Does Africa have its own (unique) definition of democracy?

Does Africa have its own (unique) definition of democracy?

Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Eti ndugu zangu watanzania;

Does Africa has its own (unique) definition of democracy?

Je, Afrika ina tafsiri yake binafsi (ya kipekee) ya neno demokrasia?

View attachment 1516346

Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, nimepokea ujumbe huu kutokwa kwa mtoto wa ndugu yangu analiyezaliwa na kuishi huko huko Ulaya (Uholanzi) na hajawaji kukanyaga huku Tanzania (Africa). Huyu dogo ana miaka 15, kama angekuwa huku Tanzania let's say labda angekuwa form II?

Just imagine wewe ndio Infantry Soldier, ungewezaje kumjibu huyu mtoto wa ndugu yako?

PUMZIKA KWA AMANI MZEE MKAPA. VITA UMEIPIGANA NA MWENDO UMEUMALIZA BABA YETU. MUNGU AKUPE PEPO ILIYO NJEMA MZALENDO MWENZANGU.

View attachment 1516337

OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

BIASHARA: Ninauza Vitabu Vya Kujifunzia Lugha Ya Kijerumani. Ich komme aus der Stadt Dar Es Salaam und verkaufe diese Deutsch-Lernbücher
This is a very critical question kijana
 
Demokrasia ni uhuru wa kujiamulia mambo. Hii inategemea mazingira ya wahusika. Je Afrika tuna aina ya kipekee ya demokrasia, hapana, kila nchi inajiamulia mambo yake inavyowapendeza wananchi wachache (wanasiasa).
Kuna wanaobadili uongozi baada ya muda maalum, kama ilivyo huko Uholanzi au Marekani, kuna walioamua mtu mmoja atawale mpaka atakapoishiwa uwezo wa kutawala, kama ilivyo China ama Urusi. Kulindana kimaslahi, kurithishana uongozi, kupo kama ilivyo popote duniani, tofauti, Afrika umma hauheshimiwi na kupewa unachotaka, pengine ni kama Marekani (electoral college vs popular votes), ila Afrika hata katiba haiheshimiwi. Je demokrasia ya Afrika ni kwa ajili ya nani?
nzuri sana hii...
 
Tafsiri ya democrasia ni moja, ni kutekeleza maamuzi/ mawazo ya wengi. Tutofautishe demokrasia na vitendo kama udikteta, wizi wa kura na kung'ang'ania madaraka. Shida iliyopo ni kujua usahihi wa kile kinachoitwa ni mawazo ya wengi kama ni sahihi au kimetengenezwa.

Off the topic, kama una vitabu elementary vya kujifunza Kitaliano au Kispaniola njoo inbox.
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty.

Eti ndugu zangu watanzania;

Does Africa has its own (unique) definition of democracy?

Je, Afrika ina tafsiri yake binafsi (ya kipekee) ya neno demokrasia?

View attachment 1516346

Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, nimepokea ujumbe huu kutokwa kwa mtoto wa ndugu yangu analiyezaliwa na kuishi huko huko Ulaya (Uholanzi) na hajawaji kukanyaga huku Tanzania (Africa). Huyu dogo ana miaka 15, kama angekuwa huku Tanzania let's say labda angekuwa form II?

Just imagine wewe ndio Infantry Soldier, ungewezaje kumjibu huyu mtoto wa ndugu yako?

PUMZIKA KWA AMANI MZEE MKAPA. VITA UMEIPIGANA NA MWENDO UMEUMALIZA BABA YETU. MUNGU AKUPE PEPO ILIYO NJEMA MZALENDO MWENZANGU.

View attachment 1516337

OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.

BIASHARA: Ninauza Vitabu Vya Kujifunzia Lugha Ya Kijerumani. Ich komme aus der Stadt Dar Es Salaam und verkaufe diese Deutsch-Lernbücher
 
Bwana Infantry Soldier,

Demokrasia kama nadharia na kanuni ya kiutawala husisitiza kwamba uhalali wa utawala wowote ule duniani ni lazima utoke kwa wananchi na siyo vinginevyo, pia uhalali wa utawala ni lazima ulenge katika kuwafanya hawa wananchi wapate maendeleo. Hapa unaweza ukawa na mfumo wa aina yoyote ile, aidha Ufalme (A Monarchy), Udini (A Theocracy) au Jamhuri (A Republic) muhimu kabisa ni kwamba lazima nguvu itoke kwa wananchi na siyo vinginevyo.

Watawala lazima watawale kwa matakwa ya wananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa baina ya watawala na watawaliwa. Watawala hawatakiwi kufanya jambo lolote lile ambalo litaathiri mustakabali wa wananchi bila wananchi kuhusishwa. Wakijiamulia tu mambo, tena ambayo yanaumiza watawaliwa basi uhalali wao wa kutawala unapotea.

Wanafalsafa wa kale kama John Locke, Thomas Hobbes na Jean-Jacques Rousseau walizungumzia kitu kiitwacho The Social Contract ambapo walisema mataifa hutengenezwa kwa makubaliano baina ya watawala na watawaliwa. Pindi watawala wanavunja hayo makubaliano na kujiamulia kufanya jambo ambalo litawadhuru wananchi wao basi wanapoteza uhalali.

Nakubaliana na Mzee Nyerere kwamba kila sehemu ina Demokrasia yake, japo lazima tukubali kwamba tunaweza kutoa tafsiri mbalimbali za demokrasia na tusiwe na tafsiri moja kuhusu demokrasia. Lakini nachelea kusema kwamba lengo la demokrasia ni moja tu duniani kote, kwenye mifumo yote ya utawala nalo ni "KUHAKIKISHA NCHI INAWALIWA KWA KUFUATA MATAKWA YA WATAWALIWA"

Hivyo basi naweza kumaliza kwa lugha ya kiingereza kwa kusema haya yafuatayo "Democracy as a value does not have a single accepted Universal definition. We can only define Democracy well through a Purposive Approach of what democracy aims to achieve within a particular society. And that is Ensuring the power to rule is derived from the people for their benefit: Suffice to say it, such benefit should always be just, moral and equitable"

NB: Tusijitie moyo, katika hili wenzetu wazungu pamoja na Ubepari wao wametushinda mbali sana. Kitendo cha kutawala kwa kufuata miiko ya kisheria kwa manufaa ya wananchi ndicho kimewafanya wafike hapa walipo leo: Sisi Afrika hata Katiba kuheshimu ni shida, utasemaje kwamba tuna demokrasia yetu ???
Asante!Wewe umenena Yale yalioko kwenye Viunga ya Moyo(mind)wangu.
 
Democracy as defined by Abraham Lincoln, the sixteenth president of the USA, is government of the people for the people and by the people. ... That is, the interest of the people should superintend over even that of government officials.
Kwa kulingana na maana hiyo hapa kwetu Africa hasa Tanzania kinachoitwa democracy si democracy kwakweli na Wala hakijawahi kuakisi maana halisi ya democracy,Bali kile kilichopo ni nguvu za mwananchi kupokwa na mtawala na hivyo mwananchi aliyepaswa awe na nguvu ya kumuwajibisha mtawala nguvu hizo zinakoma pale mtawala anapoingia madarakani Mara baada ya kushinda uchaguzi ambao kwa mazingira yake una tabia za kiuteuzi tu.Unapojadili kwamba hii tunayoishuhudia leo ni Zao la kidemokrasia tunakuwa hatujatendea haki Mfumo wa kidemokrasia kwa kuwa Hakuna sifa bainifu za kidemokrasia unazoweza kuziona katika baadhi ya tawala za Kiafrika,Kwahivyo tutafute neno lingine tuite Mfumo wetu wa kiutawala ambao itakuwa na sifa ya kiafrika.Hakuna Demokrasia ya kuzuia Maoni Kama yana lengo la kuelezea ubovu wa Mfumo ya kiutawala ya kiserikali.Jacques Rosseau wa ufaransa anaeleza kuwa "Man is born free and everywhere he is found in chains" tafsiri "Mtu huzaliwa huru lakini Kila mahali hujipata na mitanziko(pingu).
Mwisho ili tupate democracy ya kweli lazima Maslahi ya wananchi yawe na nguvu na uwezo kuliko ya watawala hata Kama watawala hao wamepewa dhamana hiyo na wananchi.
Cyrus Monroe.Political Analyst±255785310892
 
Democracy as defined by Abraham Lincoln, the sixteenth president of the USA, is government of the people for the people and by the people. ... That is, the interest of the people should superintend over even that of government officials.
Kwa kulingana na maana hiyo hapa kwetu Africa hasa Tanzania kinachoitwa democracy si democracy kwakweli na Wala hakijawahi kuakisi maana halisi ya democracy,Bali kile kilichopo ni nguvu za mwananchi kupokwa na mtawala na hivyo mwananchi aliyepaswa awe na nguvu ya kumuwajibisha mtawala nguvu hizo zinakoma pale mtawala anapoingia madarakani Mara baada ya kushinda uchaguzi ambao kwa mazingira yake una tabia za kiuteuzi tu.Unapojadili kwamba hii tunayoishuhudia leo ni Zao la kidemokrasia tunakuwa hatujatendea haki Mfumo wa kidemokrasia kwa kuwa Hakuna sifa bainifu za kidemokrasia unazoweza kuziona katika baadhi ya tawala za Kiafrika,Kwahivyo tutafute neno lingine tuite Mfumo wetu wa kiutawala ambao itakuwa na sifa ya kiafrika.Hakuna Demokrasia ya kuzuia Maoni Kama yana lengo la kuelezea ubovu wa Mfumo ya kiutawala ya kiserikali.Jacques Rosseau wa ufaransa anaeleza kuwa "Man is born free and everywhere he is found in chains" tafsiri "Mtu huzaliwa huru lakini Kila mahali hujipata na mitanziko(pingu).
Mwisho ili tupate democracy ya kweli lazima Maslahi ya wananchi yawe na nguvu na uwezo kuliko ya watawala hata Kama watawala hao wamepewa dhamana hiyo na wananchi.
Cyrus Monroe.Political Analyst±255785310892
Umeandika Makala ndefu sana kijana
 
Back
Top Bottom