Dodoma: Nicodamus Maganga (Mbunge) adai Mishahara na Posho haiwatoshi Wabunge. Ashangiliwa...

Dodoma: Nicodamus Maganga (Mbunge) adai Mishahara na Posho haiwatoshi Wabunge. Ashangiliwa...

Mbona hataji anacho pata kakomaa tu na hazitoshi?
 
Siamini nilichosikia au kusoma toka kwa huyu wa poti, jibu rahisi, jivue ubunge, rudi mtaani, uone kasheshe yake.
Ila sishangai, viongozi wetu wanatuona mbumbu sana sana, achana yale ya kujengeana nyumba na kupeana magari, bado wanataka zaidi?! Inauma sana sana aise..
 
Wabunge waongezewe posho angalau iwe pe sitting USD 50K, pia marupurupu mengine na wasimbe juu
 
Hii ni kashfa kwa watumishi wengine wa umma na wapiga kura wake. Wamshinikize aache ubunge aende kufanya kazi nyingine yenye maslahi, kazi ya ubunge sio y lazima.

Vv
 
HUYU ANATAKA AONGEZEWE MSHAHARA , UNAMSHAURI NINI ?
Naunga mkono hoja, aongezewe, lakini kabla ya kuongezewa atuoneshe ameongeza sh ngapi kwenye mfuko wa taifa: Ukiwa na akili timamu huwezi kumwambie bibi yako ukuongezee kiporo wakati unga uliopika kiporo ilikuwa Robo kilo
 
Walai mwenye shibe hamjui mwenye njaa mbunge huyu ambae mshahara wake hukatwi kodi marupurupu kibao bado anadai mshahara hautoshi??
 
Kama masihara vile, utashangaa wanaongezewa mshahara, wanajua tutapiga kelele mtandaoni baada ya wiki diamond atapiga picha kapaka lipstick [emoji168], imeisha hiyo, wameshajua asilimia kubwa ya watz weengi ni mapopoma.

Bila ya kufanya jambo la kujenga heshima, tukaheshimiana sijui tunafika wapi, sie tutakufa ila vizazi vyetu vitapata tabu, gap la mwenye nacho na asienacho linaongezeka.

Katiba mpya inaweza kuwa dawa kidogo, lakini kwa mazoea yetu, bado wataivuruga vuriga katiba mpaka basi.. Kuna kitu inabidi tukitoe, watuheshimu kwanza.
 
Niliwahi kushauri Ubunge usiwe na mshahara, iwe kama kazi ya kujitolea na wawezeshwe wanapokua kikaoni kwa posho kidogo, humo tutapata Wabunge tunaowataka na watakaotutumikia sio hawa walionunua nafasi na sasa wanaona m. 12 ni kidogo kwakua wanadaiwa. Yaani mshahara na posho za Ubunge ambazo ni zaidi ya 10m ni ndogo anajilinganusha na mtumishi gani wa umma? Daltari, Nesi au Mwalimu?
 

Maganga, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, mkoa wa Geita. Ñinakushauri, kama mshahara haukutoshi nenda kachimbe dhahabu jimboni kwako. Vinginevyo 2025 nafasi hiyo utasikia radioni .​

Huyo Maganga ni mchimbaji kitambo ndo maana anaona mshahara wa wabunge ni visenti tu
 
Uyo hatoboi 2025...
Hawa walikuwa wanatumia ubunge kupitisha biashara zao za magumashi baada ya serkali kuwa macho ubunge sasa hauna maana kwa kuwa imekuwa kusubiria mshara na posho tu.
 
"Kuna manung'uniko maslahi ya Wabunge ni kidogo, wakati sijaingia humu nilikuwa nafikiria kuna posho za kutosha, nimeangalia Mabunge mengine wanalipa kwa dola, tusiwaogope Wananchi kwenye Ubunge hakuna kitu tunatukanwa tu mitandaoni”—-Mbunge wa Mbogwe, Maganga

====

Dodoma. Mbunge wa Mbogwe (CCM), Nicodamus Maganga amewataka wabunge kuwaeleza wananchi ukweli kuwa mishahara na posho wanazolipwa hazitoshi.

Maganga aliyasema hayo jana Jumatatu Juni 21, 2021 bungeni mjini Dodoma wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22.

“Nikiwa bado sijaingia humu nilikuwa nafikiria kuna posho za kutosha. Nimeangalia mabunge mengine Afrika ya Kusini pamoja na Kenya pamoja na mabunge mengine wanalipa kwa dola,” amesema huku akipigiwa makofi na wabunge wengine.

Amewataka wabunge kueleza ukweli wananchi kuhusu malipo yao, “tumekuwa tukitukanwa kwenye mitandao. Waziri na mimi hii kazi niliiomba kwa roho yangu moja na mimi nitasema kweli daima fitna kwangu mwiko. Pesa inayolipwa posho, mishahara haitoshi,” amesema.

Huku akiitaka Serikali kuwaangalia ili wafanane na mabunge mengine amesema, “tusiwe wajanjawajanja, ninaujua utapeli wa kila aina lakini sitaki niwe tapeli wananchi wajue wana mbunge mwenye hela huku hakuna kitu kinachoendelea.”

Amesema Bunge la bajeti limebakiza siku tisa kumalizika na wananchi wanapoona wabunge wamerejea majimboni wasidhani kuwa wana fedha akisisitiza, “bungeni hakuna kitu.”

Chanzo: Mwananchi
View attachment 1826321

HUYU ANATAKA AONGEZEWE MSHAHARA , UNAMSHAURI NINI ?
Hizi ndiyo takataka mwendazake alizototuachia, wakati wafanyakazi wa Serikali wakilia kutokuongezwa mishahara kwa miaka sita dhalim alikuwa anawajibu kuwa kama wanaona mishahara haiwatoshi waende wakalime,lakini yeye katujazia vilaza Bungeni wanaoliopwa zaidi ya 12 kwa mwezi bila kukatwa kodi na bado wanaona hazitoshi. Hakika huko aliko dhalim lazima aongezewe adhabu
 
Kabla ya ubunge alikuwa anapata kiasi gani?
hawa ndo akili na maono ya Mwendazake
 
Watumishi tukidai nyongeza ya mishahara mlikuwa mnasema tuwe wavumilivu kwanza ili mjenge nchi,Sasa na na ninyi Wabunge muwe watulivu hamna Cha kuongezewa mishahara mkae kwa kutulia.
 
Back
Top Bottom