Dkt. Philip Mpango anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi wa Mkutano wa TAWIRI, Dec 6-8

Dkt. Philip Mpango anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi wa Mkutano wa TAWIRI, Dec 6-8

Naamini kabisa hili ni tangazo la zamani!, ili kesho VP awe Mgeni rasmi kwenye hiyo event, alipaswa leo awe amerejea nchini kutoka kule kwenye yale majukumu yake ya nje ya nchi, tungemuona leo akirejea!.
Kesho atawakilishwa!.
P
Kweli kabisa. Wakati wa mkutano mkuu wa Chama cha Madaktari mwaka huu, poster ilionyesha Mh Waziri wa Afya angekua mgeni rasmi. Lakini walioenda Tanga Beach Resort wanasema mh hakufika.
 
Kila mtu duniani ana safari yake. Tusiombee watu vifo kwasababu hakuna atayeishi milele. Mtu akifa usione kana kwamba wewe umependelewa sana na Mungu kuwa hai, siku yako yaja pia.
Upo sahihi. Lakini wanaohoji wanafanya hivyo kwa sababu hao viongozi wapo pale kwa sababu/ajili ya wananchi.
Kwanini wasiambiwe kinachojiri?!
 
Usisome Biblia kama novel ya James Hadley Chase utaishia kupotoka kama hivi.
Ulitaka aombewe "uponyaji" wakati haumwi? Kisa umekariri mstari usemao "ombeni mvua wakati wa masika"?
Kwa mjibu wa Biblia hatupaswi kumwomba Mungu au kuombeana baada ya tatizo kutokea, bali kudumu katika kuomba na kuombeana nyakati zote.
 
Upo sahihi. Lakini wanaohoji wanafanya hivyo kwa sababu hao viongozi wapo pale kwa sababu/ajili ya wananchi.
Kwanini wasiambiwe kinachojiri?!
Kwasababu haibadilishi chochote kwenye maisha ya watu. Sawa ni kiongozi, ila usitake kuniambia kwamba kutokujua alipo kunasababisha watu wasifanye shughuli zao za kila siku.
 
Kwasababu haibadilishi chochote kwenye maisha ya watu. Sawa ni kiongozi, ila usitake kuniambia kwamba kutokujua alipo kunasababisha watu wasifanye shughuli zao za kila siku.
Unadhalilisha ukoo wa akina Mushi.
Impact yake ni kubwa SANA:
1. Kama alikuwa matibabu nje ya nchi hiyo ni ishara kuwa wakishakuwa viongozi hawana tena imani na huduma za afya za ndani!
2. Kama 1 hapo juu ni sahihi jibu ni kuwa fedha za walipa kodi zilikuwa zinamuhudumia tangu hiyo October
3. Kama ikitokea asiwepo nchi na walipa kodi wataingia kwenye gharama kubwa kumhifadhi.
4. Ni haki ya waongozwa kujua alipo kiongozi wao na kama ni mgonjwa waambiwe anachoumwa!
 
Kwa mjibu wa Biblia hatupaswi kumwomba Mungu au kuombeana baada ya tatizo kutokea, bali kudumu katika kuomba na kuombeana nyakati zote.
Hakuna mtu anamuombea mwenzake mabaya hakuna, tatizo linaanzia wenzako ulionao wanapoamua tatizo lako kuliingiza kwenye siasa badala ya kusema ukweli, sababu ya kutokusema ukweli haijulikani. Wewe ni kiongozi wa nchi sio chama chako, unapokuwa kiongozi kuna wananchi wa kila chama wanaohitaji huduma toka kwake lakini viongozi wa CCM wanakaujinga fulani wa kuona kuwa viongozi hao ni wa CCM na wapo kwa ajili ya wanaccm! Hicho ndicho kinawafanya watu wawape kisogo na kuwakejeli, huko Hanang jambo lililotokea linawahusu watu wote lakini Waziri mkuu anasimama na kimuambia mbunge wa hapo eti hao ni wapiga kura wake! Anauhakika huo kuwa hakuna ambao si wapiga kura wa chama chochote! Huo ni ubaguzi kwenye janga na wakajiwekea vitambaa vya kijani! Unataka kura kwa maiti!
Tusiwalaumu wanaobeza kwani haya ndiyo mazao ya wabinafsi.
 
Unadhalilisha ukoo wa akina Mushi.
Impact yake ni kubwa SANA:
1. Kama alikuwa matibabu nje ya nchi hiyo ni ishara kuwa wakishakuwa viongozi hawana tena imani na huduma za afya za ndani!
2. Kama 1 hapo juu ni sahihi jibu ni kuwa fedha za walipa kodi zilikuwa zinamuhudumia tangu hiyo October
3. Kama ikitokea asiwepo nchi na walipa kodi wataingia kwenye gharama kubwa kumhifadhi.
4. Ni haki ya waongozwa kujua alipo kiongozi wao na kama ni mgonjwa waambiwe anachoumwa!
Hoja zako hazina mashiko.
 
Watanzania mmekua na roho mbaya...kusubiria taarifa mbaya...
Mungu ni mwema kila wakati...

Mimi siamini kama kweli kuna Watanzania wanaotaka mtu fulani afe, tena kiongozi wa nchi. Hiyo siamini kabisa.

Watu kuuliza ili wapate uhakika kunapokuwa na tetesi, kunageukaje kuwa watu hao wanamwombea kiongozi mabaya?

Mimi naamini, kati ya watu wenye maadui wachache sana, kama wapo, Dr. Mpango ni mmojawapo.
 
Mimi siamini kama kweli kuna Watanzania wanaotaka mtu fulani afe, tena kiongozi wa nchi. Hiyo siamini kabisa.

Watu kuuliza ili wapate uhakika kunapokuwa na tetesi, kunageukaje kuwa watu hao wanamwombea kiongozi mabaya?

Mimi naamini, kati ya watu wenye maadui wachache sana, kama wapo, Dr. Mpango ni mmojawapo.
Kuna ile kuuliza kwa huruma kuna ile kuuliza kwa kuwa na majibu yako mwenyewe...na majibu yenyewe ovu...ndo nawamaaanisha hao
 
Back
Top Bottom