Earthmover
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 24,977
- 23,799
NSSF zulumati makaa ya mawe HAYATOSHI...
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Atuambie baada ya miaka mitano zile milioni500 hazikatwi kodi ni hela kidogo hiyo? Atuambie lile gari atalopewa je? muambie je mshahara wa mbunge unakatwa kodi? atuambie toka awamu ya tano mishahara imeongezeka kwa kiasi gani? akae akijua asijilinganishe maisha na jirani yake kila nyumba ina style yake ya kula kutokana na walichojaliwa"Kuna manung'uniko maslahi ya Wabunge ni kidogo, wakati sijaingia humu nilikuwa nafikiria kuna posho za kutosha, nimeangalia Mabunge mengine wanalipa kwa dola, tusiwaogope Wananchi kwenye Ubunge hakuna kitu tunatukanwa tu mitandaoni”—-Mbunge wa Mbogwe, Maganga
====
Dodoma. Mbunge wa Mbogwe (CCM), Nicodamus Maganga amewataka wabunge kuwaeleza wananchi ukweli kuwa mishahara na posho wanazolipwa hazitoshi.
Maganga aliyasema hayo jana Jumatatu Juni 21, 2021 bungeni mjini Dodoma wakati akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22.
“Nikiwa bado sijaingia humu nilikuwa nafikiria kuna posho za kutosha. Nimeangalia mabunge mengine Afrika ya Kusini pamoja na Kenya pamoja na mabunge mengine wanalipa kwa dola,” amesema huku akipigiwa makofi na wabunge wengine.
Amewataka wabunge kueleza ukweli wananchi kuhusu malipo yao, “tumekuwa tukitukanwa kwenye mitandao. Waziri na mimi hii kazi niliiomba kwa roho yangu moja na mimi nitasema kweli daima fitna kwangu mwiko. Pesa inayolipwa posho, mishahara haitoshi,” amesema.
Huku akiitaka Serikali kuwaangalia ili wafanane na mabunge mengine amesema, “tusiwe wajanjawajanja, ninaujua utapeli wa kila aina lakini sitaki niwe tapeli wananchi wajue wana mbunge mwenye hela huku hakuna kitu kinachoendelea.”
Amesema Bunge la bajeti limebakiza siku tisa kumalizika na wananchi wanapoona wabunge wamerejea majimboni wasidhani kuwa wana fedha akisisitiza, “bungeni hakuna kitu.”
Chanzo: Mwananchi
HUYU ANATAKA AONGEZEWE MSHAHARA , UNAMSHAURI NINI ?
Kwani kuna chama gani humo chief,si ni kikao cha CCM tupu humo? Hao wameshiba mpaka wanaanza kucheua sasa,hawajui walimu,wanaishi kwa mshahara mdogo kiasi gani huku wakipigika na kazi kubwa na mazingira mabayaMbuge wa ajabu sana, Kama anataka fedha/hera jibu ni Kujitoa afanye biashara. Kazi yoyote ya Kuajiliwa haina fedha za Kutanulia. Hata hivyo kama anaona aliburge steps arudishe Jimbo watu ni wengi wa kuwatumikia watanzania. Mbuge wa ajabu sana, kumbe aliwaambia wananchi wake kuwa atarudi kwao na hera...bure kabisa sijui anatoka Chama gani???
Yaani inauma mno hadi nimekumbuka tweet ya Jamaa mmoja anamwambia Mama Samia "hivi hakuna namna ya kubana hewa mle bungeni ili wote waliomo humo wote wafe?Au kama vipi Corona impitie na yeye.
Yaani ana roho mbaya sana huyu mbaba daahh!Mpuuzi sana huyu!!! Yeye kama milioni 11 kwa mwezi na rupurupu nene bado hatosheki anawaambia nini Wafanyakazi ambao hawapati hata robo ya mshahara wake?
Hela haiwezi kukutosha kama ni mpenzi wa anasa! Sie tuliozoea maisha ya kawaida nikipewa 11M+ its a fortune! Maana nakula nini cha kumaliza 11M nzima mie zaidi ya mafuta ya gari labda sidhani kama hata familia yangu inamaliza 500K kwa mwezi!Hata ukiwa na pesa ndefu kiasi gani haikutoshi tu, labda uwe na matumizi madogo
Inbox mkuu hiyo documentAwa watu WAMEFANYA wananchi TUANZE KUOGOPA kabisaa
Wengine atukuwahi Kujua wanacholipw
kwakuwa wamelalamika tumeanza Kujua wanacholipwa kiukweli n hatarae Sanak
tunaomba mama YETU MPENDWA Apunguze HIZI POSHO pesa zingine zikajenge zahanati vijijini
Kabisa KENNYZipunguzwe Na Walipe Kodi