Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Dear Dr. Slaa

Kwanza kabisa nikupe pole kwa safari iliyo kuwa imeghubikwa na hofu na mashaka, lakini nimefarijika sana kusikia mlifika salama na mapambano yanaendelea;
Pili nikupongeze kwa kazi ngumu uliyoikamilisha mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya kiasi ambacho hata vipofu wameona. Mungu akubariki.

Dr. Slaa huu ni ujumbe wangu kwako;


Bahari ya shamu haikuwazuia wana wa Israel kuvuka kwenda nchi ya ahadi (kanani), tena ukuta wa Yeriko haukumzuia Yoshua kusonga mbele na wana wa Israel, Pia mto Yordani haukumzuia Eliya kuvuka ng’ambo, wala jiwe kubwa kwenye kaburi halikumzuia YESU asifufuke. Hivyo basi ni dhahiri hakuna awezae kuzuia mipango ya Mungu Juu ya Maisha yako.
 
Dr. Slaa kama umefikia hapa bsi utapata shida sana kwenye serikali yako utakapochukua urais 2015. Ikitokea milipuko ya silaha bahati mbaya au uzembe basi kambi nzima hasa viongozi wao watakua wametumwa na CCM, ikitokea siri zimevuja basi utasema mabaki ya ccm, kila jambo kisingizio kitakua ccm na mwisho ccm utakiita wapiganaji wa msituni au waasi.

Mimi ni bwana mdogo sana nakutahadharisha sana na hisia hasa za woga. Nimekua nikimwona Lema mara nyingi huwa hata kama ni uoga haoneshi wazi au kuelezea wazi hivi na ingekua yeye huenda angeisimamisha hiyo gari ili kupata kujua hasa nini wanahitaji.

Mwenzio Mbowe ni mjanja mno hasa kwenye siasa hizi na mara nyingi amekua akikwepa siasa hizi hata akizitumia huwa anawasukumia nyie nnaonekana hamna kitu zaidi ya kucheza na saikolojia zetu.

Nadhani kuna umuhimu mkubwa kwanza wa kujiamini kisha kujitambua. Kama huamini chombo chochote cha dola unafanya nini hapa Tanzania? wenzio hukimbia na kufanya harakati wakiwa ugaibuni mifano mingi tu unayo. Huumini vyombo vya dola, huamini, vyombo vya usalama lakini unataka kuingia ikulu vikiwepo nadhani unachohitaji ni kufanya mapinduzi ili uingia ukiwa unaisuka upya kabisa hii nchi kama ilivyo somalia la sivyo hao usiowaamini sasahivi usidhani utaingia madarakani uwaamini hata kama utakua amiri jeshi mkuu??!!!! Lazima utaona chembechembe za GAMBA tu.

Nakutakia maisha mema na matayarisho mema ya kuingia Ikulu 2015 ili watanzania tupate maziwa na asali tuishi zaidi ya ulaya bila kuguswa na wachina, benki ya dunia, IMF, wala mafirauni wengine wenye nia ya kututawala. Pia CCM wote watapelekwa The Hague, Segerea na Mikataba yote itawekwa wazi kwa wananchi waamuae upi wanautaka upi hawautaki.
 
Hawa jamaa wanadhani wanaogea na watu ambao hamnazo.
Hivi kweli wewe inakujia akilini. Mzee mzima unakua muongo.
Na Mzee Slaa anatoa maelezo ya kitoto kabisa. Hivi anatuona sisi kama nini huyu mzee?
Asipo thibitisha basi huyu mzee kila kitu atakacho ongea nitajua tu akili zake zimeanza kuliwa nauzee
Hizi njia mnazotumia kukinusuru chama chenu ni za zamanai na zitakiondoa madarakani 2015.Na kila jambo sasa ni kuliweka hadharani
 
Hizi njia mnazotumia kukinusuru chama chenu ni za zamanai na zitakiondoa madarakani 2015.Na kila jambo sasa ni kuliweka hadharani
Oya acha kunichanganya wewe si umeeleza gari mlipiga picha sasa picha yenyewe iko wapi? Naomba ubandike picha hapa.
 
Dr Wilbroad Peter Slaa wambie vijana wako waweke picha hapa ya Gari! Lasivyo Babu yangu Slaa utaonekana Muongo na Mzushi wa ajabu,picha ya gari ina hitajika hapa JF
 
Ili nimuone Dr anaakili timamu
1. Athibitishe hiyo namba ya gari sisi tuko tayari kufuatilia na kutaja gari ni ya nani.
2. Abandike hiyo picha ya gari iliyo pigwa. Na kama picha imechakachuliwa tutaielewa ninazo tools.

La sivyo huyu mzee atakuwa anazeeka vibaya.

Mkuu sijakuelewa hapo hapo penye una maanisha nini ?

Kwa hilo bandiko lako ni dhahiri uwezo wako wa kufikiria upo mashakani; nachelea kusema Dr. Slaa hana mda wa kujibizana na misukule ya Lumumba isiyo jitambua.
 
Oya acha kunichanganya wewe si umeeleza gari mlipiga picha sasa picha yenyewe iko wapi? Naomba ubandike picha hapa.

Hizi namba jeshi la polisi lichunguze ni za gari la nani

Kwa akili fupi ya Padri wenu CCM hamta iondoa madarakani!
Subirini chaguzi.Mmeona shughuli zilizofanyika juzi mikoani.Akili zimewaruka mnaanza kuwanda watu
 
Oya acha kunichanganya wewe si umeeleza gari mlipiga picha sasa picha yenyewe iko wapi? Naomba ubandike picha hapa.

Hawana Picha wazushi tu na Babu yao,unajua uongo unataka uwe na akili sana! Angalia kwenye maelezo ya Slaa anasema Traffic waliwasimamisha ndipo wakatoa taarifa! Yani wasinge simamishwa wasingetoa taarifa kwa traffic,lakini pia mleta uzi anasema walipo waona traffic wakasimama kuwambia mkasa huo! Sasa statement mbili zinapingana! Ni aibu kwa Kiongozi wa ngazi juu kama Dr Slaa ambaye baadhi ya watanzania wana muamini kuanza kujiingiza kwenye siasa rahisi rahisi kama hizi!
 
Wana wa Israel walikaa utumwani Misri miaka 400 hadi Mungu alipoamua- sasa basi!.Naamini,Iwapo kweli watu wanyonge wa taifa hili wamechoka,wamlilie Mungu angalau siku moja tu!Wafunge kula na kunywa,Mungu atatenda na kama kipindi cha Yoshua,kuta za Yeriko zitaanguka!Kama watu hawajachoka,ni vigumu sana kutokea mabadiliko yoyote!Watazidi kuzaliwa wanafiki na wasaliti ambao mwisho wa siku ndio watakaokuwa wahanga wa siasa za visasi ambazo zina hatari ya kuzaa waasi!Mkabidhini Mungu njia zenu naye atazithabitisha.


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

kama mungu atasikia usemayo na akaamua kutenda wengi wataaibika sijawahi kuona jamii ya wazushi na waongo kama baazi ya watanzania wameamua kuwa waongo na wazushi.
 
Dr. Slaa anatumia vihadithi kama hivi kujustify mamilioni anayolipwa na chama.

Dr Slaa amekuwa mtu wa wasiwasi muda wote sijui kwa nini hivi unagetemea barabara zetu zilivyokuwa na msongamano wa magari si unaweza kusema foleni yote inanifuatilia mimi.
 
msikate tamaa viongozi wa CDM...CDM kuhoji, kuanika maovu ya watawala na kuelimisha wananchi kumesaidia sana, bila CDM au chama chenye nguvu cha upinzani mafisadi watakomba vyote vilivyobaki...chonde makamanda msivunjike moyo, tupo pamoja
 
Ili nimuone Dr anaakili timamu
1. Athibitishe hiyo namba ya gari sisi tuko tayari kufuatilia na kutaja gari ni ya nani.
2. Abandike hiyo picha ya gari iliyo pigwa. Na kama picha imechakachuliwa tutaielewa ninazo tools.

La sivyo huyu mzee atakuwa anazeeka vibaya.
mkuu good wazo ni vema tukaongea kwa mifano halisi kuliko kukalia uongo na uzushi.
 
Dr Slaa amekuwa mtu wa wasiwasi muda wote sijui kwa nini hivi unagetemea barabara zetu zilivyokuwa na msongamano wa magari si unaweza kusema foleni yote inanifuatilia mimi.

Nadhani Dr Slaa anajenga hoja ya kupewa msafara kama viongozi wengine wa kitaifa! Hataki magari mengine nyuma yake asiyo yafahamu!
 
Dr Slaa amekuwa mtu wa wasiwasi muda wote sijui kwa nini hivi unagetemea barabara zetu zilivyokuwa na msongamano wa magari si unaweza kusema foleni yote inanifuatilia mimi.

Umesoma maelezo vizuri? Suala la Foleni kutoka Iringa na dalili zote ambazo si za kawaida unataka kuzipunguza hadi kwenye dhana ya foleni?

Dr.Slaa ni lazima awe na wasiwasi maana hila zote hadi TISS kuhonga vijana wa CHADEMA ili watoe ushahidi wa Uongo unaona ni jambo la kawaida wewe?
 
Ili nimuone Dr anaakili timamu
1. Athibitishe hiyo namba ya gari sisi tuko tayari kufuatilia na kutaja gari ni ya nani.
2. Abandike hiyo picha ya gari iliyo pigwa. Na kama picha imechakachuliwa tutaielewa ninazo tools.

La sivyo huyu mzee atakuwa anazeeka vibaya.



Wewe na nani mpo tayari kufuatilia?
 
Hizi namba jeshi la polisi lichunguze ni za gari la nani


Subirini chaguzi.Mmeona shughuli zilizofanyika juzi mikoani.Akili zimewaruka mnaanza kuwanda watu

siasa za kupandikiza chuki kwa watu ndo mnaona dili endeleeni nazo na kama watu wakiwashutukia sijui mtaanza siasa gani za kulia au
 
Hizi njia mnazotumia kukinusuru chama chenu ni za zamanai na zitakiondoa madarakani 2015.Na kila jambo sasa ni kuliweka hadharani
Conferate Spy:
Kuandika Namba ya gari haitoshi weka Picha ya gari hapa JF,lasivyo hii ngonjera yako inaonekana hukujipanga! Halafu msimuingize Dr Slaa kwenye mambo ya Kitoto kama haya!
 
Back
Top Bottom