Jangwani ambapo miradi yote hii ingetekelezwa na serikali kupitia DMDP. Hiyo fedha yake haitachepushwa kweli ili kukabiliana na ufuliaji ulioikumba serikali hadi kushindwa kulipa mishahara, stahiki za watumishi, wakandarasi na wengineo kwa wakati?
 

Heshima kwenu wakuu wenzangu

Kama mtambuka juzi kati member wa JF na Waziri wa Fedha alikuja humu kukana kwamba serikali haijapungukiwa uwezo wa kifedha. Hoja yake ilijikita kuonyesha serikali ina uwezo mkubwa na kujiendesha na kutekeleza miradi yake.

Naomba wakuu wa JF wamuarifu kuna jamaa amekataa maelezo aliyotoa, labda arejee tena kutoa maelezo ya ziada kupitia haya nitakayoeleza.
Binafsi kwa utafiti mdogo nilioufanya, nimebaini mambo kadhaa yanayopingana na kanusho la Mwigulu.

1. Serikali kushindwa kufanya malipo kwa wakati
Watumishi wa serikali, wazabuni na wakandarasi mtaungana na mimi, ya kwamba kumekuwa na ucheleweshaji usio wa kawaida wa serikali kufanya malipo. Wenyewe wasema malipo hayajashuka. Unaweza kusubiri malipo kwa zaidi ya miezi mitatu. Wakuu wa taasisi wamekuwa wakinawa kwamba tatizo ni BOT na Mfumo wa Malipo wa Pamoja wa TSA. Upo ushahidi wa wakuu wa taasisi kupitisha malipo kwenye mfumo wa malipo MUSE, lakini yanabaki hewani kwa muda mrefu.
Zipo nyakati ambapo katika mwezi malipo yamekuwa yakiachiwa kidogo tu hasa kuanzia tarehe 15 kuelekea mshahara. Yaani mnanyunyiziwa kidogo tu.
Inasikitisha sana unaidai serikali, umewasilisha kila kitu, imepita hata miaka miwili, halafu unaambiwa hela zipo nyingi tu. Maelezo ya Waziri ni chonganishi kati ya wadai na wakuu wa taasisi. Kwamba wanafanya makusudi kutolipa.

2. Adhabu ya kuchelewesha malipo kwa wakandarasi na mifuko ya pensheni matrilioni ya fedha

Mh.Dkt Mwigulu uje hapa utuambie serikali imekuwa na mambo mengi kiasi cha kusahau kulipa wakandarasi na wazabuni wake, ila mapesa yapo mengi tu.
Kama fedha zipo na hamtaki kulipa kiasi cha kuongeza gharama za malipo, basi wewe na wenzako mnaingiza nchi kwenye hasara kubwa sana. Kama ni hivyo, basi unatakiwa kuachia ngazi mara tu baada ya kumaliza kusoma bandiko hili. Ili tukuonee huruma basi ukiri humu kwamba hamna fedha za kutosha. Tutatunza hii siri hapa JF watu wasisikie.
Hoja yangu hii itashadadiwa na taarifa za CAG kwa mwaka uliopita. CAG ameonyesha madeni makubwa na adhabu za matriloni ya fedha kutokana na serikali kushindwa kulipa kwa wakati. Hali hii ni tete kwa ngazi zote, serikali kuu na LGAs
View attachment 3046794
View attachment 3046795
View attachment 3046796

3. Serikali kutelekeza miradi mikubwa ya maendeleo

Mfano rahisi ni kwamba, unapanga kujenga nyumba, unaishia kusafisha kiwanja tu na kumwaga vifusi ya mchanga, kisha unapotea. Au unafika mpaka kwenye lenta, mafundi wanakomaa na kudai chao,unakimbia na hupokei simu. Maana yake nini, kama sio umefulia?

Ndio hali ilivyo kwa serikali ya Mwigulu. Miradi mingi ya serikali imeshindwa kabisa kutekelezwa licha ya kuwekwa kwenye mpango, na mingine imetekelezwa sehemu ndogo kutokana na ukosefu wa fedha. CAG ameyasema hayo katika taarifa zake. CAG anaendelea kusema, kuchelewa kwa miradi hiyo kunafanya gharama za miradi kuwa kubwa kutokana na ongezeko la gharama ya vifaa na ufundi.
View attachment 3046800
View attachment 3046801
View attachment 3046805
View attachment 3046806
.....nitaendelea, ngoja kwanza niote jua. Moderator mwiteni Waziri Dr. Mwigulu Nchemba
Umeua sooooo!!!!
 
Hivi huko kufulia kunakosemwa hakuwezi kupelekea kusimama au kucheleweshwa kwa utekelezaji wa miradi ya DMDP? Mwaka huu benki ya dunia ilitoa mabilioni kwa ajili ya mradi wa bonde la Msimbazi, barabara za jijini, ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali, masoko, stendi kadhaa, maeneo ya wazi na daraja la pale Jangwani ambapo miradi yote hii ingetekelezwa na serikali kupitia DMDP. Hiyo fedha yake haitachepushwa kweli ili kukabiliana na ufuliaji ulioikumba serikali hadi kushindwa kulipa mishahara, stahiki za watumishi, wakandarasi na wengineo kwa wakati?
Uchepushaji wa mafungu unawezekana hasa kwa awamu hii wanasema wakandarasi fedha za mfuko wa barabara hazipo kitu ambacho sio cha kawaida
 
Uchepushaji wa mafungu unawezekana hasa kwa awamu hii wanasema wakandarasi fedha za mfuko wa barabara hazipo kitu ambacho sio cha kawaida
Mbona wakandarasi wamesima wanalipwa!? mpaka.wameamua kumpatia mama zawadi! au mnazungumzia wakandarasi wa Kenya?
 
Kwa hivyo kupata mshahara wa laki Saba umejiona umefika na kudharau mambo ya msingi ya nchi.
Hapana. Ila najaribu kuonesha ya kwamba mtoa hoja ni muongo. Malipo mbalimbali ya Serikali yanaendelea kutolewa tena kwa wakati. Na nilichoonesha ni mfano mdogo tu. Daraja la Magufuli pale Busisi ujenzi umepamba moto. Ujenzi wa SGR hapa Mwanza Mjini ndio usiseme hadi Kiwanda Cha Samaki Cha Vic Fish kimeanza kubomolewa wiki hii kupisha ujenzi. Nini mnataka madogo?
 
Acha tumliipe jamaa wa Stiglers ili aondoke, keshamaliza kazi, tukilipa anawasha mitambo na kukabidhi mradi. Huo mradi ni mkubwa, huwezi linganishha ni vimiradi vya bilioni kumi au ishirini.

Stiglers yote imekamilika, mitambo iko tayari yote, ni kulipa tu! Nyi wengine mnaodai msubiri.

Mwigulu ameshasema jamaa wa Stiglers hadai hata mia
 
Mbona wakandarasi wamesima wanalipwa!? mpaka.wameamua kumpatia mama zawadi! au mnazungumzia wakandarasi wa Kenya?
Wakandarasi gani wanalipwa hao magumashi utakatishaji wa pesa mfuko wa barabara (Road fund) umekauka hauna pesa madeni toka mwaka jana wanalia wakandarasi wengine wamekopa Bank wakilipwa walipe madeni dhamana zao ziko sokoni mpaka muda huu​
 
Back
Top Bottom