Pre GE2025 Dkt. Nchimbi: Maendeleo aliyoleta Rais Samia kwa miaka 3 Madarakani ni kama miujiza

Pre GE2025 Dkt. Nchimbi: Maendeleo aliyoleta Rais Samia kwa miaka 3 Madarakani ni kama miujiza

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
-Kikokotoo dhalimu ndio aliasisi ,hata hivyo mama ni msikivu Serikali imesema meimosi majibu yatatoka
-Mfumuko upi wa bei wakati takwimu zote haijawahi zidi 4%? Pili kama Kuna mfumuko wa bei ingeathiri uwekezaji na Mapato ya Serikali lakini yameongezeka mara dufu.
-Bima ya Afya imefanya nini? Sana sana Mama ameleta sheria ya bima ya Afya Kwa wote na kuweka historia , utekelezwaji wake ni WA hatua Kwa hatua ila kabla ya 2028 Kila mtu atatibiwa Kwa bima.
-Ingia TIC utaona maelfu ya biashara yaliyoanzishwa na ndio chachu ya kuongezeka Kwa Mapato ya Serikali.
-Unazungumzia Ajira Kwa Samia? Hilo sio swali ni jibu,zingine hizi hapa 👇View attachment 2968972
Sawa umesahau idadi ya PhD zilizovunwa
 
MbambaBay Port,Lake Nyasa 👇👇

View: https://youtu.be/bxsmxclzr9U?si=-T3jzJtYULhOByFu
Screenshot_20240926-084008.jpg
Screenshot_20240926-083951.jpg
Screenshot_20240926-083929.jpg
 
Hayo yameelezwa na KM wa CCM Dkt.John Nchimbi wakati wa ziara yake ya Mikoa 6 akiwa Njombe.

DK Nchimbi ameonekana kushangazwa na kufurahishwa na Wingi wa miradi na maendeleo yaliyofanyika na yanayoendelea kufanyika akisema ni kama miujiza maana kilichotakiwa kufanyika Kwa muda mrefu kimewezekana ndani ya mda mchache kabisa.

Kwa wasio fahamu,haters na wabishi hii hapa ni summary tuu ya kilichofanywa na Samia.👇👇

1-Mapato ya TRA kuongezeka kutoka wastani wa 1.5T Hadi 2.5T(ongezeko Trilioni 1 )

2-Makusanyo ya Halmashauri kuongeza kutoka Bil.800 Hadi Trilioni 1.2(Ongezeko Bil.400)

3-Ongezeko la Mapato ya Utalii Hadi 3.5T(Watalii 1.9m) kutoka 3T(Watalii 1.5mln).

4-Ujenzi wa Bandari Ziwa Nyasa(MbambaBay),Ziwa Tanganyika(Kigoma),Ziwa Victoria (Mwanza,Bukoba,Chato) na Bhari ya Hindi(Dar,Tanga,Kilwa na Mtwara).

5-Ujenzi wa viwanja wa ndege 15 Unaendelea Tanzania nzima eg Sumbawanga,Tabora,Shinyanga,Kigoma,Ruaha NP,Nyerere NP,Moshi,Iringa nk huku akikamilosja viwanja vya Songwe, Songea,Iringa na Katavi.

6-Ujenzi wa Hospital za Wilaya mpya 129 ,Mikoa 7 na Rufaa za Kanda 3(Mtwara,Kigoma na Ukerewe).

7-Ujenzi wa Vituo vya Afya vipya 402 kwenye kata za kimkakati hapo tozo za miamala (234).

8-Ununuzi wa vifaa tiba ambavyo havikuwahi kuwepo Kwenye hospital za Tanzania mfano Ultra Sound 192 ,Digital X-rays 147,CT Scan 32,MRI machines 7.

9-Ujenzi wa majengo ya Wagonjwa Mahututi(ICU) 28 na Dharula 127,

10-Upanuzi na Ujenzi wa Vyuo Vikuu vipya na kampasi za Vyuo kwenye Mikoa 14 ambayo swali haikuwa na Vyuo Vikuu au kampasi eg Kigoma,Simiyu,Njombe,Ruvuma, Rukwa,Katavi,Shinyanga,Lindi,Mtwara nk.

11-Kaongeza Bajeti Kila Wizara ila Kwa upekee ni Wizara ya Kilimo(Umwagiliaji )kutoka Bil.270 Hadi Bilioni 950.Skimu Mpya za uwamwagiliaji hectare 95,000 zimejengwa na kufufuliwa,kafungua ofisi za Kilimo Kila Wilaya na kaajiri Wataalamu na kawapa vitendea kazi.

12-Kaondoa shida ya vitambulisho NIDA,zaidi ya vitambulisho 12,000,000 vimegawiwa.

13-Ujenzi wa minara mipya 1,200 ambapo Kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali minara 728 inaendelea na Ujenzi Kwa Bilioni 126.(Kijijini kama mjini)

14-Amefikisha maji ya Bomba Kwa zaidi ya Vijiji 11,000.(Kampeni ya kumtua Mama ndio kichwani).

15-Amefikisha umeme Kila Kijiji,kazi inaendelea kwenye vitongoji na migodi ya umeme.

16-Amewasha Umeme gridi ya Taifa Mikoa Kigoma,Katavi na kazi zinaendelea Rukwa ,Lindi, Mtwara.

17-Kazi zinaendelea ujenzi wa Vyanzo vipya vya Umeme eg Mto Malagalasi,Kakono,Umeme Jua Kishapu,Joto Ardhi Mbeya nk

18-Amejenga zaidi ya Shule Mpya za Sekondari 3,200 ,shule za msingi zaidi ya 300 na madarasa 24,000 ,mabweni 137 nk

19-Kupitia TanRoads amekamilisha zaidi ya km 1,000 za lami na zingine zaidi ya 3,700 zinaendelea na Ujenzi.

20-Kupitia Tarura amejenga zaidi ya km 800 za lami na zingine zaidi ya 500 zinaendelea na Ujenzi (Hapa amefungua maelfu ya Vijijini Kwa Barabara Mpya za changarawe na madaraja). Bajeti ya Tarura aliongeza kutoka bil.270 Hadi Bil.800.

21-Sekta ya mifugo amegawa Boti za Kisiasa zaidi ya 200 na viximba zaidi ya 1300 Kwa Vijana.

22-Sekta ya Elimu kaongeza mikopo Kwa wanafunzi ambapo Sasa Diploma Hadi Chuo Kikuu wanapata,chekechea Hadi form six Elimu Bure(kafuta ada ya form Six),Kafuta Mapenato na mambo ya hivyo ya Bodi ya Mikopo.

23-Katoa Ajira zaidi ya 55,000 kada zote huku Elimu na Afya wakipewa kipaombele.

24-Anajenga na kukamilisha zaidi ya miradi ya maji 3,700 mikubwa Kwa midogo mfano mradi wa Miji 28,bwawa la kidunda na kukwamua miradi iliyokwamba kama same-mwanga,Tarime-Kiabakari nk.

25-Kwenge sekta ya biashara baada ya maboresho maelfu ya miradi imemenika Kila sekta baada ya Wafanyabiashara kurejesha Imani Kwa Serikali Kupitia sera ya Diplomasia ya Uchumi na kuifungua Nchi.Hakuna ziara ambayo mama alifanya Nje ya Nchi hajakutana na Wafanyabiashara wa Kimataifa.

26-Sekta ya michezo na Burudani.Huko Kila mtu anajua kwamba Mama alikatabati viwanja,akaleta ufunguzi wa AFL na sasa ameileta Afcon 27 na uwanja Mpya inajengwa Arusha.Likewise kuwapa mikopo Wasanii.

27-Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) 100 .Lengo Kila Wilaya na Mkoa iwe na Chuo Cha ufundi.

28-Kaongeza Boom Kutoka 8,500 Hadi 10,000

29-Amefufua sekta ya Nyumba ilivyokuwa imekufa

30-Amefungua Uchumi,Watalii na Biashara Vinamiminika mfano ni kuzinduliwa Kwa viwanda vya Vioo,magari na mbolea.

Kiufupi ni vigumu kuelezea vyote,pamoja na Changamoto ila Mama kaupiga mwingi ,Anatosha na Chenji inabakia.

View: https://www.instagram.com/p/C59CY7uMJC5/?igsh=MTNiYnozM2hubjMwZQ==

My Take
Yote hayo kafanya na anaendelea kufanya lakini hajawahi acha mradi hata 1 aliourithi kutoka Kwa Mwendazake kama Bwawa la JNHPP,Daraja la JPM,EACOP,SGR,Ndege Mpya,Ujenzi wa Mji wa Serikali na hajatoa visingizio.👇👇

View: https://youtu.be/wLGSs8-pCcU?si=6t-U9ZR8BOp4PEIh

Upuuzi gani huu unatuorodheesha. Yote hayo mbona ni majukumu ya kawaida ya serikali. Et kutuambia makusanyo yameongezeka na huku thamani ya fedha imeshuka unafikiri wananchi wajinga. Fedha yenyewe haitumiki inagawiwa tu huko mikoani vigogo wagawane huku serikali inatoza wananchi huduma ya matibabu sawa na biashara ya hospitali binafsi. Halafu niulize; kama huduma ya usambazaji umeme ikifanyika na REA imefanikikiwa kwa kiasi kikubwa kwa nini serikali inataka kuwapa kampuni ya nje ya kihindi kusambaza umeme nchini. Hii si sawa na kusambaza juu ya kusambaza au wanataka kuwapa watu binafsi kufanya uwekezaji ambao tayari umefanyika ili wao wavune tu wasipokua wamewekeza. Hii serikali ya ccm wasifikiri wananchi ni wajinga hata kama wameshindwa kuwapa elimu ya kiwango.
 
Upuuzi gani huu unatuorodheesha. Yote hayo mbona ni majukumu ya kawaida ya serikali. Et kutuambia makusanyo yameongezeka na huku thamani ya fedha imeshuka unafikiri wananchi wajinga. Fedha yenyewe haitumiki inagawiwa tu huko mikoani vigogo wagawane huku serikali inatoza wananchi huduma ya matibabu sawa na biashara ya hospitali binafsi. Halafu niulize; kama huduma ya usambazaji umeme ikifanyika na REA imefanikikiwa kwa kiasi kikubwa kwa nini serikali inataka kuwapa kampuni ya nje ya kihindi kusambaza umeme nchini. Hii si sawa na kusambaza juu ya kusambaza au wanataka kuwapa watu binafsi kufanya uwekezaji ambao tayari umefanyika ili wao wavune tu wasipokua wamewekeza. Hii serikali ya ccm wasifikiri wananchi ni wajinga hata kama wameshindwa kuwapa elimu ya kiwango.
Au siyo?

Mwanza 😂😂😂👇👇

View: https://youtu.be/E0DcZSEwtic?si=d47P7W13kkIDgzge

View: https://youtu.be/Aq7AGgVXaxQ?si=yWG5xyZEoVA5BvmI
 
Back
Top Bottom