Dodoma: Spika Ndugai awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Halima Mdee

Dodoma: Spika Ndugai awapa mbinu CHADEMA ili awafukuze akina Halima Mdee

Kwani tatizo ni kufukuzwa chama tu? Hivi kwani hawa wabunge 19 walipatikana kwa kufuata taratibu za kisheria zilizopo?

Hiiiiii bagosha!
Wakuomba udhibitisho wa kisheria ni spika? Utaratibu wa kisheria kama haukufuatwa ni juu ya hao 19 kwenda mahakamani
 
Lakini ukimsoma mbele zaidi anadai hawezi kufukuza watu ambao hawakupewa nafasi ya kujitetea, sasa kama waliitwa wakagoma kwenda alitaka wabebwe mgongoni?
Ndugai alikaa sana India inawzekana alisahau akili huko.

Waliitwa kwenye kikao hawakutaka kwenda, walitegemea CHAMA kisubiri mpaka watakapojisikia kwenda.
 
Maoni kama haya ya kwako, siyo ya mtu aliyejiunga na JF 2009. Ni kama kijana mdogo wa form six vile! Tatizo ni nini? Ukabila? Chama? au nini?
Wagwaya kumpoteza mjomba wako au nini? Basi kamtonye, njia kama hiyohiyo ndo aliyoondokea mungu wa Burigi, badala ya kujiliza humu.
 
Maoni kama haya ya kwako, siyo ya mtu aliyejiunga na JF 2009. Ni kama kijana mdogo wa form six vile! Tatizo ni nini? Ukabila? Chama? au nini?
Ni maoni au fact?
 
Nimemsikiliza huyu jamaa Mama amashughulikie haraka atamletea balaa, kwanza baya katika lote kumsema Marehemu mzee sita kuwa zile sifa kapewa boss tu lakini yeye ndio alifanya kazi lakini akasifiwa boss kwa hili kamkosea sana yule Mzee na inaonesha huyu ni mtu wa namna gani hata aliyofanya JPM au Mama atakuja kusema ni yeye aliyapitisha lakini sifa anapewa Boss kauli mbaya sana. Lingine emekebehi kauli ya Mama kuwa anatarajia kukutana na wapinzani kuongea mambo ya kitaifa kasema ya ndani kwao hawayawezi kutaka kuongea mambo ya kitaifa ya nini wataweza wapi. lingine anataka kuaminisha kuwa ni udhalilishaji wa kijinsia kwanini wanawake watupu 19 sasa aliskia toka lini wabunge maalumu wanaume sio ujinga tu. Huyu apigwe stop haraka mabega yameshapanda juu.
 
Wakuomba udhibitisho wa kisheria ni spika? Utaratibu wa kisheria kama haukufuatwa ni juu ya hao 19 kwenda mahakamani

Spika kajivisha kuwa refa mchezaji. Chadema wamefanikiwa kuonyesha udhalimu uliopo. Hiyo inatosha sana. Kwa hapa na Ayubu inatosha.

Kifuatacho sasa ni kuonana na mama.

Makubaliano kuhusiana na haki, usawa, na maridhiano ndiyo muda wake. Bila shaka mama hatazingua kwa maana kuzinguana ni matokeo ya mmoja kuzingua.
 
Ndugai hajielewi kabisa, anajidai kuwafundisha Chadema nini cha kufanya kama vile hiyo ndio mara ya kwanza jambo kama hilo kutokea.

Lakini ukimsoma mbele zaidi anadai hawezi kufukuza watu ambao hawakupewa nafasi ya kujitetea, sasa kama waliitwa wakagoma kwenda alitaka wabebwe mgongoni?

Anaonesha wazi alivyoamua kuwalinda hao wanawake kwa gharama yoyote, ila ajue kwa hiki alichofanya anajiondolea heshima.

Amejidhalilisha mwenyewe, amelidhalilisha bunge kama taasisi inayotunga sheria, zaidi ameonesha hizo sheria wanazotunga bungeni hazina maana, pia kaidharau Katiba ya nchi, ni bora ajiuluzu ili kulirudishia bunge letu na yeye mwenyewe heshima yake.
Hivi ndugai alimpa lissu nafasi ya kujitetea kabla ya kumfukuza ubunge?
 
Spika wa Bunge Job Ndugai, amemuagiza Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika, kuandika barua ambayo ataambatanisha na katiba ya chama chake pamoja muhtasari wa kikao kilichofanya maamuzi ya kuwafukuza uanachama wabunge 19 wa chama hicho.

"Aandike barua aambatanishe na katiba ya chama chake, aniambatanishie na muhtasari wa hicho kikao kilichofanya hayo maamuzi, inawezekana huyo Katibu Mkuu kaamka tu kaandika halafu na mimi nakurupuka nachukua hatua, nitakua ni Spika au kitu cha ajabu, hivyo andika ili ile barua niwape watalam waangalie, halafu namuuliza msajili wa chama hawa wajumbe walioorodheshwa ndiyo wajumbe halisi?", amesema Spika Ndugai

"Pia naangalia kwenye muhtasari ule je hawa wabunge wanaotuhumiwa kufukuzwa walipata nafasi hata ya kujieleza na walisikilizwa?, nifukuze watu ambao hawakusikilizwa popote, yaani mbunge hujawahi kusikilizwa wanandika tu fukuza hawa, viko vyama vimejaa mfumo dume, kundi la wanaume wamekaa wanafukuza wanawake 19 kwa mpigo hata kama barua hiyo inatoka CCM lazima nitawaambia 'stop' kwanza taratibu", ameongeza Spika Ndugai.

Ndugai ni mnafiki na kwa sasa hafai kuwa spika wa bunge, kila mara anabadilika kulingana na upepo unavyovuma. Katiba ipo wazi hakuna mbunge isiyetokana na chama! full stop, Mdee na wenzake katiba haiwatambui kama ni wabunge. Wale walipelekwa bungeni kwa kivuli cha Magufuri kuionyesha jumuiya wa kimataifa kuwa demokrasia ipo wakati si kweli. Namshauri Ndugai awatimue hao wabunge feki asipofanya hivyo bunge halitokuwa na maana sababu yeye anasimamia kutunga sheria wakati huo anazikanyaga
 
La Sophia hulijui weweeeeee! Ungelikuwa unalijua ungelijua kuwa aliitwa kwenye vikao HALALI vya CCM na kujieleza kabla hajachukuliwa hatua.
Mbonà kwa Sofia Simba hakutaka hayo, huyu ni mtu hatari inabidi Mungu ampumzishe Kama alivyompumzisha wa Executive.

Kwan Covid-19 hawakuitwa na kukaidi? Au kikao kile kilikuwa haramu??

Tujaribu kufuatilia mambo kwa ukaribu zaid
Mlikuwa mmeishawahukumu kabla ya kuwasikiliza. Akina Mbow, Mnyika na Pambalu hawakuwa na "Leadership Tolerance". Ulikuwa in UJINGA kujitetea ilhali hukumu iliishaandikwa. Jifunzeni CCM.
 
Nakumbuka mdee na wenzake waliitwa kujitetea kwenye chama chao lakini walikaidi pamoja na kupewa barua ya kukumbushwa. Sasa Ndugai anataka kitu gani wakati suala hili lipo wazi
 
Ni dhahiri sasa Tanzania ina utajiri wa mambo mengi na huyu spika ni miongoni mwa 'utajiri' wetu na huenda anapatikana kwetu tu duniani kote!
Tunaye huyo, tuna vyura wa kiyansi (siyo yanga!), tuna Kilimanjaro, kuna mataga, sukuma gang, Tanzania tumejaliwa!
 
Hata wakina Halima wanakiri kuwa walipokea mwaliko wa kwenda kwenye kikao HALALI cha Chadema ila hawakwenda.
Waliishajua mchezo utaendaje. Watafukuzwa, watakata rufaa, rufaa yao itatupwa mbali halafu wao wataenda Mahakamani ambako Mahakama itasimamisha uamuzi wa Baraza Kuu mpaka 2025. Chadema wamewastukia.

Swali ni Mheshimiwa Spika aliwaapisha kwa kutumia vigezo gani? Kwa nini anapata kigugumizi kuweka wazi barua aliyopokea kutoka NEC ikiwatambulisha wakina Halima kama wabunge walioteuliwa mwa mujibu wa sheria na chama chao? Mpira uko kwake, sio kwa Chadema.

Amandla...
Dogo ulisikia jana Mnyika akikiri kuw Chadema kinapokea ruzuku? Je, unajua kuwa ruzuku inatolewa kutokana na matokeo "halali" ya Uchaguzi Mkuu? Kama ruzuku Chadema wanaitambua kwanini hawataki kuwatambua akina Mdee?
 
Kama ule ushahidi wa barua Ile ya KM chadema iliyoletwa hapa mitandaoni imeanda hivyohivyo bungeni, hata angelikuwa Mbowe spika awafukuze wabunge wa CCM Kwa barua hiyo, nafsi ingemsuta.

Tuweni wakweli, Ile barua ya kuwafukuza ubunge 19, iliandikwa kitoto saana!! haikuwa na nidhamu hata kidogo

Kwa kuwa siku hizi, ukweli sio nshu Sana, basi kelele ziendelee.
Mkuu sisi hapa ni watu wazima barura zakitoto tunazijua kuwa mistari yake inapinda, je barua ya chadema nayo mistari yake ilikua imepinda?
 
Ndugai hajielewi kabisa, anajidai kuwafundisha Chadema nini cha kufanya kama vile hiyo ndio mara ya kwanza jambo kama hilo kutokea.

Lakini ukimsoma mbele zaidi anadai hawezi kufukuza watu ambao hawakupewa nafasi ya kujitetea, sasa kama waliitwa wakagoma kwenda alitaka wabebwe mgongoni?

Anaonesha wazi alivyoamua kuwalinda hao wanawake kwa gharama yoyote, ila ajue kwa hiki alichofanya anajiondolea heshima.

Amejidhalilisha mwenyewe, amelidhalilisha bunge kama taasisi inayotunga sheria, zaidi ameonesha hizo sheria wanazotunga bungeni hazina maana, pia kaidharau Katiba ya nchi, ni bora ajiuluzu ili kulirudishia bunge letu na yeye mwenyewe heshima yake.
Kwani katiba yenu inasemajebkuhusu kumfukuza mtu uanachama?
 
Natafuta kijibwa koko kibayaaa, tayari nimeshapata jina la kukiita
Usithubutu. Sawa endelea. Nilitaka kukukataza bure. Wewe hukipendi. Nilikuwa na mbwa wakati andunje anamtoa bungeni Lissu. Nikamuita Ndugai kwa kumbukumbu. Huwezi amini. Alikufa kwa kichaa cha mbwa. Nikakumbuka mwenye jina ni mteja Mirembe. Nilisikitika.
 
Aliyadai yote haya baada ya dhalimu magufuli kumfukuza Sophia Simba ccm!?


Spika wa Bunge Job Ndugai, amemuagiza Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika, kuandika barua ambayo ataambatanisha na katiba ya chama chake pamoja muhtasari wa kikao kilichofanya maamuzi ya kuwafukuza uanachama wabunge 19 wa chama hicho.


"Aandike barua aambatanishe na katiba ya chama chake, aniambatanishie na muhtasari wa hicho kikao kilichofanya hayo maamuzi, inawezekana huyo Katibu Mkuu kaamka tu kaandika halafu na mimi nakurupuka nachukua hatua, nitakua ni Spika au kitu cha ajabu, hivyo andika ili ile barua niwape watalam waangalie, halafu namuuliza msajili wa chama hawa wajumbe walioorodheshwa ndiyo wajumbe halisi?", amesema Spika Ndugai

"Pia naangalia kwenye muhtasari ule je hawa wabunge wanaotuhumiwa kufukuzwa walipata nafasi hata ya kujieleza na walisikilizwa?, nifukuze watu ambao hawakusikilizwa popote, yaani mbunge hujawahi kusikilizwa wanandika tu fukuza hawa, viko vyama vimejaa mfumo dume, kundi la wanaume wamekaa wanafukuza wanawake 19 kwa mpigo hata kama barua hiyo inatoka CCM lazima nitawaambia 'stop' kwanza taratibu", ameongeza Spika Ndugai.

 
Dogo ulisikia jana Mnyika akikiri kuw Chadema kinapokea ruzuku? Je, unajua kuwa ruzuku inatolewa kutokana na matokeo "halali" ya Uchaguzi Mkuu? Kama ruzuku Chadema wanaitambua kwanini hawataki kuwatambua akina Mdee?
Sijasikia. Wewe mzee ndio unanifahamisha. Tatizo la Chadema na wakina Mdee ni kuwa hawakufuata utaratibu. Wamejipeleka bila ridhaa ya Chadema. Ndio maana husikii Chadema wakimpigia kelele yule dada ambae inasemekana alishinda pamoja na madiwani wao. Wakina Mdee wangekuwa wavumilivu pengine wangeteuliwa ili waingie Bungeni kihalali.

Amandla...
 
Spika wa Bunge Job Ndugai, amemuagiza Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika, kuandika barua ambayo ataambatanisha na katiba ya chama chake pamoja muhtasari wa kikao kilichofanya maamuzi ya kuwafukuza uanachama wabunge 19 wa chama hicho.

"Aandike barua aambatanishe na katiba ya chama chake, aniambatanishie na muhtasari wa hicho kikao kilichofanya hayo maamuzi, inawezekana huyo Katibu Mkuu kaamka tu kaandika halafu na mimi nakurupuka nachukua hatua, nitakua ni Spika au kitu cha ajabu, hivyo andika ili ile barua niwape watalam waangalie, halafu namuuliza msajili wa chama hawa wajumbe walioorodheshwa ndiyo wajumbe halisi?", amesema Spika Ndugai

"Pia naangalia kwenye muhtasari ule je hawa wabunge wanaotuhumiwa kufukuzwa walipata nafasi hata ya kujieleza na walisikilizwa?, nifukuze watu ambao hawakusikilizwa popote, yaani mbunge hujawahi kusikilizwa wanandika tu fukuza hawa, viko vyama vimejaa mfumo dume, kundi la wanaume wamekaa wanafukuza wanawake 19 kwa mpigo hata kama barua hiyo inatoka CCM lazima nitawaambia 'stop' kwanza taratibu", ameongeza Spika Ndugai.

Delaying tactics.... Yaani huo mlolongo unaweza kuchukua 5 years.

Anachofanya sasa ni kuonyesja tu how much power he has..... Ambazo hakuwa nazo wakati ule.
 
Kama ule ushahidi wa barua Ile ya KM chadema iliyoletwa hapa mitandaoni imeanda hivyohivyo bungeni, hata angelikuwa Mbowe spika awafukuze wabunge wa CCM Kwa barua hiyo, nafsi ingemsuta.

Tuweni wakweli, Ile barua ya kuwafukuza ubunge 19, iliandikwa kitoto saana!! haikuwa na nidhamu hata kidogo

Kwa kuwa siku hizi, ukweli sio nshu Sana, basi kelele ziendelee.
Acha unazi! Utapata madhara yasiyokuhusu!! Waache hawa wafe na dhambi zao!!
Shauri yako.
 
Back
Top Bottom