BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 377
- 435
DKT. SAMIZI ATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA BARABARA NA MADARAJA ILIYOJENGWA KWA FEDHA ZA SERIKALI YA RAIS SAMIA.
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma Mhe. Dkt Florence George Samizi kipindi hiki cha mapumziko ya Bunge ameendelea kufanya ziara Jimboni kwa kufanya shughuli za maendeleo, kutembelea na kukagua miradi pamoja na kusikiliza na kutatua kero za Wananchi ili kutekeleza vyema Ilani ya CCM.
Leo Jumamosi Oktoba 18, 2022, Dkt. Samizi akiwa na Wataalamu wa TARURA wametembelea miradi ya miundombinu ya barabara na madaraja na kujionea kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Rais Samia kwa kutoa Mamilioni ya fedha kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo (Enabel).
Wananchi wamemwaga pongezi nyingi saana Kwa Rais Samia kwa ujenzi wa Daraja la kuvuka Mto Malagarasi linalounganisha Kata ya Kumsenga na Kata ya Kitanga Jimbo la Kasulu Dc, hivyo shida ya kuvuka na kamtumbwi itakwisha kwa Wananchi na sasa wataweza kusafirisha mazao, wenyewe ,wagonjwa, mifugo n.k
Mhe. Dkt. Samizi akizungumza na Wafugaji wa Kijiji cha Kumlela kata ya Mabamba walifurahia sana daraja la Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwani sasa mifugo yao inapita vizuri kwenye daraja.
#KaziInaendeleaMuhambwe.
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma Mhe. Dkt Florence George Samizi kipindi hiki cha mapumziko ya Bunge ameendelea kufanya ziara Jimboni kwa kufanya shughuli za maendeleo, kutembelea na kukagua miradi pamoja na kusikiliza na kutatua kero za Wananchi ili kutekeleza vyema Ilani ya CCM.
Leo Jumamosi Oktoba 18, 2022, Dkt. Samizi akiwa na Wataalamu wa TARURA wametembelea miradi ya miundombinu ya barabara na madaraja na kujionea kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya Rais Samia kwa kutoa Mamilioni ya fedha kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo (Enabel).
Wananchi wamemwaga pongezi nyingi saana Kwa Rais Samia kwa ujenzi wa Daraja la kuvuka Mto Malagarasi linalounganisha Kata ya Kumsenga na Kata ya Kitanga Jimbo la Kasulu Dc, hivyo shida ya kuvuka na kamtumbwi itakwisha kwa Wananchi na sasa wataweza kusafirisha mazao, wenyewe ,wagonjwa, mifugo n.k
Mhe. Dkt. Samizi akizungumza na Wafugaji wa Kijiji cha Kumlela kata ya Mabamba walifurahia sana daraja la Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwani sasa mifugo yao inapita vizuri kwenye daraja.
#KaziInaendeleaMuhambwe.