Dodoma: Spika Ndugai awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Halima Mdee

Dodoma: Spika Ndugai awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Halima Mdee

Ni dhahiri sasa Tanzania ina utajiri wa mambo mengi na huyu spika ni miongoni mwa 'utajiri' wetu na huenda anapatikana kwetu tu duniani kote!
Ndugai tukimtumia vizuri tunaweza kuingiza mapato mengi sana kwa vituko vyake
 
Ewe mungu wa majeshi hebu malizia kazi uliyoianza tupumzike sasa.
 
Kuna kitu kinaitwa precedence. Kama kila wakati ulikuwa unafanyia kazi barua bila kudai viambatisho hivyo, ukija vidai kwa mtu mwingine ni dhahiri utaonekana una lake jambo.

Na taratibu ni kuwa unapopokea barua kama hiyo ambayo unaona imekosa viambatisho ni kuwa unamwandikia aliyekuandikia ile barua kuwa hauwezi kuifanyia kazi kwa sababu ina mapungufu kadha wa kadha. Kukaa kimya bila kuijibu maana yake ni kuwa umeipokea na umeridhika kuwa imekamilika. Hii kuamka bungeni na kutoa sababu zisizo na kichwa wale mbele ni kutaka kuonyesha ubabe tu. Hawasaidii wakina Halima bali anazidi kuwafukia

Aidha, haya majibu yanatakiwa yatoke NEC sio kwake. NEC ndio wanaomtangaza mtu kuwa mbunge au la. Yeye alitakiwa awaambie NEC na hao ndio waseme kuwa wanawatambua wakina Halima kuwa wabunge halalali kwa sababu kadha wa kadha.

Amandla...
precedence ina nguvu mahakamani/sheriani sio huko mtaani na bungeni.
 
Hivi spika ni msemaji wa cdm au?

Afu kama hao watu walishafukuzwa kwa nini chama kisipeleke taarifa rasmi na orodha mpya ya wanachama wake wanaotakiwa kuwa wabunge wa viti maalumu.

Pili kwa nini chama kisiende mahakamani kuwashtaki spika na hao wabunge wake kwa kutumia jina la Chadema kinyume na utaratibu?
 
Back
Top Bottom