Dodoma: Spika Ndugai awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Halima Mdee

Dodoma: Spika Ndugai awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Halima Mdee

MIMI BABA YENU

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2019
Posts
305
Reaction score
728
Spika wa Bunge Job Ndugai, amemuagiza Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika, kuandika barua ambayo ataambatanisha na katiba ya chama chake pamoja muhtasari wa kikao kilichofanya maamuzi ya kuwafukuza uanachama wabunge 19 wa chama hicho.

"Aandike barua aambatanishe na katiba ya chama chake, aniambatanishie na muhtasari wa hicho kikao kilichofanya hayo maamuzi, inawezekana huyo Katibu Mkuu kaamka tu kaandika halafu na mimi nakurupuka nachukua hatua, nitakua ni Spika au kitu cha ajabu, hivyo andika ili ile barua niwape watalam waangalie, halafu namuuliza msajili wa chama hawa wajumbe walioorodheshwa ndiyo wajumbe halisi?", amesema Spika Ndugai

"Pia naangalia kwenye muhtasari ule je hawa wabunge wanaotuhumiwa kufukuzwa walipata nafasi hata ya kujieleza na walisikilizwa?, nifukuze watu ambao hawakusikilizwa popote, yaani mbunge hujawahi kusikilizwa wanandika tu fukuza hawa, viko vyama vimejaa mfumo dume, kundi la wanaume wamekaa wanafukuza wanawake 19 kwa mpigo hata kama barua hiyo inatoka CCM lazima nitawaambia 'stop' kwanza taratibu", ameongeza Spika Ndugai.

 
Mfumo Dume CHADEMA? Hii hii ambayo ilikua na wagombea wanawake majimbo zaidi ya 70?

Anapodai hawakusikilizwa ina maana gani ilihali waliitwa na walikataa kutokea wote? Kama walikua na hoja kwanini hawakuja kwenye kikao?

Spika akiamua kuwalinda awalinde tu ila asitafute justification zozote. Lipumba alipotimuwa viti maalum wote wa CUF sikuona akiitwa ana mfumo dume ila walimpongeza kwa kuleta nidhamu.

Sophia Simba alipotimuliwa na JPM hawakusema kuna mfumo dume ila haraka haraka spika akaandika barua kwa NEC kuwa kiti kipo wazi.
 
Kama ule ushahidi wa barua Ile ya KM chadema iliyoletwa hapa mitandaoni imeanda hivyohivyo bungeni, hata angelikuwa Mbowe spika awafukuze wabunge wa CCM Kwa barua hiyo, nafsi ingemsuta.

Tuweni wakweli, Ile barua ya kuwafukuza ubunge 19, iliandikwa kitoto saana!! haikuwa na nidhamu hata kidogo

Kwa kuwa siku hizi, ukweli sio nshu Sana, basi kelele ziendelee.
 
Spika andunje ndugai ni mwendawazimu hakuna asiyemfahamu, kama propesa LIPUMBA vuuu aliweza kuvamia chama cha cuf na akawafukuza uanachama wabunge wa viti maalum wa cuf, na spika ndugai akafanyia kazi ile barua ya mwenyekiti feki, Leo bila aibu keshasahau uhuni ule aliofanya.
 
Lengo la chadema kuwafuka kina Halima ni nini? nyie kila siku mnasema uongozi tufuate hekima katika maamuzi , mnataka kufukuza kwa kuwa ni wabunge wanakula pesa za ubunge au kwa kuwa sisi hatukupata hiyo nafasi? huo sio u dictator kweli kuamuka usiku na kufukuza wana chama wenu? tumieni busara sio kila mara mnakuwa na sintofahamu ambazo hazileti tija katika chama chenu, mnajizoofisha.
 
Kama ule ushahidi wa barua Ile ya KM chadema iliyoletwa hapa mitandaoni imeanda hivyohivyo bungeni, hata angelikuwa Mbowe spika awafukuze wabunge wa CCM Kwa barua hiyo, nafsi ingemsta

Tuweni wakweli, Ile barua ya kuwafukuza ubunge 19 kutoka KM kwenda Kwa Sipika, Jamani Ile barua haikuwa na nidhamu aisee

Kwa kuwa siku hizi, ukweli sio nshu Sana, basi kelele ziendelee
Kwani taratibu za wabunge wa viti maalumu hadi kufikia hatua ya kuapishwa IKOJE!? Ilifuatwa???? Angejibu hilo bwana spika angeonekana kweli anawapenda wanawake, otherwise tuendelee tu kutokuheshimu hata kanuni zetu wenyewe.
 
Back
Top Bottom