KWELI Dkt. Slaa alitoa kauli ya kuipindua Serikali wakati wa mahojiano

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Jaman JF jiepusheni na kusema jambo ni Kweli au Sio Kweli.

Ukweli ni kitu kigumu sana kuthibitisha.

Yohana 18:38.
Pilato akamwambia, Kweli ni nini? Naye akiisha kusema neno hilo akawatokea Wayahudi tena, akawaambia, Mimi sioni hatia yo yote kwake.
uongo ndo una nguvu kuliko ukweli
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kutafsiri neno moja katika maelezo ya jambo zima na kutafsiri jambo zima. Kwa mimi nilivyomuelewa Dr. Slaa kuhusu namna ya kuondokana na mkataba wa bandari ni kuwa serikali inaweza kufanya jambo, na isipofanya wananchi watafanya jambo dhidi ya serikali kisheria na hilo likishindikana wananchi wanaweza kufanya hata nje ya kisheria!

All in all, MAPINDIZI sio sawa na MAPINDUZI, ikiwa tutataka kumhukumu Dr. Slaa kwa kila neno alilolisema.
 
Polisi buana sasa hapo ndiyo anaenda kuipindua serikali? Si mwandishi kamuuliza hapo hakuna cha kufanya ,akasema cha kufanya kipo mamlaka yanatoka kwa wananchi ,wananchi wanaweza kuipindua serikali siyo kama yeye ndiyo ataipindua.
 
Polisi buana sasa hapo ndiyo anaenda kuipindua serikali? Si mwandishi kamuuliza hapo hakuna cha kufanya ,akasema cha kufanya kipo mamlaka yanatoka kwa wananchi ,wananchi wanaweza kuipindua serikali siyo kama yeye ndiyo ataipindua.
Kama taifa hatuwezi kuchekea viashiria vya uhaini hata kidogo. Uhaini/mahaini washughulikiwe kwa mujibu wa sheria
 
Kwa hasira zangu za karibu ningewageza Babu seya kwenye uongozi wangu.
 
Naona tangu jana mitanadoani kumemwagwa maroboti yanayosambaza viclip vya kuhalalisha makosa ya kuwakamata watu kisa wanakosoa mkataba!!
 
I see!
 
Kama taifa hatuwezi kuchekea viashiria vya uhaini hata kidogo. Uhaini/mahaini washughulikiwe kwa mujibu wa sheria

Unaujua uhaini? Unaweza kunitajia mtu hata mmoja aliyeshitakiwa kwa uhaini na alifanya kitu gani ili tujenge msingi wa uhaini wa mdude/slaa/mwabukusi.
 
NAWAPONGEZA JF KWA KUWEKA MAMBO HADHARANI KWENYE NYEUPE NI NYEUPE SI HABARI ZA RANGI YA MAZIWA.
UKWELI NI KWAMBA CHADEMA WAMETISHIA AMANI YA NCHI NA KUPANGA MAPINDUZI YA KIGAIDI
 
Wavunje mkataba wa dpw kisaha wamshitaki.wavunjee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…