Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Dkt. Slaa: CHADEMA walimteka mtu wao, wakamtesa, wakamtupa, mimi nikajua watekaji ni Usalama wa Taifa

Njaa mbaya sana, mzee anafukuzia kauteuzi laki anakosea step, kuegemea Sukumagang kunamkosesha teuzi
Yaani mzee ameshindwa kutambua kuwa atumie njia ipi kupata uteuzi? Si kweli ila anaouongea ndio ukweli kwa sababu anaongea wakati anajua kabisa hakuna anayemfurahisha hapo.
 
SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.
Hii aya hii...!Eeheeeee!
 
1. Sikubaliani naye kuhusu mtazamo wake kuhusu ripoti ya CAG kwamba isiwe public discussion. Mimi nadhani hoja za CAG zijibiwe na hao walioandikwa "vibaya." Hoja hizo zijibiwe kwa wananchi na zijibiwe mbele ya kamati ya bunge.

2. Sikubaliani na mtizamo wake kuhusu wabunge 19 ambao Chadema iliwakana. Ningemuelewa kama angeshauri mamlaka za uchunguzi zifuatilie kujua kilichotokea. Kama Chadema wanakana kuwa hawakuwapitisha wanachama wao kwenda bungeni, je nani aliwawezesha? Hilo ni suala la POLISI / TAKUKURU kuchunguza.

3. Kuhusu suala la Tundu Lissu, hivi Dr.Slaa anashindwa hata kutoa pole? Dr.Slaa anashindwa kushauri iundwe Tume ya Uchunguzi ili tujue nani alitaka kumuua mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni? Dr.Slaa anashindwa kumtaka Spika / Bunge lieleze Kamati ya Adadi Rajabu ilitoa ripoti gani ilipotakiwa na Spika Ndugai kuchunguza suala hilo?

4. Sikubaliani na kauli zake kuhusu Katiba Mpya. Kauli kwamba Katiba sio muarubaini wa matatizo ya Watanzania ni kauli zinazolenga kufifisha juhudi na harakati za kudai Katiba mpya. Hakuna aliyedai kwamba Katiba mpya ni muarubaini wa matatizo ya nchi yetu. Katiba sio muarubaini, sasa kwanini tuliandika katiba ya 1962, 1965, na 1977? Na kwanini tusiandike mpya sasa hivi kama tunaamini ya 1977 haitufai?
Jamani mbona watanzania hatujui hata tunachokitaka? Mfano yeye ameelezea swala la sheria wewe unasema mtazamo wake. Hivi watanzania tunataka katiba ya nini sasa wakati hatutaki sheria zifuatwe?
 
Alikuwa sehemu ya uhuni kama wahuni wenzake!

Je, aliripoti wapi!?
Alikaa kimya akichumia tumbo lake!
Shame. Huyu ndiyo angekuwa eti raisi!
Huyu na huyo mwenzake wakamatwe kwa kuhusika na utekajo .katujakikishia kuwa alijua hilo na akanyamaza na pia muhusika ni mlinzi wake
Ndo maana chadema ya kipindi chake ilikuwa ma matukio kuliko hii ya sasa
 
Jamani mbona watanzania hatujui hata tunachokitaka? Mfano yeye ameelezea swala la sheria wewe unasema mtazamo wake. Hivi watanzania tunataka katiba ya nini sasa wakati hatutaki sheria zifuatwe?

..Tunataka sheria nzuri, sio sheria zinazolinda watawala wabadhirifu.

..Watanzania wanadai Katiba mpya kwasababu iliyopo ni mbaya na imepitwa na wakati.
 
Ni kama vile sina uhakika nani alimpiga risasi Lissu lakini baada ya kumsikiliza Lissu na Slaa, najua Slaa ni muongo au disingenious.
Slaa anapotosha pale anapotoa mfano wa redbrigade akionyesha huenda limefanywa na Chadema. Fair enough! Slaa huyo huyo hajaeleza kwanini walinzi waliondolewa siku ya tukio na wapi Camera zilipelekwa. Walinzi na Camera ndizo zingetupa jibu ni akina nani.
Tena anakiri swali hilo anaulizwa sana, sijui kama hajui kwanini anaulizwa! na kwanini ana majibu yasiyo na mashiko
Nimesikiliza Slaa akizungumzia suala la wakina Mdee na naona anajaribu kutetea tu ugali wake. Pale ni wazi kuwa taratibu na Katiba ilikiukwa. Na sio Chadema waliokiuka. Slaa kupata kigugumizi kusema hilo ni ushahidi tosha kuwa hizo principles unazosema anazifuata sio zile alizoanza nazo.
Slaa anaelewa taratibu zilikukwa kwa ushahidi. Kwanza, walisema hawakupokea barua, Chadema wakaonyesha ''dispatch'' na kuzima uongo wa Job Yustino Ndugai

Chadema wakakana hawakupeleka majina.
Katika utawala bora ilitosha Spika kujiridhisha vyombo vya dola vingehusishwa, halikutokea.
J Y Ndugai akawaita Wanawake uani akawazawadia ubunge kwa kukiuka taratibu na ubabe tu akijua yeye ni msaidizi wa 'mungu'

Tuhuma za kughushi nyaraka ni nzito tena ikifanywa na TUME ya Uchaguzi.
Serikali ingeingilia lakini haikufanya hivyo. Slaa anasema waende Mahakamani! come on!
Anasema kuwa wawekezaji walikuwepo wakati wa awamu ya tano lakini viongozi wa chama chake kila kukicha wanatuambia kuwa wawekezaji wanaRUDI baada ya milango kufunguliwa tena.
Mawaziri wanasema hali ilikuwa mbaya sana. Rais SSH anasema wawekezaji ' Wanarudi'
Wanarudi kutoka wapi? Siyo wanakuja bali wanarudi ina maana waliondoka

Slaa muongo ongo tu ! maisha haya ya uongo ni ya kudhalilika sana
Slaa wa sasa haaminiki kabisa. Which is a shame maana kuna wakati tulimuamini sana. Kama ilivyokuwa kwa Mrema
Siyo kwamba haaminiki tu sijui kama ana heshima nyingine iliyobaki.

Anachokifanya ni ' kutaka kusikika' ili teuzi za bodi n.k. asiachwe.
Maisha ya dhalili sana

Waliomdhuru TL wanataka maridhiano hata CCM wanalaani!

Slaa anajipaka damu za watu bila sababu ! ni njaa gani hii?

Kwamba ana tupa principles , values na heshima kwa njia za hoovyo!
Anaonekana kituko mbele ya dunia!
 
Hasara ( Loss) si kigezo cha ufisadi ni metrics zinazohitaji professional opinion after Audit queries response. Ukiukwaji wa procurement process inaweza kuwa ni upindishaji wa taratibu lakini usio na hasara!

Kwenye ukaguzi Auditor anafata muongozo ulivyopaswa kufanyika alafu anaangalia taratibu zilizofatwa. Kama utaratibu haukufatwa lazima iwe query na risks zake. Wakati wa kufunga hoja inaweza kubaki na sura hii 1) Utaratibu umekiukwa lakini haukuleta hasara 2 ) Utaratibu umekiukwa na kuleta hasara. Vyote ni tatizo na hapo ndio tunapaswa kuhukumu.

Kwasasa CAG ameona jambo ambalo hajapata jibu na ameainisha risks za hilo aliloona! Sasa kabla hatujaanza siasa tungesubiri kuona serikali wamefungaje hiyo hoja then tuanze kelele!

Kwasasa wanasiasa mandumilakuwili wamebeba findings na figures zake wanahukumu watu kuwa ni mafisadi kuliko wakati wowote nchi hii imepata kushuhudia! Purely cheap politics kwa watu ambao wanajua facts ila wanatumia ufahamu wao kudanganya umma! Ni dhambi hii!
Nimeconcentrate kwenye loss ili kuua upotoshaji wa makusudi wa Jpm aliokuwa anaufanya kwa shirika la ndege..
Again nimerefer procurement process ili kuuleta uwanja wa ndege wa chato
Specifically nimerebutt claims na matendo ya mwendazake
But tunaweza kwenda query kwa query ya ripoti ya CAG kuonesha kuwa misappropriation nyingi hoja zake zipo conclusive ukichukulia walipewa siku 21 kujibu hoja..
By the way CAG anatoa opinion either qualified,unqualified au disclaimer.
Nisaidie ripoti ya taasisi yoyote aliyosema kuna ubadhirifu.
 
Naanza kuona mbadala wa jpm kwa mbali
Nahitaji watu wa kweli na wawazi
 
Jamani mbona watanzania hatujui hata tunachokitaka? Mfano yeye ameelezea swala la sheria wewe unasema mtazamo wake. Hivi watanzania tunataka katiba ya nini sasa wakati hatutaki sheria zifuatwe?
sheria gani aliyosema?
 
sheria gani aliyosema?
mimi si mtaalamu wa sheria lakini Dr Slaa ametaja kitu hapo. Kama ni mtaalamu wa sheria ndiyo fuatilia.

“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu."
 
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu."
Kuandika sheria haijibu hoja ya Zitto
Slaa anapaswa kueleza upotoshaji upo wapi na ajibu hoja kwa mantiki si general
 

View attachment 2201790
Picha: Dkt. Willbrod Slaa

Mwanasiasa Willbrod Peter Slaa amefanya mahojiano na kuzungumza mambo mengi kuhusu siasa, mahojiano haya ni mwendelezo ya interview aliyofanya wiki iliyopita.

TAARIFA YA CAG INAPOTOSHWA
“Kuna upotoshwaji kwenye taarifa ya CAG, nadhani Zito Kabwe angelisaidia sana taifa hili kama angekuwa mkweli, mimi na Zitto tulishiriki kutengeneza sheria ya ukaguzi wa fedha 2009, hata maneno yaliyopo kwenye sheria hiyo yametoka kwetu.

“Moja ya maelezo ya ile sheria inasema baada ya CAG kukabidhi ripoti yake kwa Rais kisha kuifikisha Bungeni siku saba baadaye, ripoti hiyo haitakiwi kuwa public discussion, kwa kuwa ni kama mhtasari tu wa ripoti.

“Inatakiwa Kamati ya Bunge ndiyo iifanyie kazi, mfano kuna sehemu unaweza kukuta risiti haikuonekana wakati wa ukaguzi lakini hiyo ikapitishwa na kuonekana ni wizi, tumepotosha maana ya ile taarifa ya CAG.

CAG AMESABABISHA TAHARUKI KWA RIPOTI YAKE
“Kwanza hata CAG mwenyewe amechangia kuleta hii taaruki kwa kuwa huwa ni ya awali tu na analijua hilo, inatakiwa irudi kwa akaunti ofisa wa Serikali ijadiliwe, pia CAG wakati anatoa taarifa zake hadharani hatakiwi kuingia ndani kutoa ufafanuzi zaidi kama anavyofanya.

“Unaweza kukuta ripoti hiyo ikifika kwenye Kamati ya Bunge vitu vingi vikawekwa sawa, mfano labda kulikuwa na upotevu fulani wa mambo madogomadogo ambayo kwa nje yanaonekana kama ni wizi lakini details zikiwekwa sawa kunakuwa hakuna tatizo.

UBUNGE WA KINA MDEE SPIKA HANA KOSA, NITAZUNGUMZA CHADEMA WAKISHAKAA KIKAO
“Nimeona kwenye vyombo vya habari kuwa watajadiliwa na chama chao katika rufaa yao, naona lawama zimepelekwa kwa mtu ambaye hausiki (Spika).

“Chama kilitakiwa kufungua kesi Mahakamani kuhoji Tume ya Uchaguzi kwa kupitisha majina hayo lakini sijaona kesi. Mimi nitazungumza baada ya rufaa yao kupitiwa na CHADEMA, nimesikia wanakaribia kuwajadili kwenye kikao chao.

HOJA YA KATIBA SIYO MAHITAJI MUHIMU YA WANANCHI
“Mabosi wa vyama vya siasa ni wananchi, wanatakiwa kujiuliza wanayoyafanya yanawagusa vipi wananchi, kwa sasa kuna mambo mengi ya muhimu lakini hivyo vyama vimekuwa bize kuzungumza habari za ajenda ya Katiba.

“Hawana ajenda ambazo mwananchi anaweza kujiuliza kama inaweza kuweka chakula mezani, hakuna katiba ambayo inaweza kuzungumzia kila kitu.

“Katiba yetu ina vipengele vingi vya muhimu lakini havitekelezwi, japo sijasema kuwa katiba siyo muhimu.

“Mimi ni kati ya watu waliozunguka Tanzania kukusanya maoni lakini tusipotoshe kuwa katiba ndiyo jibu la kila kitu, siyo kweli.

“Leo hii Marekani ina katiba tunayoisifu lakini Donald Trump si alishutumiwa anataka kufanya mageuzi.

KATIBA PENDEKEZWA NI MBOVU KULIKO KATIBA YA SASA
Sisi tuna maoni ya Jaji Warioba, licha ya kuwa kulikuwa kuna mambo yamekosekana lakini yapo mazuri ambayo tunaweza kuyatumia.

“Baada ya maoni hayo kupelekwa Bungeni ikachujwa ikatoka inayoitwa Katiba Pendekezwa, ni mbovu kuliko hata katiba tuliyonayo sasa hivi.

SIZUNGUMZII SUALA LA LISSU KUPIGWA RISASI SABABU UTEKAJI ULIKUWEPOA CHADEMA
“Kuna watu wananiuliza kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi, kuwa sipendi kulizungumzia hilo kwa kuwa sita taarifa zake za uhakika.

“Nitoe mfano iliwahi kutokea huko nyuma nikiwa Katibu Mkuu CHADEMA, nililetewa taarifa za mtu wangu anaitwa Joseph, huyu alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, alitekwa saa sita usiku. Kesho yake saa sita mchana nikahitisha mkutano na waandishi wa habari nikaisema sana Serikali na Usalama wa Taifa.

“Saa nane mchana siku hiyohiyo Joseph akapatikana, alikutwa ametupwa maeneo ya Ununio ameumia sana usoni.

“Mwezi mmoja baadaye kijana wangu wa Red Brigade anakuja kwangu kuniambia yeye ndiye aliongoza kukosi cha kwenda kumteka nyara huyo mwenyekiti huyo.

“Nikauliza kwa nini hakuja kwangu akasema ‘wapo viongozi wanaojua’, nikaamua kunyamaza, ndiyo maana ninapoulizwa suala la Lissu ninasema hapana, CHADEMA kwanza wajiangalie wao ndani.

“Huyo kijana (Joseph) walivyomtupa ufukweni walijua amekufa, kumbe alikuwa hajafa labda upepo ulimpiga akaamka. Miaka kadhaa baadaye tukaanza kusikia watu wanaokotwa wamekufa ufukweni, unadhani inatoa pcha gani!

“Ukiwa kiongozi lazima uwe kunasema ukweli hata kama unaona watu wako wanakosea.

SINA TATIZO LA LOWASSA
“Mimi na Lowassa tulipishana kwenye principal siyo maisha, mimi niliwahi kufanya fund rising na Jakaya Kikwete siku moja baada ya kupanda jukwaani na kumsema tena kwa mambo mazito.

“Nimeishi Ulaya, nimeona mambo ya kwenye mabunge, kuna muda inafika hatua wabunge wanapigana ngumi lakini wakitoka wanaenda kunywa bia. Unatakiwa kutofautisha maisha binafsi na siasa. Hivyo sikuwa na tatizo binafsi na Lowassa.

AWAMU YA TANO HAIKUFELI DIPLOMASIA YA KIMATAIFA
“Watanzania tuwe wakweli, tumefeli wapi, mimi nimekutana na wafanyabiashara wengi, wapo walioniambia wamchoshwa na Tanzania yenye ufisadi.

“Wapo walioamua kuondoa biashara zao huko nyuma lakini katika awamu ya tano waliamua kurejesha biashara hapa nchini, kwa nini? Ni kwa sababu kulikuwa kuna mambo mengi yanaenda vizuri, nazungumza kwa kuwa najua zaidi kilichokuwa kinaendelea.”

Chanzo: Dar24
CHADEMA NJOONI MJIBU
 
Weka evidence hapa za serikali kutoa amri ya kuua na kuteaka raia , sio evidence zenu za fulani kapotea, duniani kote watu wanapotea na wanapatikana, sio kitu kizuri lakini sio mara ya kwanza kutokea nchini, haya ni matukio ya uhalifu ambayo yako miaka yote Tanzania na yataendelea kuwepo.

Chaguzi zote Tanzania miaka yote kumekuwa na wagombea wa ccm kupita bila kupingwa, ni mwaka 2015 tu ndio vyama vya siasa vilisimamisha wagombea kila mahali, lakini bado ccm wabunge wengi walipita bila kupingwa. Chadema tuache hizi tabia za kuomba kuhurumiwa, chama kikubwa tunakuwa na maandalizi hafifu, watu hata kujaza form hawajui, kama sisi tunatambua hilo kujaza form kimakosa unakuwa nullified ni hseria kali ambayo tunatakiwa twende bungeni tukapige kelele ibadilishwe sio kusubiri huruma , tuko kwenye upinzani tunatakiwa tujiandae kikamilifu sio kutegemea huruma ya mtawala.

Shida kubwa ya chadema imejikita kwenye tetesi, tuliiniwa kura, ushahidi uko wapi? twendeni basi mahakamani wapi, kuna kesi nyingi za watu kuibiwa kula zingine tumewahi shinda, zingine tuna shindwa ni kawaida katika mfumo huu wa siasa, tetesi haiwezi kuwa sera au suluhisho, tuna kesi nyingi tumeibiwa kura ziko wapi? zinatambulika nani?, hata mimi naweza simama nikasema nimeibiwa kura hata kama nimeshindwa its normal katika siasa, kwani si DONAL TRUMP anazunguka USA nzima anadai aliibiwa kura lakini ushahidi uko wapi?, je wew unadhani ni kweli aliibiwa kura? hiyo ndio politics sio kila kitu kisemwacho ni kweli.
"2015 vyama vya siasa vilisimamisha wagombea kila mahali lakini bado CCM ilipita bila kupingwa"

Hiyo nukuu yako hapo juu inaonesha hujui unachoandika, unajifurahisha tu, sioni sababu ya kukujibu.
 
Sijawahi kufikiria kama Dr. Slaa anaweza kuwa mnafiki kiasi hiki! Kwa umri wake, hastahili kuwa hivyo. Lazima kuna kitu hakipo sawa kichwani au moyoni mwake.

Kama CHADEMA walijaribu kumwua kiongozi wao, yeye Dr. Slaa alikuwa kiongozi kwenye Serikali ya awamu ya 5, tena Serikali iliyouchukia sana upinzani, serikali iliyokuwa tayari hata kuyatengeneza makosa dhidi ya wapinzani ili kuwakomoa/kuwakomesha, alishindwa nini kuitoa hiyo taarifa? Jinai huwa haifi.

Polisi wanatakiwa kumkamata Dr. Slaa na kumhoji kuhusika kwake na utekaji na kukusudia kumwua mtu aliyemtaja. Yeye alikuwa mtendaji mkuu wa chama. Kama kuna uovu uliofanywa, yeye aliyekuwa mtendaji mkuu, ndiyo mahali sahihi pakuanzia. Hata kama hakushiriki, bado ana hatia. Maana kujua kuwa kuna uovu umetendeka halafu ukakaa kimya, ni hatia.

Lakini pia tujiulize, aliyetekwa na kujaribu kuuawa ni mzima, alinusurika, kwa nini hakwenda kushtaki, wakati watekaji walikuwa wanafahamika?

Hivi kweli tunahitaji kuumiza kichwa kujua kwanini propaganda hizi zinakuja sasa tena kwa kumtumia Dr Slaa ambaye amewahi kuwa mtendaji mkuu wa CHADEMA..?

Jibu ni moja au mawili tu kuhusu hili;

MOSI; Hii yote ni kujaribu kuipotezea ishu ya TL kupigwa risasi na bila wahusika kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria..

Lakini kulipotezea hili haiwezekani kwa sasa kwa sababu calculation ya namna ya kuutekeleza uuaji huo ulikosewa na kuvurugika kabisa beyond reparable kiasi cha tukio zima limekuwa Zimwi linalowawinda na kutaka kuwatafuna wahusika wenyewe...!!

MBILI; Kuuineza propaganda hii kwa namna anavyofanya Dr Slaa (kama kweli wameamua kumtumia) ni ujinga na upumbavu usioweza kueleweka kirahisi kwa watu...

Maana kama jaribio la kuuwawa Tundu Lissu ni INSIDE JOB ya CHADEMA yenyewe, kwanini mpaka leo vyombo vya uchunguzi na kisheria - polisi wasiingie huko CHADEMA na kuwachunguza na kuwafikisha ktk vyombo vya sheria wahusika? Je, wanawaogopa CHADEMA? If so, why waogope?

Pamoja na yoyote, lakini kwa hatua na muda ambao ishu hii imefikia, hakuna mjinga yeyote anayeweza kumwamini yeyote asemaye kuwa, eti Tundu Lissu alitaka kuuwawa na CHADEMA wenyewe...!

Ingekuwa hivi kweli, Mwendazake Magufuli aliyekuwa na chuki na hiki chama, nakuhakikishia angelishalala mbereee na CHADEMA kwa kuiondolea mbali ktk uso wa dunia kabla yeye mwenyewe hajafutiliwa mbali kwa kifo cha aibu katika Zahanati ya Mzena, DSM March 17, 2021...!!!!

Waliojaribu kumuua Tundu Lissu wanajulikana na ni haohao wanaopaswa kuchunguza tukio hili. Na wa kwanza wao tayari, hukumu ya kifo ilishapitishwa juu yake. Si mwingine bali ni aliyekuwa Rais wa Tanzania (2015 - March 17, 2021) Hayati, Mwendazake na Dikteka Uchwara John Pombe Magufuli...!!
 
Hivi kweli tunahitaji kuumiza kichwa kujua kwanini propaganda hizi zinakuja sasa tena kwa kumtumia Dr Slaa ambaye amewahi kuwa mtendaji mkuu wa CHADEMA..?

Jibu ni moja au mawili tu kuhusu hili;

MOSI; Hii yote ni kujaribu kuipotezea ishu ya TL kupigwa risasi na bila wahusika kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria..

Lakini kulipotezea hili haiwezekani kwa sasa kwa sababu calculation ya namna ya kuutekeleza uuaji huo ulikosewa na kuvurugika kabisa beyond reparable kiasi cha tukio zima limekuwa Zimwi linalowawinda na kutaka kuwatafuna wahusika wenyewe...!!

MBILI; Kuuineza propaganda hii kwa namna anavyofanya Dr Slaa (kama kweli wameamua kumtumia) ni ujinga na upumbavu usioweza kueleweka kirahisi kwa watu...

Maana kama jaribio la kuuwawa Tundu Lissu ni INSIDE JOB ya CHADEMA yenyewe, kwanini mpaka leo vyombo vya uchunguzi na kisheria - polisi wasiingie huko CHADEMA na kuwachunguza na kuwafikisha ktk vyombo vya sheria wahusika? Je, wanawaogopa CHADEMA? If so, why waogope?

Pamoja na yoyote, lakini kwa hatua na muda ambao ishu hii imefikia, hakuna mjinga yeyote anayeweza kumwamini yeyote asemaye kuwa, eti Tundu Lissu alitaka kuuwawa na CHADEMA wenyewe...!

Ingekuwa hivi kweli, Mwendazake Magufuli aliyekuwa na chuki na hiki chama, nakuhakikishia angelishalala mbereee na CHADEMA kwa kuiondolea mbali ktk uso wa dunia kabla yeye mwenyewe hajafutiliwa mbali kwa kifo cha aibu katika Zahanati ya Mzena, DSM March 17, 2021...!!!!

Waliojaribu kumuua Tundu Lissu wanajulikana na ni haohao wanaopaswa kuchunguza tukio hili. Na wa kwanza wao tayari, hukumu ya kifo ilishapitishwa juu yake. Si mwingine bali ni aliyekuwa Rais wa Tanzania (2015 - March 17, 2021) Hayati, Mwendazake na Dikteka Uchwara John Pombe Magufuli...!!
Kama vile nakuona unavyogugumia kwa maumivu😂😂😂 Amesha lala mwenzako Mungu aliamua apumzike asije dhalilika
 
Back
Top Bottom