Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Mtoto wa mfanyabiashara maarufu jijini Dodoma anayejulikana kwa jina la Jojo, Graison Kanyenye (6), anadaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakati mama yake akiwa matembezini usiku wa kuamkia jana.
Mbali na hilo, Jeshi la Polisi limesema mwili wa mtoto huyo ulikutwa ndani ya nyumba ukiwa na majeraha shingoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi amesema jana, Desemba 25, 2024 kuwa tukio litokea saa 1.00 asubuhi katika Mtaa wa Bwawani, Ilazo Extension jijini Dodoma, nyumbani kwa Ofisa Uvuvi wa Mtera, Hamis Mohamed.
Amesema Hamis (anatajwa kuwa mpenzi wa mfanyabiashara huyo) na mama yake walitoka kwenda matembezini na kumwacha mtoto huyo chini ya usimamizi wa dereva bodaboda wa Ilazo Extension, Kelvin Gilbert.
Bodaboda huyo anayetajwa kuwa walimfahamu kupitia huduma ya usafiri wanayoitoa kwa familia, aliachiwa mtoto ili amwangalie kipindi ambacho watakuwa kwenye matembezi wawili hao (Hamis na mfanyabiashara huyo).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi amesema jana, Desemba 25, 2024 kuwa tukio litokea saa 1.00 asubuhi katika Mtaa wa Bwawani, Ilazo Extension jijini Dodoma, nyumbani kwa Ofisa Uvuvi wa Mtera, Hamis Mohamed.
Amesema Hamis (anatajwa kuwa mpenzi wa mfanyabiashara huyo) na mama yake walitoka kwenda matembezini na kumwacha mtoto huyo chini ya usimamizi wa dereva bodaboda wa Ilazo Extension, Kelvin Gilbert.
Bodaboda huyo anayetajwa kuwa walimfahamu kupitia huduma ya usafiri wanayoitoa kwa familia, aliachiwa mtoto ili amwangalie kipindi ambacho watakuwa kwenye matembezi wawili hao (Hamis na mfanyabiashara huyo).