Kwa polisi ipi?
Shida ni mpaka waamue au iwe na msukumo fulani fulani hiyo kesi.Kuna kesi nyingi tu ambazo polisi wamefanya uchunguzi wao kwa umahiri na kupelekea wahusika wote kutiwa nguvuni na ushahidi mzito kupatikana hasa kwa kutumia taarifa za mawasiliano ya kimtandao.
Rejea hii habari: Laini ya simu ilivyowakamatisha wauaji wa dereva bajaji
Haya mambo yanawezekana huu muingiliano wa watu wa ghafla umesababisha mazito Dom kabla ya serikali kuhamia kina mihanyenye walikua washaridhika na mlenda wao ila baada ya watumishi kuingia na mafedha na ukiangalia jamii nyingi za kina mihanyenye ni duni sana akipata mtu wa kumpa mia mbili mia tatu hadi mumewe anamuona mbuzi maji matokeo yake hayo ,kwa kifupi jamii hiyo haikuandaliwa kupokea muingiliano wa ghaflaDodoma sahv kuna muingiliano wa wageni wengi sana
Ova
Sasa umsikilize yule RPC wao anavyoongea kwa mbwembwe....pole nyingi kwa wafiwa.Dodoma mtupumzishe aiseee
R.I.P , niliuliza hapa shida ni nn?mbona watu wamekua makatili hvi jamani!!Mama na mtoto wake wa kike, wakazi wa mtaa wa Muungano jijini Dodoma, wameuawa baada ya kufanyiwa vitendo vya ukatili na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo Septemba 6, 2024.
Waliouawa ni Mwamvita Mwakibasi (33) na binti yake Salma Ramadhan (13), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mkonze, jijini Dodoma.
Dada wa marehemu, Pendo Mwakibasi, ameeleza kuwa alipigiwa simu na mama yao mzazi kutoka Mbeya saa 8:00 usiku wa kuamkia leo, akiambiwa kuwa mdogo wake amevamiwa nyumbani kwake.
Pia soma: Miili ya wanawake wawili yaokotwa Dodoma
Alipofika nyumbani hapo, aliwakuta mdogo wake na mtoto wake wakiwa katika hali mbaya, wakitokwa damu sehemu mbalimbali za miili yao na wakiwa hawawezi kuongea.
Amesema waliwapeleka hospitali, lakini alihisi mdogo wake tayari alikuwa amefariki. Salma aliwekewa oksijeni na dripu, lakini baadaye wote wawili walifariki dunia.
Watanzania siku hizi niwanafiki sana... Majirani wameshindwa toa msaada lakini ukiwakuta wanavyo hadithia tukio utachoka...
Siku moja nilikiwa zangu stand ya daladao maeneo ya chanika... Mishale kama ya saa 12 hivi asubuhi... Kule Kuna shida ya sana ya usafiri hasa kwa wanafunzi... Nipo stand gari ikaja mwanafunzi wa kiume akawa anaikimbilia konda alimsukuma vibaya mno... Nusura ateleze aingie uvunguni mwa gari... Maajabu watu wamekausha nadhani walikuwa wanajifanya hayawahusu.... Nilimaindi sana ikabidi nisogee nimuulize konda kwa nini kamsukuma mtoto na je angemuimiza konda anatoa matusi afu watu bado wancheka wanaona kama anafurahisha NILIBADILIKA GHAFLA NIKAMSHIKA YULE MWANAFUNZI MKONO NIKAPANDA NAE KWENYE GARI INGAWA HAIKUWA ROOTI... NIKAJISEMEA HUYU NAENDA NAE HADI MWISHO... NIKAMWAMBIA KONDA UKIONGOEA CHOCHOTE NITAKUTIA MIKONDE HADI USHANGAE... AKANYWEA... GARI IMEEENDA MWISHO WA SIKU AKASHUKIA NJIANI NIKAONA KONDA MWENGINE ANATOKEA NYUMA GARI ANAIUSANYA NAULI.... NIKASEMA BAHATI YAKE... LAKINI YOTE KWA YOTE WATZ WANAFIKI SANA SIKU HIZI
Hii dunia ni kama imefika mwisho. Matukio mabaya Kila siku hadi inatisha.Mama na mtoto wake wa kike, wakazi wa mtaa wa Muungano jijini Dodoma, wameuawa baada ya kufanyiwa vitendo vya ukatili na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo Septemba 6, 2024.
Waliouawa ni Mwamvita Mwakibasi (33) na binti yake Salma Ramadhan (13), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Mkonze, jijini Dodoma.
Dada wa marehemu, Pendo Mwakibasi, ameeleza kuwa alipigiwa simu na mama yao mzazi kutoka Mbeya saa 8:00 usiku wa kuamkia leo, akiambiwa kuwa mdogo wake amevamiwa nyumbani kwake.
Pia soma: Miili ya wanawake wawili yaokotwa Dodoma
Alipofika nyumbani hapo, aliwakuta mdogo wake na mtoto wake wakiwa katika hali mbaya, wakitokwa damu sehemu mbalimbali za miili yao na wakiwa hawawezi kuongea.
Amesema waliwapeleka hospitali, lakini alihisi mdogo wake tayari alikuwa amefariki. Salma aliwekewa oksijeni na dripu, lakini baadaye wote wawili walifariki dunia.