Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Chadema punguzeni kujipa matarajio na matumaini hewa, fanyeni kwanza chama/chadema assessment kwa wananchi mpate maoni kamili kuliko kutegemea mitandao tu ambayo penetrations yake ni kidogo, mwaka 2010-2015 hamasa ya mageuzi ilikuwa kubwa sana kutoka na jitihada kubwa zilizofanywa na upinzani wakati huo Dk slaa, Lissu, Zitto, Mkumbo, Prof safari, Lipumba, Maalim seif , mwamuko ulikuwa mkubwa na agenda kubwa ilikuwa ni rushwa na kuwatetea wananchi walio chini, kuja kwa Lowasa pamoja na hamasa iliyokuwepo iliongeza hamasa hivyo kupata wabunge wengi mwaka 2015 lakini bado CCM ilishinda, siasa zilibadilika ghafla kuanzia mwaka 2015 baada ya agenda karibu zote tulizokuwa tuna pigania kuanza kufanyiwa kazi, CCM ikakubalika tena, ndugu zangu mimi sijawahi penda ccm maisha yangu yote ila speed ya mwaka 2015 hadi 2020 chini ya msukuma yule ( Magufuli) haikuwa ya kawaida, upinzani agenda ikafa tukabakiwa na matukio na matusi mitandaoni, kwa ufupi tukapoteana, tukaja na conclusions kuwa tuliibiwa kura mwaka 2020, lakini ukweli halisi tulishindwa vibaya sana mwaka 2020 , wananchi walio wengi waliamini tena ccm, watu wanasomeshewa watoto wao bure ulitegemea wata mpigia kura nani?

Mimi nimeshiriki mikutano mingi ya Tundu Lissu Dar na mikoani, walikuwa wana msikiliza tu lakini baada ya hapo majority wengi walidai kura za uraisi ni Magufuli, sijui Magufuli aliwafanyia nini, sasa chadema kama chama kikubwa cha upinzania kifanye assessment kwanza na kipate report ya matukioa yote kuanzia mwaka 2015 hadi leo, kitapata picha halisi na kuja na sera mbadala, maana dunia inabadilika hivyo sera pia zina badilika kulingana na mabadiliko ya dunia na uongozi wa sasa.
Uneandika usichokiamini, au huujui labda ukweli.

CCM kuanzia 2015 haikuwahi kukubalika kwa wananchi, walilazimisha kukubalika kwa kutegemea mauaji, utekaji, nk.

Kama kweli unaamini agenda za upinzani zilianza kufanyiwa kazi na CCM from 2015, kwanini wakalazimisha wagombea wao wengi wapite bila kupingwa kwa sababu za kitoto kama kutokujua kujaza form?

Na kwanini wale wapinzani waliofanikiwa kugombea waliishia kuibiwa kura zao kwa namna ya aibu bila hofu yoyote na ushahidi ulikuwepo wa kila aina?
 
Mtu gani amiminiwe risasi zote hizo alafu atoke?kingine mbona dreva wa lisu mbona hakupata hata mchubuko wakati walikuwa wote,na sasahivi wamemficha ubeligiji,kama kweli Chadema wanataka tujue ukweli wamlete dreva wa lissu maana ndiye aliyewaona wapigaji.
Acha ujinga. Kwani kuwaona ndiyo lazima uwatambue. Kuamini hii sababu ya kijinga ni kuonyesha jinsi gani ulivyo mjinga.

Kazi ya kutafuta wajuaji ni ya jeshi la police. Na kama hiyo ndiyo sababu yao ya kushindwa kuwapata basi kazi hawawezi na itabidi jeshi lipewe training upya.
 
Dr. Slaa na apologists wake wanataka tusiizungumzie ripoti ya CAG mpaka Kamati za Bunge zitoe blessing zao kwa sababu tutaingiza siasa!

Wanataka kutuaminisha kuwa hizo Kamati za Bunge ni apolitical na watakuwa neutral kwenye hoja za CAG!

Kutowasilisha majibu ya audit queries katika wakati muafaka ni sababu tosha ya jamii kutilia mashaka na integrity yako na ni lazima uhojiwe katika mahakama ya umma. Ukiweza kuzijibu hapo baadae, bado utabakiza tuhma ya uzembe wako.

Seriously, Slaa anataka tuamini Kamati ya Bunge iliyoundwa na Ndugai kuliko CAG ambae analindwa na Katiba ili kuhakikisha yuko above politics! Tusihoji kwa nini ATCL inaendeshwa kihasara mpaka wakina Tulia watupe kibali! Mzee kweli amechanganyikiwa.

Amandla...
 
Nakubali kwenye attachments lakini hasara ya kampuni ni kitu kipo wazi kwenye financisl statements.
Ukiukwaji wa procurement process hakuhitaji kamati ya bunge..
Kufoji viza uhamiaji hakuhitaji kamati ya bunge..
Kukiuka mkataba na wakandarasi wa bwawa la nyerere na kusababisha mradi kuchelewa hakuhitaji kamati ya bunge.
So on and so forth..
Kumbuka pia audit ni rule based na principle based
Rules ni siasa lakini principles ni standard za ukaguzi ambazo ni universal.
Hasara ( Loss) si kigezo cha ufisadi ni metrics zinazohitaji professional opinion after Audit queries response. Ukiukwaji wa procurement process inaweza kuwa ni upindishaji wa taratibu lakini usio na hasara!

Kwenye ukaguzi Auditor anafata muongozo ulivyopaswa kufanyika alafu anaangalia taratibu zilizofatwa. Kama utaratibu haukufatwa lazima iwe query na risks zake. Wakati wa kufunga hoja inaweza kubaki na sura hii 1) Utaratibu umekiukwa lakini haukuleta hasara 2 ) Utaratibu umekiukwa na kuleta hasara. Vyote ni tatizo na hapo ndio tunapaswa kuhukumu.

Kwasasa CAG ameona jambo ambalo hajapata jibu na ameainisha risks za hilo aliloona! Sasa kabla hatujaanza siasa tungesubiri kuona serikali wamefungaje hiyo hoja then tuanze kelele!

Kwasasa wanasiasa mandumilakuwili wamebeba findings na figures zake wanahukumu watu kuwa ni mafisadi kuliko wakati wowote nchi hii imepata kushuhudia! Purely cheap politics kwa watu ambao wanajua facts ila wanatumia ufahamu wao kudanganya umma! Ni dhambi hii!
 
Hivi huyu Jamaa anapozungumzi haya yote, Ana Mke au kaachwa?? Sababu za kuachwa ni zipi?? Nimepata mashaka sana alipojaribu kujiingiza kwenye sakata la Mh Lissu.

Huyu Mzee kama aliweza kumsaliti Mungu Muumba wake kwenye Upadri atashindwaje Kwa Chadema?? Apambane na Laana zake huko.
 
Dr. Slaa na apologists wake wanataka tusiizungumzie ripoti ya CAG mpaka Kamati za Bunge zitoe blessing zao kwa sababu tutaingiza siasa!

Wanataka kutuaminisha kuwa hizo Kamati za Bunge ni apolitical na watakuwa neutral kwenye hoja za CAG!

Kutowasilisha majibu ya audit queries katika wakati muafaka ni sababu tosha ya jamii kutilia mashaka na integrity yako na ni lazima uhojiwe katika mahakama ya umma. Ukiweza kuzijibu hapo baadae, bado utabakiza tuhma ya uzembe wako.

Seriously, Slaa anataka tuamini Kamati ya Bunge iliyoundwa na Ndugai kuliko CAG ambae analindwa na Katiba ili kuhakikisha yuko above politics! Tusihoji kwa nini ATCL inaendeshwa kihasara mpaka wakina Tulia watupe kibali! Mzee kweli amechanganyikiwa.

Amandla...
Hapana! Huwezi kuzungumzia hoja ambazo hazijafungwa. Kama report hii ya CAG ndio final report sasa inakwenda Bungeni kufanya nini? Kuhukumu?

Nimetoa mfano mdogo sana, Chadema imewahi kupata Audit findings za CAG ambazo zilitumika kipropaganda lakini mwisho hizo findings zilikuja kuwa closed.

Auditor akiomba details au kiambatanisho asipopata kwa wakati maana yake utaenda kujibu kwenye kamati what happened! Why mnahukumu watu mafisadi tena kwa numbers ambazo bado hoja hazijafungwa?

Mkitaka kuenjoy kuita watu mafisadi kwa short cut kama hizi basi msilalamike baadae mambo yameishaje. Tusipende kudandia hoja za kisiasa bila kuzipima sababu anayesemwa humpendi au si mlengo wako.
 
Uneandika usichokiamini, au huujui labda ukweli.

CCM kuanzia 2015 haikuwahi kukubalika kwa wananchi, walilazimisha kukubalika kwa kutegemea mauaji, utekaji, nk.

Kama kweli unaamini agenda za upinzani zilianza kufanyiwa kazi na CCM from 2015, kwanini wakalazimisha wagombea wao wengi wapite bila kupingwa kwa sababu za kitoto kama kutokujua kujaza form?

Na kwanini wale wapinzani waliofanikiwa kugombea waliishia kuibiwa kura zao kwa namna ya aibu bila hofu yoyote na ushahidi ulikuwepo wa kila aina?
Weka evidence hapa za serikali kutoa amri ya kuua na kuteaka raia , sio evidence zenu za fulani kapotea, duniani kote watu wanapotea na wanapatikana, sio kitu kizuri lakini sio mara ya kwanza kutokea nchini, haya ni matukio ya uhalifu ambayo yako miaka yote Tanzania na yataendelea kuwepo.

Chaguzi zote Tanzania miaka yote kumekuwa na wagombea wa ccm kupita bila kupingwa, ni mwaka 2015 tu ndio vyama vya siasa vilisimamisha wagombea kila mahali, lakini bado ccm wabunge wengi walipita bila kupingwa. Chadema tuache hizi tabia za kuomba kuhurumiwa, chama kikubwa tunakuwa na maandalizi hafifu, watu hata kujaza form hawajui, kama sisi tunatambua hilo kujaza form kimakosa unakuwa nullified ni hseria kali ambayo tunatakiwa twende bungeni tukapige kelele ibadilishwe sio kusubiri huruma , tuko kwenye upinzani tunatakiwa tujiandae kikamilifu sio kutegemea huruma ya mtawala.

Shida kubwa ya chadema imejikita kwenye tetesi, tuliiniwa kura, ushahidi uko wapi? twendeni basi mahakamani wapi, kuna kesi nyingi za watu kuibiwa kula zingine tumewahi shinda, zingine tuna shindwa ni kawaida katika mfumo huu wa siasa, tetesi haiwezi kuwa sera au suluhisho, tuna kesi nyingi tumeibiwa kura ziko wapi? zinatambulika nani?, hata mimi naweza simama nikasema nimeibiwa kura hata kama nimeshindwa its normal katika siasa, kwani si DONAL TRUMP anazunguka USA nzima anadai aliibiwa kura lakini ushahidi uko wapi?, je wew unadhani ni kweli aliibiwa kura? hiyo ndio politics sio kila kitu kisemwacho ni kweli.
 

Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.

TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.

“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.

“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.

CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.

“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.

UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).

“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.

HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.

“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.

“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.

“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.

“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.

KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.

“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.

SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.

SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.

“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.

AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.

“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”

Chanzo: Dar24
haya mahojiano ameyafanyia nyumbani kwake mbweni? Nyumba aliyojengewa na Mbowe?
 
Tunakushukuru sana Mungu kwa kutuondolea huyu Mamluki Chadema
Mamluki ni wale waliozunguka miaka nane kutuaminisha kuwa lowasa hafai hata kuwa katibu kata, na mafuta ya chopa wakatuchangisha. Halafu ndani ya wiki wanatuambia kama tuna ushahidi wa ufisadi wa lowasa twende mahakamani kha!
 
Ipo siku ukweli utajulikana tu,si umeona wameanza kutajana kwa majina na vyeo.

Khalid Kagenzi pia alitekwa na kupigwa na wanaCDM wenzake.

Mtangazaji wa Uhuru FM aliwahi kutekwa na kuvunjiwa vifaa akireport maandamano hapo Ufipa.

Ben Saanane alikuwa haaminiki kwa Mbowe na mara zote akigombea ndani ya chama alikuwa akikatwa ghafla kawa msaidizi wake then kapotea!.

Uwezekano wa CDM kufanya hayo ili wapate cha kuisimangia serikali upo.

Haijalishi itakuwa baada ya muda gani ila ukweli utakuja kudhihiri.
 
Hapana kaka, tusubiri majibu ya hoja baada ya ukaguzi kupitia kamati ya bunge ili zile ambazo hazina majibu ndio ziwe mjadala.

Auditor anapotoa findings report huwezi kutuhumu mpaka wahusika watoe majibu! Mfano figure tunayoambiwa ni ufisadi ukichunguza kwa makini ni queries wanapaswa kuzitolea maelezo with evidence na si ufisadi!

Mfano kama kuna viambatanisho havijawa presented hadi Auditor ameondoka itabaki pending hadi umpatie! How report ya CAG ambayo inakwenda Bungeni kwaajili ya kamati za Bunge kuhoji wahusika then mandumilakuwili waitumie kutuhumu watu? Purely politics! Hii imewahi kuikumba Chadema na kutumika kwa propaganda hadi walipopeleka vithibitisho!

Audit findings zitageuka tuhuma zikikosa majibu kwa kamati ya Bunge. Tuwe fair, majibu yakikosekana wahusika wote wachukuliwe HATUA! Ikiwemo waliokuwa mawaziri. Kwa kiasi kikubwa hii taarifa jinsi inavyojadiliwa ni kisiasa tu! Muda utaongea.

..kama ni hivyo basi hiyo ripoti isiwe public mpaka pale waliotajwa watakapotoa majibu mbele ya kamati ya bunge.

..kutoa ripoti public halafu kutukataza kuijadili nadhani ni kutunyima uhuru wa kutoa maoni.
 
..kama ni hivyo basi hiyo ripoti isiwe public mpaka pale waliotajwa watakapotoa majibu mbele ya kamati ya bunge.

..kutoa ripoti public halafu kutukataza kuijadili nadhani ni kutunyima uhuru wa kutoa maoni.
Kuna watu wamepata access ndio wanafanya political spinning. Lakini hii inakwenda Bungeni na kupitia kamati zake facts zote zitafahamika.
 
Huyu kama aliusaliti upadri leo anashindwa nini KUONGEA upuuzi na ujinga huu!!.
 
MIE NILIMPENDA DKT SLAA PINDI AKIWA CHADEMA,NI MWANASIASA MWEREVU,MKWELI,NA MZALENDO HALISI WA TAIFA LETU,MPK MDA HUU MIE NINAMWAMINI NA KUMKUBALI,
 
Kupigwa risasi Lisu sio jambo la ajabu Bwana tuacheni! Kila siku jambo lile lile!
Kuna mshkaji alikuwa anasema kama wewe, juzi juzi hapa kaka yake wa damu kauawa kwa kupigwa risasi na polisi, kwa kumdhania kuwa ni jambazi, jamaa akawa analalamika sana kuwa kaka yake ameuliwa bila hatia, akapiga kelele sana kwamba kwanini hawakumpeleka mahakamani, baada ya kumaliza kulia nikamwambia "Matukio ya kupigwa risasi ni yakawaida sana" hata Marekani yanatokea sana, jamaa alifura hasira mara dufu...
 
Hapana! Huwezi kuzungumzia hoja ambazo hazijafungwa. Kama report hii ya CAG ndio final report sasa inakwenda Bungeni kufanya nini? Kuhukumu?

Nimetoa mfano mdogo sana, Chadema imewahi kupata Audit findings za CAG ambazo zilitumika kipropaganda lakini mwisho hizo findings zilikuja kuwa closed.

Auditor akiomba details au kiambatanisho asipopata kwa wakati maana yake utaenda kujibu kwenye kamati what happened! Why mnahukumu watu mafisadi tena kwa numbers ambazo bado hoja hazijafungwa?

Mkitaka kuenjoy kuita watu mafisadi kwa short cut kama hizi basi msilalamike baadae mambo yameishaje. Tusipende kudandia hoja za kisiasa bila kuzipima sababu anayesemwa humpendi au si mlengo wako.
Ni final in the sense kuwa inatoa hali aliyoiona wakati anafanya uchaguzi na baada ya kupewa ufafanuzi na wahusika . Wabunge na Rais wanapewa kama taarifa ambazo wanaweza kuzifanyia kazi kama wakitaka. Kamati hazina mamlaka ya kufunga hoja za mkaguzi. Wanachoweza kufanya ni kumshinikiza mhusika amalizane na CAG. CAG akiridhika ndio hoja inafungwa na sio otherwise.

Chadema ilikutwa na mapungufu ambayo ilikuwa haki yao kusulubiwa. Wao walifanya manunuzi bila kufuata utaratibu na CAG ndio aliwastua wakajirekebisha.

Hivi unataka kutuaminisha kuwa hizi Kamati za Bunge la Tullia zinaweza kuwa na uthubutu wa kunyooshea vidole ujenzi wa kiwanja cha Chato na ununuzi wa ndege? Zina uwezo wa kupitisha taarifa inayotoa mathlan hati chafu kwa CCM au hati safi kwa Chadema?

Tunapozungumzia ufisadi ni pamoja na uzembe. Na mara nyingi uzembe huo mara nyingi haziwezi kutatuliwa kwa risiti za kama mnavyosema. Inabidi iangaliwe mikataba, taratibu za ununuzi, uidhinishaji wa malipo n.k.

Kuibuliwa hoja za ufisadi hazimnyimi haki mhusika ya kujitetea. Msimamo wenu ni kama mtu kusema makosa anayoshutumiwa mtu yasiwekwe wazi mpaka mahakama itakapotoa hukumu! DPP atoe ushahidi wake kwa siri ili watu wasimhukumu mtuhumiwa kabla ya Jaji kutoa hukumu.

Hamna mtu atakayelalamika kama waliotuhumiwa watasafishwa hapo baadae. Labda nyie ambao pamoja na Chadema kusafishwa mliendelea kuwatuma wakina Takukuru kwenye fishing expedition.

Amandla...
 
Back
Top Bottom