Pre GE2025 Dkt. Nchimbi: Maendeleo aliyoleta Rais Samia kwa miaka 3 Madarakani ni kama miujiza

Pre GE2025 Dkt. Nchimbi: Maendeleo aliyoleta Rais Samia kwa miaka 3 Madarakani ni kama miujiza

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ukishakuwa chawa huwezi kutumia akili.

Hivi nchi zote duniani raisi anaabudiwa namna hii? Mbona tunakuwa watu wa namna hii, kusifu kila kitu, hatuwezi kuwa objective hata kidogo.
😂😂😂🤛
 
Kuna mida ifike hizi kauli zenu zitoke kwa kujua kwamba watanganyika siyo mazuzu - wanajua kusoma na kuandika walau.
 
😃😃Aah
Samia anaendelea kufanya kazi iliyotukika na yenye baraka kwenye sekta ya Elimu Tanzania.

Julius Nyerere Memorial University of Agriculture and Technology -Butiama

View: https://www.instagram.com/p/DBkzvj9KCqi/?igsh=MW81MnBqODd6djZpbw==
wizara_elimutanzania_1729931340695.jpg
wizara_elimutanzania_1729931340117.jpg
wizara_elimutanzania_1729931340997.jpg
wizara_elimutanzania_1729931340427.jpg
wizara_elimutanzania_1729931339781.jpg
wizara_elimutanzania_1729931338418.jpg
wizara_elimutanzania_1729931336816.jpg


Kazi kama hii inaendelea Mikoa yote Tanzania.

Kutoka Tanga Hadi Katavi,Rukwa Hadi Kagera,Kigoma Hadi Mtwara ,Njombe Hadi Arusha nk nk.
 
Hayo yameelezwa na KM wa CCM Dkt.John Nchimbi wakati wa ziara yake ya Mikoa 6 akiwa Njombe.

DK Nchimbi ameonekana kushangazwa na kufurahishwa na Wingi wa miradi na maendeleo yaliyofanyika na yanayoendelea kufanyika akisema ni kama miujiza maana kilichotakiwa kufanyika Kwa muda mrefu kimewezekana ndani ya mda mchache kabisa.

Kwa wasio fahamu,haters na wabishi hii hapa ni summary tuu ya kilichofanywa na Samia.👇👇

1-Mapato ya TRA kuongezeka kutoka wastani wa 1.5T Hadi 2.5T(ongezeko Trilioni 1 )

2-Makusanyo ya Halmashauri kuongeza kutoka Bil.800 Hadi Trilioni 1.2(Ongezeko Bil.400)

3-Ongezeko la Mapato ya Utalii Hadi 3.5T(Watalii 1.9m) kutoka 3T(Watalii 1.5mln).

4-Ujenzi wa Bandari Ziwa Nyasa(MbambaBay),Ziwa Tanganyika(Kigoma),Ziwa Victoria (Mwanza,Bukoba,Chato) na Bhari ya Hindi(Dar,Tanga,Kilwa na Mtwara).

5-Ujenzi wa viwanja wa ndege 15 Unaendelea Tanzania nzima eg Sumbawanga,Tabora,Shinyanga,Kigoma,Ruaha NP,Nyerere NP,Moshi,Iringa nk huku akikamilosja viwanja vya Songwe, Songea,Iringa na Katavi.

6-Ujenzi wa Hospital za Wilaya mpya 129 ,Mikoa 7 na Rufaa za Kanda 3(Mtwara,Kigoma na Ukerewe).

7-Ujenzi wa Vituo vya Afya vipya 402 kwenye kata za kimkakati hapo tozo za miamala (234).

8-Ununuzi wa vifaa tiba ambavyo havikuwahi kuwepo Kwenye hospital za Tanzania mfano Ultra Sound 192 ,Digital X-rays 147,CT Scan 32,MRI machines 7.

9-Ujenzi wa majengo ya Wagonjwa Mahututi(ICU) 28 na Dharula 127,

10-Upanuzi na Ujenzi wa Vyuo Vikuu vipya na kampasi za Vyuo kwenye Mikoa 14 ambayo swali haikuwa na Vyuo Vikuu au kampasi eg Kigoma,Simiyu,Njombe,Ruvuma, Rukwa,Katavi,Shinyanga,Lindi,Mtwara nk.

11-Kaongeza Bajeti Kila Wizara ila Kwa upekee ni Wizara ya Kilimo(Umwagiliaji )kutoka Bil.270 Hadi Bilioni 950.Skimu Mpya za uwamwagiliaji hectare 95,000 zimejengwa na kufufuliwa,kafungua ofisi za Kilimo Kila Wilaya na kaajiri Wataalamu na kawapa vitendea kazi.

12-Kaondoa shida ya vitambulisho NIDA,zaidi ya vitambulisho 12,000,000 vimegawiwa.

13-Ujenzi wa minara mipya 1,200 ambapo Kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali minara 728 inaendelea na Ujenzi Kwa Bilioni 126.(Kijijini kama mjini)

14-Amefikisha maji ya Bomba Kwa zaidi ya Vijiji 11,000.(Kampeni ya kumtua Mama ndio kichwani).

15-Amefikisha umeme Kila Kijiji,kazi inaendelea kwenye vitongoji na migodi ya umeme.

16-Amewasha Umeme gridi ya Taifa Mikoa Kigoma,Katavi na kazi zinaendelea Rukwa ,Lindi, Mtwara.

17-Kazi zinaendelea ujenzi wa Vyanzo vipya vya Umeme eg Mto Malagalasi,Kakono,Umeme Jua Kishapu,Joto Ardhi Mbeya nk

18-Amejenga zaidi ya Shule Mpya za Sekondari 3,200 ,shule za msingi zaidi ya 300 na madarasa 24,000 ,mabweni 137 nk

19-Kupitia TanRoads amekamilisha zaidi ya km 1,000 za lami na zingine zaidi ya 3,700 zinaendelea na Ujenzi.

20-Kupitia Tarura amejenga zaidi ya km 800 za lami na zingine zaidi ya 500 zinaendelea na Ujenzi (Hapa amefungua maelfu ya Vijijini Kwa Barabara Mpya za changarawe na madaraja). Bajeti ya Tarura aliongeza kutoka bil.270 Hadi Bil.800.

21-Sekta ya mifugo amegawa Boti za Kisiasa zaidi ya 200 na viximba zaidi ya 1300 Kwa Vijana.

22-Sekta ya Elimu kaongeza mikopo Kwa wanafunzi ambapo Sasa Diploma Hadi Chuo Kikuu wanapata,chekechea Hadi form six Elimu Bure(kafuta ada ya form Six),Kafuta Mapenato na mambo ya hivyo ya Bodi ya Mikopo.

23-Katoa Ajira zaidi ya 55,000 kada zote huku Elimu na Afya wakipewa kipaombele.

24-Anajenga na kukamilisha zaidi ya miradi ya maji 3,700 mikubwa Kwa midogo mfano mradi wa Miji 28,bwawa la kidunda na kukwamua miradi iliyokwamba kama same-mwanga,Tarime-Kiabakari nk.

25-Kwenge sekta ya biashara baada ya maboresho maelfu ya miradi imemenika Kila sekta baada ya Wafanyabiashara kurejesha Imani Kwa Serikali Kupitia sera ya Diplomasia ya Uchumi na kuifungua Nchi.Hakuna ziara ambayo mama alifanya Nje ya Nchi hajakutana na Wafanyabiashara wa Kimataifa.

26-Sekta ya michezo na Burudani.Huko Kila mtu anajua kwamba Mama alikatabati viwanja,akaleta ufunguzi wa AFL na sasa ameileta Afcon 27 na uwanja Mpya inajengwa Arusha.Likewise kuwapa mikopo Wasanii.

27-Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) 100 .Lengo Kila Wilaya na Mkoa iwe na Chuo Cha ufundi.

28-Kaongeza Boom Kutoka 8,500 Hadi 10,000

29-Amefufua sekta ya Nyumba ilivyokuwa imekufa

30-Amefungua Uchumi,Watalii na Biashara Vinamiminika mfano ni kuzinduliwa Kwa viwanda vya Vioo,magari na mbolea.

31.Ujenzi wa Daraja la Jangwani

Ujenzi wa TPA Dar Port Tank Farm ,Bilioni 679.

Kiufupi ni vigumu kuelezea vyote,pamoja na Changamoto ila Mama kaupiga mwingi ,Anatosha na Chenji inabakia.

View: https://www.instagram.com/p/C59CY7uMJC5/?igsh=MTNiYnozM2hubjMwZQ==

My Take
Yote hayo kafanya na anaendelea kufanya lakini hajawahi acha mradi hata 1 aliourithi kutoka Kwa Mwendazake kama Bwawa la JNHPP,Daraja la JPM,EACOP,SGR,Ndege Mpya,Ujenzi wa Mji wa Serikali na hajatoa visingizio.👇👇

View: https://youtu.be/wLGSs8-pCcU?si=6t-U9ZR8BOp4PEIh

Huyu nae ni chawa tu wa Samia. Kwa kua kapewa cheo na mwenyewe ni mroho wa madaraka ndio anaona rais kaleta maeneleo makubwa. Et anasifia makusanyo ya TRA kuongezeka wakati tunajua shilingi imeshuka thamani kwa hivyo hela kama sio ileile itakua imepungua mtu akilinganisha thamani halisi. Maisha ya wavuja jasho yanaendelea kua magumu. Hospitali za serikali huduma ghali utafikiri ni za binafsi. Madaktari wameachwa kuendesha biashara ya matibabu kwa kutumia uwekezaji wa umma. Rushwa imeongezeka polisi na mahakama wamegeuza kazi zao kampuni zao binafsi kujipatia kipato kikubwa huku wanapewa mishahara kutoka hazina ya taifa. Nchimbi aache ulaghai hayo aliyotaja kwanza mengi ni miradi ya awamu ya 5 na mengine ni kazi za kawaida tu za serikali.
 
Back
Top Bottom