Kalifuata au kaenda kuliangalia?!
Hahahah huyu mgonjwa amekuwa kitukp kweli sasa kajipeleka ana shangaa hawajamuhoji wakati hakuwepo na alisha sema kuwa wao ndio walimshambulia sasa sijui anataka wamuhoji nini wakati majibu anayo mkononi hahahaha mgonjwa bwana
Kila kitengo hujiendesha Kwa kanuni na taratibu zake, haiwezekani mtu kutoka anakokujua Yeye atake matakwa yake Yeye yafuatwe!! Utakuwa upumbavu
Honestly, nyie watatu ingalau π πππ kuna shida ya ufahamu ktk bongo zetu....
Nimejaribu kupata logic ya hoja zenu, nimeshindwa kuona kama zina connection na mada zaidi tu kwamba ni maandishi tu yasiyo na substance ndani yake....
Kwa sababu mantiki iliyo ktk maelezo ya msingi ya mada hii ni:
ββ’ Jamaa (yeye mwenyewe - Tundu Lissu), baada ya kuona hakuna uchunguzi unaoendelea kwenye ishu hii ameamua kwenda kuomba apewe gari lake ili maisha yaendelee....
ββ’ Tena ni baada ya "..utaratibu wa kawaida kulipata kwa njia zingine " kushindikana. Kwa statement hii inaonesha wazi kuwa kumbe kulikuwa na mawasiliano yanaendelea kati ya muathirika wa unyama ule na jeshi la polisi)....
ββ’ In response, SACP Muroto akajibu kusema, jeshi linahitaji muda zaidi kujiandaa kumkabidhi gari hilo kwake....
ββ’ Sambamba na hilo, SACP Muroto akachomokea na ishu ya kutaka maelezo ya mwathirika (Tundu Lissu) kuhusu shambulio hilo (miaka mitatu iliyopita!!) something very ridiculous, right?
ββ’ In response, Tundu Lissu akamwambia, hakuna shida. Yuko tayari kutoa maelezo yake polisi kwa trh na muda mwafaka kwa pande zote.....
ββ’ Lakini wakati huohuo TL akaonesha mshangao wake kwa jeshi hilo kupitia SACP Muroto kwa kushindwa kumhoji yeye na dereva wake kwa miaka mitatu sasa baada ya shambulio licha ya Jeshi hilo kuwa limewataarifu Lissu na dereva wake kuwa wangeenda kuwahoji na kuchukua maelezo yao walipokuwa Nairobi Hospital - Kenya....
Lakini in very surprising circumstances, Polisi wakaingia mitini na baada ya hapo zikafuata mfululizo wa kauli za kisiasa kwa polisi wetu hawa huku wakiitupa sheria kule....
BAADA YA MAELEZO HAYA....
Hebu nyie watatu tuambieni hoja zenu ni nini? Mimi nawaona kama vile nyie siyo watu mnaotumia akili kufikiri. Ni kama maroboti fulani hivi....
Yaani mmeshindwa hata kung'amua kuwa hii "move" ya Tundu Lissu ina lengo maalumu la kuliweka Jeshi la polisi kwenye target yake.....
Na polisi wapende au wasipende wataingia tu (na ofcoz walishaingia wenyewe kwa hiari yao kitambo tu)...
Kwa sababu Polisi wanapoacha kufanya kazi yao au kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria badala yake wanafuata maelekezo ya kisiasa yasiyozingatia sheria zinazoongoza utendaji kazi wao kutoka kwa mabosi wao "raia" baki kabisa kina Makonda ama Magufuli, tayari ni KUPOTEA KWA KIWANGO CHA JUU SANA....!!