Dodoma: Rais Magufuli apiga simu mubashara kwenye Kongamano la CWT na kukanusha kufutwa kwa Ualimu Ngazi ya Cheti

Hii ngoma ilikuwa ishatoka hiyo, sema ikazuiliwa fasta, vinginevyo sasa hivi ingekula kwao.
 
Nadhani Kuna umuhimu wa Watanzania kuwa imara,kusoma na kuelewa. Naibu katibu mkuu alichoeleza na kipo kwa maeneno na maandishi ni mabadiliko yaliyofanywa kuondoa wanafunzi wanaopanga kwenda kusomea ualimu ngazi ya cheti kwa mwaka unaoanza wa masomo.

Kwa wale ambao wamemaluza cheti na wapo uraiani au wameajiriwa watatakiwa kwa muda wao kujiendeleza wapate diploma itakayowawezesha kujiunga ngazi ya degree.

Muda wakusoma ni miaka ambapo hiki kwa uelewa wangu si kitu kipya ni kitu kinafanya kazi. Mfano Kama mnakumbuka wanafunzi aliwahi kuwaita kilaza waliokuwa wanasoma UDOM wakaondolewa, Hawa wanafunzi walimaliza kidato Cha nne wakapelekwa kusoma diploma miaka mitatu na wapo mtaani.

Sijaelewa tunaposema Rais amekataza mnatuaminisha amekataza kipi? Amekataza watu wanaomaliza kidato Cha nne kuendelea kusoma diploma miaka mitatu Kama utaratibu ulivyo Sasa au amefuta mfumo wa kusomea cheti ambao tulishaachana nao?

Lakini pia haya Mambo unapoyakataa huoni Kama unapingana na sera ya elimu ya nchi?

Nadhani kwenye elimu tukiendelea kutumia siasa wanayofanya chama Cha walimu tunakwenda kuitumbukiza shimoni hii taaluma. Tujiulize hiyo simu iliyopigwa kwenye kikao kwanini ipigwe leo? Kwanini tangazo litoke leo? Kwamba Naibu Katibu Mkuu anaweza kutangaza Jambo Kama hili bila Baraza la Mawaziri kufahamu?

Elimu yetu ikiendelea kuendeshwa kwa matamko tutarudi walipotutumbukiza akina Mungai kufuta michezo na Mlongo kuunganisha physics na chemistry
 
Huyu mzee baba [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Fake news ni habari yakupikwa isiyo na ukweli wowote. Hii inayohusu vyeti siyo fake news kwa sababu imetolewa na mamlaka husika kwa vyombo vya habari.

Mhe. Rais kaukataa huu utaratibu haupelekei habari ya awali kuwa Fake Bali unabatilisha maamuzi ya awali. Tulinde habari na tuache habari hizi ziwepo humu kuwawezesha watu kuwa na kumbukumbu ya kila Jambo.

Naibu Katibu Mkuu ameeleza Jambo kubwa sana ambalo baada ya kubatilishwa na Mhe. Rais linakwenda kuathiri utaratibu wa udahili wa wanafunzi katika vyuo.

Utaratibu ulioamuliwa kutumika na ambao vyuo walianza kuutekeleza ni wakudahili wanafunzi wa Diploma kwa waalimu na kuachana kudahili wanafunzi wa cheti.

Endapo tunarudi kudahili waalimu wa cheti lazima serikali utoe mwongozo ili wanafunzi waliopo nyumbani wajue, wazazi wajue na watu wengine wajue.

Serikali isipotoa ufafanuzi na mwongozo wapo wazazi watawapeleka watoto kusoma cheti Cha ualimu then mwakani vyeti hivyo vikaondolewa kwenye soko la ajira.

Lakini hata Sasa hivi waalimu wanaodahiliwa kwa ngazi ya cheti wanaajiriwa wapi? Mwalimu anayeajiriwa shule ya msingi lazima awe na diploma Hawa wa cheti tunaodhani Mhe. Rais atawaruhusu waendelee kusoma watakwenda kufanya kazi wapi au tunategemea kurudisha upya mfumo wa ualimu wa cheti ambao serikali hii ilianza kuwaondoa?

Hili Jambo linahitaji mjadala mpana la sivyo wazazi mtapoteza fedha huku watoto wakisoma ualimu wa cheti usiokuwa na ajira. Bora hizo fedha watoto wakasome fani nyingine zisizo na mkanganyiko wa kisiasa.
 
Kwamba Madam Dokta Ave Maria Semakafu Naibu katibu Mkuu wa wizara ndio MPUMBAVU?
 
Aiseh Elimu yetu IPO mashakani

Hivi inawezekanaje wizara iamue X walio nje ya wizara ambao kimsingi sio wataalamu waamue Y?...
Hata mie nashangaa. Maana katika hali ya kawaida kwenye serikali yoyote najua uamuzi wowote wa kubadili sera huletwa kwenye baraza la mawaziri (ambapo rais ni mwenyekiti) ili lijadiliwe na kuridhiwa kabla ya kutekelezwa na wizara husika.

Sasa hapa ni kama naibu katibu mkuu dkt.semakafu anaenda kutolewa kafara. Sitashangaa akitumbuliwa na kama ikitokea hivyo watakua wamemuonea maana jambo kama hili haiwezekani liwe limeamuliwa hapo wizarani tu.
 
Na hii video pia ni ya uongo

Akikujibu nishtueeeee πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Vyombo vya dola vina kazi ndogo sana mwaka huu!!! Yaani huu ni ushahidi toshaaaa kuwa huyu jamaaa hatoshi na hafaiiii kuwa kiongozi mkuu wa hii nchi πŸ˜‚πŸ˜‚. Yaani anapinga tangazo la serikali yake mwenyewe???πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Tundu Lissu jiandae tu kuwa Raisi kwa kweli!!
 
Jaman msidanganywe na wanasiasa wa lumumba, hawa ni vijana wa lumumba ndo wanatengeneza haya mambo ni kutafuta kiki kwa waalimu, hapa wanataka kuwarudisha waalimu kwenye msitari kwasababu wameona ni maji ya shingo. Kimsingi wao waongeze mishahara tu ndipo wataeleweka tu tofauti na hapo mambo yatakuwa magumu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…